Jipatie maarifa kutoka vitabu bora vilivyoandikwa na Dr Brighton shoo kuusu imani, sayansi, afya, teknolojia, asili, malezi, saikolojia na mazingira

LUSIFA DHIDI YA ULIMWENGU WA ROHO #7

 ULIMWENGU WA ROHO

Hakuna Ulimwengu wa Roho

Ni muhimu tena narudia vitu vikuu vitatu katika uhai wa binadamu, na hata kiumbe mwingine yeyote yule aliye hai. Mwanga, Maji, na Usumaku. Hivi ndivyo vitu ambavyo vipo katika kiini cha uhai wa kiumbe, hivi ndivyo injini ya maisha. nimeshaeleza katika sehemu iliyopita, mwanga husisimua mabadiliko ya mifumo ya umeme ya seli, kama uzalishaji wa chembechembe za elektroni, ambapo mwili kwa kutumia chembechembe zake kama melanin hata na haem,  zinapozalisha hizi elektroni huzalisha zaidi mwanga ndani ya seli, ambao huu huchochea mabadiliko ya maumbile ya maji katika namna mbalimbali za ajabu kama mshindi wa tuzo ya mwanasayansi bora ‘’Nobel Prize’’ Prof. Montagne alivyogundua namna maji yanaweza tunza na kuunda kumbukumbu hata za vimelea katika namna za ajabu kabisa. Maji haya yanapotengeneza maumbile ya tofauti, hupelekea mabadiliko mbalimbali ya seli, ambayo haya huchochea tabia tofauti tofauti za kiusumaku, kutokana na tofauti za chaji katika molekuli za maji, na huu usumaku ambao huzalishwa ndiyo huchochea na kuongoza matendo mengi sana ya kibiolojia.

Mwili hutumia hizi injini kuongoza matendo yake mengine yote, ambayo huwa ni mithili ya ‘’Automatic processes’’, mfano, utengenezaji wa protini, marekebisho ya jenetikia ‘’epijenetikia mfano DNA-methylation, au Histone acetylation’’, uundwaji wa seli ‘’mitosis na meiosis’’, uzalishaji wa nishati ambao ndiyo msingi wa matendo haya katika Mitochondria, na kila kiungo husukumwa kutoka katika mifumo hii mikuu Kutenda sawasawa na kazi yake, yaani kama ni neva za fahamu, basi usisimkaji utaenda kulingana na majukumu yake.

Lusifa anatambua kuwa wasomi wengi hawajui iwapi Roho ‘’Spirit’’ katika mwili wa binadamu inayoongoza uhai, yaani mithili ya Pumzi ya Mungu. Na anajua ni wasomi wachache sana ambao wanatambua kiwango cha Biolojia kwa undani mpaka katika kiwango cha hii biolojia ya chini kabisa ‘’Quantum Biology’’. Kiufupi kiini cha Gari ni Joto, Mafuta, na Oksijeni.  Kwa hivi ndivyo huzaliwa Moto wenye kupelekea kutanuka, na kupoa kwa Pistons, na huko ndiko hubadilishwa kutengeneza mzunguko wa tairi na gari kutembea.  Kwa magari ya umeme, sababu ingerudi kuwa umeme na usumaku, na kwa hivi matairi huzunguka na kuliendesha gari. Mara ngapi watu wamekuwa wakijua sheria hii lakini hawawezi yatengeneza magari yao yanapoharibika? Je ni kweli kwa kuwa na joto, oksijeni na mafuta tu tunaweza pata gari? Miaka mingapi imepita watu wakiwa na vitu vyote hivi, ila mpaka karne ya 18 na 19, kutoka kwa kina James’s watt mpaka Carl benz ndo tunapata injini za kwanza za kutengeneza magari yetu?

Jibu ni kuwa, Gari ni matokeo ya maelfu ya ufundi ambao kiini cha utendekaji wake ndizo hizo sheria kuu tatu. Gari linapoharibika unahitaji fundi kwa kuwa ni yeye tu mwenye maarifa ya kuelewa namna sheria hizi anavyozibadilisha kuwa utendaji. Wengine wote wanaelewa tu kiini cha utendaji wake. Binadamu pia tunaelewa kiini cha maisha ni maji, nuru na usumaku. Lakini hakuna anayeweza kutumia vitu hivi kuunda uhai zaidi ya fundi mwenyewe ambaye ni Mungu, na ndiyo maana hata mtu anapokufa, ni kama gari linapoharibika, ni muumbaji tu anayeweza mrekebisha. Wasomi wengi dhaifu wana mitazamo ya upungufu ‘’reductionists’’, yaani, kuna kiini ambacho kinaweza elezea msingi wa utu wa mtu ‘’consciousness’’, hakuna hiko kitu.

Roho ya Mungu ‘’Spirit’’ ndiyo inaendesha msingi wa uhai wa kila kiumbe, hiyo Roho ya uhai ndiyo inashikilia, inaelewa, imeumba, mawasiliano katika hiki kiwango cha biolojia ya chini kabisa. Ipo katika viwango vya maji, na nuru, na taarifa ambazo marazote huwa ni usumaku na umeme. Utakuta Yesu akijiita ‘’Nuru ya ulimwengu, au Maji ya uzima, au Neno au kweli’’. alipoonekana Yesu kwa Danieli, au Petro, Yakobo na Yohana, aling’aa kwa mithili ya umeme na usumaku, ambao uliwafanya walipomtazama kuishiwa nguvu kama tu ambavyo huwa kwa mtu ambaye angeona walahu mionzi mikali sana ya mwanga.  Roho hii inapoongoza matendo ya kibiolojia, huwa inakuwa tu ikiwasha mifumo ambayo inapowaka sasa, inakuwa kama Redio baada ya kuichaji inavyofanya kazi, kila sehemu hufanya kazi yake. Kwa upande wa ubongo, unapowaka ubongo, ni kama umeme unapopita kwenye waya, lazima utatengeneza usumaku. Huo ndiyo utambuzi ‘’consciousness’’, kadri ubongo unavyokuwa umeendelea zaidi kama kwa binadamu na sokwe au tembo na samaki dolphin, ndipo utendaji kazi wa sehemu nyingi zaidi unavyoonyesha akili zaidi. Na sio kuwa kuna nafsi na vitu vingine, hizo ni falsafa za kishirikina. Binadamu sio watofauti sana na Wanyama, ni familia ya Wanyama. Tofauti ya binadamu na sokwe ni ndogo sana, na ndivyo ilivyo kwa panya pia, maana sote tu Mammalia. Lakini je ni nani anayeweza zungumzia nafsi ya panya? Kwani hawana maisha yote kama sisi ukiachana tu na ibada? Hata Biblia inasema Sabato iliwekwa kwa mwanadamu, na si panya! Wenda wana namna yao pia ya kuabudu, hata wao sio special sana, vipi kuhusu sisimizi, au kuhusu fangasi? Hoja ni kuwa, hakuna nafsi mbali na ubongo, hakuna roho mbali na ubongo kwa mantiki ya nafsi.

Kumbuka, kila kitu unachokijua au tabia Fulani unayoitenda ipo kwenye tishu na seli za ubongo, na tunaweza ipoteza kama tutakuathiri katika sehemu husika. Unapoona mcha Mungu anasali, kama utamuathiri sana sehemu za ‘’Ventralmedial Prefrontal Cortex’’ usidhani kama atakuwa yuleyule. Na ndivyo watu wanavyopata shida maeneo kadhaa hata wanasahau kila kitu. Hakuna ulimwengu wa roho tofauti na ubongo. ni kwamba ubongo kama kila sehemu ya mwili, huwa na mfumo wake wa umeme ambao huambatana na kazi zake. Na huo mfumo wa umeme, kitaalamu ndiyo tunasema ni matokeo ya kiwango kikubwa cha nishati katika ubongo kutoka vitu vyetu vikuu vya uhai, yaani, ubongo unachukua oksijeni nyingi zaidi, unamadini na maji mengi zaidi hasa ndani ya kimiminika chake kinachoitwa ‘’CSF’’, unafyonza mwanga mwingi zaidi, ndiyo maana unasensa za mwanga nyingi zaidi ‘’melanopsins’’, una damu nyingi sana ‘’haem’’  na mwisho, una chembechembe za nishati za seli ‘’mitochondria’’ nyingi zaidi. Hii inatosha kumfundisha mtu kutambua, Mungu alimuumba mwanadamu toka katika udongo akiwa na mifumo yote hii, kisha akampulizia pumzi yake, ambayo hiyo sasa nayo siyo kuwa iliongeza kitu kwa mwanadamu, bali iliiwasha tu hii mitambo, na kuishikilia kama dereva anavyoendelea kuongoza usukani wa gari lake. Ni dhambi kwa Mtu kusema, wala kufundisha watu, kuwa kuna ulimwengu wa roho, hizo kitaalamu ni shida za kiakili ‘’altered states of consciousness’’, na tunaweza zitengeneza kwa kutumia mapigo mbalimbali ya miziki, madawa ya kulevya, meditations, n.k.

Lengo la Lusifa katika sehemu hii ni kuwa, kama watu hawatajua ni nini hasa kilicho injini ya uhai wao, na afya zao za ubongo na mwili kwa ujumla. Kwa siri sana ataathiri vitu hivi muhimu sana kwa afya za watu hawa, na kisha atawaonesha hata hivyo wao ni sehemu ya mbali zaidi na mwili wao, bado wao wanaweza wasiguswe, kwa kuwa wao ni roho. Wengine husema, ukiathiri mwili, unaweza kuathiri na roho. Wengine husema matendo yao hayana uhusiano na roho zao.