LUSIFA DHIDI YA KILIMO #8
SAYANSI YA KUBADILISHA DUNIA KWA KUPITIA KILIMO
‘’Modern Agricultural Modifications’’
Nimeeleza sana katika kitabu cha Q8, Historia na Kiini Cha Magonjwa, historia nzima ya kilimo, na hatimaye changamoto kubwa sana zilizoikabili dunia kutokana na kilimo. Katika sehemu hii nitaeleza ufupi tu wa namna Lusifa anatambua kiini cha kazi zote za mwanadamu, zinahusiana na uhusiano wake na asili, hasa mimea, ambacho ndicho chakula chake. Na Lusifa hataki kabisa uhusiano wa mwanadamu na mimea, na anajua kwa kuangamiza mimea, mwanadamu hataweza kuwa salama tena.
Kama Nyoka
Kutokana na mabadiliko ya hali ya nchi,
kutokana na kilimo kilichoshamiri cha aina moja tu ya mazao ‘’monoculture’’,
kutokana na kukata sana miti na kufyeka mapori ilikuandaa mashamba makubwa,
kutokana na kufuga Wanyama wengi jambo litakalo wajaza maelfu ya Wanyama katika
eneo moja tofauti na mbugani, kutokana na kuwa na watu wengi katika eneo dogo
wasiofanya kazi za kujitafutia chakula, haya na mengineyo yalipelekea ardhi ya
dunia kuishiwa kabisa rutuba.
Mpaka dunia inapomaliza vita ya pili ya
dunia, maeneo mengi ambayo yalikuwa na watu wengi, au miji mikubwa, ardhi zake
hazikuwa zikisapoti kabisa kilimo. Na uharibifu huu ulianzia zamani sana maeneo
ya Asia, na Ulaya, ambako walianza na kilimo, na kisha kusambaa na Amerika, na
Afrika, hasa kipindi cha Ukoloni. Ambako tamaa kubwa ilikuwa ni kugombania
maeneo yaliyokuwa bado yana Rutuba nzuri.
Tatizo la kuishiwa Rutuba halikuwa na dawa
bora yenye mashiko zaidi ya dawa za kuichochea ‘’boost’’ ardhi walahu kuweza
kujimudu kivirutubisho walahu kusaidia mimea ikue. Hivyo matumizi ya mbolea
yalikuwa ni mapinduzi makubwa sana, toka kwa wanasayansi wa awali sana kama
‘’Harber process’’ ambayo Mr. Harber aligundua namna ya kutengeneza mbolea za
kwanza kabisa. Mbolea nyingi huwa ni madini ya Nitrogen, Phosphorus, na
Potassium. Hii ni kwa kuwa, mimea hutumia sana madini haya kutengeneza
chembechembe za seli zake za kutengenezea chakula zinazoitwa
‘’Chrolophyll’’, na hizi huipa mimea
rangi ya ukijani, zinapopungua mimea huonekana ya njano. lakini pia mimea
huitaji madini ya ‘’Phosphorus kwa ajili ya kutengeneza sana chembechembe zake
za Nyuklia, kama DNA. pia huitajika sana phosphorus katika kutengeneza
chembechembe za nishati kama ATP, n.k. zinapopungua hizi, mmea hujawa na
chembechembe zinazoitwa ‘’anthocyanins’’ ambazo hizo ndo huufanya mmea kuwa na
rangi ya damu ya mzee, au ‘’pink’’. mmea pia huitaji sana madini ya Potassium
kwa kazi za kuongoza kufunga na kufunguka kwa stomata, mawasiliano ya seli,
n.k. kiufupi, madini haya huitajika sana katika mmea, na upungufu wake huwa
haraka sana katika udongo, pale mimea inapooteshwa mingi sana.
Hoja kubwa ni kuwa, wakulima walipokuwa
wakilima sana, mashamba makubwa sana, tena mazao ya chakula ambayo hufyonza
madini mengi sana toka kwenye ardhi, ili kutengeneza chakula chake, baada ya
muda ardhi hizi ziliishiwa kabisa madini. Na huku kulipelekea sasa mazao
yasikue tena. Magugu tu ndo hukua, hii ni kwa kuwa huwa hayatunzi sana chakula
yenyewe, na hivyo hata katika ardhi yenye madini kidogo yenyewe hustawi, pia
magugu huwa na protini ngumu kama ‘’lignin’’, ambazo vimelea hushindwa
kuzimeng’enya, na hivyo hubakia ikikua tu.
Ugunduzi wa mbolea za kisasa ambazo
zenyewe zinaongeza madini kwenye ardhi moja kwa moja ilikuwa ni faida sana kwa
wakulima wote. Sasa wangeweza kulipia deni la upungufu wa madini yale makuu
matatu ‘’N-P-K’’, lakini pia wakaongeza na madini mengine mengi, kwa urahisi
sana.
Upande wa pili ulimaji wa mashamba makubwa
hupelekea kufyekwa sana kwa mapori, huku hupelekea wadudu wadogo wengi sana
kukosa kabisa chakula kutoka mimea midogo. Na hivyo wanapoona mashamba ya
wakulima, basi wote hujazana katika mimea hii mizuri, na hapo wakulima huteseka
sana kwa uharibifu mwingine mpya wa wadudu. pia vimelea wengi wa ardhi
hutegemea sana mabaki yaliyooza ya mimea na kuila, huku wakiibadilisha kuwa
udongo. sasa ardhi huwa na misimu mirefu ya ukame mpaka msimu wa kilimo, ikiwa
na mabaki machache sana. Na hivyo maelfu ya vimelea hawa hufa, na balansi ya
madini kama mzunguko wa Nitrogeni kupitia bakteria kama ‘’Pseudomonas,
Thiobacillus denitrificans, Nitrobacter, nirtomonas, etc’’ hushindikana kabisa.
Hawa hubadilisha ammonia kuwa chumvichumvi za nitrite, kuwa nitrate, au nitrogen
kwa ajili ya mimea. Hawa bakteria wengi hufa. na baadhi ya vimelea kama
bakteria kadhaa na fangasi huwa hatari sasa hata kwa mimea, kwa kuwa huitaji
kula hata mimea, na hivyo kuitengenezea magonjwa mengi sana shambulizi.
Ugunduzi wa dawa za kuulia wadudu na
vimelea katika kilimo, ulileta Faraja kubwa sana. Kwa kuwa sasa wakulima
wanaweza kutatua matatizo yao kiurahisi sana. Na ndivyo dunia nzima ilivyoingia
katika namna bora kabisa za kilimo.
Lakini ukweli ni kuwa, Pamoja na kuwa
mimea inakua, lakini bado ukuaji wake ni dhaifu. Hii ni kwa kuwa, kuna wastani
wa madini kidogo sana katika ardhi, lakini pia mimea haiwezi kuzalisha mazao
makubwa kutokana na mabadiliko ya chemistry hizi za udongo na hali za mvua. Pia
hata kutokana na athari katika mifumo ya homoni ya ukuaji wa mimea.
Habari njema tena kwa wakulima ikaja kwa
ugunduzi wa namna za kuboresha moja kwa moja biolojia za mimea, ili kuweza
kumudu mazingira haya magumu ya ardhi. Hapo ndipo kulikuwa na namna mbili, ya
kwanza ilikuwa ni uboreshaji wa mifumo ya homoni za mimea, mfano, ‘’Plant
growth regulators’’, kama vile boosters, n.k. hizi zimelenga zaidi kusaidia
ukuaji kwa kubalansi homoni za ukuaji kama vile ‘’Auxin, Abscisic acid,
Gibberellins, ethylene n.k.’’ lakini
wakulima waligundua njia hii Bado haina ufanisi sana.
Namna ya pili waligundua mabadiliko ya
kijenetikia moja kwa moja ya mimea, mfano, waligundua taaluma ya kuchanganya
jamii mbalimbali za mimea, kwa kuchagua ile inayoweza kukabiliana na hali za
ukame, au upungufu wa madini Fulani. mimea ya namna hii huwa na mafanikio
makubwa sana, hii inaitwa ‘’selective breeding’’, maana yake, kama mmea
ungehitaji kutumia miezi minne kukomaa, na hali za mvua zimebadilika zimekuwa
miezi isiyozidi mitatu. Basi ukichagua mbegu zinazokuwa haraka ndani ya miezi
miwili tu, basi utafanikiwa sana. Lakini pia, kama mmea unatumia madini mengi
sana mpaka kukomaa, basi ukiupata ambao unatumia madini kidogo tu, utakukomboa.
Hii ni kama tu ilivyo katika kuku wa kisasa wa Broiler, unaoweza wala ndani ya
week 4 hadi 6 tu. kwa wakulima wengi utasikia kauli kama ‘’Mbegu fupi’’ au
mbegu zinazostahimili ukame, n.k. hii nayo ni taarifa njema sana kwa wakulima,
na hata kwa wafugaji, ambao nao ni sehemu ya wakulima.
Kuhusu Mifugo
Kuhusu mifugo msingi ni uleule, Wanyama
hawana kinga imara sana tena. kutokana na mazingira magumu ya ufugaji, upungufu
wa virutubisho toka katika ardhi, selective breeding ambayo hushusha kinga za
Wanyama kama tulivyoona katika Q8, lakini Wanyama wanafugwa kibiashara hivyo
hawawezi kuishi maisha yao ya asili, na upungufu wa kinga utakaozaliwa
suluhisho ni madawa. na pili ni kutumia Wanyama watakaokomaa mapema sana ili kuvunwa
kibiashara.
Kama Joka
Lusifa baada ya kuwaingiza katika furushi lake wakazi wote wa dunia, furushi la mifumo yao mama ya chakula, yaani Kilimo. Sasa anajua hawataweza pambana na changamoto zifuatazo.
Kwanza kitendo cha kilimo cha mashamba
makubwa kilimaliza madini katika ardhi, halafu matumizi ya mbolea za kisasa
ziliharibu balansi ya madini moja kwa moja katika ardhi. Hii ni kwa kuwa ardhi
inahitaji balansi kubwa sana ya madini, unapojaza madini ya N-P-K unafanya
ardhi Kujawa na chembechembe za uasidi kama ‘’nitrates’’ ambazo kadri mvua
inaponyeshea, ndivyo zinavyoingia mpaka katika vyanzo vya maji. Madini kama ya
Phosphorus yanafahamika kwa asili yake ya kuunda chembechembe za uasidi
‘’phosphoric acids’’, potassium zinafahamika kwa kuathiri balansi za madini
mengi ya calcium katika complexes ambazo huundwa katika udongo, au huungana na
nitrates na kuchochea kujaa kwa hydrogen ambazo huchochea uasidi wa udongo.
chemistry ya udongo huathirika moja kwa
moja kwa matumizi ya mbolea. Maji ambayo yalipaswa kuwa safi sasa hujazwa na
aidha kemikali hizi toka mashambani, au toka mvua zenye makemikali ya asidi.
Vyanzo vya maji hupoteza viumbe wengi sana ambao wanapokufa huzalisha sumu,
mfano, tatizo la ‘’Algae blooms’’, ambao huzalisha sumu kama ‘’Mycystins,
brevicystins, n.k.’’ hizi huua Samaki wengi, na magonjwa mengi ya vyanzo vya
maji hutokana na madawa ya wakulima.
Wakulima hutumia sana kemikali kama
‘’Roundup’’, ambazo huwa na chembechembe zinazoitwa ‘’Glyphosate’’, hizi huua
mimea mingi sana, kwa kuzuia uundwaji wa chembechembe za protini ‘’amino
acids’’ kupitia chaneli inayoitwa ‘’shikimate pathways’’, na sasa basi, hii
chaneli hutumika pia na kwa bakteria. Na kwa hivyo, hizi dawa huleta matokeo
hasi sio tu kwa mimea, bali hata kwa vimelea, na hivyo kuua kabisa balansi ya
mimea. Kibaya zaidi, hizi dawa huwa na matokeo hata zinapoingia katika mwili wa
mtu, pale mtu anapokula chakula chenye mabaki ya madawa haya, humuathiri moja
kwa moja mfumo wake wa homoni. Na hii imekuwa hata na kwa madawa mengine kama
2,4-D, atrazine, na zingine nyingi, ambazo
zote maranyingi zaidi zimeonekana kufanania zaidi chembechembe za estrogens, na
kupelekea shida za uzazi, kwa wanaume kupungukiwa nguvu za kiume, kuzalisha
seli za uzazi zilizoharibika, na vivyo hivyo kwa wanawake kuwa na shida kama
viuvimbe kwenye mayai ‘’polycystic ovarian syndrome’’.
Matumizi ya mbegu fupi au za kustahimili
hali ngumu ni kama matumizi ya vimalizia madini yaliyobakia kidogo katika
ardhi. Yaani, ni kama baada ya kuula mnofu, sasa ukaacha sehemu zilizobakia kwa
mafisi. Wakulima wengi na wasomi wengi hawalelewi umuhimu wa mzunguko wa
nishati, sheria kuu ya sayansi inasema ‘’nishati huwezi iunda, au poteza,
unaweza tu ibadilisha’’. Unapotoa madini katika ardhi, jua hakuna namna ya
kuyarudisha pale bila kurejelea katika asili ya mzunguko wa awali wa ardhi ile,
ambayo mpaka sasa hivi Lusifa ameshaubadilisha.
Hii inamaanisha kuwa, uzalishaji wa vyakula duniani unazidi kudorora. Na hata vyakula vinavyopatikana, vinazidi kuwa vilivyo dhaifu. Na uwezo wa kutatua matatizo haya, unazidi kudhoofika. Lusifa anatambua sasa hivi anaenda kuwafanya wote wakazi wa dunia kusujudia tena mamlaka yake kwa ajili ya kupata vyakula. Na hili analifanikisha kwa kuwa, kadri siku zinavyozidi kusonga, wakulima wadogo wanazidi kushindwa kumudu mashamba yao kutokana na ugumu wa kilimo na hasara za hatari za mabadiliko ya hali ya hewa, wakulima wachache sana wanaomudu hili, na hawa wengi wao ni matajiri wakubwa. Hawa hulima lakini huwa hawajali mzunguko wa vyakula kusambaza chakula, wao hujali tu kupata faida kubwa. Na kitendo cha watu wengi kukimbilia mijini, na kuondoka vijijini, kunawafanya wengi zaidi kutegemea mfumo mdogo kwa lengo la kujipatia vyakula, hili tayari linawaandaa kuwa watumwa, na wanyang’anyi ndani ya muda mfupi sana uliombeleni kama Biblia ilivyotabiri.



Join the conversation