LUSIFA NA TRIKI YA ''HEGELIAN DIELECTRIC'' #10
MTAALAMU WA TRIKI YA MUDA & SANAA YA KAMALI YA
AKILI
‘’HEGELIAN DIELECTRIC’
Hegelian dielectricNina uhakika kuwa, Lusifa hana
mbinu yenye mafanikio zaidi ya hii. hii ndiyo mbinu ambayo Lusifa amekuwa
akifanikiwa kwayo kwa miaka mingi sana. Kwa ufupi sana, kuelewa maana ya sanaa
ya kamali ya akili, ambayo nimetumia neno hilo kumaanisha sanaa inayoitwa kwa
Kiingereza ‘’Hegelian dielectric’’, unaweza elewa kwa kutumia mfano ufuatao.
‘’natengeneza ajenda yangu
kuwa, Watu wanahitaji Uhuru wa kuamua lolote lile wanalolitaka ‘’hii inaitwa
-thesis’’. Na kisha baada tu ya muda nasema kuwa, au hata mimi bila kusema
itaonekana kuwa, ‘’Uhuru bila mipaka ni hatari sana’’, na hii sasa tayari
inaitwa -antithesis’’, au ukinzani. Na hivyo sasa, baada ya hii ‘’antithesis’’,
sasa ndipo naibua ajenda yangu ya msingi ambayo nitasema, ‘’tunahitaji uhuru
lakini chini ya sheria kadhaa ambazo nitakuwa nimekwisha ziandaa’’, hii ndiyo
inaitwa ‘’new thesis’’. Hii falsafa imetumiwa sana hata na kina Karl Marx ambao
walikuwa ndiyo wapinga Kristo wakubwa kabisa kutokea Duniani, falsafa hii
japokuwa huonekana kugunduliwa na mwanafalsafa wa Kijerumani ‘’Friedrich
Hegel’’ miaka ya karne ya 19, lakini
tayari ilikuwa imekwisha kuanza kutumika na Lusifa kwa miaka mingi sana.
UTANGULIZI
Lusifa hajawahi kufanya kazi
akiwa yeye kama yeye, hata nitakapokuwa nikisema Lusifa, ninachomaanisha ni
namna Lusifa anavyowasilisha Mawazo yake, na akili zake za uharibifu kupitia
binadamu, au viumbe wake. Kuelewa namna
Lusifa anavyoweza kuingiza Mawazo yake moja kwa moja kwa binadamu, unaweza
Kwenda kusoma kitabu changu cha sanaa za mazingaombwe, uchawi, na sayansi ya
ubongo. ila nitajaribu kugusia baadhi ya hoja za msingi hata kwa sehemu hii.
katika sura hii tutatazama kiundani namna ambavyo Lusifa huwa akitumia watu
kukamilisha hila zake kwa kutumia mbinu ya kwanza ambayo ni triki ya muda, na
kamali ya akili ‘’hegelian dielectric’’.
Kwanini Lusifa hawezi Kutenda
moja kwa moja yeye kama yeye, zipo sababu kadhaa, awali nilishasema kuwa Lusifa
ana mipaka ya utendaji katika sayari hii ambayo inahitaji utendaji wa mwili,
lakini pia lusifa anataka kumuonyesha Mungu kuwa ni viumbe wake yeye mwenyewe
wanaomchukia kwa udhalimu wake, lakini pia Lusifa anataka kuwateka kwa
kuwalaghai ili hatma yake asibakie hata mmoja mwenye haki. Na ndiyo maana
nilisema pia awali kuwa, Lusifa ana motisha kubwa sana ya kuwadanganya wanadamu
na kuwalaghai ilihali anajua kuwa alishashindwa kuwazuilia Wokovu wao kwasababu
mbili, kwanza anahisi kama ataweza kuwaangusha wanadamu wote wenye haki,
ataweza kuharibu mpango wa Yesu wa kurudi mara ya pili, maana hakutakuwa na
mwenye haki hata mmoja, na hivyo atachelewesha wakati wake wa kuangamia, lakini
pia, kwa kuwa Mungu amekwisha muwekea mwisho wake, basi kadri tunavyoelekea
mwisho wake ndivyo mwisho unavyomvuta zaidi, kwa kuwa mwisho wake ni Kifo, na
chanzo cha Kifo ni uovu ‘’mshahara wa dhambi ni mauti’’, basi Uovu wake
unasukumwa zaidi ili hatma yake itimie.
SAYANSI YA TRIKI YA LUSIFA KATIKA MUDA
Katika Injili ya sayansi Q1
nilieleza kuwa Lusifa amekaa katika sayari ya Dunia kwa miaka mingi sana,
karibia 6000, huku binadamu wakidumu kwa wastani wa miaka 70-100 tu. Lusifa
hasahau taarifa, huku binadamu wakihitaji kurejelea kumbukumbu zao kila wakati,
na mwisho, Lusifa anaweza kuwepo katika maeneo mengi sana kwa wakati mchache,
huku mwanadamu akiwepo katika eneo moja tu, kwa wakati mmoja.
Faida hizi humpatia Lusifa
uwezo mkubwa sana wa kumchezea akili mwanadamu. Sasa basi, hoja ya kutambua
hapa ni kuwa, wanadamu kwa kawaida hubadili mitindo yao ya Maisha, au hata
falme hubadilika toka kuwa juu, mpaka kurudi chini kabisa, walahu kwa wastani
wa kila baada ya vizazi kumi, kumbuka kizazi kwa wastani ni miaka 25-30 kwa
mujibu wa toka Watoto wanazaliwa, mpaka na wao wanazaa. Ukiweza kukaa kwa
kipindi cha miaka 250-300, utagundua kuwa dunia huwa inabadilika moja kwa moja
na kuwa ya tofauti kabisa. Sasa basi, kwa kuwa binadamu huishi kwa asilimia
kama 25% tu ya wakati huu, basi wengi wao hujikuta wakiingia katika mtego bila
wao kujijua.
Mfano, kipindi serikali mbovu
inapokuwa madarakani, na viongozi wake wakiwa wala rushwa sana, wengi wa
mafisadi hujikusanyia sana mali, wakiwakandamiza watu wa matabaka ya chini,
bila wao wenyewe kujali, huku wakiona kawaida sana, lakini kumbe, wakati Huo
Lusifa huwa anatumia hiyo faida kukamilisha mabadiliko ambayo ameyalenga miaka
kadhaa tu mbeleni, na unaweza kuta, mwaka tu baada ya kizazi cha mafisadi hawa
kupita, jamii hiyo ikibadilika kabisa, wenda kwa vita, falsafa, Imani,
mapinduzi, n.k. lakini uwezo mdogo wa binadamu wa kuweza kuishi kwa muda mrefu,
humfanya kuwa mpumbavu mbele ya faida ya lusifa ya kuweza kushuhudia muda ukiwa
chini yake.
KAZI KUBWA YA LUSIFA YA KUIMALIZA DUNIA KUELEKEA 2031±
Mara zote ninapotumia 2031,
huwa namaanisha ni kipindi kizuri cha makadirio ambacho dunia inaenda
kukamilisha miaka 6000 ± na hivyo, ni kipimo kizuri sana cha utendaji wa kiumbe
mkubwa kama Lusifa kwa kipindi cha milenia zote sita ambazo zimepita chini
yake.
ZAMA ZA KWANZA ZA LUSIFA
Hatua ya Kwanza ‘’ 0-313 AD’’
Hiki ni kipindi chote tangia
Yesu anazaliwa, anakamilisha misheni yake, na anawaachia kazi mitume yake, hiki
kipindi kilihusiana na maendeleo makubwa sana ya Ukristo katika Dunia. Lusifa
hawezi kukubaliana na Ukristo kama tulivyoona katika sura iliyopita. Katika
Biblia hiki ni kipindi ambacho katika vipindi vya makanisa saba ya Ukristo, ni
kipindi cha kanisa la Efeso, na Smirna. Kipindi hiki, sehemu kubwa sana ya
Dunia ilikuwa na Upagani. Na Ukristo ulikuwa na Nguvu sana, hii ni kutokana na
nguvu ya ukweli ambayo ilikuwa imeubeba, na Nguvu ya Mungu ambayo pia,
uliambatana nayo.
Lusifa alitumia mbinu ya Maumivu,
na maangamizi ya damu ya wakristo ili kuwamaliza. Mbinu hii Lusifa huitumia
marazote pale anapoona maadui zake ni wachache. Lusifa hutumia mbinu ya Uongo
pale maadui zake anapoona ni wengi. Katika Historia ya Dunia unaweza kugundua
kuwa kipindi hiki kilihusiana na Umwagaji sana wa damu za wakristo, mfano,
kuanzia mwaka 303 mpaka 313 inafahamika kuwa ni kipindi cha Miaka kumi ya
mauaji makubwa ya wakristo chini ya mfalme Diocletian wa Kiroma.
Diocletian Aliona Ukristo
unakua sana, na unasukumwa na watu wachache sana, na unahatarisha dola yake
ambayo tayari ilikuwa na idadi kubwa sana ya Wapagani. Hivyo akaona ili
aiunganishe dola yake, maamuzi mazuri kabisa, yatakuwa awamalize hawa wakristo.
Kumbuka hata kabla ya kipindi hiki, tayari kuanzia enzi za mitume ambao wote
waliuwawa na waroma, ukristo ulikuwa unalengwa kumalizwa kabisa. Na ndiyo maana
unaweza kuona hata kabla Paulo hajauwawa, alikuwa akikutana na vipingamizi
vingi sana.
Hoja ya msingi ambayo nataka
kuieleza hapa siyo Historia, nataka kuonyesha mchezo au triki ya kamali ya
akili. Mwanzo kabisa, Lusifa anataka kuwamaliza wakristo wote, hili tunaweza
liandika kama:
Tatizo la Kwanza ‘’thesis’’:
Kuwaua wakristo wote
Lakini Lusifa kumbuka sio
kwamba ana akili nyingi sana, naye ni Mpumbavu tu. Lusifa anatumia faida ya
taarifa na uzoefu kama nilivyoelezea awali, katika mbinu yake ya kwanza ya
kutengeneza tatizo la kwanza, anafeli, kwa kuwa huwezi kuwaua watu wote wa Mungu,
sio kuwa Mungu atazuia, ila watu wa Mungu wana haki ya kupewa ahadi ya ulinzi
sawa na mapenzi ya Mungu. Na pia, Saikolojia ya wanadamu kwa namna ilivyo,
kadri ambavyo unavyowaua watu, ndivyo wengine wanavyojifunza zaidi kuhusu hao
watu, na kwa hivyo, utajikuta unachochea zaidi ajenda zao. Na kwa hivyo basi,
Lusifa hakuwa na namna zaidi ya kutumia mbinu ya pili, ambayo hii sasa inakuja
kama Ukinzani wa ajenda yake ya kwanza ‘’anti-thesis’’
Hatua ya Pili ‘’313-karne ya 9’’
Ukinzani ‘’anti-thesis’’;
Tuungane na Wakristo na kuwapa uhuru
Hii unaweza kuiona kipindi cha
miaka kuanzia 313, ambapo unamkuta sasa mfalme wa Roma ‘’Constantine’’
akijifanya kuwa naye ni Mkristo, na hapa sasa ndipo unapokutana na kukua kwa
Upapa, huku Upapa ukipatiwa mamlaka na Dola ya Rumi. hazikuwa ni hatua za moja
kwa moja, lakini ajenda kuu zilizokuwapo hapa, zilikuwa ni kuibua hisia za
Umoja sasa, na kupingana na uhasama dhidi ya Imani ya Ukristo.
Lusifa anahama katika mbinu ya
kwanza ya Kuua ‘’Joka’’, anaingia katika kudanganya ‘’nyoka’’, hii ni baada ya
kugundua kuwa amefeli, na hawezi kuwamaliza wakristo. Anawezaje sasa
kudanganya, anacheza na falsafa ileile, kwa mtu ambaye alikuwa hana uhuru, alikuwa
hatiani kuangamizwa, anaposikia kuwa sasa anaweza kukubalika, kuheshimika, na
hata kulindwa na Imani yake. Huwa anakuwa dhaifu sana kuweza kupingana na
mithili ya nafasi hii.
Wakristo wengi sana wanajikuta
wakiungana na mfumo wa kiroma, ambao unawapa uhuru wa kuamini, lakini uhalisia
wake, unawachochea tena kuingia katika matatizo mengine.
Kumbuka, zama hizi zote zipo
katika kipindi kingine kabisa cha kanisa la Mungu, zama za kanisa la smirna,
Pergamo, na Thiatira. Na zama hizi hutambulika pia kama za Giza, ‘’Dark ages’’,
ambapo hunukuliwa pia kuanza mwaka 538AD, mpaka miaka ya 1798. Katika zama
hizi, Dola ya Rumi katika miaka ya 476AD, inagawanyika katika pande kuu mbili,
mashariki, na magharibi. Huku magharibi ikianguka kabisa hata kutawanyika
katika makundi mbalimbali ya makabila ya kijerumani ‘’germanic tribes’’, na
ndiko huko hakukuwahi kamwe kuwa na utulivu, hata kupelekea baadaye kuibuka
mataifa kadha wa kadha. upande wa mashariki ambao ndiyo uliokuwa ukishikilia
pia nembo ya Ukristo, ulidumu kidogo ili kutengeneza taswira ya kielelezo cha
Nguvu ya ukristo huu mpya ambao umepokelewa, lakini hata hivyo, nao haukudumu
sana.
Zama hizi kunaibuka pia dola
ya uislamu, kuanzia miaka ya 600’S, na Uislamu unakua hata baadaye kuunda dola
ambayo inasambaa na kuteka maeneo mbalimbali, kuanzia Afrika, mpaka Sehemu
kadhaa za Ulaya. dola ya uislamu inasambaa ikiwa pia na ajenda ya dini mpya ya
Uislamu. Kumbuka mwisho wa karne ya
tisa, hata na dola ya uislamu pia inaelekea katika kuishiwa nguvu zake katika
kuendelea kusambaa zaidi, lakini tayari ikiwa imeshasambaa maeneo mengi sana
ambayo Ukristo ulikuwa umekwisha sambaa awali.
Triki ya Akili ya Lusifa
Watu wengi huchelewa kujua
lipi lilikuwa lengo kuu la Lusifa enzi za zama za giza. Lusifa alikuwa na adui
yake mkubwa sana, na ndiye adui yake wa nyakati zote, ambaye ni Kristo, na
wafuasi wake. Sasa Lusifa hapa lengo lake lilikuwa ni kutumia chapa ya
Ukristo, kuipatia Nguvu chapa yake, na kisha kuuruhusu Ukristo kuendelea kukua
lakini yeye akiendelea kuwamaliza wakristo wakweli. Ambao sasa watakuwa
wamebakia wachache sana, maana sehemu yao kubwa imekwisha chukuliwa.
Kutumia chapa ya Ukristo
ilikuwa kupitia kuifanya Rumi kuwa imebatizwa, ilihali bado imejaa upagani.
Kuipatia nguvu ilikuwa kupitia kuukabidhi mamlaka Upapa, na kutumia dola yake
kusambaza zaidi dini hii mpya ambayo tayari upagani upo tayari kuipokea, kwa
kuwa inasehemu kubwa zaidi toka kwao. Na mwisho, kuruhusu Ukristo kukua huku
ukiendelea kuangamiza wakristo wakweli, hii ilikuwa kupitia njia ifuatayo;
Hakuna Fundisho lenye msingi
wa Imani ya Ukristo zaidi ya kuwa, Kristo ni Mungu, na ndiye Njia, kweli, na
Uzima, na alikufa, na akafufuka ili kumkomboa mwanadamu.
Mafundisho hayo unapotoa, au
kupooza, hata moja tu, huo sio ukristo tena. Lusifa akilijua hili, katika zama
hizi, anatumia mbinu mbili ili kufanikiwa;
Kwanza, Anaibua dini ya
Ukristo wa Roma ambao anajua kabisa, katika Njia, anawekwa kiumbe mwingine
yeyote yule, ila siyo Yesu, mfano, kila unaposikia, Mama maria utuombee, maana
yake njia, au ‘’mediator’’, sio Yesu tena. Hii imeshaua Ukristo. Unapoweka
kweli nyingine yeyote tofauti na maneno na Maisha ya Kristo moja kwa moja,
mfano, unaposema Sabato ni jumapili, ilihali amri za Mungu zinaitambua kama
Jumamosi, tayari unaweka kweli nyingine. Mfano wa mwisho, unaposema watu
wanapokufa huenda katika sehemu yeyote ile, unamaanisha watu hawafi, maana yake
unapingana na kauli ya Mungu aliyosema, Utakufa. Lusifa alimpinga Mungu kwa
kumwambia Eva, hakika hautakufa. Na unaweza kumgundua Lusifa hapa, huweka
Uongo, husema kuwa, Hautakufa, utaenda Mbinguni, au, utaenda kwenye mateso
‘’toharani’’, hii ni sawa na kupinga kuwa hata Yesu hakufa! Hoja yangu siyo kuzichambua
dini hizi, lengo langu ni kugundua namna ambavyo triki hizi za akili
zinavyofanya kazi.
Pili, Kuibua kwa dini ya
Uislamu. Ijapokuwa wengi huwa hawachunguzi ukweli huu kiundani sana, maeneo
mengi sana ambayo awali yalikuwa yameshamiri sana Imani za Ukristo, kama maeneo
ya Afrika magharibi, na kaskazini, na hata maeneo kadha wa kadha ya nchi za
asia na ulaya, yalikuja baadaye Kujawa na Imani mpya za uislamu. Hoja kubwa
kuhusiana na Imani ya uislamu siyo kuwa ina mafundisho hatarishi, bali inajenga
Imani kuwa Yesu siyo Mungu, wala Yesu siyo njia, kweli na uzima. Ijapokuwa
anatambuliwa vizuri sana, lakini hoja ya msingi ya kutambua ni kuwa, kwa zama
hizi zote za Giza, jamii nyingi sana ambazo zilikuwa zimekwisha kupokea Nuru ya
Ukristo wa kweli, zikawa zikizidi kuipoteza, hii ni kutokana na kuwepo na
kushamiri kwa makundi mengi sana ambayo yote, hayana nuru ya kweli ya ukombozi
wa mwanadamu.
Hitimisho katika zama hii ya
Ukinzani ni kuwa, Lusifa anatumia mbinu ya kutengeneza hatarishi nyingi sana
katika dunia, zama hizi zinahusiana na hofu kubwa sana katika jamii za watu.
Makundi kama makabila ya Goths, yaani ‘’Visigoths, ostrogoths’’, hawa walikuwa
ni watu wa mapambano mfululizo, nao wakishindana na makundi mengine ya
‘’Huns’’, ambao hawa walikuwa ni majitu ya vita, na farasi, na walikuwa
wakatili kwelikweli, walipelekea makabila mengi ya goths kusogea sana roma, na
kuchochea zaidi dhiki, inakasemwa pia makundi haya ndiyo yalichochea sana hata
kuanguka kwa dola ya roma, kulikuwepo pia makundi kama ya Vandals, ambao hawa
walishindana sana na roma ya mashariki ‘’bryzantine empire’’, hawa walikuwepo
mji wa Carthage, maeneo ya Tunisia, hata maeneo ya kuzunguka kanda yote mpaka
miji ya spain. Dola za uislamu kuanzia kwa zama za ‘’Umayyad caliphate’’, mpaka
‘’Abbasid Caliphate’’, zilikuwa ni zama za dola kupambana, na kujitanua kivita.
Lengo, dhiki hizi zilitosha
kuwasahaulisha watu ukristo wa kweli, na namna pekee ya kuendelea kuipeperusha
bendera ya ukweli wa ukristo ilikuwa kupitia dola ya rumi ya mashariki, ambayo
ilikuwa na ukristo wa roma. Na huko ndiko ulikwepo Uhuru, na Umoja katika
kumwabudu Kristo. Lakini bahati mbaya, tayari ulikuwa ni mtego wa akili.
Hatua ya Tatu ‘’ karne ya 9 mpaka karne ya 14’’
Utii kwa Sheria ya Ukristo
‘’Upapa’’ ‘’new-synthesis’’
Hii ilikuwa ni mbinu mpya kwa
zama hizi kwa serikali za roma, na upapa, lakini ilikuwa ni gemu ya akili ya
Lusifa. alishatambua kwa idadi ya vizazi ambavyo vitakuwa vimeshapita, tayari
atakuwa na kila uwezo wa kuikamilisha. Mpaka hatua hii dola ya Upapa ilishakuwa
imepata nguvu mpaka mwisho. Na pia, dola ya upapa ilishakuwa imechukua nembo ya
Ukristo kwa dunia nzima. Sasa dunia haikuwa na chapa inayoweza tambulika tena
ya Ukristo zaidi ya Upapa. Na Lusifa alivyo mjanja hapa, akaweka mtazamo wa
akili za wengi uwe aidha Ukristo ambao ndiyo Upapa, au Uislamu. Na ndiyo maana,
katika zama hizi, kulikuwa na migogoro mingi sana kati ya wakristo, na
waislamu, hasa katika kupambania ardhi iliyosemwa takatifu, ya mji wa
Yerusalemu. Vita vingi sana vilipiganwa, huitwa pia ‘’Crusades’’, na pia
kulikuwa na migogoro mingi sana, ambayo yote ingetosha kutomfanya mtu kukumbuka
kuwa, Ukristo wa kweli ulikwisha kuwa umepotea mpaka hatua hii.
Mtego wa akili wa Lusifa
Lusifa anatumia Dola ya
ukristo wa Roma kukubalika katika maeneo na jamii mbalimbali kama mjumbe wa
haki, na anapata sana Nguvu huko. Kadri anavyopata zaidi Nguvu, huku akiwa juu
sana kimamlaka, analazimisha jamii zote kutii na kukubaliana na mamlaka yake
ambayo ina sura ya kidini, au wokovu wa kiroho. Kwa nje anapozidi kukubalika
kutokana na dhiki ambazo watu wamekwisha choshwa nazo, basi yeye anachochea
zaidi dhiki kwa kugandamiza zaidi watu, sasa
mpaka kiroho.
Unaweza kuelewa hili kwa namna
ambavyo dola hii sasa hata Biblia tu kitabu cha Kristo mwenyewe hakitumiki,
watu wakiagizwa kutumikia taasisi za kidini, wakihesabiwa haki kwa msamaha
ambao kwa vipindi kadhaa iliwagharimu hata kugharamia kwa fedha, dola hii
ilishindana sana na makundi waliyopingana nayo, na iliwaadhibu kwa adhabu kali
sana hata kifo. Haikutenda kama Ukristo wa mitume, haikuvaa kama wakristo wa
mitume, haikusema pia, ila ilijitambulisha kwa sura hiyo.
Unategemea kwa ukandamizaji
huu wa upapa ambao vitabu kadhaa vimeandikwa kuelezea tu zama hizi za giza,
mfano, ‘’The Two Powers: Upapa, Ufalme, na mapambano dhidi ya Uhuru ya karne ya
13’’ kimeandikwa na ‘’Brett Edward Whalen’’ kuna ‘’A short history of Papacy in
Middle Ages’’ kimeandikwa na Walter Ullman’’’, kuna ‘’The Great Controversy’’,
kimeandikwa na Ellen G. White. Kuna mamia ya vitabu wenda msomi mdogo anaweza
Jifunza zaidi katika maktaba za historia za dunia, hasa zama za giza, mpaka
kuinuka kwa marekani. ukandamizaji ulikuwa mkubwa sana, na matokeo yake, watu
wengi sana wakaanza kuuchukia Ukristo.
Mpaka hapo watu wanauchukia
Ukristo, na kumbe hata haukuwa Ukristo ambao kimsingi ulikuwa ukiwatesa. Hii
ndiyo mitego ya akili ya lusifa. kwa mara ya kwanza anafanikiwa kutumia
Hegelian Dielectric kutengeneza Chuki kuhusiana na Ukristo, huku bado hata Ukristo
wenyewe ukiwa bado hauonekani.
Unajifunza nini kuhusiana na
muda?
Kwa vizazi visivyozidi 50, kwa
wastani wa miaka 30 kwa kizazi, au kama utatumia wastani wa miaka 70, basi
unavizazi visivyozidi 20 tu, Dunia imeshaingia katika hatua mpya kabisa, ya
Kuuona Ukristo kama ni Ukandamizaji, wakati awali Ukristo ndiyo ulikuwa Ukandamizwaji.
Hii ni mbinu ya Lusifa ya mafanikio sana. Lakini hata hivyo, bado hili halikuwa
lengo lake, hebu tuangalie hatua inayofuata.
ZAMA ZA MWISHO ZA LUSIFA
Hatua ya nne ‘’ karne ya 14 mpaka 1798’’
Tatizo la kwanza ‘’thesis’’ :
Hakuna Uhuru
Hapa Lusifa ameshacheza mchezo
wake, anajua kwa kizazi hiki jamii ya watu lazima itaanza tena kuutafuta Uhuru.
Kiukweli ni kuwa, watu hawawezi kuwa tena na historia kwa kipindi cha zaidi ya
milenia hata wakaweza kujua awali ilikuwaje, na hivyo wote wanaozaliwa katika
zama hizi, wanachojua ni kuwa Dunia haina Uhuru kutokana na mifumo yake, hasa
ya dola ya Upapa. Na watu hawa wanajua kuwa ni ngumu sana kwa dola hii kuweza
kutoka katika mamlaka yake, na ndivyo ambavyo marazote huwa inakuwa, awali dola
huwa kama vile haziwezi anguka, lakini hapo ndipo hatua ya kuanza mzunguko
mwingine huwa inaanza.
Katika zama toka karne hii ya
14, kuna ibuka matatizo mengi sana ambayo yanatokana na jamii kutaka kujitoa
katika giza la ugandamizaji wa kimwili, na kiroho. Na hapa ndipo Dunia inaingia
katika zama zinazoitwa zama za Nuru ‘’Enlightenment stage’’. Katika zama hizi,
kunatokea mapinduzi yafuatayo.
Kwanza, mapinduzi ya Kifikra.
Dunia inaanza Kujawa na watu wenye uhuru wa kifikra, ambao wanaamua kutumia
akili zao katika kutaka kujifunza wenyewe, bila kuambiwa cha kujifunza, au
kuaminishwa na mamlaka. Na hapa ndipo wanapoanza wanasayansi wakwanza kabisa
wakubwa, kama vile kina Corpenicus, Keppler, Galilei, Newton, n.k. kiufupi hawa
wote utakuta wakipingana na kweli nyingi sana ambazo awali zilikuwa
zikiaminishwa katika taasisi kubwa hasa za dini. Mfano, hapa kunaibuka sayansi
ambayo inathibitisha Dunia ni mviringo, ndiyo inayoizunguka jua, sayansi za
afya ambazo zinasema Ukifa umekufa hakuna popote unapoenda, utakuta Isaac
Newton akimtambulisha Papa kama mpinga Kristo, sayansi za ubongo zinazosema
hakuna roho ya mtu iliyo nje ya ubongo, haya na mengine yote ni matokeo ya
kuanza kwa nuru mpya ya maarifa, ambapo yanakuja kwa namna nyingine ya injili,
ambayo unaweza iita sayansi.
Mapinduzi hayaishii hapa tu,
watawa kadhaa kama Martin Luther kati ya miaka ya 1517 wanaanza kugundua Biblia
ilivyo na Habari njema, ukweli ambao ulifichwa kwa karne nyingi sana.
Anatafsiri Biblia na kuchochea tafsiri ya Biblia kwa lugha kadha wa kadha na
kuzisambaza, haya yote yanachochea hisia za kugundua hata Mungu anataka Uhuru
wa watu.
Triki baada ya kufeli kwa
Lusifa
Lusifa mpaka hatua hii alikuwa
amefeli kwa hatua kubwa sana. Maana malengo yake yalikuwa dunia iishi katika
Dimbwi la Ujinga na upumbavu kama ilivyo asili yake kwa milele yote, lakini
hakujua kuwa ilikuwa ni ahadi ya Mungu kuwa Nyakati za mwisho maarifa yataongezeka.
Na Lusifa ilimgharimu sana kufikiria namna ambayo anaweza kushindana dhidi ya
jamii hii kubwa sana ya watu ambao mpaka wakati huu walikuwa hawawezi
kudanganyika.
Awali alifikiria kuwaua kama
alivyofanya kwa Galilei aliyeuwawa kwa kufungwa na Waroma, au alivyoelekea
kuwaua Wafuasi wengi sana wapinzani wake, au Waprostentanti, kuanzia wafuasi wa
John huss, john Wycliffe, martin luther, john Wesley, john calvin, n.k. lakini
marazote hubadili triki baada ya kuona kuwa hawezi kuikamilisha, na hapa ndipo
alipofikiria njia zifuatazo ili kuzitumia kutengeneza hoja ya ukinzani.
Kuchochea Ukandamizaji wa Rumi
mpaka mwisho makusudi
Unapoelekea karne ya kumi na
saba, ambapo hizi ndizo zama ambazo katika Biblia lilipita kanisa la Mungu la
Sardi. Kipindi hiki kilikuwa na ukandamizaji mkubwa sana wa kanisa la Roma
maeneo ya Ulaya. Watu wengi huwa hawajui kwanini zama hizi zilikuwa na
ukandamizaji uliovuka mipaka, kiufupi huu ukandamizaji ulikuwa ni makusudi, hii
ni kwa kuwa, ulikuwa umelenga ajenda zifuatazo.
Kwanza, Ulilenga kuumaliza
Uprostentanti ambao huo ndiyo ulikuwa adui mkubwa wa Lusifa ambaye alikuwa
hataki kabisa Yesu ahubiriwe tena. Maana uprostentanti ulikuwa na kichwa cha
‘’Haki kwa imani, inayotolewa bure kwa neema, itokayo kwa Yesu Kristo aliye ni
Bwana na Mwokozi wa Ulimwengu, yaani Mungu’’. Hivyo kutumia Nguvu mpaka mwisho
kulilenga zaidi Muda, yaani, Lusifa alishajua mapinduzi ya maarifa yanayoenda
kutokea yatakubaliana na Uprostentanti kama atachelewa au kuuachilia kukua
katika vichwa vya watu. Na hivyo basi, akatumia nguvu zote kabla ya wakati
mfupi ambao na katika Biblia ulishatabiriwa kuwa ni kipindi cha miaka 1260 tu,
au miezi 42 tu, au toka 538-1798 ambapo atapewa mamlaka juu ya watu wa Mungu
katika zama za giza.
Hivyo mateso makubwa, mauaji
makubwa ya waprostentanti, tena wakati mwingine kuyachanganya hata na mauaji ya
wachawi ‘’witch trials’’ kama ya salem, yote na hila zote zililenga tu
kuwamaliza wakristo wa kweli. hili lilikuwa lengo lake kubwa sana la wakati. Na
alifanikiwa kwa kiwango kikubwa sana, lakini hata hivyo bado hakumshinda Yesu,
hivyo Lusifa alikuwa na mbinu ya pili hapa.
Ilikuwa ni kuwakera sana
wanasayansi na watu wa maarifa wapya wa zama za nuru, kwa kuufanya Ukristo
kuonekana na dini ya ukandamizaji, ukatili, na inayoshikilia mafunzo yasiyo na
uhalisia. Na kwa mantiki hii, wasomi wengi sana ambao hawakuweza kujifunza Ukristo
wa kweli ambao waprostentanti waliokuwa wameubeba walikimbia, waliishia
kuchukia Imani ya kikristo, wengine wakiichanganya na falsafa mbalimbali za
kubuniwa, kumbuka Ulaya ilishakuwa na vyuo vingi kuanzia miaka ya 1100, na
kuendelea vyuo kama Oxford, Cambridge, n.k.
Kadri wasomi wengi walivyozidi
kuuchukia Ukristo, au Upapa, ndipo walipoanza Kujawa na tamaa ya kutamani Uhuru
wa kifikra, bila kubanwa na hisia zozote zile za kuambiwa kuabudu Mungu.
Mafanikio ya Lusifa
Katika kitabu cha Historia na
Kiini cha Magonjwa, na kitabu cha ‘’Ubongo wa mtu mweusi’’ nimeonyesha namna
jamii nyingi za ulaya zilivyoanza kuendelea sana, toka mwanzo wa shughuli za
kilimo, hata kiviwanda. Mafanikio makubwa yalitokana na dhiki ambazo zilitengenezwa
na jamii nyingi sana nyuma yao, na hata teknolojia nyingi zilikuwa sana
kutokana na mitindo yao ya Maisha, ambayo ilichochewa na shughuli zao za
kimaisha, na hata tabia zao za nchi za kijiografia. Hoja ni kuwa, Lusifa
alifanikiwa sana kuchochea Heshima kubwa sana kuhama toka kwa viongozi wa dini
ambao walikuwa wake, na aliwachafua, hata kuhamia kwa wanasayansi na
wanateknolojia wengi, ambao hajawatengeneza, ila amewatengenezea mazingira ya
wao kuwa upande wake bila wao kutaka.
Na hii ndiyo sababu utakuta
wasomi wakubwa wengi sana wa awali, wanaanza na Imani za kutoamini Mungu, huku
wakichochea sana hisia za kutaka Uhuru.
Wengi wao ilikuwa ni haki yao kutamani Uhuru. Na Uhuru ndiyo tatizo la kwanza
katika zama za mwisho za Lusifa kama kichwa cha sehemu hii kinavyosema.
Lengo la mwisho la makusudi
kabisa katika hatua hii ya kwanza, Upapa uliongeza Nguvu makusudi, ili
kuchochea Kukua kwa taifa la Marekani. Taifa la marekani lilijengwa kwa misingi
ya Uhuru wa kiuchumi na kidini. Taifa hili ambalo ndilo lilionekana kama tumaini
pekee la waprostentanti waliokuwa na matumaini hafifi sana kwa ulaya, lilianza
kuchochewa kwa safari nyingi sana za watafuta Uhuru kulielekea, lilipata Uhuru
zama hizihizi. Lusifa alikuwa amepanga mbinu kubwa sana kupitia taifa hili,
alipanga kupitia taifa hili awakusanye waprostentanti wote, kiwe ndicho kitovu
cha uprostentanti duniani, halafu katika ardhi mpya sasa, awamalize wote hatua
kwa hatua kupitia teknolojia na falsafa mpya ambazo, atazifanikisha kupitia
kikundi cha wafuasi wake anaoshirikiana nao katika uharibifu. Unaweza kusoma
pia Q4 kuelewa namna teknolojia na falsafa za ukana Mungu zilivyosambaa sana
katika nchi ya marekani hata kuathiri kabisa maadili, lakini hata hivyo lengo
kamili bado lusifa hajakamilisha, ila mpaka mwisho wa sura hii, tutaona
ameshakaribia kabisa kulikamilisha.
Hatua ya tano ‘’ 1798- karne ya 20
Ukinzani: Uhuru wa Kifikra,
hakuna Mungu
Hili ndilo lilikuwa lengo la
Lusifa katika kipindi hiki cha wakati. Alichotaka Lusifa ionekane hakuna Mungu,
na kuwa, Mungu gani angeweza kushughulika na wanadamu katika namna ya Hovyo
kama mamlaka za dini zilivyokuwa zinafanya kama huyo Mungu alikuwa na mamlaka
kubwa kabisa ya kimaarifa.
Lakini mafanikio makubwa sana
ya jamii za watu katika hali zao za uhuru bila Imani kwa Mungu, huku jamii za
wenye Imani ambazo zikitumika kama kielelezo cha Imani zikionekana dhaifu
kabisa, kulichochea wengi kudhihaki Imani za Mungu kama hali dhaifu kabisa za
kimaendeleo ya kiakili. Jamii kubwa za watu wanaoheshimika kama wanasayansi,
wanafalsafa, waandishi, matajiri, wafalme, n.k. wote wanasukumwa zaidi katika
ukana Mungu wakiwa na Nuru mpya ya wokovu toka kisima cha Ugandamizaji wa uhuru
wa kifikra na kimwili.
Kumbuka Ufalme wa Kipapa
ulipigwa chini kwa Nguvu kubwa sana ya mapinduzi ya ufaransa ya Napoleon,
aliyefanikiwa kumteka papa mpaka kufa miaka ya 1798. Zama hizi ziliambatana na
mapinduzi katika nchi nyingi sana, kama mapinduzi ya marekani, Serbia, spania,
filipino, n.k. dunia ilipitia zama za mabadiliko makubwa sana. Ufaransa
ilikuwa kitovu cha Uhuru wa kifikra toka kwa upapa, na hii ni kutokana na kuwa,
ndiyo iliyokuwa imempokea papa kwa nguvu kubwa zaidi.
Mapinduzi haya hayakuwa kweli
yakimaanisha kuwa ndiyo ulikuwa mwisho wa ukandamizaji, na falsafa za kipapa!!
La hasha, ilikuwa tu ni namna ambayo jamii ilibadilishwa toka katika mfumo
mmoja, Kwenda mfumo mwingine. Na ilikuwa ni namna ambayo mamlaka ya papa
ilipaswa kugharamia nguvu kubwa sana jambo ambalo lilihusisha migogoro
iliyopelekea hata kuuwawa kwa papa.
Kipindi hiki sasa Marekani
ikawa ikizidi kukua kiuchumi na kiteknolojia, hasa ikifyonza sana kutoka kwa
Ulaya. Marekani ilikuwa ni kiini cha demokrasia, au uhuru kwa dunia yote.
Marekani yenyewe inatambulika kabisa kuwa ilichochewa sana na taasisi nyingi
sana za siri ambazo zilikuwa zikihusiana moja kwa moja na mamlaka ya upapa.
Lakini bado sura na umbile la uhuru lilikuwa ni namna ya kucheza na muda na
nyakati ikivuta akili za wakimbizi wengi ambao walikuwa wamechoka.
Kumbuka sio kana kama Lusifa
hakuwa na shughuli kubwa sana na mataifa ya mashariki, na Afrika. La hasha,
Lusifa anajua siku zote ukimpiga Mchungaji, Kondoo lazima watatawanyika. Lusifa
aliwekeza sana kwa kila sehemu ambayo waprostentanti waliweka kambi, lusifa
asingepoteza muda na jamii kama za wahindu, au wabuddha, au wapagani, au hata
waarabu, ambao kwao hao wote, tayari misingi mikuu ya Ukristo ilishapotezwa.
Alihangaika sana Ulaya na marekani ambapo hata teknolojia nayo ilikuwa ndiyo
iko katika kilele. Kumbuka hata maendeleo makubwa sana ya kisasa ya teknolojia
ya viwanda, yalianzia Uingereza, kisha ulaya, na baadaye marekani. Inatambulika China kuwa na
teknolojia kubwa sana mpaka karne ya 14, lakini haikudumu kwa kuwa haikuwa na
falsafa za Kikristo, na uhuru, kama zilivyokuwa nchi za ulaya. Na hata migogoro
kama falme za Mongoli zinaaminika kuidhoofisha sana china kwa zama zake za
awali za maendeleo.
Miaka ya karne ya 19 inaanza
na kuisha na jamii kuanza kutumia mitaala ya elimu ambayo haimtambui Mungu.
Wanasayansi wakubwa kama Einstein wanaibuka kuelekea karne ya 20 wakiwa na
Mungu wao katika Imani ya kipagani ‘’Pantheism’’, ambapo ni sawa tu na kutoamini
Mungu. Falsafa za ujamaa na mapinduzi ya Urusi yanachochea zaidi ukana Mungu,
huku kuanzia miaka ya 1920’s na kuendelea shule zikianza kufundisha kutokuwepo
kwa Mungu. Nadharia kama za Charles Darwin za miaka ya 1859 zikianza
kufundishwa mashuleni, na nadharia nyingine nyingi ambazo unaweza kuzisoma
vizuri katika kitabu cha injili ya sayansi Q3, zote zinaonyesha dunia sasa
ikijawa na ukana Mungu, na Yesu akipotezwa kabisa kwa namna ya kisasa sana.
Lengo la Lusifa
Lusifa alitambua kuwa katika
mfululizo wa kinabii wa Biblia, wa kitabu cha Danieli, wa miaka 2300, na
makanisa saba ya kitabu cha ufunuo wa Yohana. Yote iliishia mwaka 1844, na
kufanya miaka baada ya wakati huu kuwa ndiyo wakati wa mwisho kabisa wa ulimwengu.
Na kwa mantiki hiyo, alijua kuwa ijapokuwa atawafanya watu wengi sana kuwa
Pamoja naye kwa mantiki ya ukana Mungu, au ukinzani dhidi ya uprostentanti wa
kweli, lakini hataweza kuzuia mpaka mwisho ukweli huu. Hivyo njia ambayo
aliitumia, ni kutumia hatua hii kujiandaa na hatua yake ya mwisho kabisa. Na
hapa anatumia njia zifuatazo:
Kukandamiza Mpaka mwisho
Ukristo
Lusifa kupitia sera zake za
Uhuru na Demokrasia, anawachochea watu kuamini wanaweza Kutenda lolote lile
bila mipaka ya maadili. Na huu ndiyo msingi wa kuanzishwa kwa chama kama cha
‘’Domecratic’’ cha Marekani, ambavyo hivi, huruhusu kila tendo na hisia ya
tendo la mtu, endapo tu, halimuathiri mwingine moja kwa moja. Kwa hawa matendo
kama ya Ushoga ‘’LGBTQ’’ sio changamoto, ukahaba, mapenzi kabla ya ndoa, lugha
za matusi, matumizi ya pombe, sanaa za uchafu, n.k.
Lengo la lusifa hapa lilikuwa
tu ni kuwaumiza wakristo wengi wa kweli, ambao hata wanapokuwa pia wakienda
katika taasisi za elimu, bado hudhalilishwa kuwa ni watu wenye uelewa mdogo
zaidi kifikra. Mafundisho ya kuwa hapo zamani binadamu alitokana na sokwe, au
ujiuji wa volcano, n.k. huchochea sana hisia za maumivu kwa wakristo wengi.
Lusifa amekuwa akifanya hivi makusudi akilenga hatua ifuatayo ambayo tutaiona.
Pia hatua hii ilihusisha
vikundi mbalimbali vya watu maarufu ambao wanaheshimika, na wana mafanikio sana
kwa nje, lakini wana ajenda nyingi za kuwafundisha watu kuwa hakuna Mungu.
Unaweza kuona hili kupitia wasomi wakubwa wa maarifa ya sayansi kama kina ‘’Neil
de grasse Tyson, carl sagan, lawrence krauss, brian cox, sam smith, Richard
Dawkins, michio kaku, Richard feynamn, ‘’n.k. pia wasanii wengi maarufu wa
miziki ya vizazi vipya huwa ni wenye makufuru sana, wakifanya machukizo mengi
sana kimaadili ya kikristo, kiufupi Lusifa aliye nyuma ya taasisi karibia zote
za burudani huwahi kuonyesha uchafu wake ili kutengeneza chuki kwa wakristo,
lakini haya yote ni malengo ya mchezo wake huu
wa akili.
Lusifa katika zama hizi pia
anafanikiwa kuanzisha Uhuru wa vikundi vingi sana ambavyo navyo
vinajitambulisha kwa sura ya ukristo, lakini havina hata nukta ya ukristo, au
wakati mwingine vikiwa vya ukristo lakini vina nukta nyingi sana za upagani.
Lengo la lusifa ni kupiga miluzi mingi ili kumpoteza mbwa, huku akiwa na lengo
la kuwakusanya wapiga miluzi wengi zaidi katika mwisho wa wakati.
Kufeli kwa Lusifa
Lusifa katika karne ya 19
miongoni mwa vitu alivyofeli sana ilikuwa ni ukoloni. Lengo lake la awali
lilikuwa ni kutawala dunia, huku akiuchafua zaidi ukristo kwa kuutumia kama
mbinu njema ya kuwafikia watu, na baadaye kubadilika na kuonyesha ukandamizaji
wa kikoloni. Lakini matokeo yake, ukoloni ulifungua nuru kubwa sana ya maarifa,
na Mungu aliutumia sana Ukoloni kuwafungua waafrika wengi kimaarifa ya
teknolojia, na Mungu wa kweli. huu ni miongoni mwa mfano ambao lusifa alifeli
kwa kiwango kikubwa sana, njia ambayo Lusifa alibakiwa nayo, ilikuwa ni namna
nyingine ambayo tutaiona, namna hiyo ndiyo huitumia zaidi kwa kuwateka waafrika
wengi kiakili kama alivyofanikiwa.
Hatua ya sita ya Lusifa na ya mwisho ‘’2015-2031±’’
Utii kwa Sheria ya Kikristo
‘’upapa’’ -New synthesis’
Lusifa anatambua huwezi
kutetea uhuru kuwa watu wanapaswa kufanya lolote katika mahakama ya haki na
maarifa, utaonekana tu ni mpumbavu. Na Lusifa anatambua kuwa kama ataendelea
kuruhusu uhuru huu wa watu kuamua kuwa mashoga, au kuwa wakristo wa kweli,
baada ya muda mfupi watakaobadilishwa wengi zaidi ni mashoga, kwa kuwa Maarifa
yana Nguvu kuliko upumbavu. Hivyo basi, namna pekee ambayo anaweza kufanikiwa
hapa, ni kutengeneza upande ambao utaonekana ukishikilia maadili, kama ilivyokuwa
kwa Upapa wa rumi ya awali, lakini sasa upande huu uwe kisiasa zaidi.
Na huu ndiyo mwanzo wa
kutengeneza vyama kama vya ‘’Republicans’’ vya marekani, ambavyo ni kopi ya
Republicans ya Rumi za zamani. Vyama hivi vina ajenda ya kufanya maamuzi ya
kimaarifa, yanayosimamiwa na watu wachache wanaoaminika na jamii, watu wenye
elimu na sifa njema, wenye kumjua na kumuamini Mungu, na watu hawa sasa ndiyo
husimamia moja kwa moja maamuzi wakiwakilisha nchi zao, kwa mujibu wa sheria,
na wakitumia mamlaka za nchi.
Mpaka mwaka 2024 unapoishia,
unaweza kuona uchaguzi wa marekani ambao unawakutanisha Donald Trump wa
Republicans na Kamala Harris wa Democrats, ukidhihirisha kabisa mtego wa
Lusifa. Kamala anasapotiwa sana na wasanii wengi ambao wanaonekana watu wa
hovyo, wasio na maadili, hawana heshima kwa Mungu, na hata chama chao ndicho
kinachoonekana kuhusiana sana na kutetea haki za mashoga. Lakini kwa upande wa
Trump unaweza kuona akisapotiwa na watu wengi wa maarifa na kuheshimiwa, kama
Ben carson, Elon musk, viongozi wengi na wakristo wengi sana, na hata Trump
mwenyewe baada ya Kupita anaonyesha moja kwa moja kutokubaliana na tabia za
Ushoga, hata kutoitambua jinsia ya ushoga. Watu wengi huishia kuhisi wenda
Trump ana ajenda za ukristo, lakini ufuatao ni mtego wa akili wa lusifa.
Kumbuka awali tuliona kuwa
jamii kubwa za watu zilichoshwa na mwongozo wa dunia isiyo na maadili, dunia
iliyojaa migogoro kama vita ya kwanza ya dunia, na ya pili. Mapinduzi yasiyo na
mwisho, mabomu ya nyuklia, milipuko ya magonjwa, kukosekana kwa amani,
kukithiri kwa ujambazi na wizi, kushamiri kwa mauaji ya Watoto na ndoa na mimba
za utotoni, na kila aina ya matatizo. Mfumo wa uhuru usio na maadili unaonyesha
kuwa na kero kubwa sana kiasi hata cha kuonyesha kuwa sababu kwa migogoro kwa
baadhi ya nchi kama za Russia, ambazo zinaonyesha zikipambana sana hata kuingia
katika vita ili kutetea maadili yao. Mabadiliko ya hali ya nchi na majanga ya
asili yanaonekana kuchochewa sana na dunia isiyo na kiongozi wa maadili, hasa
kutokana na watu kutupilia mbali ukristo, na kuukandamiza.
Haya na mengineyo mengi sana,
yanapelekea sasa jamii kubwa sana ya watu kuinuka na kukubaliana na ajenda za
kuuinua tena Ukristo juu, tena katika dunia ya kisasa zaidi. Na hapa ndipo
tulipofikia mpaka mwaka 2025, jamii za wakristo zinazidi kupata nguvu huku
zikizidi kuungana na kutengeneza umoja mmoja ambao una nguvu kutokana na
kupatiwa ulinzi na mamlaka toka katika mamlaka kubwa kabisa.
Kosa kubwa sana wanalofanya
watu wengi ni kusahau kuwa hii ni hatua ya mwisho ya mzunguko uleule ambao
tulikwisha kuuona mwanzoni.
Lengo la Lusifa
Kuunganisha jamii zote za
wakristo kwa mara nyingine tena. Na mara hii kiongozi wake akiwa tena papa kama
ilivyokuwa awali, lakini kwa mgongo wa kisiasa za marekani inayoungana na nchi
za ulaya, ambapo itaonekana kana kama nguvu za mamlaka ya upapa zinatokana na
maamuzi ya watu wenye busara ambao wanachochewa na wakristo wenyewe moja kwa
moja, na watu wenye mapenzi mema na sayari ya dunia, wanaotaka kuilinda dunia,
na kulinda tamaduni njema za kila jamii.
Ajenda ya mwisho ya Lusifa
Ajenda ya mwisho ya Lusifa ni
kuwaunganisha tena wakristo wote, na wanadini wengine wote ulimwenguni bila
kujali Imani zao na itikadi zao. Na kisha kuwashawishi kuwa inapasa jamii yote
ya wanadamu kulenga kuikoa dunia dhidi ya majanga ya asili, majanga ya
kimaadili, na majanga ya kiuchumi. Na hili litafanikiwa kupitia kuwa na siku
moja ya kuabudu ya Jumapili, ijapokuwa ni kana kama ni hoja nyepesi sana,
lakini Lusifa anatambua kuwa kwa kutumia siku ya jumapili ili kuilinda sayari
na kuabudu, tayari ameshabadilisha siku ya kweli ya kumwabudu Mungu, na
anacholenga ni kuwa, kwa siku sita Mungu aliumba, na hivyo basi, kama unaweza
kuamini Kuwa Mungu ni mwumbaji, basi
unapaswa kuabudu siku ya sabato, ambayo Biblia inaitamka kama ‘’Alama ya watu
wa Mungu’’ rejea Ezekieli 20:20.
Kwa kutoabudu siku ya sabato
ya kweli, maana yake aidha hawaabudu kabisa, au wanaabudu katika siku isiyo
sahihi. Haimaanishi kuwa wasioabudu sabato hawako katika macho ya Mungu, lakini
yapo maarifa ili kuwafundisha wabadili baada ya kujua, maana neema ya Mungu ipo
wazi kwa kila mwenye kuamini baada ya kujua, kutambua hili tayari ni neema, na
hata kabla ya kutambua Mungu alishatupenda ndiyo maana akatufundisha. Lakini
hoja hapa ni kuwa, Lusifa analenga ibada ya jumapili kwa wote duniani, siyo
wote waende kanisani, ila wote wapumzike au wafanya ibada zao.
Unaweza jiuliza kwanini
Jumapili? Awali nilisema Lusifa anaumwa ‘’OCD’’ akitamani sana ibada. Kwake
anatambua watu wanapoabudu sabato wanamwabudu Mungu. Na hivyo kwa kuwa
anatamani sana ibada, suluhisho kwake ni kutengeneza siku ambayo haitakuwa siku
ya Mungu ya ibada, na kila atakaye fanya ibada hiyo, ibada itaelekea kwake
yeye. Hii unaweza thibitisha kwa asili ya siku ya jumapili, ambayo ni siku ya
kwanza ya juma, ambayo zamani ilitumiwa na wapagani kuabudu Jua, na Lusifa kwa
kuwa hajabadilika, bado malengo yake ni yaleyale, ila amekuwa tu akibadilika
namna ya kuyafikia.
Akilini mwa Lusifa
Anachojua Lusifa na wafuasi
wake ni kuwa, kwa namna ambavyo sheria hii ya jumapili inaenda kupitishwa kama
ilivyoanza kujadiliwa katika bunge la marekani, watu wote itawapasa kukubaliana
na agizo hili jipya. Watu wengi huisi wenda kutakuwa na ukinzani mkubwa sana
toka jamii za wayahudi, na waislamu. Lakini wengi wao hawataamini, kwa kuwa
tayari kuna uhusiano mkubwa sana kati ya jamii hizi zote. Wayahudi wengi
waliopo palestina ni mithili ya Watoto wa marekani kwa wanaofahamu historia
wote, lakini pia wanahistoria wengi sana hutambua mkono mkubwa sana wa rumi juu
ya uislamu tangia awali kabisa miaka ya karne ya saba, ni mithili ya mbegu huru
lakini ina matunda yaliyopangiliwa awali sana, ukiondoa fundisho la Kristo siyo
Mungu, wala hakufa na kufufuka kama inavyoaminiwa na wakristo, sehemu kubwa
sana ya waislamu huwa hawapishani sana na wakristo, na hasa, pale wakristo
wanapofunika Biblia, na kuongezea vitabu vyao.
Jamii kama za buddha, hawa
hawana Mungu Muumbaji katika Imani zao, jamii kama za wahindu, hawa ni kama
wapagani wenyewe waanzilishi wa roma, tena kibaya zaidi, jamii kubwa sana ya
waprostentanti wamesharejea katika mafundisho na mitindo ya awali kabisa ya
Roma, ya kutopendelea kuisoma, au kuichunguza Biblia. Na hivyo basi, kwa
kiwango kikubwa sana cha dhiki ambapo jamii hizi zote za kimaadili zimezipitia
kwa hatua ya tano, zote zinaenda na zimeshaelekea kabisa kukubaliana katika
kila ajenda kutoka mamlaka ya juu, ambayo ni mjumuisho sasa wa pande zote.
Ukweli ni kuwa, ni papa ndiye mtawala hata katika hatua hii.
Lusifa anajua sasa anaenda
kuwa na kundi kubwa sana la watu waliochini yake, na anajua watu hawa wote
ambao watakubaliana na kuabudu Jumapili, watadharau sana hoja dhaifu kama ya
kuwa walipaswa kuabudu jumamosi kwa kuwa ni siku ya saba ambayo Mungu alipumzika.
Na watu hawa watadharau kwa kuwa, kwa kadri ambavyo wataangalia dhiki kubwa
walizotoka, na ukilinganisha na changamoto ndogo sana ya siku ambayo haina hata
mantiki, wengi wataona wapinzani wa umoja huu kama watu wenye misimamo
iliyokithiri, misimamo hatarishi ‘’extreme fundamentalism’’.
Kumbuka, ni kikundi cha watu
wasiozidi asilimia 0.3% tu ambao wanaamini na kuliishi neno la Mungu kama
lilivyoandikwa katika Biblia, yaani kwa zote 100%. Ukisoma katika Ufunuo wa
Yohana 12:17, unaweza kuwatambua watu hawa kama watu wazishikao amri za Mungu,
na kuwa na Ushuhuda wa Yesu, ambapo katika sura ya 19:10, ushuhuda wa Yesu
ndiyo Roho ya Unabii, ambayo huwasaidia watu hawa kuweza kumshinda Lusifa kwa
kuwa huwa uwezo mkubwa sana wa kuelewa mbinu zake.
Lusifa huwachukia sana, na
hata watu wengi wa duniani nao huwachukia watu hawa. hii ni kutokana na tabia
za watu hawa, za kujiona kana kama wapo sahihi sana. lakini hoja ni kuwa, watu
huangamia kwa kukosa maarifa. Baada ya jamii kubwa sana ya watu kuungana kwa
Pamoja, mamlaka zitakuwa na Nguvu sana katika kuwagandamiza watu hawa, kwa kuwa
jamii tayari itawaona kuwa ni kinyume nao. Na kumbuka, Dunia baada ya kuungana
itaonekana kana kama ipo katika nyakati za amani kabisa kuwahi kutokea, lakini
hapo ndipo mwisho utakuwa umefika, hii ni kuwa kuwa:
Majanga mengi sana
yatakayoanza kutokea tena, yataonekana ni kana kama ni matokeo ya laana
inayotokana na kikundi kile kidogo cha watu kukataa kuungana na wenzao, na
hivyo jamii kubwa itaaminishwa kuwaona watu hawa kama watesi wao. Sehemu kadha
wa kadha katika dunia wameanza kutumia adhabu ya kunyonga waasi kama namna bora
zaidi ya kupambana na waasi waliokithiri. Lakini ukweli ni kuwa, adhabu kali
zitaanza kutolewa na jamii za watu dhidi ya makosa makubwa yanayofanywa na watu
baadhi walio kinyume na sheria, na jamii.
Biblia katika kitabu ambacho
watu huwa hawakisomi kabisa cha ufunuo wa Yohana inaonyesha kuwa, kutaambatana
na majanga mengi sana ya asili ambayo yatakuwa ni mapigo saba ya Mungu,
hakitakuwa kipindi kirefu sana, maana kadri mapigo haya saba yatakapo kuwa
yakishuka, lengo halitakuwa kuwaadhibu watu, lengo litakuwa ni kuwa, kwa kuwa
mliungana mkisema dunia ina majanga mengi ya asili, ilihali majanga yenyewe
mliyatengeneza nyie wenyewe, na mkawatesa watu wa Mungu kuwa ndiyo chanzo cha
majanga hayo, sasa myapate mliyoyataka.
Dunia itakuwa ikipitia nyakati
hatari sana na hasira za watu wote zitawaelekea kikundi kile kidogo cha watu
wanayoitii kweli yote, jamii itasukumwa kuwamaliza kabisa, na jambo hilo
litachochea sana dhiki, kipindi hiki huitwa pia dhiki kuu. Na katika kipindi
hiki, watu wengi hata ambao hawakujua ukweli wa Mungu wote, watajifunza kwa
kasi sana, na wataelewa hata kujikuta na wao wakiingia tena katika dhiki hii.
zipo hatua kadha wa kadha katika zama hizi, lakini hatma yake ni kuanguka kwa
falme kubwa, na hata jamii kuunganishwa tena kuelekea kuwamaliza kabisa watu wa
Mungu, jambo ambalo litaishia kwa Ujio wa Moja kwa moja wa Yesu.
Lengo la kuandika sehemu hii
ni kuonyesha kuwa, ni mithili ya nadharia za kufikirika ‘’conspiracy theory’’
kuhusu ujio wa yesu, lakini nadharia za kweli za kufikirika ndizo zilizojaa
upande wa pili wa wasioamini, kama ujio wa Aliens, au wafu waliofufuka. Hoja ya
msingi ni kuwa, Lusifa yupo katika hatua
yake ya mwisho ambayo anatumia tena mbinu ileile kama ilivyofanyika awali.
HITIMISHO
Sehemu hii yote imelenga
kuonyesha mbinu kuu ya kwanza ya Lusifa ya kucheza na akili za watu, kwa
kutumia faida yake katika muda, na udhaifu wa wanadamu katika muda. Lakini pia,
kutumia triki yake ya Hegelian dielectric kucheza na akili za watu. Lusifa ametumia
mbinu hii mara ya kwanza akafanikiwa, na mara ya mwisho akiitumia mpaka hatua
ya mwisho kabisa aliyofikia, na nimeelezea hatua aliyoifikia, anapoelekea, na
itakavyokuwa. ili kila mmoja akutane na neema hii ya maarifa baada ya kusoma
sura hii.
Sehemu zinazofuata tunaenda
kuangalia mbinu nyingine kubwa sana za lusifa za kucheza na akili za watu, na
kuweza kuwa na mafanikio makubwa sana mpaka hatua hii ya wakati tuliyoifikia.
.jpg)
Join the conversation