Jipatie maarifa kutoka vitabu bora vilivyoandikwa na Dr Brighton shoo kuusu imani, sayansi, afya, teknolojia, asili, malezi, saikolojia na mazingira

LUSIFA DHIDI YA NGOZI #3

LUSIFA DHIDI YA NGOZI

Kama Nyoka

Ngozi ni mlango wa fahamu ambao lusifa huutumia sana, pengine kuliko wengi wa wasomaji wanavyoweza kufikiria. Lusifa kama alivyokuwa msanii, hakuwa wakukaa katika viti vya nyuma, alikaa juu kwenye steji. Wasanii wote hukaa mbele na juu wakionekana na wote. Wengine husema wasanii ni vioo vya jamii. Ukisoma Biblia katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana, Kila Babeli au uovu unapozungumziwa, huzungumzwa ukipambwa kwa mavazi ya dhahabu, na vito vya thamani za kuvutia. Hoja ni kutambua kuwa, Lusifa kama alivyo kahaba, hujali sana mwonekano wa nje, kuliko hata uhalisia mzima wa ndani. Kama kuna kiungo ambacho kimebeba tamaa za mwonekano wa mwanadamu, basi ni Ngozi yake.

Lusifa anatambua kuwa mwanadamu huonekana kwa afya ya Ngozi yake. Lusifa anatambua Uzuri ni tamaa ya mwanadamu aliyeanguka. Lusifa anatambua uzuri kwa asili sio mbaya, lakini anajua kama wanadamu watajua namna za asili na bora kiafya za kutunza afya zao za Ngozi na mionekano ya uzuri, hatakuwa na nafasi ya kuwachochea wengi zaidi katika uharibifu wake. Lusifa anajua kwa namna ameshachochea uharibifu katika mitindo ya ulaji, mizunguko ya kuamka na kulala, fiziolojia za mwili, n.k. binadamu hatakuwa na mwonekano mzuri. Na sasa Lusifa anakuja na njia mbadala ya kutatua tatizo hili.

Cosmetics kama Mafuta ya kisasa, make-ups za uzuri, serums, creams, ointments, lipstics, sunscreens, nail dyes, eye lashes, tattoos, skin plastic implants, mawigi, perfumes, hair dyes, cleansers, n.k. hii sasa ni sample ya saloon ya uzuri ambayo Lusifa anaiweka kutatua matatizo ya shida za kutokulala, kutumia mianga hatarishi kwenye simu na vifaa vya elektoniki, kula vyakula vilivyoshamiri sukari na viongezwa kwenye vyakula, vyakula vya kukaanga na nyama nyekundu, pombe, kupungukiwa maji, n.k.

Lusifa anatambua kuwa mitindo hiyo yote inachofanya ni sawa na kuziba nyufa juu ya ukuta wa nyumba iliyopasuka katika msingi. Afya ya Ngozi hauwezi itatua kwa kutumia Cosmetics, ila unaweza kuiharibu kwa kuzitumia. Ngozi inaundwa asilimia zaidi ya 90% kwa vitu vinavyotoka ndani ya mwili, na sio juu ya Ngozi. Afya ya Ngozi inahitaji vitamini C, inahitaji vitamini A, inahitaji protini kamili iliyosheheni Amino acids zote. Inahitaji chembechembe za Collagen, elastin, inahitaji melanin, inahitaji maji, inahitaji vitamini E na selenium, inahitaji mwanga wa jua wa miale ya asubuhi yenye mionzi ya UV-A, infrared rays, na inahitaji kidogo sana Blue-lights, inahitaji kidogo sana stress zinazotokana na homoni ya Cortisol, n.k.

Lusifa ameificha taaluma hii kwa wasomi wengi, Lusifa anawadanganya mataifa kuchanganya Uzuri ‘’beuty’’  na Umahaba ‘’sexuality’’. Lusifa anatambua kuwa, mwonekano wa kila binadamu unaweza kuwa aidha mzuri kama Yusufu, Absalomu, Raheli, Sara, au Esta. Lakini pia unaweza kuwa wa kimitego kama makahaba wengi sana. Uzuri ni mpana sana kuweza kuuelezea, maana ni matokeo ya mwonekano na tabia. Lakini Lusifa hufeki mwonekano wa nje kwa mbinu za kisaikolojia, na kutengeneza mwonekano ambao huchochea Ubongo kusisimka kimapenzi. Na kisha kudanganya watu kanakama mwonekano huo ni Uzuri ambao Mungu ameuumba.

Lusifa huwa kitaalamu anachochea ‘’Estrogen look’’ ambayo mimi napenda kuiita. Wanadamu kisaikolojia huvutiwa kuelekea mwonekano unaoelekea uzazi wanapokuwa katika hatua ya kuhitaji uzalianaji. Wanaume hupenda wanawake wenye maumbile mazuri ya uzazi kama matiti na nyonga zilizoachana kwa wastani wa 1:3 kati ya kiuno na hips kwa urahisi wa kuzaa Watoto. Wanaume huvutiwa kwa wanawake wenye afya nzuri ya Ngozi kama ishara ya afya bora. Wanaume huvutiwa kwa wanawake wenye mwonekano wa kuvutia wa sura, unaoashiria kiwango kidogo cha stress cha kukomaza miili yao, yaani kama timu zinavyopenda kusajili wachezaji wadogo, ndivyo wanaume hupenda mabinti wadogo ili kuwazalia sana. Wanaume hupenda wanawake wenye sura zenye tabasamu kuashiria amani, macho makubwa na meupe kuashiria uwezo mkubwa wa kuhisi huruma au kuzingatia, nywele nyingi kuashiria estrogen nyingi, au sifa nyingi za umama. Wanaume huvutwa katika vigezo hivi kisaikolojia bila wao kujijua.

Vivyo hivyo kwa wanawake ambao huvutiwa kwa wanaume wenye mionekano ya uimara kimisuli na urefu kama ishara ya usalama na ulinzi. Wanawake hupenda wanaume wenye nguvu kiuchumi kama ishara ya usalama wao na uzao wao. Wanawake hupenda wanaume wenye sauti nzito na ndevu kama ishara ya mamlaka na uwezo wa kufukuza maadui. Wanyama majike hukimbia wanapopandwa na madume ili kutopandwa na madume yasiyo na ulemavu, au wasio wadhaifu. Wanawake pia huvutiwa na wanaume wenye mionekano mizuri ya sura kama ishara ya amani, ukarimu, na mifumo imara ya kinga kama tulivyoona katika injili ya sayansi Q5.

Hii mivuto hakuna mwanadamu ambayo anayo kwa asilimia zote 100% zaidi ya Adamu na Eva tu, shida nyingi na makosa katika jenetikia imepelekea wengi tumeathirika katika mionekano yetu. Lusifa analitambua hili, na sasa kwa kuusoma ubongo wa binadamu kwa karne nyingi, anachochea sanaa za uongo, sanaa za kufeki mionekano kuelekea katika vigezo vikuu vya uzazi kimionekano bila uhalisia.

Lusifa anachochea mavazi ya nusu uchi ili kusisimua ubongo wa wanaume kuelekea hitaji la uzazi katika mazingira yasiyohitajika, na anajua kwa kuwazoelesha mionekano ya nusu uchi, baada ya muda wengi wa wanaume hawa hawataweza kusisimka tena kwa kuwa wameshazoelea mionekano hii. na hii ndiyo sababu tafiti kadhaa zinaonyesha vijana wengi wa miaka 15 wamepungua sana hamu ya kufanya mapenzi, sio kama ilivyokuwa awali. Hii ni kama mtoto unavyompiga sana, baada ya muda huota sugu. Lengo la lusifa ni kuwafanya wanaume kutokuwa na nguvu za kiume, huku akiwaondolea wanawake kabisa thamani za miili yao.

Lusifa anajua matumizi ya Cosmetics kama make ups, lipsticks huchochea mionekano ya mafuta mafuta kuashiria estrogens, ambazo huwafanya wanaume kusisimka sana kimapenzi. Eye brows na lashes, hutengeneza kona ‘’margins’’ kwenye macho, na kuyafanya macho kuonekana na weupe kipekee sana, nguo za kubana vifua zikiyaonyesha matiti kwa theluthi walahu, huyafanya matiti kuonekana madogo ishara ya ubichi kiuzazi, na kuwasisimua sana wanaume, make ups huzifanya sura za wanawake kuficha mikunjo yote ya Ngozi, na kuchochea mionekano ya afya ya Ngozi ishara ya estrogens nyingi kwa mwanamke, na wanaume wengi husisimka zaidi. Wanawake wengi huvaa nguo zenye kuwabana ili kuonyesha tofauti za maungo yao kati ya hips na nyonga, hii huwasisimua zaidi wanaume.

Wanaume wengi huwa hawaelewi nini huwasukuma zaidi katika uzinzi wanapokutana na wanawake wa mitindo hii, ambao wamejawa na mionekano ya kimahaba, ambayo hawakupaswa kuwa nayo katika mazingira ya jumuiya. 

Lusifa amesheheni mionekano hii feki katika filamu, miziki, n.k. katika injili ya sayansi Q4 nimeelezea namna sanaa hizi zinavyochangamanishwa na mianga ya kisasa, na Camera za kisasa, na programs za kisasa katika kutengeneza filamu, music-videos, social media arts na matangazo, ambapo matokeo yake ni kuwachochea vijana wadogo kabisa kuingia katika kuangalia filamu za ngono, wanawake kuumwa matatizo ya kisakolojia, kuwazia sana mionekano yao ya uhalisia kwa kutamani mionekano feki ‘’fake-obsessions’’, wengi huishia kutokujikubali, hushindwa kuelewa tatizo lao haswa ni lipi, na hata hivyo huwa hawapo hao wanao wa tamani kimionekano.

Picha zimeshamiri za watu wenye mionekano mizuri, wakiwa katika mazingira ya kitajiri, na vijana wengi huvutiwa. Maelfu ya vijana wa kiume hushinda kwenye majimu wakikuza misuli yao, na kusahau kuwa afya za miili yao zinategemea zaidi afya ya moyo na ubongo, na sio misuli. Wala hakuna wanaokufa kwa shida za misuli bali moyo na ubongo. takwimu zinaonyesha watu wanaoishi miaka mingi, na kuwa na afya sana ni wale ambao huwa na wastani wa mionekano ya kawaida kama wayahudi, wachina, n.k. wanyakua vyuma na wajenga misuli wengi hufa mapema, na huzeeka vibaya. Hii ni kwa kuwa mwili unahitaji ‘’Mitochondria nyingi zaidi katika moyo na ubongo’’’, na sio misuli kama watu hawa wanavyofanya. Hii ni tofauti ya binadamu na sokwe. Sokwe wanamisuli mingi na huishi miaka mifupi ukilinganisha na binadamu, maana huwa na mitochondria chache sana katika ubongo na moyo, Lakini Lusifa huwachochea wanadamu hawa kutaka kuwa kama sokwe kwa kutamani sifa za uzazi, na kukosoa fiziolojia zao kwa kuwapatia mionekano ya wastani, kwa kutamani mionekano feki.

Kama Joka

Lusifa masikini baada ya kuwateka vijana wengi sana katika furushi lake la tamaa ya mionekano, huwaua wote kwa namna mbalimbali. Lusifa anatambua katika kila mbinu aliyoitengeneza katika sifa feki za uzuri, ana maelfu ya madhara kuliko faida.

Cosmetics zote ni hatari kuliko wengi wanavyohisi, kwanza, kama ilivyokuwa awali, kuanzia miaka ya 1970’s na kuendelea ndipo kiwango kikubwa sana cha cosmetics za kisasa kilianza kutumika.  Na kuanzia hapo ndipo matatizo makubwa zaidi ya Ngozi yalipoanza kushamiri. Na msingi wa Lusifa katika kuwaua watu kwa ufupi ni kama ifuatavyo.

Lusifa na Biolojia ya Hatari za Vichochea Urembo

Wengi wa warembo hukimbia sana mwanga wa jua. Kwa kuwa huamini mwanga wa jua huwazeesha, au wakakamaza Ngozi. Wengi wao hutumia Cosmetics ambazo huwa na chembechembe za kuzuia mwanga wa jua kupenya katika Ngozi.  Hizi huitwa ‘’sunscreens’’. Kati ya hizi, zote huwa na madhara. Lakini madhara makubwa zaidi huwepo kwa zinazoitwa ‘’chemical sunscreens’’, mfano, Oxybenzone. Hizi kwa asili zinapokuwa katika mafuta, hufanana sana na chembechembe za estrogens, na madhara yake ni kuwa, kadri mtu anavyozitumia, hasa anapokuwa mwanaume, humchochea sana kuwa kama mwanamke ‘’feminizes’’, hii ni kwa kuwa, husisimua sensa ‘’receptors za estrogens’’ ambazo zisingehitajika ndani ya mwanaume. Na pia, bado zimeonekana kuwa na madhara mengi sana zinapokuwa ndani ya mtu.

Chembechembe nyingi katika mafuta, kama ‘’Parabens, hydroquionones, n.k.’’ zimejikita kumpunguza nguvu enzyme anayeitwa ‘’tyrosinase’’, ambaye huyu hubadili phenylene kuwa tyrosine katika uundwaji wa melanin. Kutokana na wanawake kutotamani kuonekana Weusi unaochochewa na melanin, wengi wao hupendelea mafuta yenye tabia hizi, lakini matokeo yake ni mwili kuishiwa melanin. Kumbuka melanin ni ya msingi sana katika kufyonza mionzi ya muhimu sana ya mwanga wa jua kama UVA, na infrared rays, na kuzalisha electrons ambazo huenda kusaidia mwili kuzalisha maji katika mitochondria, na kuchochea afya ya mwili mzima. Madhara yake ni kuwa mwili huishiwa nguvu kabisa, na kadri melanin inapopungua, ndipo mionzi hatari ya jua ya UV na Blue-rays inapopenya zaidi kuingia ndani ya Ngozi, na kuathiri kila kitu katika afya ya mwili. Lusifa anajua kadri anavyoua kinga, kila mfumo wa afya utaathirika, na watu watazidi kuwa watumwa wake kwa kutegemea mifumo yake kwa madawa na matibabu tegemezi.

Cosmetics nyingi kama ambavyo huwa zikiwa na harufu nzuri sana, zimejawa na maelfu ya chembechembe zenye mamia ya Fluorides, mfano ‘’PFA’s’’, hizi zimejaa fluorides ambazo huvuta karibia electrons zote toka kwa Oxygen, na kufanya mitochondria kushindwa kuzalisha maji, wala kuzalisha nishati. Hii kitaalamu pia unaweza iita kama ‘’reduction in redox potential’’.

Cosmetics huwa zinajazwa chembechembe ambazo hata mashirika ya afya huwa wanashindwa kuzinyumbua na kujua hatari zake, ijapokuwa huwa zimejazwa kwenye ingredients. Mfano ni ‘’Fragnances’’, hizi ni hatari sana kwa afya ya Ngozi, lakini hakuna namna watumiaji wanaweza kukimbiana nayo kwa kadri maisha yamekuwa hayawezekani bila bidhaa hizi.

Watengeneza mafuta wengi wanatambua shida kubwa za watumiaji wao ni matatizo ya vimelea kama fangasi, bakteria, na shida za mwili kujishambulia ‘’autoimmune disorders’’, ambazo huchochea uvimbe na vipele, na wakati kadhaa shida hizi huchochewa sana na allergy. Watengeneza mafuta wengi huweka chembechembe kama ‘’steroids’’ ili kupunguza uvimbe, lakini madhara yake ni kuwa, chembechembe hizi sasa ndizo hushusha kabisa afya ya kinga ya Ngozi, na huifanya Ngozi kuathirika zaidi na vimelea na fangasi, hata na virusi. Matumizi pia ya viua vimelea kama kwenye ‘’cleansers’’ nyingi, ili kuua bakteria kama staphylococcus, au streptococcus, huua mpaka vimelea wazuri katika Ngozi, na hivyo kuathiri balansi ya Ngozi, na kuchochea kushuka kabisa kwa kinga za warembo hawa.

Lusifa hufurahia sana anapoona sasa warembo feki, hawana kinga kabisa katika miili yao. Kadri wanavyojiwekea mawigi, ndivyo wanavyopunguza mianga mizuri kuingia katika ubongo wao, na hivyo kupunguza afya bora ya ubongo. serums nyingi, huingia katika damu na kujaza chembechembe ngeni na hatari kwa mifumo ya afya. Mafuta mengi yamejaa chembechembe nzuri kama Retinol au Vitamin A, lakini hazina uhalisia, wala vitamin C zisizo na faida. Maana viwango vyake huwa vidogo sana. Creams nyingi huzuia matundu ya Ngozi kupumua, na kuchochea chunusi kwa baadhi ya watu wenye Ngozi laini za mafuta.

Tattoos zina madhara makubwa sana katika Ngozi, huongeza kiwango kikubwa sana cha ‘’plastics nanoparticles’’ katika damu, ambazo madhara yake ni hatari, na hayatabiriki, lakini huchafua afya ya damu, huchochea uvimbe mdogo chini ya rangi hizi. Na ndivyo zilivyo rangi nyingi pia za kisasa ambazo hupenya aidha toka katika dyes za nywele na kuingia katika kichwa, au toka lipsticks na kuingia katika mdomo, haya yote hushusha sana kinga ya binadamu, na kuwafanya maiti zinazotembea.

rejea nukuu kadhaa kuhusu madhara zaidi ya cosmetics ingredients kadhaa,

pia rejea,,