Jipatie maarifa kutoka vitabu bora vilivyoandikwa na Dr Brighton shoo kuusu imani, sayansi, afya, teknolojia, asili, malezi, saikolojia na mazingira

LUSIFA DHIDI YA MACHO #1

MACHO NA LUSIFA

Utangulizi

Kama nilivyoeleza awali kabisa, watu wengi wanahisi ulimi ndicho kitu ambacho kinawaathiri zaidi, lakini ukweli ni kuwa Lusifa hutumia macho zaidi kuathiri na kuwateka watu. Lusifa hujua udhaifu wa macho, na ameiva katika taaluma ya kucheza na ubongo kupitia macho. Kiukweli macho ndiyo mlango mkuu wa kuufikia ubongo kama Biblia ilivyosema, na ajabu ni kuwa Macho yenyewe ni sehemu ya ubongo ‘’Diencephalon in origin’’. Na hata hutumia seli za kujikinga za ‘’Oligodendrocytes’’ kama tishu zingine za ubongo, na sio za sehemu zingine za mwili.

Kama ilivyosemwa na Biblia, hata katika Upasuaji kuuelekea Ubongo, Fuvu eneo la Macho ndiyo njia nyepesi zaidi ya kuufikia ubongo. Ubongo wa mbele unaotengeneza tafakari na maana za taarifa zote za ubongo kimantiki, huamini moja kwa moja taarifa zinazotoka katika macho, kama msemo unaosema, unapoona unaamini.

Kwa kuona unaweza kuridhika, kufurahia, kusisimka, kushiba, kukinai, kuumia, kutambua Ladha, na hata matendo magumu kabisa kuweza kueleweka kisayansi, kama kutabiri. Hii inaweza kukupatia msingi wa kutambua kuwa tabia za watu zinaelemea zaidi katika taswira wanazoziona, na wanazoziunda, maana Ubongo marazote hutenda kwa namna ya kutengeneza taswira, hata pale mtu anapokuwa amefumba macho.

Mzee Lusifa hutriki macho kama nilivyoelezea katika kitabu cha Q4 injili ya sayansi, kwa urahisi sana. Hii ni kwa kuwa msingi wa tabia yake ya Tamaa huwa rahisi sana kuuambukiza kwa watu kupitia macho. Hebu tafakari mfano, Vitu vikubwa viwili ambavyo vina msisimko mkubwa zaidi kwa asili ‘’greatest natural rewards’’, ni ‘’Mapenzi na Chakula’’. Ili mtu aweze kuwaka hisia za tamaa ya mapenzi, anapaswa kwanza kuona, ijapokuwa kwa Wanyama huwa kinyume, wao husisimka zaidi kwa Harufu, lakini sehemu ya ubongo inayohusiana na harufu ‘’olfactory lobe’’ haijaendelea sana kwa binadamu kama ilivyo kwa Wanyama. Lakini hata hivyo mifumo hii miwili hufanya kazi kwa kushirikiana sana, na yote huwa haihusishi sana tafakari baada ya taarifa, yaani, watu baada ya kuhisi harufu huwa hawafikirii sana na kuamua kusisimka au laa!! Kiufupi mfumo wa harufu ni sehemu moja kwa moja katika mfumo wa hisia wa ubongo ‘’limbic system’’, na ndivyo zilivyo nguvu pia za taarifa za macho, mwanaume anapoona sehemu za maungo ya uzazi wa binti katika mionekano ya kimivuto ya kimapenzi, husisimka moja kwa moja bila kupata nafasi ya kufikiria.

Lusifa na Jopo lake wamechochea kwa kiwango kikubwa sana kujazwa kwa taarifa zisizo za muhimu katika mitandao ya kijamii, zaidi ya taarifa zenye umuhimu. Lengo lake ni kuwafanya watu kuingia katika ulimwengu wa giza la kimaarifa. Katika Q4 tuliona namna ambavyo taarifa hizi huathiri uundwaji wa ubongo, kwa kupunguza kiwango cha seli za ubongo ‘’gray matter’’’, tukaona taarifa hizi zinavyoathiri uzalishwaji wa homoni za motisha ‘’dopamine’’, tukaona zinavyoathiri falsafa na mitazamo ya watazamaji kisaikolojia kwa kuwazoelesha taarifa zisizo na uhalisia.

Lusifa amefanikiwa kuwarudisha binadamu wa karne ya 21 Babeli katika mitandao hii, au ulimwengu wa kimitandao kwa ujumla. Watu wamekuwa ni wapweke kwa nje, watu wapo ndani maranyingi zaidi. Watu wana marafiki wasiowahi kukutana nao, watu wanawawaza zaidi watu wasiowajua kuliko walio majirani yao. Watu wanakesha kufurahia shughuli zisizofanywa katika jamii zao. Watu wanavutiwa na mionekano ya watu wasio wa jamii zao. Watu wanajifunza vitu visivyo na uhalisia wala umuhimu katika jamii zao. Watu wamekuwa si wa kuwajali wakwao kama Biblia ilivyotabiri, huku wengi wao wakiwa wabinafsi ‘’narcissistic’’, hasa kutokana na mitandao hii ya kijamii.

Kama Joka

Kama kuna jambo ambalo wenda madaktari wote, na wasomi wote wangepaswa kufundishwa walahu hata kwa kiwango kidogo sana, basi ni hili. Tangia mtoto anapoundwa akiwa tumboni, huwa anatumia mwanga kama chanzo kikuu cha taarifa kuhusiana na kila ratiba, na mwongozo wa matendo yote yanayofanyika hata katika kiini cha seli zake za uhai. Ni kweli ni ngumu sana kuweza kuelewa kiwango kidogo kabisa cha utendaji wa seli za uhai, maana hugharimu taaluma pana zaidi inayoitwa ‘’Quantum Biology’’. Lakini katika taaluma hii, ndipo huwezekana kuelewa kuwa, kiini cha maisha ambayo yanatokana na Nguvu za uhai ambazo huonekana toka katika chembechembe za nishati za seli, au ‘’Mitochondria’’, hutegemea zaidi Maji, na Mwanga.

Kumbuka, Huwa naishiwa Nguvu kabisa ninapoona Yesu naye alijiita, ‘’Maji ya Uzima, au Nuru ya Ulimwengu’’. Lakini ajabu sana, Mungu alipokuwa akiumba siku ya kwanza, yalioonekana zaidi ni Maji na Nuru aliyoiumba, au Mwanga kama nilivyoelezea katika Q3. Hiyo ndiyo misingi mikuu ya uhai ukiongezea na Usumaku ambao ndiyo Nguvu ya mawasiliano katika viwango vya Quantum Biology.

 BIOLOJIA YA MWANGA KWA UFUPI

Sasa basi, unapaswa kutambua walahu kidogo kuwa, mwanga wa jua unapoyafikia maji yaliyo ndani ya seli, kwa kufyonzwa kupitia chembechembe za melanin ambazo huwa kama mashine zinazounda kompyuta zinazoitwa ‘’semiconductors’’, maana mwanga wa jua mwekundu hupenya tabaka la Ngozi kwa 10cm mpaka 30cm, na hivyo huu mwanga sasa unapoingia katika chembechembe zile za Mitochondria, huyasisimua maji ambayo huwemo mule, kumbuka maji ndani ya Mitochondria huundwa mulemule, kwa kupitia chembechembe inayoitwa ‘’Cytochrome C oxidase’’, hii huusiana na utendaji kazi wa mashine ya nishati ya Mitochondria, au ‘’enzyme ATPase’’, maji yanapokuwa yakimulikwa na mwanga ambao hautoki kwa jua, ila unatengenezwa moja kwa moja ndani ya seli kupitia chembechembe za melanin, hubadilika maumbo mbalimbali na kutengeneza maumbile ambayo huchochea tofauti za uchaji ‘’polarities’’, hizi tofauti huchochea tabia tofauti tofauti za usumaku ambao ndiyo msingi wa uendeshaji wa mitambo ya ufanyaji kazi wa seli. Seli huitaji sana maji, na ndiyo maana sababu ya vifo vyote ni upungufu wa maji ‘’dehydration’’. Utendaji wa seli huitaji sana chembechembe kuu tatu, yaani, Hydrogen Proton, Electron, na Oxygen.

LUSIFA NA BIOLOJIA YA MWANGA

Lusifa kwa kuchochea mwanga wa Taa za Kisasa ‘’Blue lights’’  wakati ambao watu walipaswa kulala, amefanikiwa sana kuharibu kizazi cha binadamu. Lusifa kwa kuwafanya watu wasilale usiku, wakikesha kwenye masinema, wakichati, wakiwa katika starehe, n.k. amewaharibia kabisa binadamu mfumo wao wa kalenda ya Biolojia ya mwili ‘’circadian rhythm’’, binadamu hukaa kwenye mimba kwa miezi tisa, huzaliwa na kuota meno kwa wakati maalumu, huanza kutembea na kuzungumza kwa wakati maalumu, huanza kupevuka katika wakati maalumu, na nyakati hizi zote hufanana kwa jamii yote ya binadamu kwa wastani. Hii ni kwa kuwa binadamu wote huwa na aina moja ya maelekezo ya kifiziolojia na jenetikia. Kama mtu angekuuliza mwili unajuaje kalenda hizi? Mfano, Ubongo wa binadamu hukomaa kabisa miaka kuanzia 25, je ubongo unawezaje Kwenda na kalenda hizi za nyakati kwa ufanisi mkubwa kiasi hiki. Basi jibu pekee ni kuwa, mwili wa kiumbe yeyote ule hufuata kalenda ya mwanga unaotoka kwenye jua. Na hii ndiyo sababu uharibifu wa kalenda hii unapelekea Watoto wanaanza kupevuka kabla ya wakati.

Mitochondria hizi katika seli ili zifanye kazi ya kuunda maji ambayo ndiyo yanaongoza utendaji wake huitaji mionzi ya mwanga wa jua tu ‘’visible light spectrum’’. Na sio mionzi mingine yeyote ile kama ya simu na vifaa vya kisasa ambavyo watu hushinda navyo. Lusifa na Jopo lake alihakikisha kuwa anachochea watu kutumia screen za LED za Blue, na ndiyo maana watu wengi huwa hawajui kwanini Taa za awali za Mwanga mwekundu zilipotezwa. Baadhi huisi wenda shida ilikuwa ni matumizi yake makubwa ya nishati, lakini La hasha! Lusifa alishagundua ili aweze kutawala akili za binadamu, hoja ya kutumia Nyaya au Vipandikizwa katika Ubongo itakuwa ni ngumu sana, lakini kwa kutumia mfumo huu ‘’Wireless’’ unaotumia tu Mwanga wa Blue, au mwanga wa taa hizi za kisasa, atafanikiwa sana. Na amefanikiwa sana kwa kuwa, kila watu wanapotumia taa hizi za kisasa, hupelekea mageti yanayoitwa ‘’UCP’’ katika ubongo Kufunguka, na mageti haya yanapofunguka, hupelekea kupotea kwa kiwango kikubwa sana cha electrons. Kwanza kumbuka, mwanga wa asili unapomulikia mwili wa kiumbe, huchochea mwili kuzalisha electrons kwa kuzisisimua melanin.

Sasa basi, watu hawa wanapokesha na mianga isiyo ya asili, au wanapoamka nayo asubuhi kwa kuzisoma emails, au meseji katika simu zao, au mfano katika mazingira yenye kiwango kikubwa cha chembechembe za Fluorides, kumbuka Fluorides huvuta sana electrons ‘’more electronegative than oxygen’’, mitochondria hushindwa kuunda maji, na hupunguza hata uhitaji wake wa Hydrogen toka katika mzunguko wa TCA cycle, mitochondria sasa huingia katika mzunguko mwingine unaoitwa ‘’serine oxidation glycine cleavage system’ ilikutatua tatizo hili,  lakini mwishowe Mitochondria hujawa na kiwango cha Deuterium, ambazo hizi huwa ni kama mbadala wa hydrogen nyepesi ambazo zimekosekana kutokana na kukosekana kwa electron. Na hizi zinapokuwepo katika mitochondria hupelekea ishindwe kufanya kazi vizuri, DNA huwa nzito isiyojifungua kirahisi, seli huitaji mwanga mwingi na huwa wazi sana ‘’switch ON’’, huu ndiyo mwanzo wa magonjwa yote.

Kukosekana kwa mwanga wa asili mwekundu katika Ubongo, kutokana na watu kuchelewa kuamka, na kukesha wakiwa na masimu au makompyuta, au kwenye taasisi zinazofanya kazi usiku zikiwa na matumizi ya taa za mianga hii ya kawaida, au blue. Huathiri mfumo wa ubongo unaoongoza matendo makubwa sana ya mwili, unaoitwa ‘’leptin-melanocortical pathway’’, huu ni mfumo ambao ungeambatana na hisia za kutulia kwa hamu za kula kwa kuzalishwa kwa homoni ya kuridhika kwa hamu za kula inayoitwa ‘’leptin’’. Lakini pia huu mfumo huongoza uzalishaji wa homoni ya ‘’Melatonin’’ ambayo huusiana na afya ya ubongo, huchuja sumu chafu katika ubongo, maana ni ‘’antioxidant’’, pia melatonin inapozalishwa huchochea Kimiminika kinachoitwa ‘’CSF’’ kusafisha Ubongo, maana hii homoni huchochea hisia za kulala, melatonin pia huchochea tezi za Ubongo kama ‘’Pituitary’’ kuzalisha homoni za ukuaji, na homoni za uzazi kama ‘’Testosterone, au kuchochea uzalishaji wa homoni kama Luteinizing hormone, n.k.’’  mwanga wa jua wa asili huchochea afya ya mfumo wa ubongo toka katika macho unaoitwa ‘’Retinal-cortical pathway’’, na watu wanaokesha sana na vifaa hivi vya usasa hujikuta wakiwa na shida za macho ‘’Myopia’’, ambapo hutokana na miale hii mikali ya mwanga, hupelekea tabaka la ndani la jicho ‘’retina’’ kujiachia toka katika ukuta wa jicho ‘’macular degeneration’’, na matokeo yake ni taswira kuundwa kwa mbele ya retina, na watu hujikuta wakiwa na shida za kuona ‘’Near sightedness’’.

popote pale mwanga wa Blue unapogonga katika tabaka la jicho hasa wakati wa usiku, huchochea mfumo wa Ubongo unaoitwa ‘’Sympathetic nervous system’’ ambao huu huchochea Stress, na huzalisha ‘’Stress hormone’’ au ‘’Cortisol’’, hii huenda katika tishu zote za mwili, na huvunjavunja mafuta, sukari, na hata protini, na hii ndiyo sababu ya mionekano ya kuzeeka kwa watumiaji wengi, hii ni kwa kuwa tabaka la Collagen linaloshikilia zaidi Ngozi nalo huathiriwa. Pia cortisol huathiri uzalishwaji wa melanin ‘’melanogenesis’’, na hivo kuathiri biolojia yote ya utendaji tuliouzungumzia.

Vijana wengi huishiwa Nguvu za Kiume kutokana na shida za mianga hii inapofika katika sehemu ya ubongo inayoitwa ‘’Hypothalamus’’, na kuifanya itanuke. Kumbuka kila kitu kitu kinapoelekea kuangamia hutanuka, iwe ulimwengu ‘’Universe expansion’’, iwe Nguo inayoisha, liwe Jicho, uwe Ubongo, hata mwili. Hii ni kwa kuwa, Seli inahitaji nishati kubwa sana kuendelea kushikilia umbile lake, na inapoishiwa Nguvu, hujiachia na kutanuka inapoelekea kufa. Sasa basi, kushinda na mianga hii, huathiri Ubongo ‘’hypothalamus’’ na kupelekea shida katika tezi ya Pituitary, na kisha tezi za uzazi ‘’Gonads’’, ambapo matokeo yake ni kuzalishwa hafifu kwa homoni hizi.  Kiwango kikubwa cha stress za Cortisol huathiri uotaji wa nywele kwa vijana wengi kama tafiti kadhaa zinavyoonyesha.

Mafanikio ya Lusifa

Watu washaingia katika kumi na nane za kutumia taa hizi za kisasa, kuamka na simu zao wakiangalia ‘’Updates’’, kuchati kwa masimu haya, n.k. na kadri watu wanavyokuwa watumiaji wa bidhaa hizi, ndivyo wanavyokuwa waraibu zaidi. Hii ni kwa kuwa mianga hii au ‘’blue lights’’ huchochea ‘’dopamine, na hata adrenaline’’, na hii ndiyo sababu kila viwanda vya teknolojia hutumia mianga hii katika bidhaa zao. Hii ni kwa kuwa zinamatokeo makubwa kiuchumi au kibiashara. Mafanikio makubwa zaidi hata hivyo ya lusifa ni kuwa, bado watu wachache sana ambao wameweza kugundua siri na sayansi hii ya uharibifu. Hii ni kwa kuwa, taaluma hii haipatikani katika mitaala ya kielimu kirahisi.