Jipatie maarifa kutoka vitabu bora vilivyoandikwa na Dr Brighton shoo kuusu imani, sayansi, afya, teknolojia, asili, malezi, saikolojia na mazingira

HISTORIA NA KIINI CHA MAGONJWA YOTE


SURA YA SABA

MAGONJWA YA MADAWA

Historia ya matibabu

Heshima na shukurani kubwa sana huwa zikienda kwa mtaalamu, Edward Jenner. Kwa kuokoa mamilioni ya Maisha ya watu. Kwa kugundua Chanjo ya kwanza kabisa ‘’vaccine’’. Neno vaccine likitokana na neno ‘’Vacca’’, linalomaanisha Ng’ombe. Hata kabla taaluma ya chanjo, ilishakuwepo katika falme za china, india, na Ottoman. Hawa waligundua unaweza jikinga na virusi vya smallpox kwa kugusana, au kukutana na mabaki ya vitu vilivyoambukizwa na virusi hivyo vya smallpox. Taaluma hii ililetwa maeneo ya Uingereza, Ulaya. Miaka ya 1800’s na Mwanamama Maria Wortley Montagu.

Mwaka 1796 Edwerd Jenner Daktari mwingereza, aligundua wakamuaji wa maziwa ambao walikuwa wakipata homa ya mafua ya Ng’ombe ‘’cowpox’’, walikuwa hawawezi kupata ugonjwa wa virusi vya smallpox. Na mwaka huohuo akamwekea mtoto mdogo wa miaka 8 aliyeitwa ‘’James Phipps’’ vitu vyenye vimelea vya mafua ya ng’ombe ‘’cowpox’’,mtoto alionesha dalili za kuumwa, lakini baadaye kidogo alipona. Baadaye Daktari Edwerd akamwekea virusi vya smallpox, na Mtoto kweli hakuumwa kabisa. Na hapo ndipo akaipa jina hii mbinu Chanjo, au ‘’Vaccination’’.

Kilichofanyika mwaka 1828 na bwana Johann Buchner kuitoa kemikali ya ‘’salicin’’, toka mti unaoitwa ‘’Willow’’, au Mkemia ‘’Felix Hoffmann’’ mwaka 1897, yeye aliitoa kabisa chembechembe ‘’Acetylsalicyclic acid’’ (ASA), toka kwenye mti huuhuu. Ndicho kilichokuwa kikifanywa kwa milenia nyingi sana na waganga wengi sana, kuanzia misri, sumeritan, mpaka na Hippocrates. Hawa wote walitambua kuwa magamba ya huu mti yana uwezo wa kuondoa maumivu, homa, na uvimbe. Hivyo mwaka 1897 kilichofanyika tu, ni kuchukua kiini chake cha ASA, na kukiuza kama Aspirin.

Mti wa aspirin

Miaka ya 1800’s, walifanya ugunduzi mwingi sana wa kuchukua viini vya dawa ambazo zilikuwa zikitumika kwa miaka mingi sana. Mojawapo pia, ni Maua ya Poppies. Ambayo yalitumika sana kutulizia maumivu kwa miaka mingi sana. Tena miaka milenia nyingi tangia zamani. Waganga wazamani walichanganya tangawizi, na maua kadha wa kadha kama ya chamomile, kupunguza shida za uvimbe, na nyingine mbalimbali.

Friedrich serturner alichukua maua ya poppies, na kuchukua kiini chake ambacho ndicho huitwa ‘’opium’’, miaka 28 mbele, mwaka 1832, mwenzake Pierre Robiquet wa ufaransa, akagundua na Codeine. Hizi zote ni dawa zinazotumika mpaka leo mahospitalini kupunguza maumivu. Karne hii hii wakagundua mpaka na Paracetamol. Dawa za kutuliza maumivu zilizochelewa kugunduliwa ni za steroids tu, ‘’Cortisone’’. Ambazo ziligunduliwa miaka ya 1949. Kumbuka miaka ya 1800 ndiyo iliyokuwa na mapinduzi makubwa sana ya sayansi, na teknolojia, hivyo wazungu wengi wa maeneo ya ulaya walitumia faida ya masomo, na taaluma nyingi sana ambazo zilikwisha sambaa ulaya yote. Ikihusiana na za afya, hasa toka kwa waislamu wengi wa zamani, ambao nao walizikusanya sana toka miji ya neo-medopersians, ambayo ilijumuisha taaluma zote toka kwa maeneo yote ambayo yalikwisha ambukizwa elimu za kigiriki, zilizohusisha elimu za afya. waislamu wanakumbukwa kwa kuandika awali kabisa machapisho makubwa, na kuyakusanya kwenye maktaba zao za awali kabisa kama za Baghdad, na kuzisambaza baadae ulaya yote enzi za kukua kwa dola yao.

Kushoto ni Poppies wenye ‘’opium’’, na kulia ni chamomile.


.........,...............(nunua kitabu kupata picha kamili)...................


Mwaka 1895 mpaka mwaka 1930 ndiyo miaka ambayo ilihusika na ugunduzi wa mionzi katika tasnia ya udaktari. Wilhelm conrad Rontgen, mwanafizikia wa kijerumani, ndiye hupewa heshima kwa ugunduzi wa mionzi ya X-Rays, miaka ya 1895. Na ugunduzi wake ulichochea tasnia ya matibabu, mwaka 1900, ikaibuka namna yake nyingine inayoitwa ‘’Fluoroscopy’’, ambapo bado mionzi ya x-rays ilichochea maendeleo zaidi, na mwaka 1970’s ikagundulika CT-Scan, ambayo ni namna ya kisasa zaidi ya kupata taswira ya 3D ya viungo. Miaka 1950’s iligundulika Ultrasound, ambayo hutumika kutazama taswira za viungo hasa vya tumboni.

Miaka kumi nyuma yake iligundulika namna ya kutazama miili kwa kutumia chembechembe za Nyuklia, au ‘’Nuclear medicine’’. Miaka ya 1980’s  ikagundulika MRI mtambo ulioniwezesha hata mimi kuweza kuuelewa sana Ubongo, katika masomo ya fiziolojia ya ubongo kwa kutazama maumbile yake ‘’neuroanatomy’’. Japokuwa tuzo hakupatiwa mgunduzi wa kweli, Daktari, na engineer, Damadian Raymond, na sababu iliyojificha ni kwasababu ni ‘’Mkristo wa dhati sana’’.jambo ambalo linaonekana kwa wengine kama, linaitia doa sayansi.

Mwaka 1928 umeandikwa katika historia ya ulimwengu kwa kazi kubwa sana ya mwanabiolojia ‘’Alexander fleming’’, kwa ugunduzi wake wa dawa ya kwanza kabisa ya kuua bakteria ‘’Penicillin’’, au ‘’first antibiotic’’. Lakini hata hivyo miaka 1500 kabla hata ya Yesu, tayari ilisharekodiwa kuwa Wamisri walishakuwa wakitumia mikate iliyochacha na asali kutibu vidonda. Bado walitumia mimea mingi na mabaki, kama yenye vitunguu saumu, n.k. fleming aligundua fangasi ‘’penicillium notatum’’ aliua bakteria ‘’Staphylococcus notatum’’, na akarekodi ripoti yake mwaka 1929. Lakini kina Florey na wenzake ndiyo waliochochea uzalishaji wa chembechembe za ‘’penicillin’’ hasa kipindi cha Vita ya Pili ya Dunia, miaka ya 1940’s. baada ya hapo miaka ya kuanzia 1940-50, ilishamiri kwa utafiti wa dawa zaidi, waligundua streptomycin, tetracycline, erythromycin, na chloramphenicol.

Miaka mingi sana kabla ya Yesu, Misri walikuwa wakitibu saratani, au Cancer, kwa kuichoma ‘’cauterization’’. Hata Hippocrates, miaka 400 kabla ya Yesu, naye aliripoti namna hii. namna bora zaidi na ya kwanza ya matibabu ya saratani, ilikuwa kupitia upasuaji ‘’surgery’’ kuiondoa. Jambo ambalo liliwezekana kwa kuwa, miaka ya 1846, walishagundua dawa za kwanza kabisa za nusu kaputi, ambazo tulishaziona, kama ‘’opiates’’, miaka ya 1860’s, pia waligundua namna bora kabisa za kusafisha vifaa, na vidonda, ‘’antiseptic techniques’’, visishambuliwe na vimelea. Hivyo ikawezekana kwa urahisi sana hata kwa wataalamu wa upasuaji wa kwanza kabisa kama ‘’Willium Halsted’’, kuondoa saratani ya Titi kwa mafanikio. Miaka ya 1895 ilipozaliwa mionzi kama tulivyokwisha ona, ikawezekana zaidi kuua saratani.

Miaka ya 1940’s walianza matibabu ya saratani kwa njia ya homoni kutokana na taaluma ya matibabu ilishakuwa kubwa sana. Miaka ya 2000 wakaanza kutumia matibabu yaliyolenga zaidi seli za saratani moja kwa moja. Na mpaka 2010’s wakawa wakitumia mbinu za kuusaidia mfumo wa kinga moja kwa  moja kuua seli za saratani ‘’immunotherapy’’. Pia zipo mbinu za kijenetikia ‘’gene therapy’’, zinazolenga kuua moja kwa moja jenetikia za saratani ‘’genes of neoplasms’’.

Kuanzia miaka ya 1980’s mpaka leo unaweza kusema matibabu yamebadilika na kuwa ya kisasa zaidi. Yakihusisha taaluma pana sana za kijenetikia, zinazowezeshwa sana na teknolojia za akili za kisasa ‘’artificial intelligence’’. Katika Q4 nimeelezea teknolojia kama za CRISPR Cas 9 Technology, namna zinavyoweza kumuathiri mtu. Watu wengi hawajui matibabu toka historia mpaka sasa, yanaonesha kabisa kufika kikomo. Lakini cha ajabu magonjwa ndiyo kama yanaanza.

MSINGI WA SAYANSI ZA MADAWA YOTE

Madawa yote yanayotumika duniani, huwa na sheria, na sababu zake kuu. Matumizi ya madawa yalianza kutumika awali kabisa katika historia ya mwanadamu. Kilichokuwa kikibadilika, ni urahisishaji wa namna ya kuitumia dawa, kwa kuiboresha zaidi kadri teknolojia inavyozidi kuongezeka.

Asilimia kubwa kabisa ya madawa, tangia awali kabisa. Ni kemikali zinazotoka kwa mimea, na viumbe wengine. Jamii mbalimbali zimekuwa kwa milenia nyingi, zikitumia sana mimea yake kadhaa, kwasababu za kimatibabu. Kabla ya wakoloni kufika maeneo mengi ya Afrika, tayari watu walikuwa na namna zao za kitabibu. Ambazo ndizo zilizowafanya wakaweza kuishi kwa maelfu ya miaka katika bara lao. Na ndivyo ilivyo hivyo hivyo kwa kila eneo.

Magonjwa

Msingi wa dawa yoyote ile, ni kuweza kuchangamana na chembechembe zingine, au sehemu zingine za mwili, kama Funguo inavyoweza kufungua Kufuri. Hii kitaalamu inaitwa ‘’Key and Lock mechanism’’. Dawa ni chembechembe ambazo zinaweza Kwenda aidha kwa tishu za mwili wa mgonjwa, au tishu za kimelea, au sumu yenye madhara, na kisha kuibadilisha utendaji wake ili isilete madhara, au kuuongezea mwili uwezo wa kujikinga.

Magonjwa marazote huusisha athari katika mfumo wa fiziolojia ya mwili. Mfano, magonjwa yanaweza kupelekea mwili kusisimka zaidi ya kawaida, wenda kutokana na sumu kadhaa za vimelea, au kitu chochote kile. Na mwili unaweza kusisimka kwa kuongeza sana Joto lake kupita joto la wastani linalohitajika, na hivyo kujikuta ukiathirika kabisa hata ukiua protini zake wenyewe. Magonjwa yanaweza kupelekea kuharibika kwa mtiririko wa utendaji sahihi wa fiziolojia ya mwili, na kupelekea baadhi ya homoni zisizalishwe. Homoni ambazo zingesaidia kuongoza hisia za hamu ya kula, msukumo wa presha ya damu, n.k.

Magonjwa huusisha vimelea ambavyo huwa vikizaliana sana katika mishipa ya damu, vimelea kama ‘’plasmodium’’ huwa wakila damu moja kwa moja, huivunja ‘’hemoglobin’’, kuna vimelea ambao huwa wakishambulia kuta za Mishipa ya damu, maini, tishu za ubongo, kuta za utumbo, mpaka katika misuli. Hawa wote husababisha madhara kwa kuzaliana katika tishu hizi, na kuathiri utendaji wa hizi tishu. Kwa kuzalisha uchafu wao, kuzalisha sumu zao, kuzuia damu katika hizi tishu, vimelea wengine kama virusi huathiri mpaka DNA za seli za wagonjwa, kwa Kwenda kuzaliana moja kwa moja katika nyuklia za seli.

Kuna magonjwa ya sumu ambayo huusisha madhara katika matendo ya metaboliki ya mwili moja kwa moja. Mfano, sumu baadhi hung’ang’ania chembechembe za mwili, au huzuia au kufungua chaneli baadhi za matendo ya kibiolojia, hata kuathiri mwili. Zipo sumu baadhi ambazo huchochea sana utendaji wa mifumo ya seli kuliko kawaida. Lakini zipo ambazo hupooza kupita kawaida. Matendo haya katika mishipa ya fahamu huweza kupelekea kiumbe kuparalaizi ‘’paralyze’’, kukakamaa ‘’tetany’’. kuna zingine huzuia damu kuganda. kuna ambazo hupoteza balansi ya madini na chembechembe kama ‘’enzymes’’, na kupelekea madhara ya mifumo mbalimbali yasiyotabirika. Na kuna sumu na vimelea ambao huathiri sana mifumo ya kinga, na kupeleka madhara kutoka kwa vimelea ambao hawakuwa hatari mwanzoni.

Mwili huwa na uhusiano wa hisabati ya jumla ya matendo yote unayoyatenda. Hii huitwa ‘’coordination’’. Kitendo cha matendo, au seli baadhi kuathiriwa na vimelea, au sumu. huwa hakiwezi kuleta madhara moja kwa moja. Hii ni kwa kuwa mwili huwa una namna ya kubalansi changamoto za maeneo baadhi, kwa kuyafidia. Lakini inapofikia hatua ambayo changamoto zimekuwa nyingi kiasi kwamba madhara ya seli, au matendo kadhaa, hayawezi kubalansiwa ‘’compensated’’, basi matendo yale huanza kuonesha udhaifu moja kwa moja kwa nje. Mfano, kama mfumo wa damu umeathiriwa sana, basi mnyama ataanza kuonyesha upungufu wa damu ‘’anemia’’, kama ni mfumo wa nishati, basi utaona ‘’mnyama hana nguvu, au kakonda’’, kama ni kuongezeka kwa asidi au ‘’respiratory or metabolic acidosis’’, basi utaona mnyama akiwa na mapigo ya juu sana ya moyo, akitapika, n.k. kama ni upungufu wa madini ya ‘’Calcium’’, basi mnyama atachanganyikiwa, misuli itaisha nguvu, n.k.

Mara zote ugonjwa unaoonekana kwa nje, ni matokeo ya upungufu wa mifumo ya mwili ambayo ilipasa kufanya matendo Fulani. na yanapofeli, basi yanapelekea udhaifu.

Yapo magonjwa pia ambayo hayatokani na vimelea, wala sumu. Bali hutokana na mwili wenyewe. Haya huwa ni matatizo ya kuzaliwa, kama ulemavu. Na mengi huwa na changamoto zinazohusiana na mifumo ya kijenetikia. Magonjwa ya muundo huu wakati kadhaa pia huchochewa sana na matokeo ya sumu, ambazo awali ziliathiri utendaji wa biolojia ya uumbaji wa mtoto alipokuwa tumboni ‘’embryology’. Wakati mwingine huwa ni mionzi, lishe mbaya, n.k. mfano mzuri ni matokeo ya mionzi ya madini mazito ‘’heavy metals radiation’’, huwa na madhara sana katika seli kadhaa, kuliko zingine.

Na hii huwa hivi, ndani ya seli kuna chembechembe zinazoitwa ‘’DNA’’, hizi chembechembe ni ndogondogo sana, na zinahusisha madini madogo madogo sana. Haya madini ni rahisi sana kusisimuliwa na kiwango cha nishati kama za mionzi. Hivyo mama mwenyeujauzito anapokuwa katika maeneo haya. kwa kuwa mtoto wake anaundwa tumboni. na seli zinafanya kazi ‘’Mitosis’’, (seli zinaji ‘’double’’, mara 36 ili kumuunda mtoto kutoka kwenye sperm na ovary tumboni, wakati huji double mara tano tu akishazaliwa). Tumboni huwa ni kwa spidi kubwa sana. hivyo DNA zinakuwa zikiwa kazini sana ‘’more active’’. kwa kuwa karibu na mionzi, basi mionzi huenda kwenye zile DNA za mtoto, na kuzisisimua chembechembe zake, na kupoteza mtiririko wa utendaji wake. Na madhara yake ni kuzaliwa kwa mtoto mwenye makosa katika uundwaji wa baadhi ya viungo vyake, hizi huitwa ‘’malformations’’, au ‘’teratogenic effects’’. Kuna nyakati husababishwa pia na sumu, ambazo nazo huenda kuathiri hatua zilezile za kijenetikia.

Magonjwa baadhi huleta madhara kutokana na msisimko mkubwa zaidi wa mwili, kuliko hata uhalisia wa vimelea, au sumu. Mfano mzuri ni asthma. Mwili husisimka na kuminya mishipa yake, aidha ya hewa, kama asthma, au ya damu. Na matokeo yake mwili huongeza spidi kubwa sana ya damu, hata kupelekea presha, ‘’Hypertension’’, wakati mwingine mirija ya mapafu ‘’bronchioles’’, huweza kujiminya ‘’constrict’’, hata kushindwa kuvuta hewa, na mtu kuathirika kwa kupungukiwa oksijeni. Wakati mwingine mwili husisimka na kupelekea Ngozi kusisimka kwa kiwango kikubwa sana kwa uvimbe. Mwili hupelekea uvimbe ‘’inflammation’’, kama namna ya kujilinda na vimelea, au hatari. Na kumbe unajiathiri wenyewe.

Kuna uhusiano wa moja kwa moja, wa magonjwa na utambuzi, au akili ya mtu. Saikolojia ni hali ya juu ya kifiziolojia, ijapokuwa watu bado hawaielewi saikolojia kiundani, maana wengi wanaosoma saikolojia, huwa hawaijui fiziolojia. Akili ni sehemu ya kwanza ya kinga ya mwili, kwa kukuonesha kile ni hatari kinaweza kukuathiri. Na ndiyo sehemu ya mwisho ya kinga ya mwili, kwa kukuambia utapona tu wala usijali. Wataalamu hutambua, hisia za kuamini kupona, huwafanya watu hata wasiotumia dawa sahihi, kupona. Hii huitwa ‘’Placebo effect’’. Husomwa katika matawi ya sayansi yanayoitwa ‘’Psychoneuroimmunology’’. Hoja ni kuwa, watu huonesha hisia wanapoumwa, kuelezea kiwango cha ugonjwa wao ulipofikia, bila wao kujitambua.

ASILI YA MADAWA

wengi sana hushangaa maajabu ya madawa. Lakini kibaya zaidi ni kuwa, wameshindwa kunufaika nazo. Dawa nyingi sana tunazozitumia, zimetokana na mimea. Ipo mimea ya madawa ambayo ina dawa katika magamba yake, hasa miti. Kuna maua. Kuna mizizi. kuna poda na majivu.

Kwanini mimea baadhi ina madawa?

Kwanini mti wa pillow unatuwezesha kwa dawa ya ‘’aspirin’’, au maua ‘’poppies’’ ya ‘’opium’’, yanatuwezesha kupata dawa za nusu kaputi ‘’anaesthesia’’ au kutuliza maumivu, mimea kama ya vitunguu saumu ‘’garlic acids’’ inaua bakteria, mbegu za maboga zinaua minyoo ‘’anti-helmintics’’, matunda ya Kigalia Africana yanazuia tishu kuharibika ‘’antioxidative’’ na kuua vimelea kama bakteria’’, aloe vera inasaidia kupambana na virusi, vimelea, inazuia tishu kukakamaa ‘’antioxidative effects’’. muarobaini, mti wa Quinine, vitunguu saumu, mdalasini, majani ya mpera, n.k.

Sababu pekee ambayo inafahamika ni kuwa, vita ambayo marazote amekuwa akiipigana binadamu, amekuwa akipambana Pamoja na mimea. Mimea inapitia changamoto marazote mwanadamu anapopitia changamoto. mfumo wa kwanza wa kinga ambao ndiyo akili ya viumbe. Huwa na namna pana zaidi ya kujikinga, na hapo ndipo inapohusiana na kila kiumbe ambacho kipo nae sambamba katika kujiokoa.

Mimea kama Pillow ambayo inaota sana maeneo ya baridi, ‘’temperate areas’’, kama ukanda wa ‘’mediterranean’’, huwa inaota sana kando na vyanzo vya maji. Ambapo huwa kuna maji, na madini mengi toka katika ardhi. Lakini kando ya vyanzo vya maji huwa na wadudu, na vimelea wengi sana. Kama bakteria, minyoo wadogo, protista, virusi, na fangasi. Hawa vimelea japo si wote, lakini huwa wanaathiri sana mimea iliyopo karibu. Na mimea mingi sana hufa. Lakini mimea ambayo huwa kando ya vyanzo vya maji huwa na sifa nyingi sana za kitabibu. Hii ni kwa kuwa, hutengenza chembechembe za kinga ‘’bioactive molecules’’. ambazo hujua kuwa kama vimelea wataishambulia hii mimea, basi itawaua. Na kwa namna hiyo mimea itabaki salama.

Na mimea mingi iliyopo katika maeneo mbali na kingo za maji, hushindwa kutengeneza hizi kemikali. Hii ni kwa kuwa, huwa na virutubisho na maji machache, ya kuweza kuwa na nishati ya kuweza kutengeneza mpaka na chembechembe za kujilinda. Na mimea hii inapotengeneza chembechembe hizi, basi kiumbe yeyote atakayetumia, naye anaweza kufaidishwa na utabibu wake. Hivi ndivyo ilivyo pia kwa maua kama ya ‘’poppies’’, nayo huzalisha chembechembe za ‘’opium’’, kwa lengo la kuwazubaza Wanyama watakaotaka kuimaliza yote, kwa kuila. Na kwa kufanya hivyo, mimea itabaki salama.

Misitu ya Congo

Hii misitu ina asilimia 50-70% ya aina zote za mimea iliyopo katika dunia nzima. Na ndiyo misitu ambayo ina aina mbalimbali zaidi za mimea yenye nguvu za kiutabibu ‘’therapeutic properties’’. Mimea mingi katika misitu hii huwa na misimu mirefu sana ya mvua, na huwa pia na viwango vikubwa sana vya viumbe mbalimbali, na hata vimelea mbalimbali vinavyoizunguka. Mimea hutengeneza kemikali zake za kujilinda dhidi ya kila namna ya uuaji unaouelekea. Dawa kama za Quinine zimetokana na miti ya misitu hii ‘’miti ya Cinchona’’, dawa za Curare ‘’zinazolegeza misuli’’, hutoka katika misitu hii, dawa za ‘’Reserpine’’ hizi hutibu shida ya presha kubwa ‘’hypertension’’, nazo hutoka katika mimea ya hii misitu. Zipo dawa nyingi sana.

Jangwani, Ukame, na milimani

Mimea ya maeneo ya jangwani, na hata milimani pia huwa na sifa kadhaa za utabibu. Hii ni kwa kuwa, mimea hii huwa katika maeneo ambayo huwa na hali zisizo tabirika za hali za hewa, huwa zinapambana na vipindi virefu sana vya ukame. Na mimea huzalisha aina mbalimbali za kemikali, za kuisaidia kupambana na hizi hali. Maeneo ya milimani pia huwa na oksijeni chache, na stress huwa ni kubwa sana. Hivyo mimea huunda kemikali za kupingana na hizi hali.

Mfano, Aloe vera ambayo husaidia sana kupona kwa vidonda, na afya ya Ngozi Imejaa ‘’antioxidant’. kama ambavyo mazingira yake huuhitaji kuwa na sifa ya ‘’anti-oxidation’’. kuna mti wa Yew, huu huwa na sifa ya kupambana na seli za saratani ‘’cancer cells’’, ambapo ili uziathiri hizi seli, unabidi kuzizuia zisiwe na hali za asidi, na ziwe na hali za oksijen, jambo ambalo mimea hii hufanikiwa. Kuna mimea ya ‘’Ephedra’’, hii hutanua njia za mapafu ‘’bronchodilators’’, nayo hutoka katika hali hizi.

SIRI YA TEKNOLOJIA ZOTE ZA MADAWA NA MADAWA YA KISASA

Kila dawa inayotumika popote pale, kama sio vitamini, au madini, au chembechembe zozote zile za vyakula kama sukari, au protini, au mafuta, au homoni, Basi ni Sumu. Dawa zote ni sumu ambazo zinaua seli za viumbe. Na teknolojia kubwa kabisa ya utabibu wa sasa, imejikita katika kutafuta namna za ndani kabisa za kuua vimelea, kwa kuwasoma namna ambavyo wao kwa wao wanauana. Mpaka sasa hivi teknolojia ya CRISPR-Cas 9 ambayo ndiyo ya kisasa zaidi katika utabibu, inahusisha kuiga namna Virusi wanavyowaua bakteria, na kuiga namna hiyo kama itawezekana kuua seli za Cancer, kwa binadamu.

Mara zote dawa ni sumu lakini hutumika kwa sababu kadhaa. Kwanza, ni

kiwango.

Binadamu ni mabilioni ya seli, lakini vimelea wengi wana seli chache sana. Hivyo kwa kutumia kiwango cha kawaida sana cha uuaji wa seli, vimelea wengi hufa. huku binadamu akibakia salama. kwasababu, yeye bado anaseli nyingi sana, ukitoa chache zilizokufa. Na hata zikiathirika, bado zinaweza kujitengeneza tena upya atakapopona.

Hii ndiyo sababu watu wanaweza kutumia dawa za mbu katika majumba yao. Dawa za mbu huwa mara nyingi na viwango vidogo vya ‘’cypermethrins’’, sumu ambazo ni hatari hata kwa watu. Lakini ukubwa wa binadamu, sumu zile huwa hazina madhara, huku udogo wa mbu, ukimfanya kuangamia haraka. Na ukipima madhara ya binadamu kuzuliwa na dawa ya mbu, na madhara ya binadamu kupata Malaria. Basi chaguo sahihi ni kwa kutumia tu dawa za mbu. Wataalamu wanatambua madhara ya matumizi ya viwango vidogo vya sumu kwa muda mrefu sana. Na ndiyo maana hushauri watu wasafishe mazingira yao, ili mbu wasizaliane. Kwa kuwa kwa kutumia kila siku madawa, kiwango kidogo kidogo huzidi kukaribia hatua hatari zaidi ya sumu.

Unapofanya matibabu ya seli za saratani kwa kutumia mionzi ‘’radiotherapy’’, au kwa kutumia kemikali sumu ‘’chemotherapy’’. Matibabu haya yote huua seli nyingi sana za saratani, lakini huua pia na za mwili. Na ndiyo maana watumiaji wa madawa ya saratani, nywele zao huisha kwa haraka sana. Hii ni kumaanisha, dawa zao huathiri seli zote za mwili zinazojizalisha haraka haraka ‘’fast multiplying cells’’, na miongoni ni seli zinazoongoza uotaji wa nywele, na hata seli za uzazi. Lakini kwanini bado tunatumia matibabu haya? Ni kwa kuwa kiwango cha seli nzuri tunazozipoteza, ni ndogo sana ukilinganisha na seli zinazobakia hai. Na seli mbaya tunazoziua, ni nyingi sana ukilinganisha na seli mbaya zinazobakia hai.

Kwa kuupunguzia mwili seli hatarishi, wenyewe humalizia kazi ya kujiponyesha, Kwa kuua seli hatari chache zilizobakia, na kuzizalisha sana seli nzuri zilizopotea, kulipia deni ya seli hai zilizokufa.

 

Utofauti

Dawa nyingi huegemea katika utofauti kadhaa uliopo baina ya viumbe. Kuna baadhi ya chembechembe, chaneli, sifa, na hata viwango vya fiziolojia, huwa tofauti kwa kila kiumbe. Kwa mantiki hii, unaweza kuzuia chaneli Fulani iliyopo kwa bakteria, ukijua kabisa kuwa chaneli hiyo haipo kwa binadamu. Na kwa mantiki hiyo, unaweza kumuua bakteria, bila kumuua binadamu. Kwa kuwa, sumu imekuwa kwa bakteria, ila sio kwa binadamu, au mnyama.

Sumu nyingi ambazo hutumika kuua mimea, kama ‘’Glyphosate’’, ambazo huwepo kwenye ‘’Roundup’’, hulenga kuathiri chaneli ya mimea inayoitwa ‘’shikimate pathway’’, ambayo huusika na uzalishaji wa protini za muhimu sana, zinazotengenezwa na mimea tu ‘’essential amino acids’’. Na cheneli hii haipo kwa Wanyama, na hivyo kwa kupulizia katika mimea, tunategemea madhara yasiwepo kwa Wanyama. Bakteria wanayo hii chaneli, na hivyo tunategemea watayapata haya madhara.

Huchelewesha Kifo

Pamoja na yote, dawa huusaidia sana mwili. Mtu mwenye presha iliyopanda sana. Matibabu kwa ‘’statins’’ kwa wakati mchache sana, humpatia ahueni, na mwili wake huweza kujiweka vizuri ili kutoruhusu tena tatizo lifikie hatua ya hatari sana. Madawa mengi huupa mwili muda zaidi wa kujipanga.

Hebu tazama hili. Mtu mzima ukimpatia sumu ambayo huchochea moyo wake kudunda kupita kiasi, basi utamuua. Lakini mtu huyu atakapokuwa anaelekea kufa kwa moyo wake kudunda kidogo kidogo sana, ukimpatia sumu hii ya kuongeza mapigo ya moyo. Basi atakuwa salama. Hii ni kwa kuwa, umerudisha mapigo yake ya moyo kwa wastani, ijapokuwa umetumia sumu. Lakini umemuongezea wakati zaidi wa kuishi, na sasa, anaweza kutafuta namna bora za kujizuia kufika katika hatua hiyo.

SIRI ILIYOJIFICHA

Madawa na teknolojia zote za matibabu. Ni neema za Mungu. Mungu wetu alitupatia neema za kuongeza wakati wa kuishi pale tunapoelekea kikomo kabisa cha Maisha yetu, ili tuzitafakari njia zetu. Hata Mungu alipomwambia Adamu, hakika utakufa. Bado hakufa ghafla, alimpatia neema. Unapokuwa unaumwa unaelekea kufa, madawa hukusaidia kupingana na kifo kwa wakati Fulani, huwa ni alarm ya kuwa kuna jambo kubwa zaidi linaweza kutokea.

Unapotumia dawa, maana yake mwili wako ulishashindwa kuishi, ulikuwa unaenda kufa. Mtu anayetumia zaidi dawa, maana yake alitakiwa awe alishakufa, na kifo kinamfatilia sana. Mwili ni hisabati ya maelfu ya matendo ya kibiolojia. Lakini dawa huenda kurekebisha sehemu za muhimu sana ambazo zingeweza kupelekea kifo kwa ghafla sana. Na kwa hivyo, huwezi kuishi kwa kutegemea madawa. Kwa kuwa madawa ni moja ya elfu katika kuwezesha Maisha. dawa ni kama usukani wa gari, husaidia kuzuia hata gari bovu lisitumbukie mtoni. Lakini haziwezi kulifanya likawa zima.

Jambo pekee ambalo watu walipaswa kulitambua ni kuwa, mpaka mtu anapoumwa. Mwili wake wote umepoteza mahesabu. Na mahesabu ya mwili yote yanategemea madini, na virutubisho. Ambavyo watu huvipata kupitia vyakula vyenye afya, na mazingira yasiyo hatarishi. Hivyo kama dawa itatumika kumaanisha kemikali ya Maisha, basi kemikali ya Maisha yenye matokeo Chanya zaidi, ni vyakula bora. Magonjwa yamezidi kuwa na nguvu kwa kuwa hata vyakula ambavyo watu wanavitumia, navyo ni sumu, kama madawa wanayotumia.

 

CHANZO CHA KUFELI KWA MADAWA YOTE

Madawa yamekuwa yakifeli sana katika utabibu wake, kwa sababu kubwa mbili. Kwanza, Vimelea vina maarifa kuliko dawa. Na pili, sumu ni hatari kuliko vimelea.

VIMELEA VINA MAARIFA KULIKO DAWA

Huwezi kuua aina fulani ya vimelea kwa mafanikio makubwa sana, na kisha hiyo mbinu ikaendelea kuwa na mafanikio kila siku. Vimelea huwa na tabia ya kubadilika, kulingana na mazingira. Kwanini vimelea huwa na maarifa kuliko dawa, ni kwa kuwa vimelea hubadilika, kipindi madawa huwa hayawezi badilika.

Kadri unavyotumia zaidi madawa, ndivyo kadri vimelea vinavyobadilika zaidi. Vimelea havina kikomo cha kubadilika. Lakini dawa zina ukomo wa kubadilika. Inahitaji wataalamu walio na upendo wa dhati kwa jamii, na akili nyingi sana, kutengeneza aina tofauti ya kitabibu ya dawa. Itakayo kuwa na sumu kidogo kwa mwili, na mpya kiuuaji kwa vimelea. Jambo ambalo mpaka sasa hivi tulivyofikia, limezidi kuwa gumu kama ilivyo ngumu kuwatokomeza vimelea.

Namna Kuu Nane za utendaji wa Madawa

Dawa zote huwa na namna kama nane kuu zaidi za kuwaua vimelea, ambazo huwa zikilenga

1.Ukuta wa seli wa nje wa Bakteria ‘’Cell wall synthesis’’

Hizi dawa hulenga kuzuia ‘’cell wall’’ za bakteria zisiundwe. Hii ni kwa kuwa, bakteria hutegemea sana ukuta wao wa nje wa seli ‘’cell wall’’, kwa ajili ya shughuli zao. Bakteria huwa na chembechembe zinazoitwa ‘’Peptidoglycan’’, wakati fangasi huwa na ‘’chitin’’. dawa kama Penicillins, Ceftriazone ‘’power safe’’, Vancomycin, n.k. hulenga kuua hizi chembechembe za ukuta, mfano penicilins na cephalosporins, huua Beta-Lactams zilizo kwenye ukuta wa bakteria, na kuwaua. Dawa za fangasi kama Echinocandins huua ukuta wa fangasi, na kuwaua.

2.Ukuta wa seli wa ndani ‘’Cell membrane’’

Ukuta wa ndani huwawezesha sana bakteria na fangasi, kuweza kuchangamana na mazingira yao, katika ukuaji na shughuli zao. Kwa fangasi mfano huwa wana chembechembe zinazoitwa ‘’ergosterol’’, ambayo huwasaidia sana. Na dawa huua hizi sehemu. Mfano, dawa kama ‘’Polymyxins’’ huua ‘’cell membrane’’ kwenye bakteria, hasa ‘’gram negative’’, ambao kwenye ukuta wao wana chembechembe zinazoitwa ‘’lipopolysaccharides’’, hizi ndizo huwafanya hawa bakteria kuwa hatari sana. Lakini kwa fangasi pia kuna dawa zinaitwa ‘’Amphotericin B’’, nazo huwaua sana fangasi, kwa sheria hii.

3.Uundwaji wa Protini ‘’Ribosomes’’

Vimelea huitaji protini kwa ajili ya kukua. Na ili kuunda protini huitaji kuwa na ribosome (70s) ambayo ni tofauti na ribosome ya binadamu (80s). na dawa nyingi sana za bakteria hulenga kuua hii ribosome. Dawa kama Gentamicin, Tetracyclines, Erythromycin, linezolid, n.k. zote zimelenga kuathiri uundwaji wa protini kwa bakteria.

4.Chembechembe za Nyuklia ‘’nucleic acids’’

Kila kiumbe kinahitaji DNA ili kiweze kuishi. Maana hizi ndizo zinazowezesha uwepo wa kila chembechembe ya uhai, kwa kuziunda. Na DNA huitaji marazote kuendelea kujizalisha yenyewe ‘’DNA replication’’, kwa msaada wa mashine za seli ‘’enzymes’’, na hivyo basi, kama utaathiri matendo haya ya DNA, kwa kuiathiri yenyewe moja kwa moja, au kwa kuathiri mashine zake ‘’enzymes’’, basi unaweza kumuua kimelea. Na hapa kuna dawa nyingi sana.

Mfano, Ciprofloxacin, enrofloxacin, rifampin, n.k. hizi huwaua sana bakteria. Kwa virusi kuna dawa kama Acyclovir, zidovudine, efavirenz, n.k. na kwa protista kuna dawa kama ‘’chloroquine’’ inayotumika sana kwa malaria.

5.Matendo ya Kimetaboliki ‘’metabolic pathways’’

Vimelea huwa na matendo mbalimbali ya kibiolojia ya kuendesha Maisha yao, ndani, na nje ya seli zao. Matendo haya huwa hayafanani marazote na ya kwa binadamu. Na hivyo, ni rahisi kutengeneza dawa ambayo, inaweza kulenga kuwaathiri vimelea hawa tu. Mfano wa matendo ya kipekee kwa bakteria, ni uundwaji wa vitamini B9 kwa bakteria ‘’folic acid synthesis’’, ambayo huwasaidia sana katika uundaji wao wa protini, na chembechembe za nyuklia. Dawa kama Sulfonamide, Trimethoprim, n.k. huathiri matendo haya, na kuwaua bakteria.

Minyoo wengi sana huuwawa kupitia namna hizi, hasa zinapolenga kuathiri mfumo wao wa fahamu. Kwa kuruhusu madini ya calcium mengi sana, hata kimelea kuanguka na kufa. Mfano ni Praziquantel. Nyingine husisimua sana sensa, au ‘’receptors’’ za msisimko, hata kiumbe huanguka na kufariki. Mfano ni ivermectin, pyrantel, n.k. Zingine hublock mfumo wa nishati ‘’ATP’’ za kimelea, na kimelea hulegea mpaka kufa.

6.Mpangilio wa Virusi, na namna za Kuvamia ‘’viral entry, assembly and relaese’’

Virusi huingia ndani ya seli ya mtu na kutumia mtambo wake huyo mtu, kujizalisha. virusi hujipangilia kuwa sawa kupitia aina zao kadhaa za protini. Kwa kutumia dawa ambazo zinaweza kuzuia mipangilio hii ya virusi, ni rahisi sana kuwaua. Hapa zipo dawa nyingi sana, kama vile enfuvirtide, maraviroc, ritonavir, oseltamivir, n.k.

7.Mhimili wa Kimelea ‘’Cytoskeleton’’

Vimelea wengi, hasa aina za minyoo. Huitaji sana protini ambazo ndizo huunda mhimili wao, au ‘’skeleton’’ yao, kwa ajili ya kujizalisha, na kutembea. Ukiathiri protini hizi, huwa ni rahisi sana kuwaua. Dawa kama Albendazole, huua minyoo wengi sana kwa kuwatibulia mhimili wao ‘’microtubules’’. Hata Griseofulvin ni dawa ya kuulia fangasi, ambayo hutumia sheria hii hii.

8.Kulenga Sumu za Vimelea ‘’virulence factors’’

Vimelea wengi huwa na chembechembe zao za sumu, ambazo huzitumia ili kushambulia viungo vya wanaowashambulia. Hizi huwa ni kama majiko yao ya chakula, yasipowaka hawali. Dawa kadhaa huzimisha ‘’neutralize’’, hizi kemikali. Na matokeo yake, kimelea hufa. Mfano mzuri ni ‘’anti-toxins’’ zote, au pia chembechembe za kinga ‘’antibodies’’

Namna Vimelea vinazishida Dawa Akili

1.Huimeng’enya dawa.

Vimelea kama baadhi ya bakteria, huzalisha vimeng’enyaji mfano, Beta-Lactamase, ambao huivunja dawa ya Penicillin, isiweze kuharibu ukuta wake wenye Beta-lactam. Na hii hupelekea dawa kama penicillin, na Cephalosporins, kama Ceftriazone kushindwa katika baadhi ya mazingira.

2.Hubadili Target ya Dawa.

Mfano dawa zinazolenga Kwenda kujishikisha katika 70s ribosome, bakteria hubadilisha hii ribosome yao. Na dawa kama macrolides ‘’erythromycin’’ hufeli, au tetracyclines, zote hufeli katika baadhi ya mazingira. Hasa kwa watumiaji wa muda mrefu, au walaji sana wa nyama za Wanyama waliochomwa sana dawa hizi.

3.Husukuma nje dawa

Bakteria wengi huwa na protini maalumu kabisa, ambazo hutoa nje ‘’pump out’’ dawa zote walizozipata. Tena kabla hazijaleta madhara. Na hii huwa ni sababu ya kufeli sana kwa dawa za tetracyclines, na ‘’fluoroquinolones’’ kama ciprofloxacin,  ‘’enrofloxacin’’ au ‘’fluban’’ kwa baadhi ya ‘’trade names’’.

4.Kutotumia njia za kimetaboliki zilizolengwa na dawa

Mfano zile dawa za ‘’sulfonamides’’, ambazo zililenga sana uundwaji wa vitamin B9 kwenye bakteria ‘’folic acid synthesis’’, bakteria wengi huiruka hatua ile, na kutumia hatua nyingine. Hii hupelekea dawa hizi kufeli.

5.Kuunda Koti la kujikinga na dawa ‘’Biofilm formation’’

Bakteria huunda koti, au hujizungushia protini, na chembechembe zingine. Na kuzifanya dawa zinazotaka kuwashambulia, kushindwa. Na hii hutokea sana kwa magonjwa ya muda mrefu. Mfano, bakteria wanaoitwa ‘’Pseudomonas aeruginosa’’, huunda koti hili, kwa wagonjwa wa ‘’cystic fibrosis’’.

6.Bakteria husambaziana mbinu zao za kujikinga na dawa. Hii huwa kupitia chembechembe zinazoitwa ‘’plasmids, transposons, au kwa kutumia virusi wanaoitwa ‘’phages’’. Na hizi njia huitwa ‘’horizontal gene transfer’’. Bakteria wengi kama ‘’staphylococcus aureus’’, huwa fasta sana katika kusambaziana hizi sifa.

7.Vimelea kama Bakteria huzaliana haraka sana. Na hubadilika haraka sana. Hii huwafanya ndani ya muda mfupi sana, kuweza kuizoelea dawa, na kuishinda. Na upande wa virusi, mfano ‘’RNA-Viruses’’, kama virusi wa UKIMWI, na Influnza. Hawa hubadilika kwa spidi kubwa sana. Na hii ni kwa kuwa, huwa na makosa mengi sana katika uzalishaji wa DNA zake ‘’DNA-replication’’, makosa haya yanatokana na mashine zake za seli ‘’enzymes’’ zinazoitwa ‘’reverse transcriptase’’, kufanya makosa sana katika utendaji wake. Hivyo kila wakati huwa wanabadilika. Na ni ngumu kutengeneza dawa yoyote ile ya kuwamaliza.

8.Virusi huwa wakiichangamanisha ‘’integrate’’, DNA yao, kwenye DNA ya mtu wanayemshambulia. Mfano, Virusi wa UKIMWI, au virusi wa Herpes. pia huwa wanaweza kuingia katika hatua ya kulala ‘’dormant stage’’. Katika hatua hizi zote, hakuna Dawa inayoweza kuwapata. Huwa hawapatikani kwa dawa yoyote ile. Na baada ya muda, huwa wanarudi na kuendeleza madhara.

9.Huwa wanatumia mtambo wa seli wa mgonjwa mwenyewe. ‘’host’s machinery’’.  Na hii ndiyo hufanya kazi kuwa ngumu sana kuwapata virusi wa Hepatitis B. kwa kuwa hujishikisha katika chembechembe ‘’enzyme’’ ya nyuklia  ‘’ DNA Polymerase’’ ya mtu husika. Na kwa mantiki hii, ni ngumu sana kuweza kumuua kirusi huyu.

10.Virusi huwa na ujanja wa kubadili sensa zao ambazo mfumo wa kinga ungeweza kuwagundua. Hii huitwa ‘’antigenic variation’’. Na hasa kwa ‘’influenza’’, au ‘’UKIMWI’’, ambapo kirusi anabadilisha ‘’MHC’’ au ‘’major histocompatibility class’’, ambazo mfumo wa kinga unazitegemea ili kuweza kuwaua virusi kwa kuwakamata.

11.Kumuua kimelea, hasa wanaojificha sana. Hupelekea kiwango kikubwa sana cha sumu kujaa katika seli. Na hii hupelekea madhara makubwa zaidi ya dawa au sumu zenyewe katika seli, kuliko hata kimelea mwenyewe.

vimelea wengi tu wangeweza kufa kwa dawa baadhi, lakini viwango vya dawa za kutosha kuwaua, tayari zinaweza muangusha mtu kwa kumuua kwa ‘’overdose’’. Hivyo ukaribu wao sana na metaboliki za wanaowaathiri, huwapa faida sana. Maana kinachoweza kumuua yeye, kinaweza kumuua pia na mgonjwa wake.

JE MFUMO WA AFYA UNAWEZA KUOKOKA?

Katika hatua hii ya kwanza. Hakuna kipingamizi cha kuwa, safari ya kushindana na vimelea kwa kutumia madawa ya kuwaua. Hakuna namna ya kuweza kuwafikia kiutaalamu. Vimelea ndiyo wanazidi kuwa bora, walioshindikanika. Huku taaluma za afya, tukiwa tumeshamaliza mbinu zetu.

Tangia historia za misri, mpaka leo hii, tumeshamaliza mbinu zote za kitabibu, na kwa mantiki hiyo, kuna kila sababu ya kuhofia kuwa kama watu hawatakuwa makini kujilinda na afya zao, wakitegemea dawa kuwasaidia, wanaweza kujikuta wakiangamia na matumaini yao.

SUMU NI HATARI KULIKO VIMELEA.

Kadri watu  wanavyohangaika na vimelea, wakiamini kuwa hao ndiyo tatizo kubwa sana. Kumbe vimelea ni kama watu wanaobeba maiti Kwenda kuizika. Wao hawamuui mtu, ila wanaenda kumzika, na kumfukia ardhini. Vimelea huja dakika za mwisho kuamua hatma ya Maisha ya mtu, na kushindana nao tumeshaona kwa sasa hivi sio kazi rahisi. Lakini hebu tumwangalie muuaji mwenyewe kwanza.

Muuaji mkubwa kabisa wa Maisha ya watu, ni sumu. Sumu ni chembechembe zote ambazo hazihitajiki katika miili ya watu. Sumu hazina kituo maalumu, huenda na kuathiri seli, au tishu, au chaneli, au chembechembe, mpaka nyuklia za seli, sumu huathiri chochote kile mwilini. Sumu huwa zina ngazi, kuanzia sumu hatari kabisa ambazo zinaweza kumuua mtu ndani ya sekunde chache, mpaka zinazohitaji kipindi cha miaka kumi kuonyesha madhara yake.

Hakuna kitu kigumu kukidhibiti kama sumu, maana huwezi kuiua sumu. Japokuwa tumeshindwa kuwaua vimelea, lakini sumu ndiyo hatuwezi kabisa. Vimelea huelekea katika sehemu moja, na unaweza kuwagundua, lakini sumu huwezi kuzigundua. Vimelea huwa na matokeo ya ghafla ambayo unaweza yagundua na kuyabadilisha, lakini matokeo ya sumu yakishatokea huwa hayabadilishiki kirahisi. Watu wengi wana maarifa na vimeleaa, lakini watu wachache sana wanazifahamu sumu, na matokeo yake. Inahitaji akili nyingi sana kuzitambua sumu. Maana huwezi kuzingundua. Sumu huwa chache sana, na uelekeo wake huwa haueleweki.

Historia za Sumu

Kwa miaka mingi sana nyuma, kiwango kikubwa sana cha magonjwa kilikuwa kinatokana na magonjwa ya vimelea. Kama vile magonjwa ya virusi, na magonjwa ya bakteria. Sehemu zingine magonjwa kama malaria ‘’protista’’, na hata minyoo kama kichocho ‘’schistosomiasis’’ kwa baadhi ya sehemu. Magonjwa kama ‘’smallpox’’ yameshika sana rekodi huko nyuma ya kuua watu wengi zaidi. Lakini sasa mambo yamebadilika.

Baada ya kuvuka miaka ya 1800’s, na kuingia miaka ya 1900’s, tena hasa baada ya kumaliza vita ya pili ya dunia 1945’s, dunia  iliingia katika namna mpya ya ulimwengu, ambayo ilikuwa ni ‘’zama za viwanda’’. Katika zama hizi, kuliambatana na kiwango kikubwa sana cha usasa ‘’modernization’’. Watu wengi sana walikimbilia mitindo ya usasa, kutokana na namna ilivyokuwa na mwonekano wa mvuto, na anasa.

Kadri miaka ilivyokuwa ikizidi Kwenda, ndivyo watu walivyogundua hata namna za vifo nazo zimekuwa ni namna za usasa. Watu wakaanza kufa kwa namna tofauti kabisa na namna za zamani. Watu wakawa wakifa kwa magonjwa mapya kabisa. Kwa mara ya kwanza kukaibuka Ugonjwa mpya kwa kushamiri kwa ‘’Saratani’’. Ilikuwepo zamani, lakini sio kwa namna kama ya kisasa. Lakini pia kukaibuka matatizo ya mfumo wa moyo ‘’cardiovascular problems’’, ambayo ndiyo yanaongoza kwa idadi kubwa zaidi ya vifo mpaka sasa. Kukaibuka matatizo ya mfumo wa mapafu, ambayo yameshamiri sana hasa yakiambatana na saratani. Zikaibuka changamoto za mfumo wa nishati, na insulin, shida za kisukari ‘’diabetes mellitus’’, watu wengi wakaanza kupata vitambi, na kuathirika mifumo yao ya kihomoni.

Kukaibuka matatizo mengi sana ya Maini, kufeli kwa figo kukazidi kupamba moto. Idadi kubwa sana ya Watoto wanaozaliwa na ulemavu ikaongezeka. Wanawake wanatoa mimba ‘’abortions, na stillbirths’’, idadi yao ikaongezeka. Matatizo ya kiakili yakaongezeka, idadi kubwa sana ya watu wakaanza kupata changamoto za kisaikolojia, na za kiviungo moja kwa moja. Kadri siku zilivyokuwa zikizidi kusonga, hata miaka ya watu hawa ikazidi kupungua.

Baada ya matatizo haya kuzidi kusonga, na kushamiri. Ndipo wanasayansi walipogundua kuwa changamoto kubwa inayochochea haya yote, ni Sumu. Na sio vimelea. Na sumu nyingi sana zilionekana kutokana na matumizi ya bidhaa nyingi sana za kisasa.

Kuanzia moshi wa Tobacco

Pombe nyingi sana zinazonyweka kwenye vilabu

Bidhaa za sukari za kisasa. Juisi za viwandani, biskuti, pipi, soda, energy drinks, n.k.

Mionzi mingi sana kutoka kwa vifaa vya kielektroniki.

bidhaa nyingi sana za mafuta mabaya.

hewa chafu sana kutoka katika mazingira

matumizi ya mbogamboga nyingi sana zilizopigiwa madawa.

Matumizi ya bidhaa za GMO zenye ‘’allergens’’ na ‘’carcinogens’’ nyingi.

matumizi ya madawa mengi sana yanayoua hisabati za fiziolojia ya miili, mfano kwa kuua bakteria wazuri, na kuongeza sumu.

kutumia sana bidhaa za nyama.

kutumia maji ambayo yametoka katika  mitaro yenye mabaki ya madini chuma, au maji yenye mabaki ya madawa shamba ‘’viuatilifu’’.

kutokuwa na muda mrefu na mazingira mazuri ya kupumzika.

kutopata mazingira mazuri ya kufanya mazoezi na kutoa nje sumu.

Na mitindo mibaya ya kujiathiri kisaikolojia kama mitandao ya kijamii, miziki mibaya, tabia za uzinifu zinazoharibu uthabiti wa mifumo ya homoni ya upendo, na haya yote huongeza zaidi stress, na kupunguza uwezo wa ku refresh mwili dhidi ya sumu.

Baada ya wanasayansi wengi kugundua kuwa kuna tatizo jipya lililoibuka, linaloua sana watu, ambalo  ni sumu, ambazo zimesambaa zaidi katika matumizi ya watu ya kila siku. Wengi waliandika ripoti nyingi sana, zinazoonyesha madhara mbalimbali ya sumu, ambapo hata mimi mwandishi pia nimeandika ripoti, na kitabu kabisa cha ‘’injli ya sayansi Q4’’. Lakini jambo ambalo watu wengi bado hawajalitambua hapa ni hili.

SUMU NI ZA KITAALAMU ZAIDI YA VIMELEA

SUMU

VIMELEA

Huwa kwenye vitu vizuri, na vitamu. Kama vile soda, nyama, pizza, pombe, sigara, dawa za kulevya, filamu za mapenzi, miziki ya mabiti, n.k.

Huwa kwenye vitu hatarishi na vibaya kama vile, kinyesi, vyakula vibichi, sehemu za utoaji taka mwili, vitu vilivooza, n.k.

Huwa na uraibu, kwa kuwa huwa na matokeo ya kisaikolojia.

Hazina uraibu. Huwa na matokeo ya kupooza, au kusisimsha. Matokeo yake ni ya athari katika fiziolojia ya ubongo

Hutenda kwa muda mrefu sana. Zinapotenda kwa wakati mfupi sana, huwa hazina mafanikio ya kuwapata wengi, maana wengi huzikimbia.

Hutenda kwa muda mfupi sana. Zinapotenda kwa wakati mrefu, huwa hazina mafanikio. Wengi hujikinga nazo.

Madhara yake huwezi yabadilisha, maana huwa yanaharibu hata viungo vya kubadili madhara yake. Mfano, huaribu sana ini, figo, na ubongo.

Madhara yake unaweza yabadilisha. Kama hutakuwa na madhara ya sumu awali yake.

Ni vigumu kuzigundua. Huwa zinakuwa kidogo kidogo. Ili zikijikusanya kwa aina zake nyingi, huwa nyingi sana.

Huwa ni rahisi sana kuwagundua. Huwa wanakuwa wengi, lakini katika eneo dogo.

Zinaharibu fizilojia na jenetikia zote za mwili

Wanaharibu aina maalumu tu za fiziolojia, na jenetikia za mwili.

Zimeshawateka wengi, na zinaenda kumaliza uthabiti wa afya za watu kwa kiwango kikubwa sana. Zina ajenda za kitaalamu sana, na mtu wa kawaida huzigundua akishakuwa kitandani hajiwezi.

Wameshashindikana, na wanasubiria sumu zianze kuonesha mauaji yake, na zenyewe zitamaliza afya za watu, bila mpinzani.

 

Mpaka sasa hivi inatambulika kuna matatatizo makubwa nane ambayo hayawezi kutibika, yanayosababishwa na mitindo mbalimbali ya kiafya. Na watu wengi hawajui kuwa kupitia matendo haya, wagonjwa wengi watarajiwa watajikuta wakiingia katika hatua mbaya sana za Maisha yao.

SHIDA NANE ZA SUMU ZISIZOTIBIKA

1.Kugandana kwa Sukari katika chembechembe za mwili ‘’Glycation’’

Ulaji sana wa sukari kupitia bidhaa kama soda, biskuti, keki, n.k. hupelekea sukari Kwenda kujishikamanisha katika chembechembe zingine za mwili, kama vile Protini, na mafuta ‘’lipids’’, na kuunda kemikali sumu zinazoitwa ‘’Advanced glycation end products’’, au ‘’AGE’s’’. hii kitaalamu inaitwa ‘’non-enzymatic binding’’. hizi ‘’AGEs, huua tishu, huchochea uzee, huchochea uvimbe ‘’inflammation’’, husababisha magonjwa ya kudumu, kama Kisukari ‘’diabetes, alzhemimer’s, and Cardiovascular diseases’’.

2.Kukakamaa na kuisha kwa tishu ‘’Oxidative stress’’.

Hii hutokana na sumu nyingi ‘’free radicals’’, Kwenda kuua seli za mwili. Na hii hutokana na matumizi ya bidhaa kama pombe, vitunza vyakula vingi ‘’preservatives’’, sigara, nyama hasa nyekundu, n.k. hizi huchochea kuzeeka haraka, kujaa kwa mafuta kwenye mishipa ya damu ‘’atherosclerosis’’, na matatizo ya kuzeeka au kuisha kwa ubongo ‘’neurodegenerative diseases’’.

3. Kufa kwa Chembechembe za nishati za seli ‘’Mitochondrial dysfunction’’

Vinywaji vya viwandani vyote vyenye sukari ‘’fructose’’, mfano, ‘’high corn fructose syrup’’. Huwa na fructose ambayo huua enzymes tatu  za mitochondria moja kwa moja. Pia uwepo wa vitunza vyakula kama ‘’sodium benzoate’’, huathiri pia mitochondria. Bidhaa nyingi za kisasa huua hizi mitochondria. Na hupeleka kupungukiwa nishati ya mwili, kukakamaa kwa misuli, shida za kimetaboliki, na magonjwa ya kudumu.

4.Kufeli kwa insulin ‘’insulin resistance’’

Seli inashindwa kuchukua insulin, na kupelekea sukari kujaa kwenye damu, na mtu anazidi kuwa dhaifu. Wala nyama huwa ni vigumu kukimbia tatizo hili. Na hasa walevi. Pia wanywa soda huathirika kutokana na tabia za fructose, kuchochea mafuta mengi kwenye ini. Madhara yake huwa ni kisukari, kitambi, matatizo ya moyo, kuishiwa nguvu za kiume, kuchelewa kupona vidonda, n.k.

5. Ukuta wa seli kuathirika ‘’’cell membrane instability’’

Mtu anayekula nyama anawezaje kukimbia tatizo hili. Ikiwa mwili wake anaujaza kiwango cha mafuta hatari ‘’saturated fatty acids’’. Ambazo kadri zinavyolimbikizana katika ukuta wa seli, zinaharibika haraka kutokana na ‘’oxidation’’, na kupeleka seli kuharibika kutokana na ukuta wake kuharibika. Mnywa soda naye, na wenzake wengi wa kumfanania huteseka kwa hili. Hii huua mawasiliano baina ya seli, huathiri uwezo wa seli kufyonza virutubisho, na seli hufa. Na idadi ya miaka ya mtu huzidi kupungua.

6.Uvimbe wa kudumu ‘’chronic inflammation’’

Mtu anayekula nyama huwa na kiwango kikubwa sana cha asidi katika utumbo wake kutokana na protini nyingi sana za asidi ‘’acidic amino acids’’. Hizi hupelekea utumbo kuchubuka sana, na kwa kadri mtu anavyotumia sana. Ndivyo tatizo linavyodumu sana. Mtumiaji wa sembe naye anajikosesha kambakamba ‘’fibres’’, madhara yake ni bakteria wa kwenye utumbo wake kupungukiwa chakula, na kuanza kula ukuta wa utumbo, wakila protini ‘’mucin’’, katika uteute wa utumbo ‘’mucus’’, na kisha kuuacha utumbo wazi. Na sumu za ‘’free radicals’’ huuchubua utumbo na kupelekea uvimbe, na hata kansa kwa wala nyama. Wanywa soda nao huwa na shida hii hii. na huchochea pia matatizo ya metaboliki, na magonjwa ya mwili kujidhuru ‘’autoimmune’’.

7.Kufelisha uwezo wa seli kuiongoza jenetikia yake ‘’epigenetic dysregulation’’.

Hii hutokana na kila mtindo hatarishi. Kuanzia katika kukesha katika screen za video kwa filamu, au mipira. Kusikiliza sana miziki ya mabiti ya frequency hatari kama 440Hz. Kutumia bidhaa zenye vitunzaji ‘’preservatives’’ nyingi sana. Kutumia mboga mboga zenye madawa, hasa za jamii za Chinese, spinach, strawberries n.k. haya yote huifanya miili kuwa hatarini sana kuweza kupata magonjwa.

8. Kuathirika kwa Mfumo wa bakteria wazuri wa tumboni ‘’Dysbiosis’’

Hii inatokana sana na vyakula vya viwandani kama nyama za kusindikwa ‘’processed meats’’, bidhaa za sukari, nyama, na madawa mengi ‘’antibiotics’’. Na watu hunywa sana madawa kwenye maziwa, na kwenye kuku wa broiler, bila wao kujijua. Haya yote huchochea changamoto za mfumo wa ulaji, na umeng’enyaji, changamoto za kinga, na shida za uvimbe.

MAGONJWA KUMI YA SUMU YASIYOTIBIKA

1.Kisukari ‘’Type-2-Diabetes’’.

Hii ndiyo ile iliyochochewa na kufeli kwa insulin ‘’insulin resistance’’, uvimbe wa muda mrefu ‘’chronic inflammation’’, na matumizi makubwa ya bidhaa za sukari na pombe.

2.Presha ‘’Hypertension’’

Hii nayo imesababishwa na kufeli wa insulin, kunakochochea sukari kujaa katika mishipa ya damu, na kufanya mishipa kuwa midogo. Pia michubuko ya ‘’oxidative stress’’, hupelekea mishipa ya damu kuvimba, na pia madini chumvi mengi kutokana na ulaji wa nyama, huchochea tatizo hili.

3.Mafuta mabaya ‘’Dyslipidemia’’

Changamoto za kuzidi kwa cholesterols mwilini huwezi kuzizuia, kama unakula nyama za broiler, au zozote zile kwa wingi, ukiachana na samaki toka maji salama. Mafuta mabaya hujaa zaidi kutokana na kufeli kwa insulin, kunakochochea kuundwa zaidi kwa mafuta toka sukari, na pia shida za kufeli kwa mitochondria.

4.Shida za moyo ‘’cardiovascular disease’’

Kujaa kwa sukari katika mishipa ‘’glycation’’ huchochea tatizo hili, michubuko ya ‘’oxidative stress’’ huchochea tatizo hili, uvimbe ‘’inflammation’’, huchochea tatizo hili, na kujaa kwa mafuta kwenye mishipa ya damu. Na haya yote ni matokeo ya mitindo ya kisasa, mtu anakula mkate, na blueband, anategemea sukari, na trans fats zote zitaishia wapi?

5.Kujaa kwa Mafuta katika ini bila kunywa pombe ‘’non -alcoholic fatty liver disease’’

Hii hutokana na sukari nyingi hasa za ‘’fructose’’, kubadilishwa, na kuunda mafuta, ambayo hujaa kwenye ini. Kwa kuwa inatambulika kuwa, sukari ya fructose iliyo kwenye bidhaa za kisasa, yote huishia tu kwenye ini. Hakuna sehemu nyingine kwenye mwili inapoweza kutumika.

6. Saratani ‘’cancer’’

Uvimbe wa kudumu, mfano kutokana na ulaji wa nyama, michubuko ya ‘’oxidative stress’’, kupungukiwa kambakamba katika lishe, mtu hali mihogo, wala magimbi, wala dona. Yeye anakula tu sembe, haya yote huchochea madhara yanayoweza kupelekea uvimbe wa kudumu katika sehemu mbalimbali. Kufeli kwa mitochondria huchochea ukuaji rafu wa seli, ambao huchochea saratani.

Inatambulika kuwa ukuaji wa saratani huitaji sana uasidi ‘’acidic environment’’, kutokuwa na oksijeni ‘’anaerobic states’’. Na hizi zote ni hali zinazochochewa kwa utumiaji wa protini za Wanyama, kama vile nyama, na maziwa. Lakini pia sukari za kisasa na bidhaa za viwandani huwa na asidi ambazo huongezwa kama vitunza vyakula, na kuwa na kaboni dioksaidi nyingi. Haya yote huchochea zaidi saratani.

7.Kuisha kwa Ubongo. ‘’Dementia/alzheimer’s’’

Hii nayo ambayo huitwa pia aina ya tatu ya kisukari ‘’type-3 diabetes’’, huusiana moja kwa moja na kufeli kwa insulin, kugandana kwa sukari ‘’glycation’’, na hata kuchubuka kwa tishu za ubongo kwa ‘’oxidative stress’’.

8.Shida ya uzazi kwa wanawake. Polycystic ovarian syndrome ‘’PCOS’’

Hii hutokana na changamoto za kihomoni zinazochangiwa sana na kufeli kwa insulin, kufeli kwa metaboliki za mwili, lakini sasa hivi inafahamika hata kutumia sana mbogamboga zenye mabaki ya viuatilifu ‘’pesticides’’, huchochea tatizo hili kwa wanawake.

9. Kupungukiwa kinga ya mwili ‘’immunity failure’’

Hakuna namna mtu anaweza kuwa na kinga kwa matumizi ya bidhaa za viwandani, zenye vitunzaji vingi sana vya vyakula. Vinavyoua kinga ya mwili. Mfano, emulsifiers, stabilizers, artificial flavors, artificial sweeteners, preservatives, food colors, n.k. hizi huua chembechembe nyingi sana za mawasiliano ya kinga, kama interleukins, interferons, cytokines mbalimbali, n.k.

Kibaya zaidi, kadri unapozidisha sukari mwilini, ndipo sensa zako zinazoitwa ‘’ACE-2 receptors’’ zinazalisha zaidi ‘’angiotensin converting enzymes’’ ili kuruhusu maji mengi zaidi  kufyonzwa kuzuia ‘’hypertension’’, kwa kubadili ANGI kuwa ANGII, na kuchochea ADH kuzuia upotevu zaidi wa maji. sasa virusi huitaji hizi sensa za ‘’ACE-2’’ ziwe wazi, maana ndiyo hujishikisha hapo, kwa hiyo kadri mtu anapotumia zaidi hizi bidhaa, ndipo anapokuwa na urahisi zaidi wa kupata maambukizi ya virusi.

10. Matatizo ya Ubongo ‘’Neurological and psychological problems’’

Unaweza kusoma kitabu cha Q4 kuelewa hili. Kila zinapotumika bidhaa hizi, huathiri ubongo kwa kubadilisha viwango vyake vya sensa ‘’receptors’’, na kupeleka matokeo ya kudumu ya kiafya ya ubongo ‘’neuroplasticity disorders’’. Na haya huathiri akili za watu, na afya yao ya kimaamuzi moja kwa moja. Na kupelekea kizazi cha watu wapumbavu kwelikweli.

HATMA HATARISHI KABISA KUHUSIANA NA ONGEZEKO LA SUMU

Marazote mpambanaji mkuu kabisa wa mfumo wa kinga wa mtu, ni mwili wake. Ukiathiri uwezo wa kinga ya mtu, lazima mtu ataishia utegemezi mkubwa sana kwa madawa. Kinga za watu wengi sana zimezidi kuathiriwa sana kwa ongezeko la viwango vya sumu katika mitindo ya Maisha yao. Kadri ongezeko hili la sumu linavyozidi kusonga mbele, ndivyo hatari zaidi za afya zinavyozidi kuongezeka zaidi.

Tumefikia hatua ambayo hali za watu za afya, zipo mashakani sana. Na tunaenda katika hatua ambazo, hali za kimwili za watu ukichanganya na dhiki za Maisha, hazitakuwa sawa kabisa.

KWANINI MADAWA MENGI YANAZIDI KUFELI ZAIDI

Tunaelekea katika hatua ambayo ni vigumu sana kuwa na dawa za kuwatibu watu. Hii ni kwa kuwa, kutokana na kiwango kikubwa sana cha sumu katika vyakula vya viwanda, na masumu ya bidhaa za viwandani. Magonjwa mengi yanatokana na kufeli kwa mawasiliano ya sehemu mbalimbali za mwili. Na magonjwa mengi hayana sababu moja. Ni vigumu sana kuweza kutibu magonjwa haya kwa kutumia dawa moja. Inahitaji dawa nyingi sana. Na kadri dawa zinavyokuwa nyingi sana, ndivyo zinaleta matokeo hasi ‘’adverse effects’’ kwa wingi sana. Hii ni kwa kuwa, baadhi ya dawa hupingana katika namna zake kiutendaji.

Magonjwa mengi tuliyokwisha yaona, na mengineyo ambayo huwezi kuyatibu. Kadri unavyojaribu kuyatibu, ambapo huwa ni kupitia kugeuza dalili ‘’reverse symptom’’. Kama presha imepanda, wewe unashusha. Matibabu ya mtindo huu,  huwa hayaongezi uwezo wa mwili kupandisha presha yake, huwa tu yanalenga utumiaji wa chembechembe za dawa ambazo huweza kupandisha presha. Matumizi ya chembechembe humaliza kabisa balansi ya awali ya mwili. Na huwa na matokeo ya utegemezi zaidi kwa madawa.

Zamani dawa nyingi zilikuwa na mafanikio makubwa sana. Hii ilikuwa ni kwasababu, miili ilikuwa bado na nguvu kubwa sana za kiafya. Miili ilikuwa na virutubisho vingi sana. vilivyotokana na mitindo sahihi sana ya kimaisha. Usasa ulipelekea vyakula dhaifu sana kiafya. Hata kuishia na sumu nyingi zaidi katika miili. Hizi zimeufanya mwili kushindwa kabisa kujirekebisha, pale matatizo ya magonjwa yanapotokea. Na hivyo kufeli kwa dawa kunazidi kuchochewa kwa mitindo hii ya afya.


SURA YA NANE

MAGONJWA YASIYOFAHAMIKA’’

Mshindi wa Nobel prize George Ward

Nukuu Kutoka Kwa Mshindi Wa Tuzo Ya Mwanasayansi Bora ‘’Nobel Prize’’  George Wald Ambaye Ni Professor Wa Biology Chuo Cha Harvard Kuhusu Genetic Engineering

‘’Injinia ya mabadiliko ya kijenetikia, inawasilisha katika jamii zetu matatizo ambayo siyo tu hayajawahi kutokea katika historia ya sayansi, lakini pia katika Dunia’’.

Ni afadhali ya madhara ya X-Rays, ambayo, huwa tu ikilemea katika genes Fulani, lakini hili janga kubwa hupelekea kusukumwa kwa genes mbele na nyuma, sio tu katika jamii ya viumbe Fulani, bali kuvuka mipaka kwa kushambulia jamii zote za viumbe’’

Kwa mtazamo wa bwana Wald, ukweli kuwa Samaki hawezi kukutana na kujamiiana na Nyanya! ni kwasababu tofauti hizi. kati ya nyanya, na Samaki. sio za mlipuko au kujitokea tu. ‘’random’’. bali ni sababu ambazo, ni matokeo ya mabadiliko ya muda mrefu ya ‘’evolution’’, mpaka kupelekea jamii iliyo imara ( msomaji kumbuka sayansi imejawa na imani ya evolution)

Wald alikuwa akionya kuwa, viumbe hai ni matokeo ya mifumo iliyojengwa kwa miaka mingi sana. na hivyo, sio jambo la kubadili tu mifumo hii ndani ya usiku mmoja, kwa kuwa madhara yake, yatakuwa ni kukinzana na mifumo ambayo, itapelekea madhara makubwa sana kuwahi kutokea.

Na pia akakazia kuwa, hata madhara yake yatakuwa makubwa sana. Ambayo, hayajawahi kuonekana au kuelezwa na mtu yeyote yule.

Wald alisema kuwa, mabadiliko ya kijenetikia yatapelekea matatizo makubwa katika jamii ya watu. Ambayo, ndiyo yatakuwa kwa mara ya kwanza kuonekana. na akazungumzia kutokea kwa magonjwa mapya ya Wanyama, magonjwa mapya ya mimea ,aina mpya za cancer na milipuko mpya ya magonjwa.

Kadri tunavyoikaribia miisho ya milenia ya saba. Kumekuwa na milipuko mikubwa sana ya magonjwa yasiyofahamika. Magonjwa ambayo yamekuwa ni ya kipekee sana. Baadhi ya magonjwa yamekuwa ni matokeo ya miunganiko ya magonjwa tofauti tofauti, na udhaifu tofauti tofauti. Hata kupelekea dalili tofauti tofauti zinazotofautiana kati ya mtu, na mtu.

Magonjwa yasiyofahamika asilimia kubwa sana ni matokeo ya changamoto zinazoathiri mifumo ya kijenetikia. Kadri mtu anavyoathiri mifumo hii, anapelekea  madhara mbalimbali yanayopelekea matatizo ambayo huwa hayatambuliki kabisa katika taaluma za afya. Kwa ufupi sana kuna teknolojia baadhi ambazo huchochea sana matatizo ya kijenetikia. Na hizi ni matumizi ya bidhaa za G.M.O, na teknolojia za kisasa za kubadili chembechembe za jenetikia ‘’genome’’ za watu.

Sehemu hii tutaangalia kwa ufupi sana msingi wa uharibifu huu kwa teknolojia hizi zote mbili..


KUPATA FULLCOPY WASILIANA NASI KUPITIA

Email: brightonshoo7@gmail.com

Dr. Brighton Shoo, (+255)7406 109 88

Softcopy price, 7000/=Tsh

Hardcopy Price, 12000/=Tsh

YALIYOMO

UTANGULIZI

SHUKURANI

SURA YA KWANZA

MNARA WA BABELI

SURA YA PILI

JAMII MPYA, NA HALI MPYA ZA KIMAISHA

KUZALIWA KWA HALI KUU MBILI ZA KIMAZINGIRA DUNIANI.

Tofauti za Kijiografia Zilizochochea Biolojia za Kanda hizi

Nyanda za baridi

Nyanda za Joto

SURA YA TATU

KUINUKA KWA KILIMO KATIKA BONDE LA ASIA-ULAYA, NA AFRIKA KASKAZINI

KWANINI KILIMO KILISHAMIRI ULAYA-ASIA + AFRIKA KASKAZINI, NA HASA BONDE LA RUTUBA?

SABABU ZA KUSHAMIRI KILIMO KATIKA UKANDA HUU

KILIMO NA KUKUA KWA KASI KWA ULAYA-ASIA NA AFRIKA KASKAZINI

KUZALIWA KWA MAANDISHI

KUKUA KWA TEKNOLOJIA

SURA YA TATU

MAGONJWA  YA MAZINGIRA

KIFO CHA UDONGO

WANYAMA WAKUFUGWA NA MAZINGIRA

ONGEZEKO LA JOTO NA MAZINGIRA

UGONJWA WA MAZINGIRA

BADILIKO LA HISABATI ZA MIMEA

MADHARA YA KUUMWA KWA MIMEA

UPANDE WA PILI WA SHILINGI

SURA YA NNE

UGONJWA YA VIMELEA VYOTE NA WADUDU WADOGO’’

HISTORIA YA VIMELEA WADOGO

KUUMWA KWA VIMELEA

MABADILIKO YA VIMELEA

Mfano wa mabadiliko

UTENDAJI WA KIJENETIKIA ULIOLETA TATIZO KWA VIUMBE WENGINE

Wanapodanganywa watu kuhusu ‘’mutations!!

Mfano wa mabadiliko hatarishi ya vimelea

SURA YA TANO

MAGONJWA YA WANYAMA

KUPANDIKIZA WANYAMA ‘’IN BREEDING’’

VIMELEA NA MAGONJWA YA WANYAMA

UBORA WA VIMELEA NI UDHAIFU WA WANYAMA

SUMU ZA VIMELEA

MAGONJWA YA NYANI, POPO, NA PANYA

Kuhusu Nyani, Popo, na Panya

VIMELEA HATARI WENGI ZAIDI HUFA

VIMELEA, WANYAMA, MAZINGIRA NA BINADAMU

SURA YA SITA

MAGONJWA YA BINADAMU

NJIA ZA AWALI KABISA ZA MAAMBUKIZI

MAGONJWA YASIOAMBUKIZWA

ZAMA ZA MAGONJWA

SURA YA SABA

MAGONJWA YA MADAWA

Historia ya matibabu

MSINGI WA SAYANSI ZA MADAWA YOTE

Magonjwa

ASILI YA MADAWA

Kwanini mimea baadhi ina madawa?

Misitu ya Congo

Jangwani, Ukame, na milimani

SIRI YA TEKNOLOJIA ZOTE ZA MADAWA NA MADAWA YA KISASA

kiwango

Utofauti

Huchelewesha Kifo

SIRI ILIYOJIFICHA

CHANZO CHA KUFELI KWA MADAWA YOTE

VIMELEA VINA MAARIFA KULIKO DAWA

Namna Kuu Nane za utendaji wa Madawa

Namna Vimelea vinazishida Dawa Akili

JE MFUMO WA AFYA UNAWEZA KUOKOKA?

SUMU NI HATARI KULIKO VIMELEA.

Historia za Sumu

SUMU NI ZA KITAALAMU ZAIDI YA VIMELEA

SHIDA NANE ZA SUMU ZISIZOTIBIKA

MAGONJWA KUMI YA SUMU YASIYOTIBIKA

HATMA HATARISHI KABISA KUHUSIANA NA ONGEZEKO LA SUMU

KWANINI MADAWA MENGI YANAZIDI KUFELI ZAIDI

SURA YA SABA

MAGONJWA YASIYOFAHAMIKA’’

Mshindi wa Nobel prize George Ward

MATUMIZI YA  BIDHAA ZA G.M.O  ‘’UKOLONI WA AFYA USIO NA KINGA’

HISTORIA NA STORI KABLA YA  SAYANSI YA UUAJI WA G.M.O.

UDANGANYIFU MKUBWA WA MIFUMO YOTE YA FAHAMU

SAYANSI  YA UDANGANYIFU NA UUAJI HATARI ZAIDI WA BIDHAA ZA MABADILIKO YA KIJENETIKIA

G.M.O ‘’GENETIC MODIFIED ORGANISMS

MSINGI KATIKA KUELEWA SAYANSI GENES!!!

KUHAMISHA GENES KUTOKA KWA KIUMBE MMOJA KWENDA KWA MWINGINE

MFANO WA MAAJABU YA HII TEKNOLOJIA

kuchelewesha kifo kwa msaada wa genetic engineering!

SAYANSI YA MOTO KATIKA UJENZI WA KIJENETIKIA INAYO UMBUA WATAALAMU WA G.E

kuegemea katika nadharia zilizopitwa na wakati

uwepo wa chembechembe zinazoitwa ‘’spliceosomes’’

molekuli za kusapoti protini!!

uwepo wa viboresha protini ‘’chaperones’’

kucheza na dna za viumbe

Namna kadhaa za kuingiza genes katika DNA

kufeli kwa dawa ‘’antimicrobial resistance’’ na kusambaa kwa genes mpya

shida ya switch za kijenetikia ‘’promoter ‘’

G.e na kuamshwa kwa hatari zilizolala

madhara ya kusambaa kwa genes hatari

Kuhusu Kirusi Wa Camv Promoter

kuharibu mfumo mzima wa uhusiano wa mwili

kuharibu mfumo wa code za mwili

kujaa kwa genes mbalimbali‘’gene stacking’’

kubadili viwango vya virutubisho kwa mimea

allergy

matatizo ya kibinadamu na giza la maarifa

SAYANSI YA  KISASA ZAIDI YA KUBADILISHA UBINADAMU WA WATU NA VIUMBE HAI WENGINE ‘’HUMAN GENOME EDITING

Historia Fupi

matatizo ya kwanza kabisa ya kimtazamo yaliyoathiri hata wataalamu wa leo

MISINGI YA KUZINGATIA KABLA YA KUELEWA ‘’GENOME EDITING’’

Mtazamo Uliopitwa Wakati Wa Mendel  Wa Mwaka 1856-1863

Upana Wa Kijenetikia Tofauti Na Mtazamo Wa Mendel ‘’Waddington’’ 1957

Hakuna Uhusiano Wa Moja Kwa Moja Kati Ya Gene Na Sifa Fulani ‘’Thomas Woodward Na James P.Gills’’

Msingi Wa Kuelewa Unaoitwa ‘’Weismann Barrier’’

Mtazamo Uliopitwa Na Wakati Wa Dna Kama Msingi Wa Maisha. ‘’Genetic Determinism’’.

lengo la kuwadanganya wengi juu ya dna

TEKNOLOJIA YA KUBADILISHA GENES ZA VIUMBE ‘’GENE EDITING TECHNOLOGY’’

‘’CRISPR-CAS 9 SYSTEM’’

utangulizi

‘’START OF HUMAN GENOME EDITING’’

Namna Dna Inajiponya Au Poneshwa Baada Ya Kuikata Kwa Kutumia CRISPR CAS 9

wanabiolojia wanavyotumia mbinu hizi kuingiza genes zao wanazozitaka kwa kiumbe

Umegundua Namna Dna Yako Inavyoweza Danganywa

faida za hii teknolojia ya kuedit gene ni zipi

Hatari Za Sayansi Ya Mabadiliko Ya Kijenetikia Kwa Jamii Za Binadamu

Daktari wa China aliyebadili genes za mtoto

MATATIZO HALISI YA TEKNOLOJIA YA KUEDIT GENES ZA WATU

Yanaharibu Na Kuhatarisha Kuliko Watu Wanavyojua

Yanahatarisha Kuharibu Vizazi Vya Watu Kama Watu Wabaya Wataamua Kuharibu Jumuiya Kubwa

SURA YA NANE

MAGONJWA YA UBONGO

Nishati Inayosahaulika

NAMNA ZA KISASA ZAKUUA HARAKA SANA UBONGO

Siri iliyofichika

Kuchochea Uzalishaji Mkubwa Wa Homoni Za Msisimko ya Ubongo

Miziki

Hatma ya Miziki

Kwanini Jamii Itapasuka ‘’Collapse’’?

Mitandao ya Kijamii

Hatma ya mitandao ya kijamii

Filamu, Magemu na Mipira

Hatma ya filamu, magemu, na mipira

Namna Nyinginezo

SURA YA SABA

MAGONJWA YA KUELEKEA KUFELI KWA DUNIA

JIOGRAFIA YA DUNIA.

UDONGO

Hatma ya Ardhi na Udongo

Ardhi haitibiki

HALI ZA HEWA

Hatma za hali za hewa

VYANZO VYA MAJI

Hatma ya vyanzo vya maji

UCHUMI

Hatma ya Uchumi

Siasa na Dini

Hatma Kubwa Ya Siasa Na Dini