Jipatie maarifa kutoka vitabu bora vilivyoandikwa na Dr Brighton shoo kuusu imani, sayansi, afya, teknolojia, asili, malezi, saikolojia na mazingira

UBONGO WA MTU MWEUSI




KISA KIFUPI CHA MTAA MMOJA WA JIJI LA PENTAGON

Mara moja nilikuwa nikipita katika mtaa mmojawapo ulioshonana sana katika Jiji la Pentagon. Kulikuwa na watu wengi sana wanaosongamana katika njia na eneo dogo sana. msongamano huu ulitokana na wengi wa watu hawa kuwa wakifanya biashara, na wengine wakipita, na hata wengine wakifanya makazi katika eneo dogo. Idadi ya watu ilizidi idadi ya makazi, na kutokana na kiwango kikubwa cha joto katika eneo lile, kulikuwa na kiwango kikubwa sana cha hewa nzito. Ikiwemo kaboni dioksaidi.

Uchafu mwingi uliokusanywa maeneo kadhaa na kuvunda, ukaribu wa vimitaa vidogo ambavyo watu hawa baadhi huwa wakijificha kujisaidia, kutokana na uchache wa vyoo, na gharama za vyoo vya kulipia. ulichochea hewa nzito ambayo, watu wengi wa maeneo haya hawakuwa wakiihisi! Kwa kuwa, wameizoea.

Bado eneo hili halikuwa na utulivu wa sauti. Kulikuwa na sauti endelevu ya aidha viwanda, vyombo vya usafiri, makelele ya watu, miziki toka kwa watu na clubs, na matangazo ya wafanyabiashara. Watu kwa wastani walikuwa wakiongea kwa sauti kubwa ukilinganisha na maeneo mengine, na wao walikuwa wakiona kawaida. awali nilifika eneo hili nikiwa nasikiliza muziki kwa kutumia ‘’earphones’’, na sasa, nilikuwa siusikii tena kwa kuwa, sauti ya mazingira ni kubwa sana. Lakini watu wa eneo hili wao wanaona kawaida kabisa, na tena, bado wanapiga na miziki kwa sauti ya juu zaidi.

Kipindi naendelea na safari yangu, nilikuwa nikijikuta mhanga wa kusisimuliwa sana kihisia na wadada wengi sana wa maeneo haya ambao, wengi wao walikuwa wakiwa wamevaa nguo fupi sana zinazoonyesha maungo yao ya karibia na sehemu za uzazi, mapaja, matiti, na wengi wao walikuwa wamejiremba sana sura zao. lakini kwa utafiti wangu mfupi niligundua kuwa, vijana wengi wa maeneo haya, kwao haikuwa hivyo. wao waliona kawaida sana. Wala hawakuwa wakiwasindikiza mabinti hawa kwa macho!

Taswira nyingi sana katika eneo hili zilikuwa zinazoonyesha matangazo yenye rangi kali sana za mng’ao, rangi nyekundu, bluu, nyeupe, na nyeusi. Na matangazo mengi yalikuwa katika muundo wa kushangaza, yaani, Kuna bidhaa nzuri ajabu sana iliyopo pale! Au labda kuna huduma bora sana eneo hilo. Wengi walikuwa wakionyesha taswira zinazokazia utofauti, na upekee wao.

Baada ya muda kadhaa nilipatwa na njaa. Nikawa nikitafuta sehemu ya kula. Nilikutana na sehemu nyingi sana ambazo watu walikuwa wakiuza juisi za sukari sana. Juisi za muwa, ambazo huwa wanachanganya na ndimu. Juisi za matunda mchanganyiko baadhi, zenye sukari kali sana. Wengi walikuwa wakiuza Supu ya pweza, na supu za aina nyingine nyingi. Walikuwa wengi wakiuza vyakula vya kukaanga, na baadhi ya watu pia walikuwa wakienda kununua kwenye ma ‘’supermarket’’ vyakula vya kupaki moja kwa moja. Nilifanikiwa kupata mgahawa mmoja ndani ndani sana ambao, niliona wengi wakinunua vyakula hapo. Na walikuwa wakila huku wengine wakiwa wamekosa kabisa hata sehemu ya kukaa, na walikuwa wakila huku wamesimama. Nikaagiza ugali wa dona na mboga za majani, nikakosa, wakasema upo wa sembe. Nikasema nipatie wali na maharagwe kama upo, wakanipatia. Watu wengi hapa walikuwa wakila wali na Samaki wakurostiwa, wali na nyama za ng’ombe, chipsi na mayai ya kisasa, au na kuku wa kisasa kama broiler.

Joto ni kali sana, lakini watu bado wanakunywa maji kidogo sana. Kipindi najiuliza kwanini, nikagunda huwa wanakunywa maji ya baridi sana. Maana, hayo hukata kiu mapema. na hivyo kwa kunywa maji kidogo, unaweza okoa gharama ya kunywa maji mengi sana. Maana huku, maji ni ya kununua. Lakini kipindi naendelea kutembea, niligundua mtaa huu kwa chini, ulijawa na chupa nyingi sana za juisi za ‘’energy drink’’, soda za kopo, na chupa za maji ambazo zote, zilikuwa zimekusanywa sana karibu na sehemu za wauzaji wa vyakula, na mabarabarani. Hii ilikazia hitimisho la utumiaji uliokithiri wa bidhaa za sukari, katika maeneo haya, na bidhaa za baridi kali.

Mitaa mingi niliyokuwa nikipita niligundua kuwa walikuwa wakisikiliza miziki ya wasanii kadhaa, ambao wote walikuwa wa ‘’Bongo flavour’’, na miziki waliyoipenda sana, ilikuwa ya msanii mmoja mwanadada aliyekuwa akiimba miziki ya kucheza sana, na mabiti ya kujirudia. Na pia, wapo wasanii wa kiume ambao nyimbo zao zote zilikuwa ni aina ya ‘’dance music’’, miziki ya ki ‘’Nigeria’’ ilisikilizwa sana pia. Kuna aina ya muziki ambayo ilikuwa inafikisha mpaka mabiti 250 kwa dakika, ni kama ‘’electronic music’’, ila inaitwa ‘’Singeli’’, nayo ilikuwa ikipigwa sana.

Na miongoni mwa vitu vilivyonishangaza sana ni kuwa, aina zao za muziki zina aina moja ya ujumbe, yote ilikuwa imejikita kuzungumzia mapenzi, kufanya mapenzi au migogoro ya mapenzi, hasa kutokana na pesa. Na muziki mwingine niliousikia kwa baadhi sana ya maduka, ulikuwa wa dini, ambao nao, ulifanania sana na ule wa wenzao, na pia, kuna uliokuwa ukirudiarudia sana maneno machache yaleyale, lakini ulikuwa wa muda mrefu sana.

Kwa muda mfupi sana nilikwisha kuwaonea huruma hawa watu kwakuwa, mfano. idadi kubwa ya watu hawa na Maisha yao yalivyo, lazima watakuwa na stress sana. Hilo nililithibitisha hata kabla ya kuendelea mbele zaidi, maana, niligundua wengi wao wakiwa ni watu wenye kupenda sana vitu vya kuwaliwaza, kuwaburudisha, kuwasahaulisha! Niliona wakibishania sana mipira, wengine walikuwa wakiwafuatilia sana manabii baadhi. Pia walikuwepo wasanii wengi sana karibu na maeneo haya, na wote! Walikuwa muda mwingi sana wakizurura katika mitandao ya kijamii.

Nikamuuliza kijana mmoja aliyekuwa akiuza madafu eneo nililoamua kupumzika kidogo, nikamuambia ‘’ukipata nafasi ya kufanya kazi nyingine nzuri kama unayoifanya, au yakuifanania kwa maeneo mbali na maeneo haya unaweza kuikubali? ‘’ akaniambia ‘’hapa nilipo nimetoka huko mbali, na Maisha huko yalikuwa magumu zaidi, kwangu hapa ndipo kama bustani ya edeni!!’’

HISTORIA FUPI YA HILI ENEO

Hili eneo ambalo linakaribiana na mji wa Dar es Salaam. Kwa ujumla maeneo haya yote huwekwa katika kundi la miji ya nyanda za chini Pwani ‘’sio nyanda za juu pwani’’. Maeneo haya huwa hayana ardhi kubwa sana yenye Rutuba ya kufanya kilimo (Kilimo Kikubwa kinachozungumziwa), na pia, huwa hayana mabonde mengi na maji ya mito mengi kama kwa maeneo mengine ya pwani za juu, ya kuyawezesha kwa kilimo kikubwa. Watu wengi maeneo haya huwa wakifanya shughuli za Biashara na uvuvi. Wengine huiita hii miji kuwa, miji ya biashara.

Hapo zamani kipindi cha Jamii nyingi za Bantu zilipokuwa zikiteremka toka kaskazini, kupitia bonde la ukanda wa Kongo, na kuanza kutengeneza Jumuia kubwa ‘’small empires’’, au unaweza ita ‘’Chiefdoms’’, ambazo ndizo kama jumuiya za makabila baadhi, mfano ‘’Wanyamwezi’’, n.k.

basi kipindi jamii hizi zilipokuwa zikizidi kukua na kupata nguvu, zilipelekea wakazi wengi ambao hawakuwa na jamii zenye nguvu, kama ilivyokuwa kwa jamii za ‘’Khoisan’’ walivyosukumwa mbali, ndivyo ilivyo pia hapa, wenyeji wengi wa pwani walikuwa pia ni wabantu, wa jamii kama za wa kwere, zaramo, ndengereko, wadoe na makabila ya kuzunguka mto Rufiji. Lakini makabila haya yalifika pwani katika zama tofauti tofauti, na historia kadhaa mbele tutaona zinaonesha wengi wa makabila haya walikuwa ni wahamiaji, waliotoka katika jamii kubwa zaidi za awali. Na walijikita zaidi katika uwindaji na ukusanyaji, na kisha uvuvi na biashara. Hivyo awali hawakuwa na jamii zenye nguvu sana, tofauti na makundi yenye ustadi zaidi wa kilimo ya kibantu yaliyozidi kushuka katika bonde la Tanzania, na hivyo walisukumwa mbali zaidi. Hawakuwa na nguvu za kushindana na wabantu hawa waliozidi kuwa na nguvu. Hawa wabantu wengi walikuwa ni wakulima, na kwa hivyo, walichukua maeneo mengi sana yenye Rutuba.

Maeneo ya pwani yalianza kujawa na watu waliokuwa na jamii zisizokuwa na nguvu sana, ni kama ilivyokuwa kwa maeneo ya milimani walivyokuwa wakisukumwa makabila ya waliokuwa na jamii ambazo hazikuwa kubwa sana, pale makabila yenye nguvu yanapochukua ardhi zenye rutuba.

Huku pwani jamii nyingi za awali kabisa zilianza kushughulika na shughuli za uvuvi wa Samaki. Na kisha, zilikuwa zikifanya biashara na makabila ya maeneo ya kati. Nitaelezea historia ya lugha ya Kiswahili, lakini kwa awali kabisa ni muhimu kujua kuwa, kutokuwa na makazi ya kudumu kwa jamii hizi za awali kabisa, kulizifanya kupokea lugha ya kibantu moja kwa moja, ambayo ni lugha matokeo ya koo kadhaa kuu za bantu, ambazo zote zilikuwa zikifanana.

Sasa basi, kuanzia mwaka 100AD inanukuliwa na baadhi kuwa, miji hii ya pwani ilishakwisha anza kufanya biashara na maeneo ya India, China na Misri. Na biashara hizi zilizidi kuendelea na hata dhidi ya jamii nyingi sana za nchi za kiarabu.

KUKUA KWA MAENEO HAYA YA PWANI

Unaposafiri, mara zote unajiandaa sana. Wasafiri wengi huwa wakijiandaa sana kiuchumi. Wasafiri wengi wa awali kabisa kufika katika pwani hizi, walihitaji msaada mkubwa sana wa wenyeji wao. Walihitaji wafasiri wa kuwawezesha kuingia ndani zaidi ya miji ya nchi kwa ujumla. Walihitaji wenyeji wakuwapatia mahitaji ya msingi katika maeneo mapya.

Hii iliwapatia fursa wenyeji wa maeneo haya ya pwani, kuweza kutengeneza thamani kubwa sana, kwa kuwa, wao ndiyo walikuwa waamuzi wa kwanza wa thamani za mabadilishano ya huduma na vitu, au huduma na fedha. Thamani kubwa ya nchi yeyote ile haijawahi kuwepo miji ya Pwani. Lakini, pwani ndiyo kituo kikuu cha mabadilishano.

Hii inamaanisha kuwa, wafanyabiashara wakubwa zaidi, walikuwa ni wageni wenyewe waliofika pwani hizi. Wao waliangalia thamani ya vitu katika nchi zao wanazotoka, na upatikanaji wake katika makazi mapya. Namna nyepesi kabisa ilikuwa ni hii, kutengeneza makazi ya kudumu katika maeneo haya, na kuwatumia wenyeji hawa wa pwani kurahisisha ubebaji wa vitu vya thamani, na kisha wao kuvisafirisha kuelekea katika nchi zao. Wenyeji wengi wa pwani ndiyo walioshiriki katika usambazaji wa bidhaa na huduma katika ya jumuiya za ndani, na za wageni. Walibeba wakati mwingine kama watumwa, au wakati mwingine kama wasaidizi.

Vituo vingi vya huduma vilianza kufunguliwa maeneo haya na wageni. idadi kubwa ya watu ilianza kujaa katika maeneo haya kwa ajili ya kufanya kazi za wageni. Wanawake wengi walianza kuzaa na wageni hawa, wengi wao wakiwa waarabu. Hakukuwa na lugha zaidi ya Kiswahili, lakini misimu, rahaja na hata lafudhi nyingi zilianza kushepiwa kwa mchangamano na waarabu.

Wageni wengi walihitaji burudani katika maeneo haya, na wasanii walinufaika kwa huduma hizi. Wenyeji wengi wa maeneo haya walinufaika pia kwa kuuza maeneo yao mengi kwa wageni, wakati huu sasa, waliuza kwa wabantu waliosukumwa kibiashara zaidi kuja pwani, na kwa wageni. Wenyeji hawa wengi waliendelea kusambaa hata kufika maeneo ya visiwani, ambako awali, hakukuwa na makazi ya wengi zaidi ya wavuvi, lakini ugunduzi wa waarabu kuhusu upekee wa visiwani, ulihamasisha zaidi mchangamano kama uliokuwa upande wa pili wa bara.

ASILI YA MWAFRIKA MASHARIKI

Hakuna ubishi kuwa jamii nyingi za maeneo ya Afrika Mashariki zilianza kushuka kutokea maeneo ya kaskazini. Zingine zilishuka mpaka kufika kabisa kusini, ila baadae, zikaanza kupanda tena juu kama ‘’Wangoni’’. Rangi za Waafrika kuanzia Rangi za weupe kabisa, mpaka Weusi kabisa, zinathibitisha kabisa uhusiano wa kiwango cha mionzi ya Jua kwa kadri unavyokaribia Equator, na ongezeko la mwonekano wa Weusi unaotokana na ‘’melanin’’ inayozalishwa kujikinga na upenyaji zaidi wa mionzi katika ngozi.

Na hata ongezeko la ukubwa wa mwili (makabila kama wanubi, wajaluo, wakamba, wamaasai, wajaluo, wasukuma, wabantu karibia wote, n.k.) ‘’ingawa sio kwa siku hizi za madhara ya afya’’. Ilikuwa ni kwa lengo la kurahisisha zaidi upotevu wa joto kali katika maeneo haya ya equator, kutokana na kiwango kikubwa cha miale mikali ya jua. Pia hata nywele laini, zilizonyooka kwa watu wa asili ya Afrika, kunathibitisha kiwango kikubwa cha joto ambalo liliwachochea kuwa na matundu yaliyojiminya kutengeneza umbile la ‘’C’’ ili kutoruhusu mionzi mingi kuathiri Ubongo, na pia nywele za Waafrika hunyooka ili kuruhusu kupotea kwa joto kirahisi, tofauti na nywele za ulalo ambazo hulenga zaidi kuzuia kutopotea sana kwa joto kutokana na baridi kali. Nywele za Waafrika hutambulika kwa Weusi wake, ambao maranyingi ni kutokana na kiwango kikubwa sana cha ‘’eumelanin’’ na Jua linapokuwa kali sana, nywele hupoteza ‘’Pigments’’ hizi na kuwa za rangi ya wekundu.  

Uwezo mkubwa wa Waafrika kimifupa, na misuli ‘’athletic characters’’, ni matokeo ya safari yao ndefu zaidi kutoka Kaskazini kabisa mwa dunia, mpaka kuelekea kusini, pia mitindo ya Maisha ya waafrika hawa ya uwindaji, na ukusanyaji iliwahitaji sana kuwa bora katika matumizi ya misuli, jambo lililowachochea sana kimaumbile yao. katika Q42 nimeelezea hata sifa za uimbaji sana wa miziki, hasa ya kucheza, namna kunavyohusiana na safari ndefu katika ubongo.

Kiwango kikubwa cha Testosterone kwa Waafrika, kama inavyooneshwa na baadhi ya Report, kinaweza kuzungumza kutokukua sana kwa nywele kwa Waafrika wengi wakiume. Hii ni kwa kuwa, testosterone inapokuwa nyingi, huchochea kukua sana kwa nywele za mwilini, kama vinyweleo, ndevu, n.k, lakini pia hubadilika na kuzalisha ‘’Dihydrotestosterone’’ au DHT ambayo huenda kwenye kichwa ‘’scalp’’, na kuzuia kukua kwa nywele zaidi. Wanawake wengi wa Kiafrika pia huwa na ‘’Estrogens’’ nyingi sana, ambazo ndizo huwapa maumbile makubwa, kama ya ‘’Hips, makalio, n.k.’’.

Kumbuka, hoja hizi usipokuwa msomi mzuri unaweza ziunganisha katika fikra za kiubaguzi ‘’racism’’, lakini si kweli, mbeleni tutaona namna jamii zote zilikuwa sawa kabisa awali, lakini mitindo ya kimaisha, baadhi iliwafanya kubadilika na kuathirika kiakili kabisa ‘’kama jamii baadhi za Afrika waliokuwa wakila mpaka nyama za watu’’, na wengine walibadilika sana kiafya ya mwili, kama homoni, na kupelekea vizazi vya watu wenye magonjwa mengi, wengine huko ulaya mpaka wakazamia kwenye ‘’Ushoga’’, wengine wakawa na taaluma sana na elimu, falsafa, vita, n.k.

KWANINI MAENEO YA KATI YALIKUWA NA WATU WACHACHE?

Kabla ya kukimbilia kuangalia makabila kama ya Wagogo, waliopo sana Dodoma na sehemu baadhi za Singida, ni wengi sana hawa watu, kwa takwimu za zamani sana, walizidi hadi milioni moja na laki tano, inajulikana waliathiriwa sana na utumwa. Na hata bado baadhi huamini hakukuwepo kabila la Wagogo, bali ni jumuiya tu iliyoundwa kwa jamii za wamanghala, wabambali, wayenzele, na wanghulimba, ambao walikuja kuitwa kama Wagogo, na huisiwa kuwa watu hawa walikuwa ni wakulima, baadhi wawindaji, wengine wafugaji, na wengi wao walikuwa waoga hasa dhidi ya jamii za wanyamwezi, wahehe, na wambugwe. Lakini hizi sio sababu kubwa.

Zipo sababu nyingi, kwanza kabisa, kama nilivyoelezea katika Q3 kuwa, maeneo haya ya bonde la kati, kipindi cha awali kabisa kipindi baada ya Bara la Afrika kumeguka, kujitenga toka ‘’Mid-Atlantic Ridge’’, Bara la Afrika katika maeneo ya Bonde la Afrika Mashariki, kulitokea mithili ya mikunjo iliyopelekea mabonde kama maeneo mengi ya Congo, na Miinuko ambayo ilipopasuka, ilipelekea Bonde la Ufa, ambalo, lilipoinuka lilikusanya maji mengi sana kutoka katika maji ya kutoka gharika kuu, na maji mengine yote yalisukumwa kushuka katika mteremko kuelekea katika Bahari ya India, upande wa Mashariki. Kadri maji yale yalipokuwa yakishuka, yalipelekea maeneo yote ya nyanda za kaskazini kuwa na kiwango kikubwa cha mmomonyoko wa udongo, uliopelekea udongo mwekundu, miamba ya magma, na viwango vikubwa vya madini karibia tu na usawa wa ardhi.

Lakini maji haya yalianza kuishiwa nguvu yalipoanza kufika katika ukanda wa kati, na hapo yakapelekea kiwango kikubwa sana cha Mchanga uliojaa katika maeneo mengi ya kati mwa Tanzania, hii ilichochea hali ya ujangwa katika maeneo baadhi kama ‘’Dodoma’’, manyara, n.k. na tokea maeneo haya, maji mengi yakaanza kutengeneza chaneli maalumu zilizopelekea mito mingi katika maeneo ya nyanda za juu pwani, na miji ya kati kama Morogoro.

Hivyo basi, kutokuwepo kwa mimea mingi na rutuba katika maeneo ya kati, kulipelekea wakazi wengi kutafuta makazi katika maeneo ya mbali na miji hii, maana hata Wanyama wa kuwindwa hawakuwa kwa wingi.

Lakini pia zipo sababu za karibuni za miji hii kutokuwa na watu wengi, mojawapo ni kuwa, miji hii ilitumika kama Njia, au ‘’Routes’’ za wafanyabiashara wengi sana, ikiwemo wa ‘’Watumwa’’. Na wengi wa wakazi wa maeneo haya, walisukumwa kuenda mbali zaidi. Na pia hata wengine huisi kuwa, miji hii ilijazwa na makabila ya watumwa ambao baadae walikuwa hawana tena hata makazi maalumu.

UFUPI KUHUSU MAKABILA YA TANZANIA

Pamoja na kuwa makabila mengi ya Wabantu (ambao ni karibia asilimia 95% ya Tanzania yote). kuwa ni watu walioshuka toka kaskazini kupitia mabonde ya Congo, makabila mengi ya nyanda za juu kusini ni matokeo pia ya jumuiya nyingi zilizotokea kanda za kusini, au Afrika ya kusini. Afrika Mashariki ina makabila mengi sana ambayo yaliundwa kupitia jamii za watu waliotokea ‘’Ethiopia’’, sudani, misri, n.k.  na jamii hizi nyingi ni jamii za maeneo ya Kaskazini.

Kwa upande wa Kaskazini, Hawa ni mchanganyiko wa jumuiya mbalimbali, baadhi zikiwa za wabantu na makabila mengine, mfano ‘’Batrezi’’, banyankole, banyoro, Bahaya, kuna makabila kama ya ‘Chagga’’ kupitia jina lao, wengine huthibitisha kuwa hawa ni matokeo ya ‘’Kuchanganya’’ jamii mbalimbali za bantu, pia kuna jamii za ‘’Nilotics’’ mfano, Maasai, hawa na jamii baadhi za kenya kama Wajaluo walifuata tu mkondo wa mto nile, hata kufika na kutawala eneo kubwa sana la Afrika mashariki.  

Wanyaturu pia ni wenyeji wa Ethiopia wanaoaminika kushuka chini wakitafuta nzige kutokana na njaa kubwa, wanyiramba wakitokea sudani, wakatua kanda Jirani na wakurya kwa kitambo kabla ya kushuka zaidi hata kanda za singida, na wengine wakielekea pande zingine, wabarbaig au wamang’ati ambao ni nilotics pia, walioshuka kupitia kenya hata kufika manyara, singida, n.k.

Hoja ni kuwa, wengi huwa hawajui kuwa, Jamii za Waethiopia, huwa wanaonekana kuzaa sana. Hii huwapelekea kuwa na idadi kubwa sana ya watu. Na muda mwingine huisiwa wenda, mifumo hafifu ya kuweza kuwamudu watu wao, hupelekea jamii hizi nyingi, kuendelea kushuka kutafuta maeneo yenye uhafadhali zaidi wa kujikimu. Haimaanishi hatuna jibu la kwanini, wenda watu hawa wanazaliana sana? La hasha, ila sio mada katika sehemu hii. watu wa asili ya ethiopia wengi wanaonekana kuzunguka Mashariki, na magharibi, mwa bonde la Ufa, hata na kwa upande wa kenya. Miongoni mwa wanaozungumziwa sana kwa ukanda wa Tanzania, ni makabila kama ya wairaqw (wamburu).

Ukanda wa Kalahari ‘’Namibia’’, maeneo ya manyara, Dodoma, n.k. yanahisiwa kuhusisha sana jamii za jumuiya za ‘’Khoisan’’ ambao wengi wao, ndio waliokuwa wenyeji wa awali kabisa wa mabonde mengi ya Tanzania kabla ya kusukumwa na Wabantu, waliotokea Afrika ya kati, na kasakazini. kwa sasa, wapo maeneo ya kusini mwa Afrika, lakini hata hivyo kuna makisio mengi sana juu ya uwepo wa makabila ya jamii zao, katika maeneo baadhi katika miji baadhi kati kusini.

Wabantu wengi, mfano, Wahehe chimbuko lao ni mtu aliyeitwa ‘’Mufwimi’’, alikuwa mwindaji, aliyetokea Ethiopia ‘’Kwa Mujibu wa Wikipedia’’. lakini hoja ni alitokea ‘’Kaskazini’’, akipita Kenya, kabla ya kufika Tanganyika. Wengi walimfananisha na ‘’Wakamba’’ kabila la kenya kutokana na Ukubwa wake wa mwili. Hata tu kwa Makabila makubwa zaidi matatu, yaani, Wasukuma, Wanyamwezi na Wachagga. Na kisha ukaja kuangalia na makabila mengine yote, bado utaona wote asili yao walishuka toka maeneo ya kaskazini. Tanzania ina makabila zaidi ya 125, katika haya yapo ambayo yamesogea toka nchi Jirani, kama Wamakonde wa Msumbiji, au wangoni wa Kusini mwa Afrika, lakini wote bado asili kabisa ilikuwa ni kaskazini.

Wanyakyusa walitoka kaskazini, wakipita bonde la mto nile, na inaaminika na baadhi kuwa, hata kabla ya kufika Rungwe, mpaka Malawi, waliishi pia Morogoro. Waha ni wabantu pia waliotoka Congo. Wazaramo hata neno lenyewe humaanisha, ‘’Wahamiaji’’. Inaaminika wazaramo walikuwa ni matokeo ya koo mbalimbali ambazo zilifika pwani, hata kabla ya miaka ya 1600. Na wakazi hawa wanaonekana kuweka makazi yao ya asili kabisa katika eneo la sasa, la wilaya ya kisarawe, mkoani Pwani. Mahali panapoitwa leo ‘’Mwanarumango.

Wakurya nao inaaminika walitokea maeneo ya kaskazini, ‘’Misri’’, na wabantu hawa walishuka kupitia Kenya hata kutengeneza jamii zao zilizo kenya na zilizo Tanzania, kama ilivyo kwa wajaluo, amba oni nilotics. Wakurya walikuwa na migogoro sana ya ardhi na wamaasai, ambayo inaaminika ilichochea vita zilizowasukuma zaidi wamaasai mbali na bonde la Serengeti.

KUKUA KWA THAMANI YA PESA  PWANI ZA KUSINI

Kuendesha Maisha kwa kazi ngumu za kilimo, na ufugaji. kuliambatana na changamoto kubwa sana katika maeneo mengi ya miji, ya Katikati mwa nchi. Lakini stori haikuwa hivyo katika miji hii. mtu angeweza kuchukua kitu kwa thamani ndogo eneo moja, na kisha akaenda kukiuza kwa thamani kubwa sana kwa wageni katika maeneo haya. Na akapata faida kubwa sana ya kuweza  kukidhi mahitaji yake, kutokana na thamani ndogo sana ya Maisha kwa wenyeji mpaka wakati huo.

Watu wa maeneo haya wakaanza kuwa ni watu wajanja sana wa lugha, kama tu ilivyo kwa miji mingine kama hii. kwa kuwa hiyo iliwawezesha kuunganisha pande zote mbili za mabadilishano. Watu hawa toka zamani walikuwa ni waokotaji na wawindaji, na pia, wengi wao walikuwa bado ni wavuvi. Hawakuwa ni watu wakuzoelea matumizi ya misuli sana. Lakini kwao lugha na ujanja wa kutengeneza faida bila kazi kubwa, ulikuwa mpaka mwisho. Miji hii ilikuwa na thamani kubwa sana ya pesa.

Nguvu Ya Wanawake

Tofauti na kanda zingine zote, miji hii ilikuwa na nguvu kubwa sana ya wanawake. Hii ilitokana na kuwa, awali kabisa kulipokuwa kukitokea migogoro ya kushindania maeneo, wanaume wengi wa jamii hizi waliuwawa. Na mara nyingi wanawake hawakuwa wakiuwawa, na hivyo, wengi wao walikimbilia maeneo haya ya pwani wakiwa na Watoto wao, na wanaume kadhaa. Lakini pili, Jamii nyingi za huku hawakuwa wakikumbana na changamoto nyingi za vita kupambania maeneo yenye rutuba. na hivyo, hakukuwa na kipaumbele sana cha kupata mtoto wa kiume, au mjeshi ‘’warrior’’ hii ilichochea sana kuinuka kwa nguvu kubwa ya jamii za wanawake.

Tatu, wageni wengi walikuwa ni wanaume, na mara nyingi huwa ni wanaume wanaosafiri sana kutafuta maeneo mapya, hivyo, wageni hawa walihitaji sana wanawake. Na wanawake wengi wa maeneo haya walianza kupata nguvu kwa kuweza kuchangamana na wageni waliokuwa na nguvu sana za kiuchumi, na kijamii. Nne, shughuli nyingi za pwani zilikuwa sio za kutumia misuli, zilikuwa ni biashara ambazo, wanawake wengi walizimudu vizuri zaidi, na hata shughuli za uvuvi, bado wanawake walihitajika sana katika kuwatengeneza na kuwaweka sawa Samaki kibiashara.

Mwisho, uchache wa wanaume, kukosekana kwa nguvu dume za kiutawala, na uwingi wa nguvu za wanawake kulipelekea wanawake wengi kutumia akili sana kuwapata wanaume. Wanawake walikuwa wakiwalinda zaidi wanaume zao. Na huu ndiyo mwanzo wa sanaa nyingi za miziki ya kuwateka wanaume kwa kuwaliwaza, na taaluma za kuwateka wanaume, kwa wanawake wengi wa pwani.

Saikolojia ya Usaliti na Ukoloni

Wakoloni wengi kabla ya kushambulia ngome kubwa za maeneo ya ndani ya nchi. Walihitaji sana wapelelezi. Wapelelezi walihitaji sana wafanyabiashara wenyeji wa awali kabisa ambao, nao walikuwa chini ya jumuiya zao kadhaa. Hawa waliwasaidia sana kuelewa ramani nzima ya ngome kadha wa kadha. Maana walikuwa tayari na uzoefu na miji yao.

Kwao hii ilikuwa bado ni namna ya biashara. Kumbuka, tabia hii  ilifanywa na karibia jamii zote zilizokuwa dhaifu, waliungana na wakoloni ‘’allies’’. kwa lengo la maslahi baada ya kushinda. Falsafa hii iliendelea kwa maeneo kadha wa kadha hata baada ya uhuru, bado wengine waliendelea kupendelea maslahi kwa ujanja ujanja wa kibiashara.

UCHAMBUZI KWA UFUPI JUU YA TABIA ZA WATU WA ENEO HILI

Watu hawa kwa kipindi kirefu sana wamekuwa sio watu wa kufanya kazi ngumu. Ni watu wa kufanya kazi zisizotumia sana nguvu za misuli kwa wastani. Mfano, kufanya biashara aidha kwa kukaa, kutembeza, kutumia usafiri mfano, kutumia wanyama, n.k.  bado walikuwepo wavuvi, wasanii, wafasiri, wapishi, n.k.

kiwango kidogo cha matumizi ya misuli kilienda sambamba sana na kiwango kidogo sana cha hamu ya kula vyakula vya nishati, na hata pia vyakula vingi vya wanga vilikuwa havilimwi katika maeneo haya, vilitoka mbali sana na vilipatikana zaidi kwa  gharama. Hizi sababu zote kwa Pamoja zilichochea utumiaji wa vyakula vyenye sukari sana, na vyenye msisimko sana. Ili ku ‘’boost’’ hamu ya kula zaidi.

Inafahamika pia kuwa, wasafiri wengi sana huwa si wapenzi wa ubebajii wa vyakula vizito, ambavyo vinaongeza mizigo, na viwango vyake vikubwa vya maji, huongeza uharaka wa kuharibika. Na sasa basi, wasafiri wengi hupenda vyakula vyenye sukari nyingi, ili kutumia kiwango cha chakula kidogo, na kupata nishati nyingi ‘’calories’’. Pia, vyakula vya asili ya kukaanga, na kukausha, huweza kukaa kwa muda mrefu sana bila kuharibika. Na taaluma hizi zote zilizidi kushamiri maeneo ya pwani, wapishi wengi iliwapasa kuiga kwa dhumuni la biashara.

Vyakula hivi kwa ujumla vina kiwango kidogo sana cha maji, vipo ‘’concentrated’’, na hivyo, vina kiwango kikubwa sana cha ‘’msisimko’’ au ‘’stimulant effect’’. Matumizi ya chumvi kuzuia kuharibika kwa chakula, nyama za kuchoma, vyakula vya kukaushwa, vichochea Ladha vingi, n.k. yalishamiri sana.

Kumbuka kabla ya kuendelea tumeshaona katika Q4 kuwa, matumizi ya vyakula vyenye tabia za kusisimua sana ulimi na ubongo kama hivi vya kukaanga, sukari, viungo vya vyakula, ambavyo vingi huku vilikuwa vikitokea nchi za India, na uarabuni. n.k. huwa vina virutubisho vichache sana. Kwa kuwa, uandaaji wake huaribu virutubisho vingi sana.

Pia, kiwango kikubwa cha sukari tamu, ambayo huwa ni chembechembe za ‘’fructose’’ kwenye vyakula hivi, huathiri kabisa mwili, kwa kujaza sana mafuta katika maini, huathiri chembechembe za seli za kuzalisha nishati zinazoitwa ‘’mitochondria’’, kwa kuua watenda kazi wake ‘’enzymes’’, kama ‘’AMP Kinase1, CTP, n.k. na pia, matumizi sana ya bidhaa ya nyama za kukaanga, na bidhaa zingine za kukaanga, huathiri ukuta wa utumbo, ufyonzwaji wa virutubisho tumboni, viungo vya vyakula huua sana bakteria wazuri wa tumboni, huathiri utendaji wa kijenetikia. Na katika ubongo, vyakula hivi huchochea sana uraibu.

Hii ni kwa kuwa, chembechembe zile za utamu ‘’fructose’’ huenda kusisimua sana sehemu ya ubongo ya uraibu, ambapo hata madawa ya kulevya kama ‘’heroine, cocaine, na nicotine’’ huenda kuisisimua, sehemu inayoitwa ‘’Nucleus accumbens’. Sasa basi, uraibu wa vitu hivi vya tamu tamu, kwa watumiaji wa bidhaa hizi, huwa ni ngumu sana kuviacha, na huzidi kuvitamani hata wanaposhindwa kuvimudu. Hii tayari huwazidishia kutumia kila mbinu ya ujanja aidha wa lugha, au biashara, ili kupata faida waweze kurejelea katika maeneo yaleyale ya uraibu.

Maeneo mengi sana katika miji hii huwa tayari yakimilikiwa, na gharama za kuyanunua huwa ni kubwa sana. Tatizo hili huwafanya watu wengi wa maeneo haya, kushindwa kumudu kupata makazi, na njia pekee, huwa ni kutafuta maeneo duni yasiyo na gharama, na kuweka makazi yao dhaifu, na maeneo haya huwa na watu wengi sana, na huwa na miundombinu dhaifu sana.

Hali hii huwafanya kuwa ni wahanga wa virutubisho vya muhimu kabisa katika afya. Hii ndiyo sababu, kama ilivyo kwa miji mingine duniani ya kuifanania miji hii, milipuko ya magonjwa inapotokea, huwaathiri watu wengi sana. Kutokana na hali duni tayari za afya za wengi wa watu hawa.

Ulaji mbaya, makazi mabaya, na kushindwa kupata hali bora za Maisha kama za watu wengi ambao tayari wanamiliki hali za juu kabisa za Maisha, hutengeneza msongo wa Mawazo, hali za kutamani bila kuweza kumudu, na zinginezo. huamasisha sana matumizi ya madawa ya kulevya, au bidhaa za kulevya kwa watu hawa. Kijana ambaye asingeweza kumudu kuendesha familia yake, na asiwe na uwezo wa kuondoka maeneo haya, hujikuta hata familia yake tu ikimshinda.

Suluhisho pekee la kutatua tatizo hili, ni kujisahaulisha. Hapo ndipo kukaibuka matumizi sana ya pombe, sigara, kupenda starehe za gharama ndogo, miziki ya kupumbaza ubongo kama bendi mbalimbali za zamani kabisa, na wakati mwingine, hata baadhi walianzisha vikundi vya awali kabisa vya ugaidi na ujambazi, na wengine  wakaanzisha biashara za kikahaba kama za kujiuza.

KUSHAMIRI KWA URAIBU WA NGONO NA MAPENZI

Zipo sababu nyingi sana. Kwanza, matumizi hafifu sana ya misuli, kutumia sana vyakula visivyo na nishati bora kwa mwili, vyakula vyenye mafuta mengi hasa vyakukaanga, kuishi sana katika jamii zenye mchangamano wa wakati wote na wanawake wenye malengo ya kuwatega wanaume, haya na mengine mengi yalipelekea idadi kubwa sana ya wanaume kupungukiwa nguvu za kiume.

Kadri matatizo haya yalivyozidi kushamiri, taaluma mbalimbali na vyakula vya kutatua tatizo hili vikazidi kushamiri. Matatizo haya yalichochea falsafa mpya ya kuwa, heshima za wanaume wengi zinazidi kupungua kutokana na kupoteza uwezo wao wa asili.

Tatizo!! Wasomi wengi wanachanganya kwakuhisi mara nyingi shida huwa ni nguvu za kiume, lakini ukweli ni kuwa, shida huwa ni kuathirika kwa tabia za kiume. Hii ni kwa kuwa, madhara yote yanayopelekea kuathiriwa kwa nishati ambazo mwanaume anazihitaji, huaribu utaratibu wa kudumu wa wastani wa homoni za kiume. kwa kushamiri kwa mafuta na ‘’estrogens’’. kutokana na mitindo mibaya ya chakula na maisha.

Huwaondoa wanaume kutoka hali yao ya kupuuzia vitu na shida kwa asili ‘’stoic philosophy’’, na kuwafanya kuwa ni watu wa kujali na kuumia hata kwa vitu vya kijamii, sifa ambazo sio za kiume kwa asili. Wanaume wa maeneo haya kwa mara ya kwanza wakaanza kufanya ngono kwa lengo la kijamii sasa!! Afanye ngono kuzidi wenzake, au mpaka amridhishe mke wake, au kuzidi alivyokuwa awali!! Sababu hizi na nyinginezo zikaanza kuchanganya saikolojia ya ngono, na maisha kwa ujumla.

Malezi dhoofu marazote hupelekea Watoto na vijana wadogo kuanza kushiriki katika tendo la ndoa kabla ya utu uzima. Hili kama tulivyoliona katika Q5, hupelekea mvurugano wa mfumo mzima wa hisia na kujitawala katika ubongo. madhara yake ni kuwa, vijana hawa wanapofikia wakati wa ndoa, huwa tayari wana uwezo mdogo sana wakuwa waaminifu katika ndoa zao, hii ni kutokana na athari zilioathiri utendaji wa ‘’Oxytocin- katika social bonding’’ katika mahusiano ya awali kabisa.

Na sasa basi, ugumu wa Maisha na idadi kubwa ya watu, viliwapelekea wanandoa hawa kusalitiana pale zinapotokea changamoto kubwa za kiuchumi, au kijamii, katika ndoa zao. Hii ni kwa kuwa, tayari uwezo wao wa awali wa uvumilivu katika mapenzi wengi wao walishauathiri. Hii inaletaje shida? Vijana hawa huwa na shida nyingi sana za mahusiano, mapenzi, na usaliti. Na pale inapotokea nafasi ya kuwasilisha hisia zao kama kupitia miziki, basi huwasilisha sana machungu yao, hiki ni kielelezo cha kutumika sio tu katika miji ya pwani hasa za kusini zenye idadi kubwa sana ya watu kwenye eneo dogo, bali hata na maeneo mengi yenye tabia hizi.

Msingi wa Tabia Za Uchafu Katika Ngono

Ijapokuwa wengi hawatambui msingi wa sababu za tabia kama za ushoga ‘’homesexuality’’, na mapenzi hata kwa kutumia kinywa ‘’oral sex’’. Katika miji mikubwa kabisa ya awali, kama miji ya Sodoma, Ugiriki, Fransisko, Miami, New York, Paris, n.k. miji hii ilikuwa ina asilimia 100% ya mitindo yote ambayo kwa maeneo haya ninayoyaelezea bado sana kuyafikia, japo inaelekea. Mitindo mibaya ya namna niliyoielezea, yote ilianza katika namna ileile ya wageni, biashara, ugumu wa Maisha, uraibu, na utumwa.

Hawa watu waliishiwa kabisa nguvu na tabia za kiume. Na suluhisho la kuendelea kupata msisimko kupitia uke, haikuwezekana. Hii ni kwa kuwa, msisimko endelevu wa kihisia, hasa kupitia kutazama taswira za mihemko ya kihisia, huufanya ubongo kupunguza mhemko wake kwa hisia. Hii ni ili kuzuia, kushtushwa shtushwa na hisia.

Idadi kubwa ya wanawake wanaojirahisisha kwa ngono, huongeza idadi ya wanaume wanaofanya zinaa, wanaume hawa wakati huo huo wapo katika mazingira wanayopata lishe dhaifu, na makazi hatarifu. Hii huufanya Ubongo kupunguza msisimko wake katika mapenzi ‘’brain receptors desensitization’’, ambapo, kwa matendo yaleyale sasa mtu hasisimki tena kwa kiwango kikubwa.

Sasa ili mtu asisimke tena, suluhisho ni kutumia sensa chache zilizobakia  ‘’sensory receptors’’, kuzisisimua sana, mpaka mwisho, ili ubongo uweze kupata msisimko sawa na ule wa zamani ulipokuwa mzima. Na hapa sasa, hutumia sehemu za nyuma ya maumbile ambazo huwa ni ngumu sana, na hivyo,  huweza kusisimua sana uume. Lakini pia kutumia mdomo ambao nao una uwezo wa kujishepu kutengeneza msisimko mkubwa, huweza kusisimua. Kwa kufanya hivi, watu hawa wasio na nguvu za kiume, hujihisi kusisimka tena.

Kwa upande wa wanawake ambao wao fiziolojia yao ya ubongo mara zote, hukinzana na kusisimka mpaka mwisho, pale wanapokuwa hawako na wanaume wanaowaamini, kutokana na sehemu yao ya ubongo inayoitwa ‘’Anterior cingulate cortex’’ kutojizima ‘’shut-off’’, kwao pia namna ya kujiridhisha huwa kupitia, matumizi ya madawa, usisimuwaji wa Clitoris kwa kutumia viungo vingine kama vidole, na haya yote ni matokeo yanayotokana na ubongo wa watu baadhi walioathiriwa sana, wa miji ya namna hii kama Miami au Paris, kutokuwa sawa.

MSHAMBA AKIFIKA MJINI

Kama ilivyo kwa dawa za kuzuia maumivu kwa wagonjwa wa saratani, ‘’opioids’’ zinapotumika kwa watu wasioumwa, huwa ni madawa ya kulevya yenye mhemko mkubwa sana. Ndivyo ambavyo huwa kwa watu wote ambao hawakuwa waathirika, na kisha wanapofika katika maeneo haya kwa mara ya kwanza. Kukutana na misisimko mikubwa sana katika kila tendo, katika kila hisia. huwafanya kuwa ni waraibu wa ghafla, na tena, kwa kiwango kikubwa zaidi.

KUKUA KWA USANII

Miji yote mikubwa hushamiri sana kwa usanii. Ugumu wa Maisha ya jamii, na uchache wa fursa za nje, husukuma sana matumizi ya vipawa vya ndani katika kutengeneza fursa. Msingi wa usanii mara nyingi huwa ni upekee. wasanii hupata nguvu sana katika jamii kubwa za watu, kwa kuwa, mara nyingi miziki huwa na uwezo wa kuzungumza na kufariji watu kwa lugha zote mbili, lugha ya maneno, na lugha ya hisia. Uchakataji wa muziki katika ubongo huusiana na uzalishwaji wa homoni za msisimko, hasa dopamine.

Lakini ili muziki ukue unahitaji usikilizaji uliolengwa kibiashara zaidi, na sio kutuliza tu hisia za watu. Na kwa namna hiyo, utumiaji wa midundo ‘’drums’’, na ala zinginezo, tena kwa mapigo ya haraka haraka, na mengi kwa wakati mmoja ‘’polyrhytms’’,  huchochea sana uzalishaji wa dopamine kwa kiwango cha kupelekea uraibu. Unaweza rejea Q4, sehemu ya sayansi ya ubongo ya muziki.

Muziki wa mtindo huu ambao huchochea sana kupumbazwa kwa ubongo kama tulivyoona namna urudiaji rudiaji wa mabiti kwa kiwango kikubwa sana, huathiri utendaji wa sehemu ya mbele ya ubongo, matokeo yake huwafanya watu kuwehuka kihisia. Hupelekea hisia za kucheza, huchochea kupungua kwa stress, na huu ndiyo msingi wa watu kununua na kununua zaidi muziki.

Kadri muziki unavyohusisha zaidi visa vya kijamii, ndivyo unavyopata mashabiki wengi zaidi. Miji hii mingi kutokana na urahisi wa usafirishaji, mawasiliano, na biashara, ilishamiri kwa haraka sana kuweza kupata vifaa vya awali kabisa vya uundwaji bora zaidi wa muziki wa kisasa.

 

UGENI NA UVUNJIFU WA MAADILI

Miji mingi tokea awali sana ndiyo iliyohusisha sana matumizi ya usiku kwa shughuli za siku. Tokea matumizi ya taa za mafuta, mpaka taa za umeme kwa kila mji, miji yote ilihusisha sana matumizi ya usiku. Wakati wa jioni miji mingi sana ya pwani ilihusisha watu toka maeneo mbalimbali kuelekea maeneo ya kingo za Bahari, kubarizi.

Kadri watu walivyokuwa hawafahamiani, ndivyo pia watu walivyokuwa huru zaidi kujiachia bila kubanwa na sheria za maadili, ambayo, kadri unavyokuwa mzawa, ndivyo unavyofatiliwa sana utovu wako wa kimaadili. Hivyo wageni wengi, wa mbali na karibu, walijikuta wakiwa huru sana katika Kutenda matendo yasiyo ya staha kabisa katika miji hii. jambo hili liliwaathiri sana Watoto wa maeneo haya. Ambao kwao, hapa ndipo palikuwa nyumbani.

Kadri siku zilivyoendelea kusonga, vijana hawa wengi wakakua wakiwa wamezoelea matendo haya ya uvunjifu wa maadili. Hii ilihusisha matumizi ya lugha chafu, matendo machafu, mionekano mibaya, na kuiga matendo ya nje yasiyo mazuri kimaadili. Unaweza kurejea Q4 kuelewa zaidi msingi wa mmomonyoko huu kisaikolojia.

UTANGULIZI

Hakukuwa na  namna ya kuelezea ufupisho wa kitabu hiki bila kutumia kisa juu. Kisa hicho ni sehemu ndogo sana inayoweza kukuonesha kuwa, misingi ya tabia nyingi sana katika jamii yoyote ile. Uharibifu wa kitabia katika jamii yoyote ile. Unaweza kuwa na historia yenye sababu pana sana. Hii ni kusema, kwa mtafiti au msomi wa kawaida, ni ngumu kuelewa! Na ni rahisi kusema kuwa, watu Fulani huonesha sana tabia Fulani, kutokana na jambo moja Fulani. huu huwa ni udhaifu sana wa kujifunza misingi ya tabia Fulani, kwa lengo la kuwasaidia watu. Tabia hazitabiriki, hii  ni kwa kuwa, utokeaji wake huwa una mnyororo mrefu sana.

Kama ungekutana na mtu anayeonekana yupo timamu  kabisa barabarani, aidha kwa namna anavyoonekana na hata kimavazi, lakini anaonesha kuchanganyikiwa huku akilia! Sio busara kusema mtu huyu ni kichaa kwa kuwa anaonyesha tabia isiyozoeleka, busara ni kufuatilia historia yake kwa ufupi mpaka alipofikia hatua hiyo. Na huo ndiyo msingi wa matibabu yote ya kidaktari, huanza na ukusanyaji wa historia.

Natambua ni vigumu sana kwa mtu mmoja kuweza kuzoelea taarifa nyingi sana kuhusiana na watu, Historia na mazingira yao, na fiziolojia zao, hata akafikia kiwango cha kukaribia kuelewa kabisa  sababu za misingi ya matatizo mengi ya kitabia , na hata hali zao. Lakini hata hivyo, inawezekana kwa neema za Mungu, kwa kuwa, Mungu hataki yeyote apotee.

Kitabu hiki ni matunda ya Upendo wa Mungu. Katika kitabu hiki tutajifunza kiundani kwanza kabisa, sababu za msingi za awali kabisa za hali za kijamii kwa kila eneo, kisiasa, kiutamaduni, kimazingira, kiimani, na kiuchumi.

Baada ya msomaji kuelewa sababu za msingi kabisa za msukumo wa hali na tabia yake, na ya jumuiya yake. Lengo sasa la mwandishi litatimia la kuweza kueleza ni kwa namna gani inawezekana sasa, kucheza na jamii yeyote ile kama inavyochochewa na wataalamu wachache, ambao hata na wao kwa wakati mwingi hawajielewi. Lakini wanashiriki katika kukamilisha haya, ambayo yamelenga zaidi katika uharibifu wa hali na tabia za binadamu wenzao. Kisa cha Pentagon mwanzoni kabisa kilihusisha ubainifu wa hali kadhaa zisizo za kawaida, uchambuzi zaidi tutauangalia kwa sehemu za mbele.

Kumbuka pia kuwa, Kama kuna jambo limekuwa likileta changamoto kubwa sana kwa wasomi wengi, ni maamuzi binafsi ya watu ‘’free will’’. Watu hawatabiriki. Maamuzi ni siri ya mtu isiyotabirika. Kama kuna jambo linaloibua hisia za maumivu sana, ni pale watu baadhi wanaposemwa kuwa wana uwezo mdogo wa kuzaliwa, katika kufanya maamuzi yao. Ubora wa maamuzi ya mtu, hupimwa kwa matokeo ya anachoamua. Matokeo hafifu, duni, na ya kudharaulika kwa baadhi ya vikundi vya watu, mara zote huwasukuma baadhi kuwadhania watu hao ni dhaifu kwa asili. Na huu ndiyo mgogoro mkubwa sana wa hisia za ubaguzi ‘’racism’’.

Siri ya nguvu kubwa iliyojificha nyuma ya kila tabia, na inayosababisha kila tabia ya mtu, na jamii yake, imekwisha elezwa na wataalamu wengi sana wa sayansi za tabia. Kitabu hiki kina ajenda kuu moja, Tabia nyingi za ajabu za watu huwa zikihamasishwa, na hata kutengenezwa. Tabia hizi hazitengenezwi na sababu moja, zinatengenezwa na vitu vingi sana. Ambavyo, Pamoja na uwingi wake, bado kuna sababu zilizo na nguvu zaidi. ambazo kwa hizo, baadhi ya watu huzitumia kwa faida yao kuwaathiri wengine. Idadi kubwa ya watu hudharau kutawaliwa kimwili na kifikra, lakini muitikio wao huthibitisha zaidi kuwa wao ni mateka mahututi kabisa.

Hakuna uwezo mkubwa wa watu baadhi katika kufanya lolote lile zaidi ya wenzao kwa kila wakati. mara zote uwepo wa sababu za kina huwa ndiyo msingi wa tabia Fulani. matokeo yanapokuwa yakionekana mara zote, huwa pia kuna sababu. Uharibifu pia, huwa una sababu. kitabu hiki kinarejelea historia nzima ya dunia mpaka ilipofikia kwa mtazamo mpya kabisa ambao haujawahi zingatiwa.

Historia ndiyo nguzo pana zaidi ya kujifunza sayansi tena zaidi hata ya fiziolojia, Jiografia ndiyo maabara pana zaidi ya kujifunza sayansi zaidi mara elfu ya maabara, inahitaji uwezo mpana sana wa kujifunza katika mazingira yasiyotabirika, kuliko mazingira yaliyotabirika, kama mazingira ya katika utafiti wa kawaida wa kisayansi.

Kupitia kitabu hiki msomaji ataelewa kwanini kila bara duniani lina watu wenye hali na tabia hizo walizonazo, msomaji ataelewa kwanini wengine wanaonekana kuwa na mafanikio zaidi ya wengine, msomaji ataelewa kwanini wengine wanaonekana kuwa wadhaifu au tabia Fulani kuliko wengine, lengo hapa halitakuwa kujifunza historia. Lengo ni kuanza kujifunza kusoma sababu za hali mbalimbali za watu, ili iwe rahisi sasa kuelewa lengo kuu la mwandishi la kwa namna gani, kwa kuiga utaalamu huo kushepu hali na tabia, sasa unaweza kutengeneza tabia za hovyo kabisa, na hali ngumu zaidi kwa watu, tena kuwatawala kabisa kifikra kama inavyoendelea hali hiyo sasa hivi.

kupitia mlinganyo kielelezo uliotengenezwa kwa logic pana zaidi kutokana na elimu za tabia. B(p) = Eqm ± . Tutatazama ni kwa namna gani, kama ambavyo ni rahisi kwa miaka mitano tu ya awali ya ukuaji wa mtoto,  inavyowezekana kuweza kumtengeneza awe mpenda kazi, au mvivu. Basi pia kwa kipindi cha miaka kumi tu, inawezekana kutengeneza kizazi kilichoharibika kabisa.

UPEKEE WA KITABU

Kipa hajawahi kuwa sehemu kubwa ya mchezo uwanjani, lakini amekuwa ni mwamuzi mkubwa sana wa matokeo ya mechi. Kipa huwa na mpira kwa wakati mchache zaidi ya mchezaji yeyote yule. Kipa anapokuwa na muda mwingi zaidi na mpira zaidi ya wachezaji, basi ujue mpira umekwisha, na ni matuta ya penati sasa. Mpira ni Maarifa, wachezaji ni sehemu yenye watu wengi zaidi duniani, ambazo ni sehemu za Bara la Ulaya, na Asia. Makipa ni sehemu za watu wachache sana duniani, ambao ni Marekani, na Afrika. Kipa wa  marekani ameshapoteza mpira katika nafasi yake. Kipa pekee aliyebakia kutegemewa kwa ushindi, au Nuru ya Maarifa,  ni Afrika. Kama Waafrika tutaipoteza nasi nafasi hii, basi hakutakuwa na nafasi zaidi ya ushindi kwa maarifa.

Kumbuka, hakuna nafasi ya kucheza zaidi ya Matuta ya penati. Hakuna nafasi ya kuelewa zaidi maarifa, zaidi ya namna hii inayotumika katika uandishi huu. Msomaji yeyote hata aliyesoma soshiolojia, fiziolojia, ethnobiolojia, na anthropolojia za watu wote duniani, bado hajui vingi tutakavyoviangalia humu. lengo ni kushinda hisia za uovu, na kuinuka, na kuokoka kutoka katika madhara yote ya kutuangamiza.

Kwa miaka maarifa yamekuwa yakitegemewa kutoka kwa watu wenye sifa na nafasi kubwa sana za kuheshimika, lakini sasa ni wakati wa makipa, wachezaji wote wamekwisha shindwa. Sitatumia muda mwingi kuelezea wasifu wa mwandishi, maana makipa wote huvaa namba dhaifu au ndogo zaidi katika timu. lakini ndiyo huwa na muda mwingi zaidi wa kuiangalia mechi toka inaanza, kumbuka! hakuna kipa aliyewahi kushinda ‘’ballon D’or’’ au tuzo ya mchezaji bora.

SHUKURANI

Mungu alituamua tuwe Waafrika tutakaotumika katika dakika za jioni kabisa kusaidia jamii zetu, maana mimi kwa mfano, sikuwahi chagua kuzaliwa nilipozaliwa, wala katika familia niliyozaliwa. Kwa kazi zote ntaendelea kumshukuru kwanza Yeye Mungu wetu. Uandishi wa kitabu hiki ulichochewa tokea nikiwa mdogo sana na Baba yangu, Marehemu Godwin Efraim Shoo.

Alikuwa na Vitabu vingi sana, ambavyo Pamoja na kutengeneza Library ‘’maktaba’’ yangu binafsi chumbani kwangu, nikiwa darasa la Tano, bado vingi sana vilishamiri katika kila kabati nyumbani, nilivisoma vitabu karibia vyote. Vitabu vilishamiri aina nyingi sana za taaluma, na historia, na stori. Vingi nilizidi kuvielewa zaidi kadri muda ulivyosonga. Lakini kikubwa zaidi, nilipokuwa mdogo nikijifunza kusoma vizuri, Baba yangu alinizoelesha kutumia Biblia kama kitabu cha kujifunzia kusoma, siwezi kusema niliisoma Biblia yote, ila ninachokumbuka stori zake zilinifanya niisome sehemu kubwa sana, popote palipo na stori, kasoro Ufunuo wa Yohana, na pale vinapozungumziwa vizazi vya watu.

Nilipopata tu Nafasi ya Kwenda kusoma Shule ya Sekondari, nikapewa nafasi ya kuwa ‘’Librarian’’ au ‘’Mtunza maktaba’’ wa kwanza kabisa, kwa maktaba ambayo haikuwahi tumika kwa miaka mingi sana, maktaba ilikuwa nzuri sana, japokuwa vitabu vyake vingi havikuwa vya kiwango cha ‘’ordinary level’’, lakini kumaliza kwangu syllabus kabla ya wakati, kulinipa muda mwingi sana wa kupitia vitabu hivi vizuri.

Waadventista wasabato japo ni watu wakawaida sana, ila wana maarifa makubwa sana. Nilipokuwa kidato cha Pili, nilipata nafasi ya kujifunza zaidi nao, nilisoma vitabu vyao vingi sana, hasa vya Ellen G. White, nilipendezwa sana nao hasa kutokana na uwezo wao mkubwa wa kuelewa vitabu vyote vya Biblia ikiwemo na Ufunuo wa Yohana, na Danieli, tena bila kukinzana kimaarifa popote pale katika Biblia yenyewe na ukweli wa kila Nyanza, kama sayansi, historia, na falsafa. Tofauti kidogo na wengine, ambao kuna wakati huacha baadhi ya maswali kwakuwa na majibu ya mitazamo binafsi, Nyumbani kwa asili Baba alikuwa ni Mlutheri, na mama alikuwa ni Mkatoliki. Walinizoelesha kujifunza Biblia, na walinipa Uhuru wa kuamua Imani yangu kwa uhuru.

Unapokuwa mwanafunzi na unapenda sana sayansi, lugha, Jiografia, na Historia. Watu huisi utabadilika tu uendeleavyo kuchagua fani mojawapo. Lakini stori huwa haipo hivyo marazote, hata Pamoja na kuendelea na PCB kwa ‘’A-level’’, lakini bado nilitumia muda sawa pia na kwa Jiografia, Historia, Siasa, Jamii za Siri, na Biblia. Changamoto kubwa niliyoipata ilikuwa tu ni kuweza kujifunza sana ‘’Advanced Mathematics’’ kwa kuwa, Baada ya kupata nafasi ya Kuendelea na masomo ya Chuo Kikuu katika fani ya ‘’Veterinary Medicine’’, bado ilinibidi nijifunze zaidi ‘’Modern Theoretical Physics’’, jambo lililonigharimu sana, lakini hata hivyo nilifanikiwa kwa kiwango cha msingi wa kimaarifa.

Veterinary Medicine ni fani ambayo kwa haraka naweza sema, inampatia mwanafunzi wake upana zaidi wa kuelewa sayansi za afya na maisha. Hii ni kutokana na namna masomo yake yanahusisha uchambuzi wa kina sana wa kila kiumbe, kuanzia wadogo kama minyoo, virusi, fangasi, protista na bakteria, kisha Wadudu kama viroboto, kupe, nzi, mbu, n.k. kisha Wanyama wadogo wa porini kama Nyoka, panya, sungura, konokono, n.k. kisha makundi kwa makundi ya Wanyama, utajifunza paka, mbwa, nguruwe, punda, farasi, ngamia, kuku, mbuzi, kondoo, ng’ombe, Samaki. utasoma wanyamapori kama simba, tembo, twiga, viboko, faru, swala, nyumbu, pundamilia, na tena kwa aina zao, Wanyama hao unapokuwa unajifunza, utajifunza kwa wastani wao na Binadamu. Kuna masomo ambayo utajifunza moja kwa moja kumhusu binadamu, kama ‘’afya ya jamii’’. 

Taaluma hii bila kuficha, hutoa msingi mpana zaidi wa kuelewa sayansi zote za misingi ya afya na maisha, kuanzia viungo ‘’anatomy’’, fiziolojia, Utendaji wa magonjwa ‘’patholojia’’, madawa, vyakula, vimelea vyote, jenetikia, teknolojia za kisasa, upasuaji, mionzi, n.k. kitu pekee ambacho hautakipata, ni ubora mkubwa wa kitabibu! Hii ni kwa kuwa, hautakuwa na muda wa kutosha na kiumbe mmoja mmoja, au uamue kuwekeza ‘’specialize’’ kwa Wanyama baadhi tu.  hii nimeisema ili kuonesha ni kwa namna gani, asili ina malengo yake katika machaguo yake.

Mfumo wa elimu husaidia sana kuwatembeza watu maeneo mbalimbali nchini, na hata nje ya nchi. Lakini hauwezi jua maeneo yote kwa kuyafika, ila kwa kuongeza uwezo wa kuzingatia. Namshukuru sana awali kabisa Baba yangu mkubwa ‘’Frank Mmary’’ huyu ni mtaalamu wa ‘’Anthropolojia kwa kuijua nchi nzima ya Tanzania, na Afrika’’. Ametembea vyakutosha, na anajua vya kutosha, alinipatia Courses kadhaa katika kujifunza ‘’soshiolojia’’. Namweka sambamba kabisa na ‘’Prof-Jared Diamond’’, huyu kwangu ni wa muhimu sana. Siwezi kuficha kutumia sehemu yake kubwa sana ya tafiti zake, lakini nasikitika kuwa hata na yeye bado kuna vitu alichanganywa pia, lakini kupitia kitabu hiki, sehemu kubwa itafahamika kwa vizazi vijavyo.

Kila msomi anapokuwa hajui, huwa anatengeneza Imani ‘’Hypothesis’’, ambayo atakuwa akitenda kuitegemea. Na huo ndiyo msingi wa Ubongo, hata kama unajenga jengo ambalo hujawahi lijenga au liona, huwa unatengeneza kwanza taswira yake kichwani, kupitia network za ubongo zinazoitwa ‘’Default mode network’’. Wanasayansi wengi hutengeneza Imani kwanza katika nadharia ya ‘’Evolutionary science, na Big Bang’’, hasa pale wanapokuwa hawajui. Na hapo ndipo panapowafanya ‘’average minded’’, Kitabu hiki kinatumia sayansi kujifunza. historia na falsafa zote, zimejikita toka kwa Biblia, na Rekodi za uhakika, sio mamilioni ya miaka ya Radio-Carbon datings, nilishaeleza katika Q1 na Q3, hazina uhalisia katika vipindi virefu hizi mbinu .

Labda wengi hawaelewi kuwa, Baba wa Sayansi mara zote huitwa ‘’Isaac Newton’’ na ‘’Galilei Gallileo’’, hawa wote nao waliweka Biblia kama mimi ninavyofanya, siyo hivyo tu, sidhani kama kuna majitu yaliyokuwa ‘’technical’’ kama ‘’Nikola Tesla, Leonard Da Vinci, na John Von Neumann, wenda na wengine wasiopo katika rekodi, lakini wote walisema nilichosema.

kinachowashangaza wengi juu yangu leo, ni kwanini niiweke Sayansi mikononi mwa Mungu! Na mshangao huu ndiyo ulioifanya sayansi ianguke mpaka leo hii hakuna jipya, hata zaidi ya 80% ya tafiti zote ni matokeo ya kukopi na kupesti kazi zilizokwisha fanyika, hakuna nadharia mpya iliyo bora, tuzo za sayansi mwaka 2024 mfano zote ni matokeo ya Chat GPT au Roboti, Ubongo wa wengi umeishiwa kabisa Nguvu. hakuna kitabu unachoweza linganisha na Biblia linapofika swala la Maarifa, na ndiyo maana, hata kwa mwanasayansi kipenzi wa wengi ‘’Albert Einstein’’ ambaye ilionekana kana kama hana Imani kwa ‘’Mungu na Biblia’’ kutokana na Uyahudi wake, falsafa za kutoka katika nadharia yake ndiyo imechochea kuiua sayansi, haina matumizi makubwa maishani, ni ngumu kwa wasioielewa, na hata hivyo, ni sahihi kabisa kwa maelezo ya walioifanyia kazi kabla yake, wakina ‘’Poincare, na Lorentz’’, kabla ya yeye kuikopi ‘’plagiarize’’ na kuipa tafsiri zake, na kufanywa ‘’hero’’ kwasababu za siri sana.

Kumbuka, wanasayansi wasio makini huisi ni Imani za kufikirika kupaa kwa Yesu kinyume na matokeo ya ‘’gravity’’, lakini wanasayansi makini wanatambua fizikia bado ina miujiza mikubwa zaidi ya kupaa kwa yesu, kama asili ya kani ya gravitation ‘’unawezaje kutengeneza gravitation’, bado kuna ‘’three body problem’’,wanabiolojia wanatambua hakuna muujiza mkubwa duniani zaidi ya chembechembe zinazounda ubongo ‘’molecules’’  kutengeneza utambuzi ‘’consciousness’’, wanakemia wanatambua hakuna muujiza kama namna maelfu ya chembechembe, na kani zilivyo katika balansi yenye usawa wa asilimia 100%, bila kosa hata la 0.01 unit ambalo lingepelekea kusiwepo uhai, wanajiografia wanatambua hakuna muujiza kama namna ilivyo sayari ya Dunia tu, kati ya matrilioni ya sayari na nyota, yenye sababu matrilioni kusapoti Maisha. na wanahistoria wanaoana ni muujiza sana kila taarifa inayotokea, ilishanukuliwa na Biblia, na Biblia ndiyo msingi wa Maarifa ya kweli na uhai.

VITU VYA KUZINGATIA KATIKA KUSOMA

Kitabu hiki hakina msingi wowote wa kuonyesha kuwa kuna kundi Fulani, ni dhaifu kuliko kundi lingine. Hayo yanaweza kuwa ni madhara ya kusoma juu juu. Mfano, kwa kisa pale juu, kwanini kulikuwepo na makabila dhaifu? Utakaposoma zaidi huko chini, utaelewa kuwa, hawakuwa dhaifu, ila mfumo wao uliwafanya, na sasa kujua mfumo wao, unapaswa kujifunza zaidi.

Kitabu hiki kitatoa ufupisho sana wa mada za historia za mazingira, na tabia za jamii Fulani. hii imelenga katika kupunguza ukubwa, na kumchosha msomaji, historia tu ya Kijiji kimoja ingeweza kuhitaji kitabu kizima, vipi kuhusu dunia? Na sasa basi, tutazingatia zaidi hoja za msingi, ili tuweze sasa kuingia katika mada za muhimu kabisa na lengo la mwandishi.

UPATIKANAJI WA KITABU

Utangulizi na ufupisho wote wa kitabu, unaweza upata bure kabisa, kupitia blog, ya injili ya sayansi. Lakini kupata kitabu kizima itahitaji gharama za kukinunua. Sababu kubwa ni kuwa, ‘’Ilipo hazina ya mtu, ndipo ulipo moyo wake’’, kitu ukikigharamia, utajua thamani yake. Lakini kuonyesha kuwa hatujali zaidi maslahi ya kibiashara, bali tunajali kusaidia jamii. Kitabu hiki kitauzwa kwa thamani ndogo sana, si sawa na vitabu vingi katika shelves za Amazon.

YALIYOMO

KISA KIFUPI CHA MTAA MMOJA WA JIJI LA PENTAGON.. 2

HISTORIA FUPI YA HILI ENEO.. 5

KUKUA KWA MAENEO HAYA YA PWANI 6

ASILI YA MWAFRIKA MASHARIKI 7

KWANINI MAENEO YA KATI YALIKUWA NA WATU WACHACHE?. 9

UFUPI KUHUSU MAKABILA YA TANZANIA. 10

KUKUA KWA THAMANI YA PESA  PWANI ZA KUSINI 12

Nguvu Ya Wanawake. 13

Saikolojia ya Usaliti na Ukoloni 14

UCHAMBUZI KWA UFUPI JUU YA TABIA ZA WATU WA ENEO HILI 14

KUSHAMIRI KWA URAIBU WA NGONO NA MAPENZI 17

Msingi wa Tabia Za Uchafu Katika Ngono. 18

MSHAMBA AKIFIKA MJINI 19

KUKUA KWA USANII 20

UGENI NA UVUNJIFU WA MAADILI 21

UTANGULIZI 22

UPEKEE WA KITABU.. 25

SHUKURANI 26

VITU VYA KUZINGATIA KATIKA KUSOMA. 30

UPATIKANAJI WA KITABU.. 30

SURA YA KWANZA.. 38

MABADILIKO YA AWALI KABISA YA MWANADAMU NA VIUMBE HAI 38

Historia ya Mwanadamu. 38

Badiliko La Ghafla. 39

Swali La Kifalsafa : Vimelea Na Parasites Kama Virusi Na Wanyama Walanyama Walitoka Wapi, Kama Uumbaji Haukulenga Kifo?. 42

Maisha Baada Ya Badiliko. 44

SURA YA PILI 47

KUZALIWA KWA FALSAFA KUU MBILI ZA DUNIA MPAKA MWISHO WAKE. 47

KAINI MKULIMA ‘’FOOD PRODUCTION SYSTEM’’ 47

HABILI-MFUGAJI/MWINDAJI/MKUSANYAJI- ‘’HUNTERS AND GATHERERS’’ 48

VIPINDI VYA UKUAJI WA JAMII ZOTE DUNIANI 49

Toka Uumbaji Mpaka Babeli. 49

Kuzaliwa Kwa Demokrasia. 50

Falsafa Iliyofichika. 51

KUELEKEA MWISHO WA ZAMA ZA AWALI 52

Mnara Wa Babeli Na Mwisho Wa Zama Za Kwanza. 53

TOKA BABELI MPAKA MIAKA YA 2000. 53

Kushamiri Kwa Falsafa Ya Kilimo Katika Bonde La Ulaya-Asia ‘’Eurasia’’ Na Afrika Ya Kaskazini ‘’Northen Africa’’ 54

Kwanini Kilimo Kilishamiri Ulaya-Asia + Afrika Kaskazini, Na Hasa Bonde La Rutuba?  56

Kilimo Na Kukua Kwa Kasi Kwa Ulaya-Asia Na Afrika Kaskazini 59

Kuzaliwa Kwa Maandishi 60

Kukua Kwa Teknolojia. 61

Kwa Hiyo Wa-Afrika, Marekani & Australia Walikuwa Na Bahati Mbaya!. 62

Maadili Afrika. 64

Kukua Kwa Biashara, Usafirishaji Na Afrika. 65

Kwanini Ulaya-Asia Na Afrika Kaskazini Zilikuwa Na Nguvu Na Teknolojia Zaidi Ya Afrika, Australia Na Marekani, Na Sio Kinyume?. 66

Kielelezo Cha Mduara Wa Maarifa, Ugunduzi Na Nguvu Cha Shoo. 69

Kosa Kubwa Lililo Wagharimu Waafrika Na Wamarekani?. 76

SURA YA TATU.. 79

RAMANI ZA TABIA.. 79

SAYANSI YA RAMANI ZA TABIA.. 81

Utangulizi 81

Nini Maana Ya Environmental Brain Sensory Potentials ‘’EBSP’s’’ 84

NYANDA ZA JUU.. 86

KUSINI ‘’NYANDA ZA BARIDI’ 86

Jiografia fupi 86

Nini maana ya Tropiki, na Sub-tropiki?. 89

Kwanini Iringa na Mbeya Zinaongoza Uzalishaji wa kilimo Tanzania?. 89

BIOLOJIA ZA WATU KWA ASILI KWA MAZINGIRA YA KUSINI JUU. 90

Kufanya Sana Kazi na Kuwa na Nguvu. 90

Kuwa na Mapafu imara na Mwonekano wa wastani wa Ufupi 91

Kuwa Na Mwonekano wa Weusi 92

Kuwa na Kinga sana ya Mwili 92

Tabia za Ulaji 93

SAIKOLOJIA ZA WATU KWA ASILI KWA MAZINGIRA YA KUSINI JUU.. 94

Asili Ya Upole Na Kutowehuka Kirahisi 94

Msukumo Mdogo Wa Utandawazi na Teknolojia. 97

Uwezo Mkubwa Wa Kitaalamu Na Kitaaluma. 97

Maendeleo Makubwa. 98

CHANGAMOTO ZA KISAIKOLOJIA ZA WATU WA NYANDA ZA JUU KUSINI 99

Upweke Hasa Kwa Wanawake (Huwasukuma Zaidi Kwa Manabii Na Makanisa)  99

Imani za Ushirikina. 100

Ushamba ‘’Less Exposure’’ 102

Changamoto Za Kifamilia Na Maamuzi Magumu. 103

KASKAZINI ‘’NYANDA ZA BARIDI’’ 104

Jiografia. 104

Mlima Kilimanjaro. 104

Historia Inavyojenga Msingi Wa Tabia Za Watu Wa Kaskazini 105

BIOLOJIA ZA WATU WA NYANDA ZA KASKAZINI 106

SAIKOLOJIA ZA WATU WA NYANDA ZA KASKAZINI 107

Kujiaminii Sana. 107

Msukumo Wa Unywaji Wa Pombe Na Matumizi Ya Madawa Na Bangi 108

Hatari Za Kuwehuka. 109

Ujanja, Usomi, Udini, Na Uchumi 109

KANDA YA ZIWA.. 111

Jiografia. 111

Historia Fupi Yenye Kujenga Msingi Wa Tabia Za Watu Hawa. 112

Bahaya. 112

Basukuma. 113

Wakurya Na Wajita. 114

BIOLOJIA ZA WATU WA MAENEO YA KANDA YA ZIWA.. 115

Wanyama Na Magonjwa. 116

SAIKOLOJIA ZA JAMII MBALIMBALI ZA WATU WA KANDA YA ZIWA.. 117

Uwezo Mkubwa Kitaaluma. 117

Msukumo Mkubwa Wa Maadili 118

Kupenda Sana Sifa ‘’Baadhi Ya Wahaya’’ 119

Kuchelewa Kustaarabika ‘’Baadhi Ya Wasukuma’’ 121

Kutunza Jadi Zao, Na Kupenda Utawala. 122

Imani Za Ushirikina Na Uganga. 123

UWANDA WA KATI, MAGHARIBI NA KUSINI 126

Jiografia. 126

Uwanda wa kati. 126

Uwanda wa Magharibi 126

Uwanda Wa Kusini 128

BIOLOJIA ZA WATU WENGI WA KANDA HIZI 129

Kwanini Kanda Hizi Zinaongoza Kwa Afya Dhaifu Zaidi?. 129

SAIKOLOJIA ZA WAKAZI WENGI WA MAENEO HAYA.. 131

Uvumilivu Na Upambanaji 131

Usanii Na Sanaa. 132

Umoja Na Undugu. 132

Imani Za Uchawi ‘’Sumbawanga’’ 132

NYANDA ZA MASHARIKI KATI, PWANI MPAKA VISIWANI 134

Jiografia. 134

Uwanda wa Kati Mashariki na Sehemu Za Pwani 134

Uwanda Wa Pwani 135

BIOLOJIA NA SAIKOLOJIA  ZA WATU WA MASHARIKI, PWANI, MPAKA VISIWANI. 137

WAZAWA WA MIJI HII 138

Uhakika Wa Chakula. 138

Matokeo Ya Uhakika wa Chakula. 139

Kutowazia Sana Baadae. 139

WAGENI WA MIJI HII 141

Wafanyabiashara. 142

Tamaduni Nyingi 144

SURA YA NNE. 146

SAYANSI YA KUKOLONI WATU KWA KUWATEGENEZEA TABIA BILA WAO KUJIJUA   146

Lengo La Kuitumia Tanzania. 146

Upekee Wa Tanzania Zaidi Ya Afrika Nzima?. 147

Siri Kuhusu Tanzania. 149

Matokeo Ya Awali Ya Saikolojia Ya Watanzania. 150

Vita Iliyofichika Kuhusu Tanzania. 150

SAYANSI YA KUHARIBU TABIA ZA WATU NDANI YA WAKATI MFUPI 152

Mlinganyo Wa Hisabati ya Tabia. 152

MALENGO YA UHARIBIFU.. 153

Kuua Uwezo Wa Watu Kuujua Ukweli  ‘’Abstractive Destruction’’ 153

Mfumo Wa Elimu. 154

Chochea Uhuru Wa Kimaarifa. 156

Ondoa Uhitaji Wa Ukweli 156

Kuua Mifumo ya Kusapoti Elimu ya Kweli 157

Matokeo Katika Hisabati. 158

Kuua Uwezo Wa Watu Kuuishi Ukweli ‘’Integrative Destruction’’ 158

Ukweli katika Ubongo. 158

SAYANSI YA KUUA UWEZO WA WATU KUUISHI UKWELI. 160

KUTUMIA VIWANDA VYA VYAKULA ‘’Food Industry’’ 160

Chochea matumizi ya Bidhaa za sukari, kama soda, Biscuits, Energy drinks, Fruit Juices, n.k  160

Chochea Matumizi ya Nyama na Protini za Wanyama. 162

Chochea Matumizi ya Bidhaa Zote Hatarishi, kama Pombe. 163

Chochea Matumizi ya Madawa katika Kilimo na Ufugaji 163

KUTUMIA VIWANDA VYA DAWA ‘’Drug Industry’’ 164

Kutumia Sanaa Za Michezo, Burudani Na Usanii 166

Hisabati ya Matokeo yake. 167

KUIBUA NAMNA BORA MBADALA WA UKWELI ‘’Creative Destruction’’ 168

Hakuna namna ya kufuga Wanyama wa kisasa bila madawa. 168

Unawezaje Kuuza Duka bila kuhusisha Bidhaa za Kisasa zenye Madhara  168

Unawezaje Kuwa Mwanasayansi ilihali unamwamini Mungu. 169

Mifumo yote ya Mali ipo mikononi mwao. 169

Binti anawezaje kupendeza kwa kuvaa mavazi yakujifunika sana. 170

Tutakula nini sasa, maana hivyo ndivyo vyakula vyetu. 170

Matokeo ya Hisabati yake. 170

KUTAWALA WATU WASIO NA UPINZANI ‘’Mental Colonialism’’ 171

Wanafaidika nini na kutawala?. 171

 

SURA YA KWANZA

MABADILIKO YA AWALI KABISA YA MWANADAMU NA VIUMBE HAI

Historia ya Mwanadamu

Sitarudia asili ya mwanadamu, na ulimwengu mzima kama tulivyoona katika Q3.(unaweza soma kitabu kizima Bure kabisa katika blog ya Injili ya sayansi) Hapa tunaenda kuangalia mabadiliko makubwa kabisa ya viumbe toka hatua yao ya kwanza, mpaka kufikia hatua yao ya mwisho, yaani hali zetu sisi.

Ni kinyume kabisa na mtazamo wa wanamabadiliko wa ‘’evolution’’. Binadamu wa kwanza, na viumbe wote wa kwanza walikuwa bora kabisa, tena katika ufanisi wao wa asilimia 100%, na kadri siku zilivyokuwa zikizidi kusonga, basi na hali zao zikazidi kuwa dhoofu. Sio kwamba viumbe wa kwanza walikuwa mambumbumbu kabisa tena zaidi hata ya nyani, na kisha wakaanza kuwa bora mpaka hali zetu tulizonazo leo.

Binadamu alikuwa katika hali ya ubora sana, kisha akaathiriwa hata kuwa katika hali ya udhaifu kabisa, na kisha akapanda na kuanza kurejea hali ya ubora angalau tena, na kisha akashuka katika ubora, akawa dhaifu kama hali zetu tulizonazo hivi leo.

Rejea kielelezo cha ramani fupi ya kielelezo hiki ninachokisema.


 



  



Ukiangalia mabaki ya viumbe wengi wa zamani ‘’fossils’’, walikuwa wakubwa sana. Wanahistoria huona vichwa vya Wanyama wazamani kuwa vilikuwa vikubwa sana ukilinganisha na vichwa vya Wanyama wa sasa hivi. Ukiangalia migodi ya mafuta, na makaa ya mawe, unapata taswira ya uwingi na ubora sana wa vyakula, na mazingira katika jamii ya zamani sana. Lakini pia, jamii za zamani hazina mabaki mengi sana ya maandishi, vifaa vya teknolojia, n.k. hii ni kuonyesha kuwa walikuwa na uhitaji mdogo sana wa vifaa hivi kwa kazi zao, ni kama ndege asingehitaji drone ya kurukia hewani. Uwezo mkubwa wa kumbukumbu hupunguza sana uhitaji wa makablasha kama vitabu vya kutunza kumbukumbu pale unaposahau.

Adamu aliweza kuwaita majina viumbe wote, kumaanisha, alijua Biolojia ya viumbe wote, maana, huwezi mwita mnyama jina bila kumjua ‘’ sheria za Taxonomy’’, kumbukumbu ya viumbe vyote isingekaa kwa kichwa cha kiumbe wa kawaida, alikuwa na uwezo asilimia 100%, hakuwa mla nyama, wala mtumiiaji wa bidhaa za kisasa, hakuwa na madhara yoyote katika Ubongo. Aliweza kuzungumza na Mungu aliyemuumba, alijua sheria nyingi sana za uumbaji wake, au fiziolojia yake, hakufanya vitu kwa msukumo wa dhiki, bali kwa msukumo wa utajiri, alikuwa na uwezo mkubwa zaidi.

Kiwango cha oksijeni kilikuwa bora sana, na hivyo, alikuwa na uwezo bora zaidi wa uzingatiaji. Hakuwa na changamoto zozote zile za kiafya. Na hali ilikuwa hivyo kwa viumbe wote, mimea, Wanyama, wadudu, mpaka bakteria, virusi na wengineo.

Badiliko La Ghafla

Adamu alipotenda Dhambi kwa makusudi yake kwa mara ya kwanza. Alidhihirisha kuwa Mungu sio mkamilifu, kiuwezo, na Upendo. Kosa hili ni sawa na Gari kumkataa Injinia wake. Hivyo, Adamu kila alichokifanya, kilipoharibika, hakikupata Fundi. Mungu alishalijua hili maana alimwambia, Ukitenda Dhambi, Hakika Utakufa. Na sio, Ukitenda Dhambi, Hakika Nitakuua! Mungu hakumuua Adamu, bali Uzee ulimuua, magonjwa, vita, dhiki, n.k. Haya Yote ni matokeo ya  mfumo kujiendesha bila muumbaji wake.

Mungu aliviumba viumbe vyenye Uhuru wa Kifikra ‘’free will’’ katika hali ya ubora kwa asilimia zote 100%. Lakini alikuwa bado akiviwezesha kuendeleza hali hiyo ya ubora kupitia uwepo wake. Mungu alilenga viumbe hivi vitakapoweza kutumia uhuru wao wa kifikra katika kuelekea wema tu, bila uasi, basi angevikamilishia hali ya umilele katika ubora. Lakini pia, alilenga kama havitatumia uhuru wao wa kifikra katika wema, basi atavipatia mpango wa kuviokoa lakini si kupitia uhai tena, bali kupitia kifo ambacho watakuwa wamekielekea.

Adamu alipoonesha kutokubaliana na Mungu, yeye mwenyewe ndiye aliyejitenga na Mungu, akaenda mbali naye. Uwezo wa Mungu ambao ulikuwa ukisimamia ufanisi wa matendo yote ya kimwili ya binadamu, ukawa mbali naye, mwili wake ukaanza kukosa uwezo, ukaanza kufanya makosa, ukawa unaelekea katika kuharibika, na kifo kwa ujumla. Wote tunafahamu, kila unapozeeka, ndipo makosa yanapoongezeka ya mifumo yako ya jenetikia, na kifo kinakukaribisha.

Wanasayansi huwa tukishuhudia tu namna ambavyo mwili hurekebisha makosa yake panapotokea changamoto, huwa tunaona tu namna ambavyo mwili huwa ukifuata maelekezo yake ya asili katika Kutenda biolojia zake. Lakini mtu anapokufa, Pamoja na kuwa kila kitu tunaweza kuwa nacho, ila hatuwezi kumfufua! Hii ni kwa kuwa, uhai sio umeme, wala sio usumaku, wala sio nguvu za ATP, Uhai ni Nguvu isiyoonekana iwezayo kusukuma matendo yote ya kiumbe hai.

Kifo kitaalamu huwa kinatokana na sababu moja kubwa zaidi, inayoitwa ‘’Multiple organ failures or dysfunction’’. Yaani, viungo vyote kwa Pamoja vinapofeli, au poteza wastani wake wa utendaji bora, basi kifo utokea. Hii inamaanisha, uhai pia ni matokeo ya usahihi na ufanisi, wa hisabati ya utendaji wa viungo na mifumo yote ya mwili.

Wanabiolojia wengi huwa hawajui kwanini mwanadamu hawezi kufa ghafla kirahisi, ijapokuwa marazote huwa anazingirwa na changamoto nyingi sana zinazotaka kumuua. Mfumo wa kinga wa kila kiumbe haujawahi kutulia, kila wakati huwa unapambana kuzuia kifo, tena kwa akili nyingi sana kuliko jambo lolote lile ulilowahi kuliona. Mfumo wa kijenetikia, wakati wote huwa unapambana kupunguza makosa katika namna unaumba viungo mbalimbali, makosa muda wote huwa yakitokea katika biolojia za mwili.

Hakuna jambo linalomzunguka mwanadamu ambalo halina hatari kwake, kuanzia mwanga wa jua, hewa anayovuta, maji anayokunywa, chakula anachokula, sauti anazosikia, Mawazo anayoyafikiria, na hata dawa anazotumia. Hivyo Maisha ni kama kondoo anayezungukwa na dubu ambao ndiyo wanamlisha, hayana usalama. Lakini bado tunaishi. Hii inamaanisha kuwa, kuna Neema kubwa sana ya Mungu hata pale ambapo mwanadamu alipoamua kujitenga naye, bado Mungu hakuruhusu ujinga wa mwanadamu umuangamize moja kwa moja.

Uwepo wa mipaka ya uhai, inamaanisha kuwa kifo ndicho chenye mamlaka zaidi. Chukulia mfano, maji ambayo binadamu anakunywa, bado akitumbukia ndani yake, lazima atakufa! Binadamu aliyeishi miaka 70, na kisha akafa mwaka 10 AD, mpaka leo amekufa. Kifo kimemchukua kwa miaka 2000, wakati uhai ulimchukua kwa miaka 70 tu. Kifo ndicho kina nguvu zaidi. Wastani wa kufa marazote ni 99%, wakati wa kuishi ni 1%. Unaweza kumuua mtu kwa vitu vingi sana, mfano, moto, maji, jiwe, sumu, ajali, n.k. lakini vipi kuhusu kumfufua mtu?

Badiliko la Ghafla lilikuwa ni Kifo kutawala juu ya Uhai. Ambapo kutawala huku kwa kifo, kulihusiana na kufeli kwa mifumo yote ya muhimu ya Maisha. lakini neema ya Mungu, ilihusisha kutumia kifo, kuleta tena wokovu, yaani, kwa Kufa kwake Muumbaji, kulilipa Deni la haki yake mwenyewe, lakini kwa sharti la mwanadamu kutumia tena Uhuru wake uleule wa dhamira, katika kuchagua uhai.

Kifo kina maana gani? Kifo kinamaanisha, Mungu mtoaji wa uhai, ataendelea kuishi milele. Wote wanaomuasi, itawapasa kupotea milele. Kifo kinamaanisha aibu, fedheha, ujinga, udhaifu, uovu, n.k. na ndiyo maana hakuna anayependa kufa! Kama ukimvua mtu nguo hadharani, hatakubali! Lakini kiburi chake kikowapi akishakufa? Ukimpiga mtu hatakubali, ukimtukana hatakubali, lakini akishakufa! Itampasa kukubaliana na kila hali.

Swali La Kifalsafa : Vimelea Na Parasites Kama Virusi Na Wanyama Walanyama Walitoka Wapi, Kama Uumbaji Haukulenga Kifo?

Magonjwa ya Vimelea ‘’microbial infections and diseases’’, huwa yanatoa maswali mengi sana kwa wasomi, Kwanini yawepo? Au Wanyama wala wenzao ‘’carnivores’’, huwachanganya sana wasomi juu ya maswali ya nini maana ya Uumbaji uliolenga uhai tu? Maswali ya kwanini kuna viumbe hawawezi kuishi bila kuwadhuru wenzao, yaani  ‘’Parasites’’, pia huchanganya sana watu.

Lakini swali hili jibu lake ni rahisi sana. Unapomfunga Baba kwa kosa alilofanya, unategemea familia yake itaishi vizuri? Hivi ukimuuzi Mungu kwa Kufuru, unategemea familia yake ya Malaika italifurahia hilo? Wanyama ni familia ya mwanadamu. Na ndiyo maana, Wanyama marazote huwa wanamuogopa mwanadamu, au wanajilinda dhidi yake. Wanadamu na Wanyama wote ni familia ya viumbe hai wenye mwili, hata tu mtoto mdogo anajua Sokwe kafanana na Baba yake. na ndiyo maana, Salmonella anayemuathiri Kuku, ndiye anayemuathiri mwanadamu. Na dawa inayomuua salmonella huyu, ikizidishwa inaweza muua hata kuku na mwanadamu. Hivi unajua Samaki anaumwa pia TB ambayo hata binadamu anaweza ipata, kitaalamu inaitwa ‘’Atypical mycobacteriosis’’.

Mwanadamu ndiye mtawala wa viumbe vyote, na Wanyama ni familia yake. Kosa lake liliathiri mpaka Wanyama wadogo zaidi. Mfumo mzima wa viumbe ukaelekezwa katika mteremko wa kifo. Tafiti nyingi sana bila kukuchosha kwa kuziorodhesha, zinadhihirisha inavyowezekana sana hata kwa kuangalia baadhi ya viumbe ambao walikuwa wala nyasi, walivyoanza kula nyama. Hata Binadamu alikuwa mla mimea tu, ila akaanza kula na nyama. Na sio tu alikula nyama za Wanyama, historia inaonyesha hata visa vya kula binadamu wenzao, hata Biblia inasapoti hili katika zama Fulani za dhiki za kuzingirwa na jeshi la washami, wamama kadhaa walikula Watoto wao, lakini historia inathibitisha pia hilo kupitia vikabila baadhi ambavyo sitavitaja, lakini vilikutwa na mitindo hii.

Wachache hutishwa na meno marefu ya Wanyama wala nyama ‘’canine teeth’’, lakini meno haya yapo hata kwa ‘’Kulungu maji wa China’’ au ‘’chinese water deer’’ unaweza muita, na wanyama hawa hula nyasi tu. kama isingekuwa neema ya Mungu kwa mabadiliko ya Wanyama kama simba kuanza kula nyama tu, basi idadi kubwa ya Wanyama wala nyasi wangeikausha dunia kwa mwezi tu, na stori nzima ya Uhai isingetokea.

Wengi wa Wanyama wala nyama, huwa hawahisi Ladha ya utamu sana wa nyama. Hata idadi ya seli zao za kuhisi Ladha kwao ‘’tastebuds’’ ni chache sana, wastani wa 200 mpaka 500. Huwa wanamotisha tu na nyama kwa kuwa Maisha yao huwa ni magumu na ya kutumia akili sana mpaka kupata chakula, na hasa anapoelekea kuzeeka. Tofauti na wala nyasi, ambao huwa na maelfu ya tastebuds, na huwa na urahisi wa kupata chakula, na ndiyo maana huzaliana sana hawa Wanyama.

Bakteria, Virusi, Protista, Minyoo, n.k. hawa wote huwa na kazi nyingi sana katika ulimwengu. Hawa ni kama mashine za kubalansi hali za chembechembe zisizo hai ‘’inorganic’’ za dunia. Hawa hubalansi chembechembe za madini, hewa mbalimbali katika anga, ufyonzwaji wa virutubisho aidha katika mimea, au katika miili ya viumbe. Unaweza vuta picha ingekuwaje tumbo la ng’ombe lingekosa hawa vimelea? Au Unaweza vuta picha ingekuwaje utumbo mkubwa wa binadamu ungekosa hawa viumbe? Maana wao ndiyo husaidia sana kuzalisha hata chembechembe za muhimu sana katika hali ya kutulia ya Ubongo, kama ‘’dopa, GABA, Serotonin, n.k.’’ bado husaidia uchakataji wa madini mbalimbali, hivyo ni muhimu sana kutambua kuwa, hawa viumbe walilenga ubora zaidi wa mifumo ya Maisha.

Baba yao mkubwa Adamu alipoasi, nao walitenganishwa na uwezo wa ukamilifu wa Uhai, wakaanza kuathiriwa. Wakawa wadhaifu hata kutegemea tu baadhi ya viumbe wengine. Wengi wao hata wanapokuwa virusi hatari kabisa, sio kuwa huwa wamelenga hivyo!! La hasha, hujikuta tu wakisukumwa na wimbi la makosa katika mifumo yao ya kijenetikia ‘’mutations’’. Watu wengi hawajui kuwa, binadamu ndiye muuaji mkubwa zaidi hata ya virusi, minyoo na bakteria. Maelfu ya masumu ya viwandani, milipuko ya mabomu, madawa makali, n.k. huwaua hawa viumbe, huwadhoofisha hata hujikuta wanabadilika na kuwa viumbe wa ajabu kabisa, kumbuka wana akili hawa!! Kadri wanavyojilinda, na umewaathiri sana, wanakuwa hatari sasa sio tena rafiki. Ila hitimisho ni lile lile yote haya huonesha uasi, umepeleka kila aina ya makosa katika ulimwengu. ‘’unaweza kusoma kitabu cha injili ya sayansi cha historia na kiini cha magonjwa, kuweza kuelewa vimelea hawa walibadilikaje na kuanza kusababisha magonjwa.

Maisha Baada Ya Badiliko

Mwanadamu kwa mara ya kwanza sasa akaanza kuzoelea kuishi Maisha katika Udhaifu wake. Dunia bado ilikuwa na utajiri mkubwa sana wa maliasili, malighafi, hali bora ya hewa, n.k. lakini hata hivyo, Uharibifu katika kila mfumo wa ulimwengu ulikuwa ukizidi kuendelea. Mabadiliko kidogokidogo ya tabia ya nchi yalisonga mbele, viumbe siku kwa siku walizidi kudhoofika kutokana na kushindania sana maliasili, na stress zikaanza kutawala katika vichwa vya viumbe katika ulimwengu.

Kwa mara ya kwanza Wanyama katika dunia ikawapasa kujisambaza katika uso wa nchi. Hii ilitokana na kuwa, baada ya dhambi kuliibuka migogoro tofauti tofauti kati ya viumbe. Na hivyo kukabiliana na hizi tofauti, iliwapasa viumbe mbalimbali waanze kutafuta kanda zao watakazo kuwa na amani zaidi.

Fiziolojia mbalimbali zilibadilika na kuwa sehemu mpya ya Maisha ya viumbe. Mfano mzuri kabisa, ni kupungua kwa uwezo wa Ubongo hata kuanza kwa uzoefu mpya wa Kusahau. Binadamu awali kabisa alikuwa hawezi kusahau, lakini sasa akaanza kusahau. Kusahau kulilenga kumsahaulisha kumbukumbu za maumivu, kama vile, kifo cha mtoto habeli, n.k. lakini pia binadamu na viumbe wakaanza kuzoelea kuchoka, na kuzeeka, na hata kufa.

Binadamu akapoteza uwezo wa ku control hisia zake za kiuzazi, na pia akawa na uwezo dhaifu katika mfumo wake wa umeng’enyaji. Hii ndiyo mifumo injini kuu ya kuishi, hata binadamu akiwa kichaa, akaumwa shida yoyote ile ila akawa tu hajafariki. Ili aweze kuishi yeye na kizazi chake, anahitaji kula, na kuzalisha. Udhaifu wa mifumo hii ndiyo mwanzo wa kuzaliwa hisia za Uchi, au Aibu ya uchi. Kama Adamu alivyohisi yu uchi baada ya Kutenda dhambi, ndivyo kila binadamu baada tu ya kujitambua, hujihisi hatia anapoonekana uchi, hii ni kumaanisha kuwa, sasa hivi mtu huyu mfumo wake ‘’subconscious mind’’, unatambua kuwa ana udhaifu wa asili wa kushindwa kujizuia, na kujitawala, na hii hali ya kudumu inatengeneza msingi wa aibu, binadamu anaanza kuhisi kuwa yeye ni sehemu ya kifo, ni mdhaifu, anatamani kujificha.

Familia ni sehemu kubwa sana katika historia ya mwanadamu. Wanadamu wakaanza kuoana na kujitenga na familia zao. Kadri walivyokuwa wakijitenga na familia zao, ndivyo walivyozidi kusambaa katika uso wa nchi. Ijapokuwa dunia ilikuwa na bara moja, lakini bado ilikuwa ni sehemu kubwa sana ya ardhi ya kutosheleza mtawanyiko mkubwa wa viumbe. Hata katika mtawanyiko huu wa familia kadhaa, bado kulikuwa kuna familia ambazo walikuwa waaminifu kwa Mungu wao, na kulikuwa pia na familia ambazo hawakuwa waaminifu kwa Mungu wao. Kulikuwa na familia za mitala, yaani mume mmoja dhidi ya wake wengi, na kulikuwa na familia za mume mmoja na mke mmoja.

SURA YA PILI

KUZALIWA KWA FALSAFA KUU MBILI ZA DUNIA MPAKA MWISHO WAKE

Natamani Prof. Jared Diamond angekisoma hiki kitabu. Falsafa kuu mbili zilizozaliwa katika Dunia hii. na kusababisha migawanyiko yote ya mitindo ya Maisha tunayoiona leo. Ilianzia mwanzoni kabisa kwa Watoto wa Adamu. Kulikuwa na Watoto wawili wa Adamu, yaani Kaini, na Habili.

Kaini alikuwa -MKULIMA/ MFUGAJI  ‘’Food Production system’’.

Habili alikuwa-MFUGAJI / MWINDAJI/ MKUSANYAJI ‘’Hunters, Nomads and Gatherers’’.

KAINI MKULIMA ‘’FOOD PRODUCTION SYSTEM’’

Ni kweli kabisa kuwa, falsafa ya Kulima ilianza baada ya baadhi ya watu kuamua kuwa na makazi ya kudumu, katika sehemu Fulani. na kisha, kuanza kutunza vyakula vyao hata kwa vipindi ambavyo hawatakuwa wakilima.

Falsafa ya kilimo ndiyo msingi wa maendeleo makubwa ya jamii zote kubwa duniani. Kunapokuwepo na wakulima, Jamii hukua haraka sana. Hii ni kwasababu.

-Huwepo chakula cha kutosha hata katika kipindi ambacho watu hawalimi, na kwa hivyo, watu hazaliana sana kwasababu, huwa wana uhakika wa chakula.

-Huwepo na wataalamu wengi wa fani mbalimbali. Hii ni kwakuwa, huwa kuna uwepo wa chakula chakuwatosha wakulima, na wanataaluma wengine.

-Huwa na Nguvu zaidi ya jamii za wasio wakulima. Wakulima huwa na uwezo wa kuwawezesha wanajeshi, wanateknolojia, wana Uchumi, wasanii, n.k.

Jamii zote kubwa kabisa za awali ziliendelea sana kutokana na uwepo wa wakulima katika maeneo yao. Hawa waliwezesha jamii kujikusanya kwa Pamoja, na hata kuanza kuelekea katika uundaji wa falme ambazo zililenga usimamiaji wa idadi kubwa ya watu, ambayo ilianza kuibua migogoro ya kijamii.

Ni makosa kutengeneza mtazamo wa kuwa mfumo wa kilimo uliibukia Katikati ya maendeleo ya binadamu kama Prof Jared anavyohisi. Maendeleo ya kilimo yalikuwa ni falsafa iliyokuwa inafahamika ya muda mrefu, na wanadamu walichokuwa wakikifanya ilikuwa tu ni kutumia mazingira yao kufanya linalowezekana zaidi kwa wakati huo.

Falsafa ya Kilimo hata baada ya miaka 2000 ya kwanza kupita na kuangamia kwa dunia kupitia gharika ya Nuhu, ‘’unaweza rejea sayansi nzima katika Q3’’,  bado ilibakia katika vichwa vya binadamu wote kwa asili. Wanadamu walisukumwa kuchagua kati ya falsafa hizi aidha kutokana na mazingira yao, au kutokana na maamuzi yao. Yakobo ni kielelezo kizuri sana cha mfumo huu wa kazi za kudumu katika mazingira Fulani. Esau ni kielelezo cha makazi ya kuhamahama, au uwindaji. Falsafa hizi mara zote zimekuwa zikishindana huku ya makazi ya kudumu ikishinda.

HABILI-MFUGAJI/MWINDAJI/MKUSANYAJI- ‘’HUNTERS AND GATHERERS’’

Hii ni falsafa ya kutumia mazingira moja kwa moja kila siku, katika kujitafutia mahitaji. Wawindaji na wakusanyaji na wafugaji, huwa na makazi ya kuhamahama kulingana na malisho, huhama kulingana na upatikanaji wa vyakula. Huwa hawaundi jamii kubwa za watu, hii ni kwa kuwa, huwa hawatulii eneo moja.

Jamii za watu hawa huwa na idadi ndogo sana ya watu. Hii ni kwa kuwa, hulenga msimu wa kuzaliana ambao hauhusiani na shughuli za safari za masafa ambayo Watoto hawataweza kusafiri. Hivyo huzaa kwa mpango. Pia, huwa hawakusanyikani kwa wingi kwa kuwa, huwa hawapendelei ushindani wa malighafi chache zilizo katika mazingira.

Jamii hizi mara nyingi huwa hawana utunzaji wa chakula kwa muda mrefu. Na hii ni kwa kuwa huwa hawalimi. Hivyo basi, jamii hizi huwa hawana chakula cha ziada cha kuwalisha wataalamu wengine tofauti na wao wenyewe wakusanyaji au wawindaji. Kwake muwindaji hata aone swala mia, bado atamuua mmoja au wawili tu. Hata waua wote na kisha awatunze! Sasa basi, hii hudhoofisha kuzaliwa kwa taaluma zingine ukiachana na taaluma kuu.

VIPINDI VYA UKUAJI WA JAMII ZOTE DUNIANI

Jamii za binadamu zilianza kupitia vipindi mbalimbali vya ukuaji vikiongozwa na falsafa hizi kuu mbili. Falsafa hizi zilikuwa zikipingana katika kila zama za dunia, hebu tuangalie vizuri.

Toka Uumbaji Mpaka Babeli.

Zama hizi zilianza tokea familia ya Adamu, mpaka Mnara wa Babeli. Katika kipindi hiki chote kulikuwa na falsafa hizi kuu, yaani, upande wa kaini ambao ulijikita katika kujenga jumuiya mbalimbali kubwa. Ambazo zilihusisha maendeleo makubwa sana ya jamii kadha wa kadha. Historia ya kaini inaonyesha kuhusisha kushamiri kwa sanaa kama za miziki, usanii, kilimo. Pia familia za kaini zinaonyesha kuhusisha sana ndoa za mitala, ambazo zinaonyesha kiwango kikubwa sana cha uzalianaji katika hizi jamii.

Jamii za kaini pia zilihusisha ufugaji sana. Hii ni kwa kuwa mifugo walikuwa wakichangamana na kilimo moja kwa moja. Mifugo ilisaidia katika kutoa mbolea za kulimia, lakini pia nguvu kazi. Mifugo ilikuwa sehemu ya mgawanyo wa taaluma mbalimbali katika jumuiya.

Biblia inaonyesha kuwa jamii za kaini, ndizo zilizoanzisha msingi mkubwa sana wa kukua kwa miji. Miji na watu wengi sana walishamiri katika upande huu, na falsafa hizi.

Je Wajua

Jamii hizi ndizo walizoanzisha teknolojia za ‘’Breeding’’. Yaani, kuchanganya viumbe Fulani, ili kupata viumbe wenye sifa za utofauti. Kulenga kupata viumbe bora zaidi. Hizi teknolojia zilihusisha kuchanganya mimea kadha wa kadha ili kupata mimea ambayo, itakuwa na mazao bora zaidi. Pia kuchanganya Wanyama mbalimbali kwa kuwazalisha, ili kupata Wanyama watakao kuwa bora zaidi.

Kuzaliwa Kwa Demokrasia

Jamii hizi zilikuwa na watu wengi sana. Na hivyo, kuepuka changamoto za migogoro ya watu kutokana na kupishana kifalsafa. Iliwapasa kutengeneza mfumo wa kuvumiliana, wa demokrasia ya wengi, kwa kila tofauti walizo nazo. Na hivyo basi, jamii hizi zilihusisha kundi kubwa sana la watu ambao walikuwa waasi sana kutokana na demokrasia. Hii ni kwa kuwa, walikuwa huru.

Jamii hizi zilihusisha kuibuka kwa maovu makubwa ya mvunjiko wa maadili. Hii ni kwa kuwa, binadamu kwa asili wanapokuwa wakijiona kuwa wamejitosheleza, huwa na asilimia kubwa sana ya kuelekea katika uovu. Wanawake wa jamii hizi walikuwa na mitindo ya ukahaba hata kuvutia wanaume toka jamii zingine za sethi, ambapo walikuwemo vijana wengi wacha Mungu, na hii ilipelekea kuzaliwa kwa wanefili ‘’majitu’’.

Japokuwa huwa kuna midahalo kadhaa juu ya wanefili ni nani? Lakini hiyo ni hoja rahisi sana. Wanefili walikuwa ni Watoto matokeo ya watu toka familia ya seti waliokuwa ni wachaji sana, na kuitwa ‘’Wana wa Mungu’’, dhidi ya ‘’Wana wa Binadamu’’ au ‘’familia za uovu, ambazo zilitapakaa sana katika falme hizi za kaini’’. Ndoa hizi zilipelekea Watoto ambao walikuwa na Uwezo mkubwa sana, hii ni kwa kuwa, ‘’wana wa Mungu’’ huwa na uwezo mkubwa sana, rejelea watu kama Suleimani, Danieli, Yusufu, Daudi, Samsoni, Ayubu, Paulo, n.k. mara nyingi watu hawa waliobarikiwa wanapoelekea katika uovu, huwa wanapelekea Uovu mkubwa sana kuliko hata kawaida. Na matokeo yao ni kuwa, hata familia tu za seti nazo wote waliangamizwa katika gharika hata akabaki Nuhu peke yake na familia yake.

Jamii nyingi za seti walikuwa ni kinyume na jamii za kaini. Jamii hizi hazikuwa za kuchangamana sana kama zilivyokuwa za kaini. Jamii hizi hazikuwa na mfumo mkubwa sana wa kilimo, na sanaa kama jamii za kaini. Jamii hizi zilihusisha sana kiwango cha kawaida tu cha ufugaji, kilimo, na uwindaji, na hata ukusanyaji.

Jamii hizi hazikuhusisha mikusanyiko ya mithili ya falme katika maeneo kadhaa. Hawakuwa na familia za mitala. Hawakuwa na mifumo ya demokrasia, wao walitii moja kwa moja sheria za Mungu. Jamii hizi walijitenga mbali na miji mikubwa ya uovu wa jamii za kaini, kabla ya kuja kuangamia kwa kuruhusu kuchangamana tena Pamoja kupitia wanefili.

Falsafa Iliyofichika

Wengi hawajui kuwa Mungu hupingana na falsafa zote za kujikusanya wengi katika eneo moja, kujilimbikizia mali kwa uhakika wa Maisha ya nyakati zote, na kujipa uhuru kwa kila tendo. Falsafa hizi ni kinyume na ndiyo maana, Biblia huamasisha kutojilimbikizia mali.  Mfano, husema katika Mathayo 6:34 ‘’ Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe’’ au hutoa kisa cha Tajiri mpumbavu aliyekuwa mkulima, na kisha baada ya kulima na kuvuna sana, akajisemea sasa ntakaa na kufurahia Maisha yangu yote! Na Mungu akamwita ‘’leo wewe mpumbavu naihitaji roho yako’’.

Mfumo wa viumbe wote duniani unahitaji Imani kwa Mungu juu ya kesho. Yaani, hakuna kiumbe asiyefanya kazi, lakini hakuna kiumbe anayejitaabisha ili ajaze ghala yake. (umewahi ona ghala ya vyakula mbuga za Wanyama? ) Hii ni kumaanisha viumbe wote, mara zote, hukabidhi hatma yao ya kesho kwa Mungu. Falsafa hizi za wana wa sethi za kutojiegemeza sana katika kilimo, au shughuli zingine zinazolenga uzalishaji wa kuzidi, ziliwafanya kuwa waaminifu sana kwa Mungu wao. Na kamwe hawakuwa na siku ya kutulia maana, iliwapasa kufanya kazi ili wale.

Kumbuka; Haimaanishi binadamu hapaswi kuweka akiba! La hasha, hata Biblia inasisitiza busara za wadudu ‘’Chungu’’ katika kujiwekea akiba  (Mithali 6:8), na mithali 6 ilikuwa ikionya tabia za Uvivu, kutofanya kazi. Na hata pia haimaanishi ‘’Wakusanyaji na wawindaji, hawakuwa wakiweka akiba kabisa’’.  Ila tatizo huanzia katika Falsafa zinazolengwa na Kuibuka katika uwekaji huu wa akiba.

Kwanini Falsafa Ya Kaini Hushinda?

Hawa marazote hushinda kwa kuwa, hujikusanya na kuwa na jamii kubwa sana ya watu wenye ujasiri wa kufanya sana maovu, kama vile vita, n.k. hawa hushinda pia kwasababu huaribu sana mazingira, kiasi cha kupelekea kupungua kwa Wanyama wa kuwinda, mimea ya vyakula vya asili ya kuokoteza, na malisho ya mifugo. Je wajua ulimaji wa kilimo chochote kile, kwa kurudia rudia zao moja hilohilo, kwa kiwango kikubwa huua kabisa ardhi? Na ndiyo mwanzo wa uhitaji wa mbolea.

Sababu hizi hupelekea jamii za falsafa ya wana wa sethi kujikuta tu aidha, wakizidi kujitawanya zaidi mbali nao, au, wakijikuta tu nao inawapasa kuiga mifumo ya watu hawa. Mbeleni tutaliangalia hili katika mtazamo wa tofauti kabisa.

KUELEKEA MWISHO WA ZAMA ZA AWALI

Falsafa ya kaini ilishamiri sana, hata kuibadilisha kabisa falsafa ya sethi. Jamii yote ya wanadamu katika zama hizi walijikuta wakiingia katika uovu mkubwa sana, mpaka kumfanya Mungu kuamua kuangamiza kabisa kizazi chote.

Nuhu kutoka falsafa ya seti, anapatiwa neema, na kisha anaanza kuwahubiria watu kuacha uovu. Lakini watu hawawezi kumsikiliza kwa kuwa wameshaathiriwa na uovu, na Mungu anaangamiza kizazi chote hiki cha wakulima Hodari, na wasanii maarufu zaidi, na wajenzi wakubwa zaidi wa awali, na unakuwa ni mwanzo wa mwisho wa zama za kwanza.

Kuna Ushahidi wa kutosha wa kisayansi wa gharika hii ya Nuhu. Unaweza rejea kusoma Q3 kuona namna ambavyo, mabaki mbalimbali ‘’fossils’’ yanadhihirisha gharika hii. lakini pia masomo mbalimbali ya miamba ‘’geology’’, yanadhihirisha gharika hii. lakini pia elimu za ulimwengu, nyota, sayari na mwezi, nazo zinadhihirisha sana gharika hii ya nuhu. Hakuna ukinzani juu ya upana wa sayansi inayothibitisha ukweli huu.

Mnara Wa Babeli Na Mwisho Wa Zama Za Kwanza

Baada ya kutoka kwenye gharika. Binadamu wanaanza kuishi katika dunia iliyojaa mimea, na Wanyama, tena yenye Rutuba ya kutosha. Lakini idadi yao bado inakuwa ni ndogo sana kuweza kuijaza dunia. Dunia sasa imebadilika, dunia ina mabara sio tena eneo moja kama ilivyokuwa mwanzoni. Na kwa mantiki hii sasa binadamu wanaweza kutengana hata kujikuta wapo katika maeneo tofauti kabisa.

Kujengwa kwa Mnara wa Babeli ambako kulilenga kuwakusanya tena watu katika eneo moja, kulifanyika katika maeneo ya Mesopotamia, miji ya kuzunguka Iraq ya leo. Chini tutaangalia maeneo haya kiundani zaidi ili tuweze kuyaelewa kiundani, lakini hata hivyo, bado kunakubaliana na falsafa ileile ya kaini. ya kilimo, na uwepo wa watu wa sanaa za ujenzi ‘’craftsmen’’, na wafalme.

Mungu anatenganisha yeye mwenyewe ufalme huu wa falsafa ya awali ya kaini. Na matokeo yake, mabadiliko yafuatayo yanatokea, lakini huu ndiyo mwisho wa zama za kwanza za awali.

TOKA BABELI MPAKA MIAKA YA 2000

Baada ya kutawanyika toka mnara wa Babeli, kulikuwa na makundi mbalimbali ya watu waliokuwa wakielekea katika kanda tofauti tofauti za dunia. Kulikuwa na makundi makubwa makuu matatu, yaliyotokana na Watoto wa Nuhu, yaani, Hamu, Yafeti, na Shemu. Watoto hawa walianza kuelekea maeneo mbalimbali kulingana na kanda zao, ambazo wanaonekana kuelekea kutokana na mtazamo wa historia.

 hoja kuu ni zifuatazo.

Kushamiri Kwa Falsafa Ya Kilimo Katika Bonde La Ulaya-Asia ‘’Eurasia’’ Na Afrika Ya Kaskazini ‘’Northen Africa’’.

Rejea picha zifuatazo katika ramani ya Dunia.

Bonde zima la Ulaya na Asia, na kaskazini mwa Afrika, lilishamiri sana kwa kilimo. Hii ilitokana na sababu tutakazoziona. Tambua pia kuwa, ukanda huu wa Asia, Ulaya na Kaskazini mwa Afrika, sifa zake pia zinapatikana katika maeneo kadhaa duniani, japokuwa ni kidogo ukilinganisha na eneo hili.  Mfano ni maeneo ya bonde hilo la California, Chile, Cape town South Africa, n.k. lakini hata hivyo, ukanda wa Ulaya-Asia + Afrika ya kaskazini ndiyo ulikuwa bora zaidi, na hii ni kutokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa zaidi cha sifa za kusapoti kilimo.

Kulikuwa na Bonde Moja kubwa sana ambalo kwa Kiingereza huwa likiitwa ‘’Fertile Crescent’’, au ‘’Bonde la Rutuba’’ ambalo, linapatikana maeneo ya Mesopotamia. Msomaji ni vema kutambua kuwa falme zote kubwa zilizowahi kutawala dunia, ziliegemea zaidi katika bonde hili. Kuanzia Babeli, Wamedi na Uajemi ‘’Medo-Persians’’, Wagiriki, na hata Warumi.

Bonde hili huwa napenda kuliita ‘’Mjini Duniani’’. Huku ndiko idadi kubwa sana ya watu ilikuwepo, lakini hebu tuvute taswira hatuelewi chochote, na tuanze kutazama tena kuanzia awali kabisa katika maendeleo ya binadamu baada tu ya mgawanyiko toka mnara wa babeli.

TOKA MNARA WA BABELI

Idadi kubwa sana ya  watu ikaanza kushuka toka maeneo ya Babeli, ambayo nayo yalikuwa mazingira ya miji hii hii ya Persia. Na sasa basi, wapo walioshuka kuelekea chini kabisa mwa Bara la Afrika, wapo walioishia kaskazini, wapo walioelekea mashariki kabisa ya Asia, kama China, wapo walioelekea magharibi kabisa mwa Ulaya, na hawa ndiyo walioendeleza safari hata kuifikia marekani, hii ni kutokana na uwepo wa kina kidogo cha maji zama za barafu ‘’ice ages’’, unaweza kurejea Q3 kulielewa zaidi hili.

Falsafa za Maisha bado zilikuwa zilezile kuu mbili. Yaani, mtindo wa kilimo, na kufuga au kuwinda na kuokoteza na kufuga kwa kuhamahama. Watu walichagua kati ya falsafa hizi kulingana na mazingira yao.

 

Kwanini Kilimo Kilishamiri Ulaya-Asia + Afrika Kaskazini, Na Hasa Bonde La Rutuba?

Tazama ukanda huu ulioshamiri sana kwa kilimo, na picha hii ambayo nimeitoa katika kitabu cha ‘’germs, steel and guns’’, inaonyesha rangi nyeusi ambayo ndiyo bonde hili la rutuba.

sababu za kushamiri kilimo katika ukanda huu

Ukanda huu una tabia ya nchi ya ‘’Mediterranean’’. Sifa za kanda hizi ni kuwa, huwa na mvua chache sana, na huwa na vipindi virefu sana vya jua. Hii hupelekea kukauka kwa mimea mingi sana kutokana na kiwango kidogo cha maji. Mimea ambayo huweza kustawi katika ukanda huu, huitaji kuwa na uwezo mkubwa sana wa kustahimili ukame. Ambapo, huitaji kuwa na mizizi mikubwa sana, au mipana sana. Na huitaji kuwa na matunda makubwa sana. Hii mizizi kama ya miogo, au viazi Maana yake ni kuwa, huifadhi kiwango kikubwa sana cha maji na virutubisho, kwa ajili ya kujipatia chakula chake kwa wakati wa ukame.

Hii tayari ni faida kwa mkulima. Kwa watu walio katika maeneo haya, walichoweza kukifanya ilikuwa tu ni kukusanya kiwango kikubwa cha mimea ya namna hii. na kuipanda katika eneo moja ikiwa peke yake, ikizaliana sana. Na kwa hivyo, wakaweza kuzalisha kiwango kikubwa sana cha mazao.

Maeneo mengi ya marekani, na Afrika. Yalikuwa katika kanda tofauti tofauti, hasa kanda za ‘’Tropical, na Equatorial’’. Huku kulikuwa na kiwango kikubwa sana cha mvua. Hizi zilisababisha kuwepo na kiwango kidogo sana cha mimea yenye namna hii ya kutunza mizizi. Maana mimea haikuhitaji kutunza sana chakula, maana mvua zilikuwa za uhakika. Mfano, tazama jedwali chini linaloonyesha sehemu, na idadi hii ya mizizi mikubwa.

Unaweza ona namna ambavyo bonde letu lote la nchi zetu za chini ya jangwa la Sahara, Jiografia haihusishi uwepo wa aina hata moja ya mimea yenye aina hizi za mizizi. Na unaweza ona namna ule ukanda wa bonde la rutuba ulivyo na mimea mingi ya namna hizi za mizizi. Na hiyo tayari ilikuwa ni sababu kubwa sana ya kuendelea sana kwa kilimo katika ukanda ule.

Mimea ya mizizi hii mikubwa katika mabonde haya ya rutuba, pia ilikuwa na sifa moja kubwa, ilikuwa na uwezo wa kujichavusha yenyewe ‘’self -pollination’’. Hii iliiwezesha kuzaliana sana hata bila kutegemea kuwepo kwake mingi katika eneo moja. Hii tayari ilikuwa sifa kubwa sana kwa wakulima. Wakulima sasa waliweza kuizalisha hii mimea, na hata kwa kuichanganya ‘’breeding’’, ili kuweza kuzalisha aina mbalimbali za mimea bora kabisa.

Pili, ukanda huu wa ‘’Ulaya-Asia-Afrika kaskazini. Upo katika mstari mmoja tambarare, ‘’horizontal axis’’. Yaani, ukanda wote huu unapitia mara nyingi zaidi, tabia za nchi, na majira yanayofanana. Hii inasaidia sana kusambaa sana kwa taaluma za kilimo, mbegu, uhitaji, na maarifa yoyote yale katika ukanda huu wote, kuhusiana na kilimo. kwa namna yanafanana . Hebu tazama picha chini.

Hii picha inaweza kukuonesha namna ambavyo hata aina moja ya mbegu, au taaluma, au hata wafanyakazi wangeweza kutoka sehemu moja, na kuelekea sehemu nyingine katika ukanda mmoja.

Wanyama wa kufuga ni miongoni mwa sababu kubwa sana iliyochochea kushamiri kwa kilimo katika mabonde haya. Afrika inatambulika kwa kuwa na Wanyama wengi sana wakubwa, kama tembo, n.k. lakini Afrika haikuwa na Wanyama wapole wa kufugika. Afrika ilishamiri sana Wanyama mwitu, wakali, ambao ni vigumu sana kufugika. Lakini hata kwa aina zingine za Wanyama kama Swala, Pundamilia, uwoga wao kupindukia haufai kwa kufugika. Mnyama wa kufugika anahitaji kuwa na upole wa kiasi, na asiwe na ukali wa kuhatarisha kama Wanyama mwitu wengi waliomo Afrika.

Tazama jedwali chini na kisha utaona namna ambavyo Wanyama wapole wakufugika wala majani wote wakubwa, kwa asili hawakuwa wenyeji wa Afrika bonde la chini ya sahara. Walikuwa wenyeji wa bonde la ‘’Ulaya-Asia, na Afrika kaskazini’’. Sasa hivi tunatambua Wanyama wa kufugika kwa wastani wana Ubongo kidogo mdogo kuliko jamii zao waliomwitu.

Wanyama hawa wakufugwa waliendelea kuzalishwa kwa kuchanganywa wao kwa wao, na kuzidi kutengeneza jamii za Wanyama ambao ndiyo wakawa wapole, na bora zaidi kwa kufugwa.

Kilimo Na Kukua Kwa Kasi Kwa Ulaya-Asia Na Afrika Kaskazini

Kama tulivyoona awali kilimo kilipelekea ulaya na Asia, na kaskazini mwa Afrika, kuanza kukua kwa kasi kubwa sana ukilinganisha na maeneo mengine yote ya Dunia. Hii ilitokana na kuwa, kilipatikana chakula cha kutosha kwa wakulima, na wanataaluma wengine wote. Ikiwemo, wanasanaa ‘’craftsmen’’, wasanii, wanafalsafa, wanasiasa, wanateknolojia, n.k.

Biblia hurejelea stori ya Yusufu aliyechochea ulimaji mkubwa Misri kwa miaka saba, na kisha Utunzaji mkubwa wa chakula kwa miaka saba, na uundwaji wa dola kubwa zaidi ya Misri. Hii ni kama ambavyo historia inavyothibitisha maendeleo ya awali kabisa makubwa zaidi ya Misri, kutokana na Kilimo, kilichochochea sana hata sanaa za Ujenzi wa Pyramides, na maandishi.

Kukua kwa jamii tena kwa mara nyingine katika ukanda wa mediterranean. Ukianzia na miji ya Mesopotamia, ambapo falme kubwa nyingi au zote ziliegemea sana. jamii kubwa kabisa za kwanza zilianza kukua katika maeneo haya. Watu walizaliana sana kutokana na uwingi wa vyakula, watu walikaribiana sana na hata kupelekea migogoro iliyopelekea maendeleo makubwa ya mifumo ya uongozi, au falme za awali kabisa.

Kuzaliwa Kwa Maandishi

Maandishi mengi yanaonekana kuanza katika miji ya Misri, na miji ya Sumaritan, ukanda huo huo tunaouzungumzia. Wanasayansi wengi hutafakari nini hasa kilikuwa chanzo cha kuanza kwa uandishi. Ila inafahamika mpaka leo kuwa, uwepo wa Wanyama wengi, mazao mengi, watu wengi, kulipelekea binadamu kuhangaika sana kuweka kumbukumbu ya idadi yao. Kuna wakati waliweka aina mbalimbali za vitu kuwakilisha idadi Fulani ya vitu, baadae wakaanza kutumia alama, na baadae wakaanza kutumia alama mbalimbali kwa sauti maalumu za kutamkwa.

Uwepo wa watu ambao wangekuwa wakihangaika na kutatua maswala haya, kwa kuwa na muda mwingi nje na shughuli za kuwinda zinazokutaka kuwa kazini kila wakati. Basi kuliwawezesha kuweza kufanikiwa kuchochea maandishi yaliyowasilisha ala mbalimbali za sauti, au alama mbalimbali za vitu. Zipo namna mbalimbali za uandishi wa lugha, lakini nyingi zinafanana kiasili. Mchangamano mkubwa wa watu ulichochea kusambaa kwa haraka sana kwa taarifa hizi au maandishi kutoka eneo moja kuelekea eneo lingine.

Kukua Kwa Teknolojia

Watu wengi sana hata mimi kwa wakati kadhaa nyuma, tulikuwa na mtazamo mmoja tu kuwa ‘’Uhitaji huchochea Ubunifu’’. Ni kweli, lakini sio mara zote. Mara nyingi, ‘’Ubunifu huchochea Uhitaji’’. Hakuna aliyekuwa na stress za kutamani kupaa, kabla Ndege haijagunduliwa. Vitu vingi ambavyo huwa tukivifanya, hatukujua awali kama tungepaswa kuvifanya, lakini kadri unavyokuwa na kubadilika, ndivyo unavyochochea uhitaji mpya.

Inafurahisha hata vitu maarufu kabisa kama Umeme vilipogunduliwa awali kabisa, bado watu wengi sana walivipinga. Injini ya Carl Benz ya gari la kwanza kabisa, hakuna aliyekuwa na muda nayo. Watu hawakuwa na muda na magari. Waliamini zaidi farasi. Lakini muda ulivyosonga, kila mtu hakuamini alipojikuta akihitaji gari. Nadharia nyingi sana za sayansi, mfano ‘’Lamarckism ambayo haina miaka mingi toka ikubalike, hata Relativity ya Poincare, Lorentz na Einstein’’ zimewahi kutupwa lakini baadae wakazipa tuzo. muda mwingine hata waliozifanyia kazi huwa wamekwisha kufa. Nakumbuka simu za ‘’Smartphones’’ zilipoingia nchini Tanzania kwa mara ya kwanza kabisa, bado wengi walizikimbia wakiamini ni mbaya sana, mara zinanyonya damu! Lakini leo hii kila mtu anaziamini na kuzihitaji.

Hii ina maana gani? Wagunduzi wengi wa teknolojia walikuwa ni watu waliokuwa huru kufanya mambo yao, bila dhiki yoyote ile. Walikuwa katika jamii hizi za ‘’mediterranean’’. ambapo, chakula kilikuwa cha kutosha. Unaweza kumbuka hata maendeleo ya wagiriki, kukua kwa falsafa au sayansi katika miji ya Athens. Ambapo kulikuwa na chakula kingi, hasa kutokana na ushindi wa majeshi ya Ugiriki ‘’spartans’’ ambao waliteka malighafi na vyakula kila waliposhinda vita, na kuzijazia nchi zao vyakula. Hivyo hivyo ndivyo ilivyokuwa na kukua kwa elimu zama za Dola ya Uislamu, Kukua kwa Ujenzi ‘’Engineering’’ katika zama za dola ya Rumi, hata China mpaka mwaka 1400 ilikuwa inaongoza kwa teknolojia kwasababu ya Kilimo.

Ukoloni japo tutauangalia kiufupi lakini nao unadhihirisha ni kwa namna gani, kushamiri kwa malighafi kwa nchi za ulaya, kulichochea sana maendeleo ya teknolojia. Ijapokuwa, teknolojia yenyewe haihitaji ukoloni. Na hata ukoloni kiuhalisia una mchango mdogo sana katika kukandamiza eneo moja, au kuliinua sana eneo jingine. Kwa mantiki ya dola moja kuitawala dola nyingine, karibia kila nchi imewahi kutawaliwa na dola nyingine.

Maendeleo ya teknolojia, sayansi, falsafa, na maarifa kwa ujumla. Hayajawahi kutokana na jitihada za mtu mmoja, au upekee wa mtu mmoja. Hata kauli hii, haijawahi semwa na mtu mmoja. Prof. Jared ameisema, lakini hata mimi katika Q2 niliisema. Mara zote huwa teknolojia ni ngazi kutoka kwa waliotangulia, na sio aliyetangulia. Hakuna zama katika dunia hii ambapo kilianza kitu kipya, ila kuna zama ambapo kitu fulani kilishamiri zaidi.

Hata kwangu neno, ‘’wakati wa mwisho, Maarifa yataongezeka’’, huwa naelewa kama ‘’Maarifa yatasambaa zaidi, yatakusanywa yote, yataboreshwa zaidi, na yatafanyiwa kazi zaidi’’. Na sio kuwa kuna jambo jipya. Mara nyingi tumekuwa tukivifikiria vitu na kutovifanyia kazi, na ghafla huwa tukiona vikifanyiwa kazi na wengine, wenda kutokana na nafasi zao, au urahisi zaidi kutokana na misaada na kuchangamana na wataalamu mbalimbali katika jumuiya zao, wagunduzi wajinga huisi walianzisha wao. Je wajua, Newton hakuwai iona Rocket, lakini alijua ukienda na spidi ya 11.2km/s, utaivuka kani ya mvuto wa gravity, na miaka mia tatu mbele yake, ikawazekana! Da vinci, hakuwai iona ndege wala parachuti, lakini alijua na kuchora, mfano wa kielelezo cha Parachuti ambalo lilipoboreshwa, liliwezesha kupaa! Tena miaka mia nne mbele yake!

Kwa Hiyo Wa-Afrika, Marekani & Australia Walikuwa Na Bahati Mbaya!

Tukirejea katika falsafa yetu ya awali kabisa. Waafrika wengi sana walishuka katika Bonde la Sahara na kuendelea na safari kuelekea kusini mwa Afrika, na maeneo mengine mengi ya kati. Watu wote toka mnara wa babeli walikuwa wakishuka kama vikundi vidogo vidogo vya watu. Watu hawa waliendelea na falsafa ileile ya zamani ya ‘’Kuwinda, na Kukusanya’’. Wengi wa watu hawa walikuwa wakiishi katika mabonde ambayo yalikuwa na Wanyama wengi, na mimea mingi sana ya asili, ya vyakula.

Kwa kuwa Afrika haikusapoti sana Kilimo, jamii nyingi sana za wakazi, mfano kwa Afrika, jamii kama ‘’Bantu, Khoisan’’, Pygmies, na wengine. Walikuwa ni wawindaji sana wa Wanyama, na wakusanyaji. Hawakuwa na makazi ya kudumu, walikuwa wanahamahama, hawakuwa wakiunda jamii kubwa za jamii za watu. Na hii ilikuwa hivyo hivyo na kwa wakazi wa marekani, kama ‘’Maya’’ au ‘’Indians’’, pia ilikuwa hivyo hivyo kwa jamii za Australia.

Nikisema wakusanyaji namaanisha watu waliotimamu kama tu wale waliopo ‘’ulaya-Asia na Afrika Kaskazini’’, na tena mara nyingi walikuwa hata wakifanya biashara Pamoja. Ng’ombe wengi sana wa wabantu walinunuliwa toka ukanda wa Afrika magharibi na kaskazini. Maana hata hivyo, wabantu wengi sana tunaamini walikuwa ni wenyeji toka Maeneo ya Nigeria, na Cameroon. Wanyama kama Ng’ombe hawakuwepo kwa asili ukanda huu wa Afrika. Na hata baadhi ya makabila walishuka na mazao kadhaa, maana Afrika ilikuwa kwa asili na mazao ya aina mbalimbali za  Mtama zaidi, na Magimbi. Mazao kama Ndizi yalitoka Asia, Mahindi marekani, Ngano ilitoka zaidi Ulaya.

katika vyakula vyote vilivyoshuka hakuna hata kimoja kinachofikia jamii za mtama kwa virutubisho. Mfano tu kiwango cha madini ya Calcium kwenye mtama gramu 100, unapata milligram 350. Hii ni zaidi ya vyakula vyote vilivyoshuka. Na jamii hizi za mtama mfano, uwele, ulezi, mtama wa kawaida ‘’kodo-millet’’ huondoa kabisa mafuta mabaya mwilini ‘’triglycerides’’. Pia kwenye Maganda yake kuna ‘’peroxidase’’ ambazo huzuia seli za saratani zisisambae. Kiufupi mtama ni mara nyingi sana bora zaidi ya mahindi, na ngano, na mchele. Afrika magharibi pia ilikuwa na aina ya mchele ambao ulishuka, ukiachana na uliotoka China.

Waafrika walikuwa watu wenye afya sana. Walikuwa ni watu ambao wakati mwingi zaidi walikuwa katika miondoko, aidha uwindaji, au ukusanyaji wa vyakula. Walikuwa ni watu wenye misuli yenye nguvu sana, lakini changamoto yao kubwa ilitokana na mitindo ya Maisha yao kama ifuatayo.

Kutokuwa na Mifumo ya kilimo. Kutokana na uwingi wa aina za Vyakula, mifumo ya uwindaji ambayo mara nyingi zaidi watu huwa hawana makazi  ya kudumu sana. Haya  Yaliwapelekea kuibuka kwa vikundi mbalimbali, au makabila. Ambayo, walikuwa wakishindana mara kwa mara katika vita za wao kwa wao. Hii ni kutokana na kushindania maeneo, au Sifa za jamii ipi ni bora sana, hii mara nyingi hushamiri kwa jamii ambazo hutumia sana misuli.

Migogoro ilishamiri zaidi kwa kuwa, hakukuwa na kilimo ambacho kingewafanya watu hawa watengeneza jumuiya kubwa ambazo zingewahitaji kuwa na Uongozi wa kutawala maadili ya jumuiya nzima. Vita za makabila zilishamiri sana. Hakukuwa na wataalamu wa fani mbali na fani za uwindaji na ukusanyaji. Teknolojia kwa maeneo mengi sana ilikuwa ndogo.

Maadili Afrika

Jamii za Afrika hazikuwa na watu wengi sana, kama zilivyokuwa jamii katika kanda za mediterranean. Huku wanaume walikuwa ndiyo watafutaji wa chakula kila siku kunapokucha, na wanawake walikuwa ni walezi na wazazi wa nyumbani. Wanaume Afrika walikuwa ni walinzi na wapambanaji wa vita. Mwanaume alipaswa kuwa na maadili ya ukakamavu wa kiume kila wakati. Afrika ilishamiri Falsafa ya Mwanaume anayezoelea tabia za mapenzi huwa ni mdhaifu, na si mpambanaji mzuri vitani.

Pia Afrika iliaminika mwanamke anayemchochea sana mwanaume kwenye mapenzi anamfanya mwanaume huyo kuwa mdhaifu. Sio kana kama hii falsafa ilikuwa ya pekee sana Afrika, hata maeneo mbalimbali kama miji ya Ugiriki falsafa hii ilisambaa, na Uarabuni. Jambo hili lilichochea sana uwepo wa gepu kubwa sana kati ya wanaume na wanawake.

Ijapokuwa Afrika ilishamiri sana kwa mila potofu sana kwa baadhi ya zama katika historia. Kama vile ukeketaji wa wanawake, ndoa za mitala, Imani za ushirikina, ibada za miungu n.k. mara nyingi huwa ni hoja zisizo na nguvu maana tabia za zama za ujinga penginepo kitovu chake kilikuwa ‘’Mediterannean’’ yaani ‘’Ulaya-Asia’’ ambako hata Ushoga ulizaliwa.

Tatizo pekee lililoiathiri Afrika ni mfumo wa Uongozi wa makabila mengi, ambao kitaalamu huitwa ‘’Kleptocracy’’ hili ni janga la Afrika. Hii ina maanisha, Afrika imekuwa sana na Viongozi wanaopenda Kujilimbikizia Mali za umma, kwa tamaa zao. Hii ilikuwa ni hali ambayo Afrika haikuanza nayo jamii nyingi ziliposhuka toka mnara wa babeli. Waafrika zamani walikuwa wanapenda sana usawa, kitaalamu waliitwa ‘’Egalitarians’’. Lakini hebu vuta picha  Raisi kama ‘’Mobutu’’ wa Congo!!! Mtu anaweka Mabilioni ya mapesa ya nchi kwa akaunti yake tu, na nchi yake anashindwa hata kuisambaza japo tu mfumo wa Simu.

Hili janga la mifumo mibovu kabisa ya Uongozi ilianzia pale ambapo Viongozi wengi wa makabila tokea awali hawakuwa wakichaguliwa kwa sababu za sifa za uongozi, bali aidha za uwindaji, au Nguvu za vitani. Viongozi hawa hawakuwa na tume za ushauri, maana mifumo ya uwindaji haina nafasi sana juu ya taaluma zingine. Tabia hizi ziliwajengea viongozi hawa tamaa ya kupenda kujilimbikizia sana jambo ambalo liliendelea kurithishwa hata kwa jamii za baadae. Karibia Afrika yote tatizo hili limesambaa, Nchini Tanzania tuliwahi pata bahati ya kupata Raisi mzuri sana ‘’John Pombe Magufuli’’ ambaye alipigana sana dhidi ya mifumo hii ya ‘’Kleptocracy’’ iliyosambaa nchini, lakini hata yeye hakufanikiwa, maana hii mifumo inasababu za kisaikolojia ambazo kitabu hiki kinazichambua kwa kiwango kikubwa sana.

Kukua Kwa Biashara, Usafirishaji Na Afrika

Kuanzia miaka ya 1400, Dunia ilikuwa imeshamiri sana kwa maendeleo ya teknolojia za usafiri na biashara. Hii ilitokana na maendeleo ya kasi sana ambayo yalikuwa yamekwisha tokea katika kanda nyingi sana za Ulaya-Asia, na Afrika ya Kaskazini. Jamii hizi zilikuwa na migogoro mingi sana ya vita, na kutawaliana. Kumbuka kanda hizi hazikuwa na vita za kila siku kama vita za makabila ya Afrika. Jamii hizi zilikuwa zikipigana na kisha Ufalme mmoja unatawala, na kadri unavyoishiwa nguvu, unaibuka mwingine kwa vita kali hata kuupindua. Vita zilihusisha umwagaji mkubwa zaidi wa damu, lakini ulihusisha kushabiiana sana kwa maarifa kila jamii zinapokuwa Pamoja. Na maarifa haya ndiyo yalikuwa msingi wa hitaji la malighafi zaidi, na ugunduzi zaidi.

Miaka ya 1400 na kuendelea kulikuwa na safari nyingi sana za majini kwa wafanyabiashara wengi sana kama, Christopher Columbus, Vasco Da Gama, Bartholomeu Dias, Vasco Nunez de Balboax, Nyuma kidogo walikwepo kina Marco Polo, wengi wao hapa walitoka Spain, Portugal, na pia kulikwepo wafanyabiashara toka China, India, Uarabuni, n.k. wengi walizunguka dunia nzima hata na Afrika. Na kupitia hawa Afrika ilifahamika sana, Utajiri wake, Uhitaji wake, Udhaifu wake, na huu ndiyo ulikuwa mlango wa Afrika Kibiashara, kukua kijamii, na hata Ukoloni.

Kwanini Ulaya-Asia Na Afrika Kaskazini Zilikuwa Na Nguvu Na Teknolojia Zaidi Ya Afrika, Australia Na Marekani, Na Sio Kinyume?

Ni kweli tumeshaona kuwa ukanda wao ulikuwa wa mstari wa ulalo uliochukua eneo kubwa na kuwezesha zaidi kujamiiana kimaarifa, kivita, kilimo, n.k. kuliko Afrika iliyo kwa wima, na bado ina majangwa kama Sahara ambayo kuvuka ni shughuli, bado Afrika kuna mito mizito yenye maporomoko isiyosapoti safari za majini hata kuweza kuchochea maendeleo ya meli, na mashua kubwa. Tumeshaona pia kuwa ukanda wa mediterranean tu ndiyo uliokuwa na mimea yenye mizizi na matunda ya kusapoti sana kilimo kutokana na hali za hewa za kiangazi, na mvua chache. Ila bado haya sio majibu, kwanini isiwe kinyume?

Ndiyo, Tumeshaona kilimo kilivyosapoti wanataaluma wa teknolojia zingine n.k. tena wengine husema hata na hali za baridi huwafanya watu kuhitaji joto muda wote, hivyo huitaji ujenzi mara zote wa kulitunza joto, ingawa huwa hawawezi kutetea kwanini maeneo mengi tu yenye baridi zaidi, ndiyo hayana maendeleo kabisa. Ndiyo unaweza sema Afrika ilikuwa na falsafa za uwindaji sana na ukusanyaji, hivyo walikuwa hatarini zaidi kutoendelea kwa jamii kubwa, na ndiyo maana hata waliweza kutawaliwa kipindi cha ukoloni. Lakini Bado Hujajibu swali. Kwanini isiwe kinyume?

Hili linaitwa swali Gumu la Kifalsafa la kwanini? ili kuweza kujibu maswali kama haya, hauhitaji kufikiria kwa kiwango cha kawaida tu cha Sayansi. Ambayo inakwambia tu sababu za imewezaje kutokea, au ‘’How’’. Maswali kama haya wanasayansi ambao hujaribu kutumia sababu za ‘’Evolution theory’’ kuyajibu. huaribu kabisa maana. kwa kuwa, huwa wanapelekea hata kuibuka kwa falsafa za ubaguzi na ukandamizaji, au ‘’Racial segregation’’’.

mfano kusema, mtu wa kwanza alifanania aina za Sokwe, halafu alitokea Olduvai Gorge, Tanzania. Halafu akaanza kusambaa na sehemu zingine za dunia, hata akafika Ulaya n.k. mitazamo hii ni kama inakuonyesha kuwa mtu atakayebaki Afrika maana yake atakuwa bado ana Usokwesokwe, na ndiyo maana utakuta ‘’Adolf Hitler’’ akikitumia kitabu cha ‘’Charles Darwin’’, yaani ‘’Origin of Species, and Descendants of Superior man’’ kumaanisha Waafrika, wayahudi, na wengine kuwa bado wana asili za usokwe, huku wao wakiwa watu wa kisasa zaidi ‘’Superior Race’’. Hii kitaalamu inaitwa ‘’ Eugenics’’. Kumbuka, vipo vitabu maarufu kama ‘’Anatomy of Restlessness’’ ambavyo vinaonyesha, kadri unavyotembea zaidi, ndivyo unavyoendelea zaidi, kwa hiyo, kama mtu alitokea Afrika, basi aliyefika Ulaya-Asia, ametembea sana? Ameendelea sana, na vipi kuhusu aliyebaki? Maana yake hajatembea sana, bado ana usokwesokwe, hana akili sana!! ( hoja hizi ili uzipinge, inabidi ung’ang’anie kuwa zimetafsiriwa vibaya, au msomaji hana akili za kutosha kuweza kuzielewa)

kumbuka pia, Afrika ndiyo ina aina mbalimbali za jamii za watu ‘’high genetic diversity’’, ukitafsiri kinyume kama wanavyofanya hawa watu, unaweza pata jawabu hasi kuwa watu walitoka Afrika na kuelekea Kaskazini, na utafeli kama wanavyofeli hawa watu. Watu walitoka Babeli kuja Afrika, na kwa kuwa Afrika ipo Wima, ina mazingira na majira tofauti tofauti, basi Jenetikia ya kisasa zaidi ya ‘’Epigenetics’’ mfano, ‘’Lamarckism’’, inatuthibitishia kuwa, watu lazima watabadilishwa badilishwa sana katika jenetikia. Na ndiyo uhalisia wa Afrika kuwa na ‘’diverse genetics’’. 

Unaweza danganya Watoto wadogo kuhusu fuvu la mtu wa kwanza, na mabaki yake kwa kuunganisha vipisi vya mifupa isiyo hata na uhusiano, kama wana nadharia hawa wanachofanya, lakini msomi mzuri anatambua tabia hizi za wanasayansi wa sanaa za kufikirika, wanaochochea tu kuua sayansi, na familia zao.  (rejea Q3 unaweza elewa mbinu za upotoshaji mkuu wa wanasayansi hawa, hasa kwa vifaa vyao vya kupima muda-Radiocarbon datings, K-Ar datings, na matabaka ya dunia ‘’geologic layers)

Wanasayansi husema kuwa nadharia hii wala haimaanishi hivyo, ila tu ni makosa ya kuitafsiri. Hata wanasayansi wasioamini huu ukandamizaji, ila wanaitumia hii nadharia. huwa wanahangaika sana mithili ya watu ambao hawajawahi Kwenda shule, wanapojaribu kutaka kuitumia kujibu maswali kama haya ya kifalsafa. Tatizo kubwa ni kuwa, nadharia hii imepinduliwa juu chini, na chini juu. Mtu alifika Afrika kutoka Babeli, na siyo alitoka Afrika Kwenda Babeli.

Siku zote anayechelewa kufika, huwa anachelewa Kuanza.

Kuelewa msingi wa sababu, ambazo ndizo zinakupa Jibu la swali la kwanini? haikuwa kinyume kwa Afrika kupiga hatua kabla ya Ulaya-Asia. Rejea kwanza kielelezo kifuatacho, na kisha nitatoa maelekezo yatakayojibu swali hili kiundani zaidi. Zaidi ya hapa hakuna jibu lingine lolote ambalo linaweza maliza utata wa swali hili la kifalsafa, na likatunza ukweli wa sayansi.

Kielelezo Cha Mduara Wa Maarifa, Ugunduzi Na Nguvu Cha Shoo



B, t=T


NGUVU

A t=0





A, t=0-X’s

                 

Tafsiri Ya Kielelezo Cha Mduara Wa Maarifa Na Nguvu

A ni Mnara wa Babeli. t=0-X, ni Muda ambao watu wote toka walipotoka mnara wa Babeli walikuwa sawa kwa kiwango Fulani katika maarifa, teknolojia, afya, falsafa, na hata idadi.

B ni mwisho wa Milenia ya 7, yaani t=2031±. Ambapo jamii za binadamu wote wamekwisha changamana hata kufikia mfanano kabisa. Kama watu wa maarifa wanaongea lugha moja kila nchi. Kama wanadini wana kiongozi mmoja. Kama wajinga wapo kote, na wanasababu wote za kuwa wajinga, na wanaongea lugha moja. Kama wachawi, mashoga, kama wasanii, kama wanasayansi, n.k.

Mstari Mwekundu Waliopita Ulaya-Asia Na Afrika Ya Kaskazini

Huu mstari una maana ifuatayo. Japokuwa ukipima umbali wake, na mstari wa kijani, yote inalingana kabisa kiumbali. Lakini mstari mwekundu unawakilisha jamii za Ulaya-Asia. Ambazo, Upande wa Ugunduzi, kwa sehemu ya kwanza mpaka kufikia wakati Fulani. Ugunduzi ulikuwa juu sana. Ugunduzi ulikuwa juu sana, ukilinganisha na Kiwango cha Ugunduzi kwa Mstari wa Kijani, hii ni kwa kuwa, Njia waliyoipita ilikuwa ni mithili ya Kupanda Mlima, Ijapokuwa mpanda Mlima atatumia Nguvu nyingi sana, ila atakapofika juu, ataona umbali mrefu sana.

Nini maana ya Kupanda Mlima?

Kuishi katika Ukanda wa Mediterranean, ambao ulipelekea kukua kwa kilimo. Haikuwa kazi rahisi. Historia ya Kilimo haikuwahi kuwa Nyepesi. Na Ugumu wa Kilimo pia Ulichochea kukua zaidi kwa falsafa za uwindaji, na Ukusanyaji. Bado hata kilimo kilipofanikiwa, kulikuwa na changamoto kubwa sana za Milipuko ya Magonjwa.

Kwanini Kilimo Kilipelekea Milipuko ya Magonjwa?

Kilimo kilichochea kuchanganya aina mbalimbali za Mimea na Wanyama wanaofanana, kwa lengo la kuongeza uzalishaji. Kadri unavyowachanganya Wanyama hawa, unawapelekea kuwa na Kinga dhaifu sana. Matokeo ya kuwa na kinga dhaifu, ni kupelekea Kuanza kwa mashambulizi ya vimelea. Lakini pia, Wanyama hawa unapowafuga kwa Pamoja katika sehemu ndogo, unasababisha kuwepo kwa kiwango kikubwa sana cha mbolea, (kazi kubwa ya vimelea ni kuvunja vunja uchafu kama kinyesi, ili kurejesha virutubisho katika ardhi, unapobeba mbolea, unabeba nyumba yao vimelea) ambayo itakuwa ikitumika hata katika kilimo cha mimea. Mara zote hizi mbolea huwa ndizo nyumba za vimelea. Na kwa mantiki hiyo, ufugaji na kilimo kilipekea kuibuka kwa kiwango kikubwa sana cha Magonjwa.

Inafahamika kuwa idadi kubwa sana ya magonjwa ya binadamu, yanatokana na Wanyama. Penginepo, hata magonjwa makubwa yote yanaonekana kuhusiana na Wanyama. Mfano, Measles imetoka kwa N’gombe (Rinderpest), Tuberculosis imetoka kwa Ng’ombe, Small pox imetoka kwa Ng’ombe na Wanyama wengine, Flu kwa Nguruwe na Ndege, Pertussis kwa Nguruwe na Mbwa, Falciparum Malaria kwa ndege, Salmonella kwa ndege, Leptospirosis toka kwa mbwa, Brucellosis kwa ng’ombe, Psittacosis kwa Ndege, kuna UKIMWI toka kwa nyani, kuna Tauni ‘’Black Plaque’’ hii iliua zaidi ya Robo ya watu wote wa Ulaya kuanzia mwaka 1346. Kuna Influenza, Cholera, n.k. vimelea vingi humwathiri binadamu moja kwa moja, au, hubadilika toka kwa Wanyama, na kuanza kumuathiri binadamu moja kwa moja. Je wajua!! Hata magonjwa yasiyo ya kuambukiza, bado yametokana kwa ulaji wa nyama, bidhaa za kisasa, na uharibifu wa mazingira rejea Q4 (utaona uhusiano mkubwa wa Saratani na shida za mfumo wa moyo na nyama, n.k.)

Changamoto za uwepo wa  idadi kubwa ya watu, zilipelekea migogoro mingi sana ya kisiasa. Ambayo watu wengi walipingana kwa hoja, kutetea misimamo yao. Kushindana kwa dola, huku kote kulichochea sana kuongezeka kwa Ugunduzi juu ya namna bora ya kutatua changamoto.

Ulaya-Asia pia imewahi kupitia vipindi vingi sana vya ukame mkubwa. Kukosekana kwa chakula kwa maeneo na maeneo, na haya yote yalichochea sana kuongezeka kwa Ugunduzi. Hasa katika kutafuta namna ya kujiokoa.

Yesu Kristo alizaliwa katika  miji hii. tena katika nchi iliyo maeneo ya Katikati kabisa mwa dunia. Hii ni kumaanisha kuwa maarifa yatapaswa kusambazwa kwa dunia nzima. Ujumbe wa ukristo haujawahi kuwa rahisi hata leo. Watu hujifunza katika mazingira magumu sana, hasa enzi hizo za Rumi ya Ubepari. Haya yote yanaonyesha ni kwa kiwango gani maeneo haya yalipitia changamoto kubwa sana hata kabla ya kufikia Ugunduzi mkubwa sana.

Nini maana ya Kupungua kwa Nguvu katika hatua ya kwanza?

Kipindi jamii nyingi za Afrika, na Marekani. Zikizidi kuwa na watu wengi kulingana na maeneo yao. Na zikizidi kuwa na vyakula na malighafi za kutosha, ambazo jamii hizi nyingi, hata thamani ya mali zao kuna wakati hawakuziona. Mara nyingi ukiwa na nyingi sana, huwezi kuona thamani sana. Mambo yalikuwa kinyume katika jamii za kaskazini.

Vita zilikuwa ni nyingi sana. Ufalme uliondolewa kwa ufalme. Zama za Giza kwa mfano, kuna maelfu ya watu waliokufa. Kuna vita zilipiganwa mfano kati ya Ufaransa na Uingereza, hadi miaka mia. Toka ufalme wa Persians, mpaka Ugiriki, mpaka Roma, mpaka roma inagawanyika, mpaka vinaibuka vikundi hatari kama ‘’Vandals, Huns’’, kuibuka na Kutawala kwa dola ya Uislamu, kuibuka kwa dola ya Ottoman, Ugandamizaji wa Papa ulaya zama za giza, milipuko ya magonjwa kama ‘’Black Plaque, Influenza, small pox’’, kuibuka kwa dola ya Mongolian, zama za mapinduzi, ya ufaransa, vita za Napoleon, Mapinduzi ya nchi nyingi za ulaya, Russia, Vita za Makabila ya Ujerumani ‘’Vita za Balkan’’, vita ya kwanza ya dunia, vita ya pili ya dunia, n.k. haya yote ni sehemu ndogo tu ya migogoro ambayo iliwafanya watu wa Ulaya-Asia kuwa sio watu wakutulia kiakili. Inatambulika hata leo, Bara la Asia ndilo limemwaga damu nyingi zaidi. Kila ufalme ulipotawala, watu wote waliotawaliwa walikuwa watumwa. Nchi kama Russia zilipitia vita nyingi sana.

Kuelekea katika Ugunduzi mkubwa zaidi. Watu walipitia maumivu makubwa zaidi. Walitumia nguvu kubwa zaidi. Upande wa pili, jamii nyingi zimeanza kushuhudia mauaji makubwa sana baada ya Ukoloni kutoka miaka ya 1880’s, mpaka uhuru miaka ya 1960’s kwa wastani. Lakini hata hivyo tayari kulishakuwepo unyanyasaji wa Utumwa. Lakini utumwa haukuwa sehemu za Afrika tu, sema tu Watumwa toka Afrika walikuja kupendelewa zaidi kwa kuelekezwa marekani kuanzia miaka ya 1500’s mpaka 1900’s.  Ukoloni haukuwa na malengo zaidi ya ujinga na tamaa, na ndiyo maana hata nchi nyingi za Asia kama China bado zilikoloniwa na Wamagharibi. Na hata wao wenyewe wakoloni, walipopigana vita ya kwanza, bado walielekea kukoloniana.

Hivyo hitimisho hapa ni kuwa, watu hawa walipitia kipindi kigumu sana. Ni rahisi kusema walipiga hatua kwa ugunduzi wa unga wa risasi ‘’Gun-powder’’ huko china, lakini huo sio ugunduzi wenye kuleta amani. Ni rahisi kusema waligundua Chanjo, lakini hautaambiwa hali zao za kiakili mpaka wanaigundua hiyo chanjo. Ulaya imeshuhudia katika historia miji mingi sana ikiisha watu karibia wote kabisa kwa vifo vya milipuko ya magonjwa.

Hatua Ya Pili ya Kushuka Ugunduzi

Hatua hii inahusisha sasa Baada ya kugundua Mambo makubwa sana, hata kufikia kiwango Mr. Isaac Newton, Leibniz, Georges Curvier, na wengine wengi mpaka Ellen G White, wanaweza kuelezea Maarifa katika Lugha moja, yaani, Sayansi, Uumbaji wa Mungu, na Unabii wa Hatma ya miisho ya Dunia.  Watu hawa baada ya kufika kilele chao cha Ugunduzi, wanaanza kushuka na kuingia katika Hali ya Udhaifu sasa.

Jambo linalotokea ni la watu hawa kuanza kupeleleza  sehemu mbalimbali zingine za dunia. Kwa lengo la kuweza kupata ahueni. Wakiwa na hofu kubwa, lakini wamejawa na ujasiri wa kuzoea shida yeyote. Wanafika maeneo ya ndani kabisa ya Dunia. Na cha Kustaajabisha!! Wanagundua kuwa, kuna sehemu ambazo wapo nyuma kabisa yao. Na hicho ndicho kielelezo cha Nguvu zao kuanza kuongezeka tena. Hii ni kwa namna wanavyoweza kuwatawala wenzao na kujimilikia nguvu nyingi sana.

Kielelezo cha Kushuka Kiugunduzi kinamaanisha, kadri wanavyoanza kufanya utawala kwa wenzao, huku wakijiona wao ni wapekee kiuwezo. Akili zao zinadhoofika. Kwa kuwa, Ugunduzi waliokuwa nao haukuwahitaji Kutenda hivyo, wakazidi kusahau misingi hii. Wakasahau nidhamu, na upole wa Baba zao kabla ya kuwa na ugunduzi huo na kuwarithisha. Kushuka kiugunduzi kunahusiana na kutoruhusu kujichosha kimawazo, kufanya vitu kulingana na mihemko ya kihisia isiyo na muelekeo wa nidhamu. Huu ndiyo mwanzo wa kushamiri ulaya kwa elimu za kijinga kabisa, kama Nadharia za mabadiliko ‘’evolution’’, Big-Bang, Uwepo wa jinsia ya Mashoga, Uharibifu wa Afya za watu kutaka kuwatawala kiakili wenzao, n.k.

Kadri Ugunduzi unavyowashuka, ndivyo wanavyozidi kupata Nguvu. Hii ni kutokana na kuzidi kutumia mbinu zao za uharibifu katika nafasi ya uwezo waliokuwa nao awali.  Mwisho wa milenia ya saba, hakuna nchi ambayo itaweza kuwa na Nguvu ya Jumla juu ya nchi nyingine zote, ila itazipasa zote kuungana na kutengeneza mfumo mmoja wenye Nguvu, ili kuweza Kutenda ajenda zitakazopitishwa ikidhaniwa na wote, lakini kumbe bado tu ni za wachache.

Mambo Ya Kustaajabisha

Asilimia kubwa sana ya vita ambavyo watu toka bara la ‘’Ulaya-Asia’’ walishinda, havikutokana na uwezo wao au bunduki zao. Vilitokana sana na Magonjwa ambayo walikuwa nayo, lakini kwa kuwa wao walikuwa na kinga nayo, hayakuwaathiri. Lakini kwa wageni waliowafikia, wengi wao walikufa sana. Mfano, inakadiriwa asilimia 90% ya Wamarekani wa kwanza kabisa ‘’Red Indians’’, ambao wanakadiriwa kufikia Milioni 20. Walikufa mpaka wakabakia Milioni Moja tu, kutokana na Magonjwa waliyokuwa nayo Wazungu waliofika marekani.

Lakini pia, idadi kubwa sana ya Waafrika, wamarekani, n.k. walioshindwa na wazungu. Wengi wao walikuwa ni wajinga sana. Wengine waliwapokea na mabunduki yao wakiamini yale ni mafimbo tu. Wengine waliwapokea wakiamini wale ni watu wema sana. Wengine waliwashinda baadhi, ila hawakuweza kutumia silaha zao. Wengine walisalitiana wao kwa wao. Kiufupi wengi waliangamia kwa kukosa Maarifa ambayo sasa hivi wanayo.

Kwanini Nimesema Ugunduzi Na Sio Maarifa?

Maarifa ni kila taarifa inayolenga kuokoa uhai wa jamii kiakili, na kimwili, huku ikilenga kujenga jamii bora zaidi kiufahamu wa Maisha bora kwa kila kiumbe hai. (Tambua: watu wanaangamia kwa kukosa maarifa, sio ugunduzi, Danieli hakuangamia kwa kuwa alikuwa na maarifa, ila enzi hizo bado ndege, wala umeme haukwepo). Ugunduzi ni taarifa yeyote mpya yenye uwezo wa kipekee kiutendaji. Ugunduzi unaweza kuwa kinyume kabisa na Maarifa. mfano, kuna mtu aligundua kuwa mwanaume anaweza mwingilia mwanaume mwenzake na akasisimka.

Ugunduzi wa Unga wa risasi na rocket-ranger, ulilenga kuua, na ugunduzi wa Printa ya kwanza kabisa ya umeme, ulilenga kusaidia uandishi, na usasa. Hii mifano yote sio ya maarifa, ni ya ugunduzi. Maarifa ni namna jamii itaweza kuishi kwa amani, wakiwa na chakula bora, na afya njema ya kiakili, bila kufurahia maumivu ya wengine, wala uharibifu wa mazingira kwa ujumla. Afrika ambayo ilikaribia sana sifa hizi, ilikuwa karibu na Maarifa zaidi hata ya Ulaya-Asia. Ambao walikuwa na ugunduzi mkubwa, lakini walikuwa mbali na maarifa, maana walimwaga sana damu (vifo vikizidi, rejea: watu wanaangamia kwa kukosa maarifa)

Unaweza thibitisha hili kwa namna ambavyo, ili wawe na maarifa iliwapasa nao waweke bunduki, na vikundi vya siri vya kisasi pembeni, na kisha waanze kuishi kama Waafrika. Damu kubwa waliyoimwaga na maumivu waliyoyapata, na afya za ubongo na mwili walizoziharibu, zinalingana sawa sawa na ugunduzi walio nao, ili kuwasaidia walau wasiangamie kabisa. mfano, kama wasingegundua Chanjo, ni nani leo hii angeandika historia yao dhidi ya milipuko ya magonjwa ya virusi?

Kumbuka haimaanishi Maisha ya Afrika yalikuwa ni kielelezo cha Maarifa moja kwa moja, bado waafrika walikuwa na upumbavu mwingi sana kama tutakavyouona, na ndiyo maana walikuwa na Maarifa kadhaa, lakini hawakubadilika kabisa Kiungunduzi ambao haukutegemea sana uwepo wa dhiki.

Mstari Wa Kijani Uliopita Afrika Na Marekani Ya Kale

Mstari huu unamaanisha kuwa, watu hawa Kinguvu hawakubadilika sana mpaka katika hatua ya mwisho, wamekuwa wakiongezeka kwa kiwango kidogo sana. Na mwishoni kabisa, wanaelekea kuwa kama wale wa mstari mwekundu. msingi  wa Maarifa ya Msingi kabisa ambayo walipaswa kuwa nayo, nao waliyaacha kwa Kwenda mbali na mstari mnyoofu, na tofauti na mstari mwekundu, hawa hawakuenda mbali na maarifa kwa namna ya ugunduzi, na changamoto nyingi, wao walienda mbali na maarifa kwa namna ya kupuuzia maarifa wakifanya vitu kwa kawaida sana, hata kutokujua thamani zake, na mwishowe kuwa mbali na maarifa.

Hawa watu hawajawahi kutengeneza soda za chupa za cocacola. Kiwango cha nguvu ambacho watu wanapaswa kuwa nacho, ndicho hicho hicho walichokuwa nacho toka awali. Hapaswi mtu mmoja kumtawala mwenzake. Hii ni kuonyesha si watu ambao walijilimbikizia sana nguvu dhidi ya wenzao kama ilivyo kwa wenzao. Lakini dakika za mwisho kabisa, nao wanaungana na mstari mwekundu, na kuwa sawa na mstari mwekundu kifalsafa za mamlaka za kutengeneza matabaka.

Shida zote zilizotokea hapo Katikati kama namna inavyoonekana wanavyozunguka, ni matokeo pale walipoacha kufuata mtindo wao wa asili ambao walipaswa kuuishi. Hata hivyo, bado hatujafikia mwisho wa miaka 7000, ambapo ndicho kitakuwa kipimo kizuri zaidi cha kupima hatma ya ulimwengu kwa mzunguko mrefu zaidi.

Kosa Kubwa Lililo Wagharimu Waafrika Na Wamarekani?        

Hawa napenda kuwaita ‘’watu wa kuchukulia vitu kawaida’’. Afrika hawana kitu chenye thamani kwao, ili mradi wanaishi, na wanapata vitu kirahisi, basi kwao hawana muda wa kujishughulisha kutafakari. Utajiri wa malighafi, na mazingira yasiyo na ushindani mkubwa, viliwapumbaza kuwaza mahitaji makubwa mawili tu, yaani kula na kuzaliana. Ujinga hutawala popote watu wanaporidhika, ndoa za mitala, ukeketaji wa wanawake, ukandamizaji wa kijinsia, ibada za miungu na miti, ushirikina, na kuua walemavu na albino.

Afrika haikuwa na jumuiya kubwa za kifalme, ilikuwa tu na vikabila vidogo vidogo tena vingi sana. Watu walikuwa na ubaguzi sana, hasa wao kwa wao. Hawakuwa wepesi kushirikiana, na kukuza Ugunduzi wao. Wageni waliochanganyikiwa walipowakuta watu hawa ghafla wakiwa na Afya, malighafi na mazingira bora, huku wakiwa wajinga. Ilibidi Damu na maumivu mengi yaweze kuwaamsha watu hawa, na ndiyo maana leo hii, hakuna vikabila tena vya kubaguana, ila kuna Tanzania moja, au leo hii, wanawake na ma albino wapo serikalini.

Lengo ni kuweza kutofautisha maarifa, na ugunduzi. Lengo ni kungundua kuwa Afrika ilikuwa na Maarifa kama vyakula bora, ndoa ni ya mume na mke, watu wanapaswa kuishi kwa kuridhika na uwezo wao, Mungu anapaswa kuabudiwa, lakini, hawakuwa na maarifa yote, na hawakuwa na Ugunduzi, kwa kuwa walijihisi hawahitaji ugunduzi.

Jibu Kwa Ufupi

Waandishi wa Habari hupenda uwape hata hoja za kitabu kizima kwa neno moja. Swali la kwanini sio Afrika, au Marekani. Ni ‘’Asia-Ulaya’’. Jibu lake ni kuwa, Ukipima Nguvu waliyotumia, Ugunduzi uliofanyika, Maarifa waliyotumia, na Muda waliyotumia. Yote ni sawa kabisa.  Ni uelewa hafifu tu ndiyo unaweza sema mtu anayekunywa soda ya Chungwa ya Kopo amefanikiwa kuliko anayekula Chungwa toka kwenye mti.

 

 

Kielelezo Cha Jibu

Una watu wawili wanaoenda sehemu moja na wanatakiwa wafike kwa wakati mmoja. Mmoja anapita njia ndefu sana, na anatumia nguvu nyingi sana. ili afike kwa wakati kutokana na urefu wa njia yake, inambidi akimbie au abuni mbinu ya kisasa ya kumrahisishia sana safari yake. Na pia, anagundua maeneo mengi sana. Kwa upande wa mtu mwingine, yeye anapita njia fupi sana, tena moja kwa moja. Yeye anaona vitu vichache sana, na anaonekana hana ubunifu mkubwa sana.

Kwa Wajinga wote, huyu wa kwanza anaonekana ana mafanikio makubwa zaidi ya huyu wa pili. Lakini katika fizikia, nishati huwa haipotei, au haiwezi tengenezwa. hawa watu wote wana nishati ileile. Na katika Ubongo, huyu wa kwanza uwingi wa taarifa alizoziongeza ambazo ni nje ya lengo kuu, hazimpi faida yoyote, maana tayari zimeshapunguza uzito wa taarifa kuu, kwa kujaza taarifa zisizo hitajika. Kujifunza kwa makosa, hakumfanyi mkosaji kuwa mwanafunzi bora zaidi ya mwanafunzi asiye mkosaji.

Ipi Ni Jamii Bora Zaidi

Jamii pekee ambayo ilikuwa bora zaidi. Ilikuwa ni ‘’Israeli’’ kabla ya 70AD. Au kabla ya kuanguka kwa Jerusalemu na kuchukuliwa mateka. Jamii hii ilikuwa na misingi yote ya maarifa, kuanzia ulaji, mavazi, elimu, ibada, mtazamo wa kijinsia, n.k. lakini hata hivyo, bado ilianguka kwa kuendeleza misingi ya ubaguzi kwa kujiona bora zaidi ya wengine, na kukataa mfumo wa usawa kwa wote kwa kumkataaYesu Kristo. Na matokeo yake, ikaanguka, kama jamii zote Duniani zilivyoanguka, na kwa hivyo, hakuna jamii iliyokuwa imekamilika zaidi ya jamii zingine zote. Ila tu zilitofautiana katika aina za madhara.

SURA YA TATU

 RAMANI ZA TABIA

Tabia ni Matendo ‘’action’’ juu ya  Muitikio ‘’Reaction’’  wa jambo Fulani, au ni ‘’Muitikio ‘’reaction’’ juu ya matendo Fulani ‘’action’’. Kula sana inaweza kuwa ni tabia inayotokana na kuhisi sana njaa, au kuhisi sana njaa kunaweza kuwa ni tabia inayotokana na kula sana. Mara nyingi tabia huchanganywa na mazoea kimaana, watu wengi huzungumzia tabia pale hali hizi zinapotokea zaidi ya mara moja. Ni rahisi mtu kusema ‘’hii siyo tabia yake!!’’ akimaanisha, tendo linalotendwa kwa mara moja tu na mtu fulani, linaweza kuwa, siyo tabia yake, bali tu ni msukumo wa kiakili au kihisia wa huyo mtu kwa wakati huo.

Ni kweli tabia ni matokeo yanayohitaji muda hata kujidhihirisha. Tabia haijengwi kwa mara moja. Na pia huwa haijidhirishi kwa mara moja.

Sehemu hii tutaangalia namna ambavyo, tabia sio tu matokeo ya muda. Bali pia ni matokeo ya eneo ambalo mtendaji yupo. Ramani ya Tabia inamaanisha kuwa, kama ilivyo miti Fulani huwa ikiota sana maeneo Fulani, na miti mingine isiote maeneo hayo. Vivyo hivyo na tabia nazo hutofautiana kulingana na maeneo husika. Miti inayoota jangwani, sio sawa na miti inayoota kondeni, tabia za watu wengi wa kanda za Joto, sio sawa sana na Tabia za watu wengi wa kanda za baridi. Japokuwa tabia ni ngumu kidogo kuziweka katika  makundi ya kiramani kama ilivyo miti. Lakini bado ukichukua ramani na kuziangalia tabia za watu, bado utagundua maeneo mbalimbali yanatofautiana kitabia, kulingana na mazingira yake.

Kwanini tunao ujasiri wa kuzipangilia tabia katika ramani, ni kwasababu kwa kiwango kikubwa sana watu hutenda, au huitikia mwito wa matendo Fulani, kama matokeo ya fiziolojia zao za ndani ya miili yao kwa wakati huo. Au kama matokeo ya matendo yaliyochochewa na jenetikia zao kwa wakati huo. Hebu chukulia mfano huu, Kungekuwa kuna mto Fulani unaopitisha maji Fulani yenye madini sumu ambayo huathiri sana hatua Fulani za maendeleo ya ubongo, kwa kiwango kidogo sana kuweza kugundulika kirahisi. Na watu wa mji unaotumia maji haya wakawa hawalijui hili, wakawa wakiyatumia maji haya kwa muda mrefu. Watu wengi wa mji huu watakuwa waathirika wa afya ya akili kwa kiwango Fulani. watu wa miji Jirani itakuwa ni rahisi sana kutengeneza hisia za kuwa watu toka mji huu ulioathirika kuwa hawapo sawa sana kiakili. Kwao, watu hawa watawaona kama watu waliowadhaifu kwa asili, na watawatengenezea ramani kuwa, ukanda Fulani! watu wake hawapo sawa.

Jamii nyingi sana zimekuwa zikiwa na dhana kadha wa kadha, ambazo kwa nje ni kama za kibaguzi. Utakuta mfano kwa Tanzania ikisemwa kwa baadhi ya watu, ‘’Wachagga wabahiri sana, au wachumi sana’’, au ‘’wamasai wanakimbia sana’’, au ‘’wahehe wanaweza kujinyonga kwa hasira’’, au ‘’watu wa tanga wanapenda sana mapenzi’’, au ‘’wahaya wanapenda sana sifa’’, n.k. zipo sifa nzuri pia kwa watu hawa hawa, labda, upole, ufanyaji kazi, utu wema, n.k. hoja ni kuwa, kwa akili za watu wengi sana, kila anapotoka sehemu moja Kwenda sehemu nyingine, huwa anatengeneza taswira kamilifu ya jamii ya watu anaoelekea kuonana nao. Watu wengi hutengeneza taswira kulingana na historia walizonazo, na makisio yao. lakini katika sehemu hii, tutaenda kuangalia sababu za msingi kabisa, zinazochochea tabia Fulani, katika mazingira Fulani.

Kwanini Tujifunze Ramani za Tabia?

Kama mazingira yako yanaweza kuwa na vichocheo vingi ambavyo vinakusukuma katika Kutenda tabia zisizo njema, basi inaweza kuwa ni hatari kubwa sana. Yapo mazingira ambayo yanaweza kukuchochea kufanya uasi, au yanaweza kukuchochea kuwa mdhaifu, na kibaya zaidi, ni mazingira ambayo yanaweza kukuchochea katika Kutenda mambo ambayo yanaweza kukuangamiza kwa haraka sana.

SAYANSI YA RAMANI ZA TABIA

Miongoni mwa vitu vikubwa sana ambavyo ninamshukuru Mungu kwa kuvigundua, ni vitu nilivyoviita ‘’EBSP’’, au ‘’Environment Brain Sensory Potentials’’. Rejea kisa cha mtaa mmoja wa jijini Pentagon. nilichokielezea mwanzoni kabisa mwa hiki kitabu.

Utangulizi

Kwa kawaida Ubongo huwa una hatua mbalimbali katika ufanyaji kazi wake. Kuanzia hatua ya kutulia kabisa, mpaka hatua ya shughuli kubwa sana. Katika ubongo, kila hatua huusiana na mawimbi maalumu kwa wakati huo. Mfano, kuna Mawimbi ya Delta (0.5-4Hz) haya ni pale mtu anapokuwa amelala fofofo, au amerelax vya kutosha. Kuna Mawimbi ya Theta (4-8Hz), haya ni pale mtu anapokuwa amerelax kawaida tu, ndoto za mchana mfano mtu anavuta taswira yupo sehemu Fulani, n.k. kuna mawimbi ya Alpha (8-13Hz), haya huwepo mtu anapokuwa ametulia huku yupo macho, anaweza kuwa amefumba macho. Kuna mawimbi ya Beta (13-30Hz), haya mtu anakuwa anatafakari kwa kina, na mwisho ni mawimbi ya Gamma (zaidi ya 30Hz) hapa ni pale ambapo kuna shughuli nzito za kiakili au tambuzi zinapoendelea kufanyiwa kazi.

Unapopima Chaji ya Ubongo kwa mazingira ya kawaida kabisa, seli za Ubongo huwa zina chaji ya (-70mV) katika kuta zake ‘’neuranal membranes’’, hii ni kumaanisha, Ubongo sasa upo ‘’stand by’’ kuweza kupokea taarifa mpya.

Ubongo mara zote upo katika mzani sawa ‘’equilibrium’’ na mazingira yake ya nje. Kunapotokea tu mabadiliko katika mazingira ya nje, ubongo hugundua kuwa hapa kuna kitu kimeharibika. Na kwa hivyo, huongeza umakini. Na umakini huu huusiana na kutafuta nini inaweza kuwa sababu, na utatuzi wa tatizo lililokwisha kutokea.

Kwa mantiki hii, Mazingira ya nje nayo yanapaswa kuwa katika hali ya Kutulia kama tu ulivyo Ubongo kwa wakati mwingi. Hii ni kwa kuwa, kadri kama yatakuwa yanabadilika, basi yanaufanya ubongo usiweze kutulia. Ili ubongo wa kiumbe yeyote yule uweze kutulia, sharti mazingira yake kwanza yatulie. Mazingira hata hivyo, mara nyingi huwa yametulia. Mazingira huwa na viwango vyake vya asili vya utulivu.

Mfano;-Hewa safi, Oksijeni (21%), Kaboni dioksaidi (0.03%), Nitrogen (78%), Argon (1%), na Mvuke.

-Maji ya Joto la kawaida ‘’room temperature’’, 25.5°c  yenye madini kidogo toka katika ardhi, kama Sodium, Calcium, Iodine.

-Sauti kwa asilia ya mazingira huwa kati ya 500Hz mpaka 4000Hz. Inapaswa kuwa ya asilia, laini, na haipaswi kuwa mfululizo ‘’not continous’’.

-Hewa haipaswi kuwa na Harufu yoyote kali. Na inapokuwepo inapaswa kuwa kwa muda maalumu tu. Isiwe mfululizo. Harufu za matunda mazuri, maua, perfumes, moshi, uozo, n.k. zinapaswa kuwa kwa kiwango kidogo, na sio endelevu.

-Ubongo unapaswa kuzoelea taswira za miundo ya asilia. Macho hayapaswi kuona taarifa za kushtukiza, usizozitegema kuziona, na taswira zote za kihisia. Kadri tunavyoona, ndivyo tunavyoungana na asili, taarifa zote ambazo tunaweza kuziona lakini sio za asilia, zinatuondoa katika asili yetu.

- Joto la kawaida kati ya Nyuzi (22°c mpaka 24°c) huuwezesha mwili kuwa timamu na bora zaidi. Joto chini ya nyuzi 20°c na juu ya nyuzi 27°c, huufanya mwili kuanza kuhangaika kuurejesha mwili katika wastani wa kawaida.

- Hali ya Ukijani. Watu wengi hata wasomi wasio wataalamu wa Ubongo huwa hawajui kwanini, Ubongo huvutiwa na mazingira yenye Ukijani. Ubongo unapoona hali ya ukijani, huwa unaamini kuwa maeneo hayo yana Vyakula vya Kutosha, Huamini mimea haiwezi kukua bila maji, na hivyo, huamini pia kuna maji ya kutosha. Ubongo pia huamini kuwa mimea itatoa Oksijeni ya Kutosha, Ubongo huenda mbali zaidi, huamini kuwa eneo hili lina amani, halina viumbe wakatili wakukata miti. Haya yote huufanya Ubongo kuzalisha homoni nyingi sana za Dopamine, Serotonins na Endorphins, ambazo huufanya Kufurahia. Ni kama ngonjwa anapofurahia anapomwona daktari wake amefika.

-Sura zenye Tabasamu ‘’smiling faces’’, na sura tulivu ‘’plain faces’’. Mazingira kwa asili huwa yana viumbe ambao muda mwingi zaidi, sura zao huwa ‘’plain’’. Kwa miaka yangu mitano katika taaluma ya Utabibu wa Wanyama, natambua ni vigumu kwa mtu wa kawaida kugundua kuwa mnyama kama ng’ombe amekasirika, au paka, au ndege. Ijapokuwa mbwa atakubwekea, lakini ndani ya muda mfupi utamwona sura yake ikiwa imetulia. Viumbe wote huvutia, ukimtazama ngamia, punda, farasi, n.k. Ubongo huwa hausisimki kwa sura hizi, wala huwa hauoni tashwishwi, ni kama ilivyo kwa namna viumbe wote Watoto hupendwa, kwa namna sura nzao ndogo nzuri huonesha amani, Ubongo hupenda amani. Sura zilizochoka, ubize, kufeli, ghadhabu, kwa asili sio sehemu ya mazingira ya asili.

- Udongo wenye rangi ya Weusi kwa mbali, chembechembe ndogondogo zisizo na mawe makubwa, mitelemko ya kawaida, mazingira ya namna hii huchochea hisia za usalama. Huondoa hofu ya nguvu za mafuriko, hatari za ajali, kukosekana kwa vyakula kwa kukosa rutuba, n.k.

-Upepo baridi wa kawaida, huu huashiria uwezo mzuri wa eneo kudhibiti joto la jua kali. Uundwaji wa mawingu ya mvua, n.k.

-Mwisho, Mazingira yenye viumbe wengi wa jamii mbalimbali. Mfano, Ubongo wa binadamu unapokuwa katika mazingira yenye Binadamu wengine, huwa unajisikia amani sana. Hii ni kwa kuwa, huamini ubora na nguvu ya jumuiya katika mazingira hayo. Binadamu ni viumbe wa kijamii, huvutiwa sana na jamii. Wanapofika eneo lisilo na watu, huwa na mashaka wenda kukawa na hatari zilizowafanya wengine wahame au kulimbia eneo hilo.

Mazingira mara zote huzungumza na Ubongo katika lugha ya kitaalamu sana ambayo, kwa kuangalia tu juu juu mtu anaweze asielewe nini Ubongo unataka.

Katika mazingira ya mtindo huo niliyoyazungumzia. Ubongo huwa na utulivu wa kiwango kikubwa sana. Hii ni kwa kuwa, huwa kuna kiwango kidogo sana cha vichochezi vya kuusisimua sana. Mazingira ya mtindo huu huufanya ubongo kuwa na ufanisi mkubwa zaidi, au ufanisi bora sana.

Nini Maana Ya Environmental Brain Sensory Potentials ‘’EBSP’s’’

Tuna watu wawili. Mmoja yupo ‘’Kariakoo’’ Jijini Dar es salaam, na mwingine yupo ‘’Lupembe’’ Mkoani Njombe. Tunaenda kuwapima watu hawa Ubongo wao katika mashine ya ‘’ EEG’’ kuangalia viwango vyao vya Shughuli za umeme wa Ubongo katika mizunguko yao ya siku nzima. Katika mazingira yao hukohuko. Tunawapima na kisha, tunarejea jaribio hili kila siku kwa kipindi cha miezi mitatu.

Na baada ya hapo, tunakuwa tumeshajua wastani wa viwango vya shughuli za umeme wa ubongo wa watu hawa, ‘’brain sensory potentials’’. hizo ndizo tunazoziita ‘’EBSP’s’’. baada ya kuzijua hizi, hatuna tena haja ya kuhangaika kujua wastani wa tabia za watu hawa. kwa kuwa, tayari tunajua nguvu ya matendo, na muitiko wa tabia za watu hawa. Kwa kuwa, ni Ubongo wao ndiyo una Sukuma matokeo yote ya tabia za watu hawa kupitia utendaji wa mfumo wake wa umeme wa ubongo.

Umuhimu wa EBSP’s

Inamsaidia mtu kujua ni kwa kiwango gani, mazingira yake yanamuathiri. Watu wengi sana huwepo katika mazingira ambayo kiuhalisia huathiri kila sekunde ubongo wao. Madhara haya huwa hayajioneshi kwa mara moja, lakini kila siku yanazidi kuua Ubongo kama tutakavyoangalia kidogo hapo chini.

EBSP’s hudhihirisha ni kwa namna gani, kila eneo lenye viwango vinavyofanana vya sifa za kimazingira, hufanana hata kitabia. Watu wengi sana huumwa, huwa wahanga wa shida mbalimbali, huangaika na madawa. Lakini kiuhalisia msingi wa matatizo yao, hutokana na mazingira ambayo huwa wanayaishi kila siku.

Msomaji anapaswa kutambua kuwa, ijapokuwa mtu anaweza patwa na msongo wa Mawazo sana kutokana na kuachana na mpenzi wake. Lakini ukweli ni kuwa, kiwango kikubwa zaidi cha msongo wa Mawazo aliyonayo kimepandishwa zaidi na kiwango cha msongo ambacho alishakuwa akichochewa nacho kila siku katika mazingira yake.

Sehemu hii hatutazungumzia kila tabia, lakini tutagusa miongoni mwa kanda mbalimbali na hatari ambazo wako hatarini zaidi kuwa nazo, kutokana na viwango vikubwa vya EBSP’s kama tutakavyoangalia.                  

NYANDA ZA JUU

KUSINI ‘’NYANDA ZA BARIDI’

Jiografia fupi

Maeneo haya yana baridi kali sana. Kiwango chake cha baridi hubadilika kulingana na usawa wake kutoka pwani ya Bahari. Kwanini maeneo haya yana baridi? Ni kwa kuwa, yapo usawa wa juu sana toka usawa wa chini, au bahari. Hewa katika anga, ni kama maharagwe kwenye maji katika sufuria, huwa mengi sana chini kwenye sufuria kuliko juu, sababu ni ‘’density’’ kubwa huyafanya yatuame sana chini, hewa pia huwa nzito sana usawa wa chini, na huwa nyepesi sana usawa wa juu.

Na hiki kitendo cha kuwa nyepesi sana usawa wa juu, hufanya maeneo ya juu sana kuwa na hewa nyepesi, au presha ya anga ndogo, au huitwa ‘’low atmospheric pressure’’. Hii presha kuwa ndogo, husababisha Joto nalo kuwa dogo sana.

Kwa sababu, hisia za Joto hazitokani na mionzi ya moja kwa moja ya joto toka kwa jua, bali inatokana na mionzi ya jua kuichoma dunia, na kisha dunia kuzalisha joto ambalo watu hulihisi kupitia hewa inayochemka sasa kutoka katika dunia. Hewa ya joto inapokugonga ndipo inakuchochea kuhisi joto. Hii hewa kadri inavyopanda kuelekea juu huzidi kupoteza nishati au joto lake, na inapofika juu kabisa, huwa ya baridi sana kama ilivyomiji mingi ya nyanda za juu.

Kuelewa hili, vuta picha unajipulizia spray, utaona unahisi sana baridi, kwanini? ni kwasababu, ndani ya chupa ya spray kuna presha kubwa maana imejazwa sana, na kadri inavyojaa sana ndivyo molekuli zake zinapogongana sana, na kuwa za moto sana, ila nje unapoipulizia, kuna presha ndogo sana, hivyo unavyoipuliza spray, zile molekuli za hewa hutanuka sana kwa kuwa nje hakuna mgandamizo tena, na hapo inapojitanua, kama wewe unapojitanua kitandani unapohisi sana joto, basi hupoteza joto lake haraka sana, na huwa ya baridi sana kama unavyohisi inapokugusa. Hivyo ndivyo ulivyopia upepo pale makambako unapokugusa, huo upepo ungekugusa ulipokuwa pale chalinze au Bagamoyo, usingeuhisi wa baridi, lakini ulipopandisha mlima kitonga, ulipoteza joto jingi sana.

Kwa maeneo kama ya milima kama Kilimanjaro, unaweza ona Barafu kabisa. Hii ni kwasababu, kiwango kidogo cha hewa husababisha presha kuwa ndogo sana, na joto kuwa dogo sana. Na hivyo basi, mvuke wote unaoweza pita maeneo haya ukiwa umebebwa na upepo huganda kama vile mvuke unavyoganda kuzunguka chupa ya soda ya baridi sana inayowekwa mezani.

Maeneo haya huwa hayana mvua nzito kama maeneo ya nyanda za chini kusini. Hii ni kwakuwa, kwanza hupokea mvua kwa pande zinazotazamana zaidi na upepo. Na pili, bado anga lake kuwa jepesi, tena lenye baridi sana, husababisha mvuke mwingi wa maji kuwa katika namna ya kama vumbi la barafu ‘’fog’’, (rejea namna maeneo haya yanavyoonekana yakiwa yamejawa na mvuke, hata usione mbele wakati mwingi sana). Hii inamaanisha, anga lake halina uwezo wa kubeba kiwango kikubwa cha hewa ya mvuke hata kuja kutengeneza mvua nzito.

Na hivyo maeneo haya, huwa na mvua nyepesi nyepesi. Na kitendo cha anga lake kuwa jepesi humaanisha pia kuwa, hata kiwango cha hewa ya oksijeni huzidi kupungua kadri unavyopanda kuelekea juu zaidi. Kwa pande ambazo huwa nyuma ya upepo ‘’leeward side’’, huku hupokea mvua chache zaidi, na huwa kukame sana.

Maeneo haya huwa hayana misitu mizito sana. Hii ni kutokana na kuwa na mvua na maji kidogo. Huwa hakuna mito mikubwa sana maeneo haya, ila huwa kuna chemichemi na mito midogo. Huwa kuna viumbe wachache sana katika mbuga ndogondogo katika maeneo haya. Na wengi wao huwepo maeneo ya chini au bondeni mwa miinuko, au huitwa kwenye ‘’vinyungu’’.

Maeneo haya huwa yana vipindi vifupi sana vya Jua. Huwa muda mwingi sana kukiwa na mawingu, au kukiwa na ‘’fog’’ yaani anga likijaa mawingu. Hii ni kwa kuwa, kwanza hewa inapopaa tu huishia kuunda mawingu kutokana na baridi kali. Pia, kipindi cha usiku, hewa nyingi ambayo huwa ikipaa hewani, hutengeneza wingu la mvuke ‘condense’’, na maeneo haya, anga la hewa la joto huwa juu na la baridi huwa chini, na hujitenga. hii hupelekea mawingu kudumu kwa wakati mrefu sana. Pia jua linapokucha, hupelekea hewa ya joto kupaa ambayo ndani ya muda mfupi tu kwa wakati wa mchana, hupelekea tena kuundwa kwa mawingu.

Maeneo haya huwa na mvua za mara kwa mara lakini zilizo nyepesi nyepesi. Ukijumlisha na hali ya baridi. Maeneo haya huwa yakiwa na asili ya ukijani kwa wakati mwingi sana. Na hii huchochea sana kilimo kwa maeneo ya mabondeni, na kando ya vimito vidogo. Maeneo haya huambatana na kiwango kikubwa sana cha miti, aidha ya mwitu, au ya kupanda. Miti yake huwa haiwi mikubwa sana, ila huwa ya wastani mpaka midogo, na hustawi sana. Kiwango kikubwa cha miti na ukijani huchochea kiwango cha oksijeni, na mbogamboga nyingi sana na matunda.

Maeneo haya huwa hayana nyasi nyingi za pori. Ni mara chache sana kuona wafugaji wa Wanyama wakubwa kama ng’ombe maeneo haya. Hii ni kwa kuwa, hali zake za ardhi hazisapoti uotaji wa nyasi nyingi sana za kusapoti Wanyama wakubwa. Nyasi nyingi huitaji kina kirefu cha udongo ulioshiba maji, lakini maeneo ya huku huwa na matabaka mafupi ya ardhi Kwenda chini, na huwa na miinuko ambayo ni hatari kwa Wanyama wakubwa. Na pia, mazingira ya wafugaji wengi huwa ni Maisha ya kuishi maporini wakiwa na mavazi rahisi sana, mitindo hii ya Maisha si rahisi kuiishi katika maeneo ya baridi kali.

Kiufupi maeneo haya huwa yana kiwango kidogo sana cha Wanyama, hata na Samaki. Wakazi wengi huwa hawapati protini nyingi za Wanyama kwa kiwango kikubwa kama ilivyo kwa wakazi wa mabondeni.

Mazingira mengi ya nyanda hizi huwa yana utulivu mkubwa sana. Huwa kuna kiwango kidogo sana cha misongamano ya watu, au mikusanyiko ya watu wengi katika eneo dogo kama ilivyo kwa jamii nyingi za kusini. Hii huchochewa pia na hali ya utulivu wa shughuli nyingi kulingana na hali ya joto inavyozidi kuwa ndogo.

Maeneo haya huwa katika ukanda wa Sub-tropiki.

Nini maana ya Tropiki, na Sub-tropiki?

Tropiki ni ukanda uliopo karibia sana na mstari wa equator, yaani ni eneo linalotoka equator nyuzi sifuri, mpaka kufika nyuzi 23.5° kaskazini, na kusini. Maeneo ya Tropiki mfano Morogoro, huku tropiki ikikolea zaidi katika miji ya Dar es salaam, na Zanzibari. Huwa na wastani wa jotoridi wa 25-30°c. maeneo haya huwa na kiwango kikubwa sana cha mvua, na mvua zake huwa sio za vipindi vya kubadilika badilika. Ukipima kiwango cha mvua katika maeneo haya, kinaweza kufika kuanzia 1200mm, mpaka 2500mm. ni mvua nyingi sana.

Tropiki huwa ni maeneo yenye misitu mizito. Na utaona mimea kama Minazi, Michikichi, miti ikishonana sana. Mazao hukua sana kutokana na uhakika wa maji. Maeneo haya hushamiri sana kwa kilimo kama cha Mpunga unaohitaji maji, mihogo, Cocoa, Kahawa, Miwa, michikichi, na matunda kama maembe. Morogoro wanalima sana Mpunga, na hata mahindi, ijapokuwa uzalishaji wake hauwezi shindana na wa shinyanga, au Mwanza.

Kwanini Iringa na Mbeya Zinaongoza Uzalishaji wa kilimo Tanzania?

Ijapokuwa sub-tropiki ni maeneo yanayoanzia nyuzi 23.5° mpaka 35° kusini na kaskazini mwa equator. Na tunategemea maeneo haya kuwa na mvua za msimu, kuwa na wastani wa nyuzi joto za 20-30°c kulingana na msimu. Maeneo haya huwa hayana sana mvua nyingi, huwa na maeneo makubwa ya usavana kuliko tropiki.

Na maeneo haya ya Iringa, Njombe na Mbeya, na Songwe, kulingana na hali zake za baridi na mvua za msimu, yanaweza kuzalisha sana kilimo cha mazao yasiyohitaji mvua nyingi sana, matunda matunda mengi kama machungwa, zabibu, ‘’citrus fruits’’, maparachichi, chai, mahindi, ngano, na mbogamboga.

Kwanini sasa maeneo haya yanayazidi maeneo ya tropiki kiuzalishaji?

Sababu ni kuwa, maeneo haya ya tropiki huwa na mvua kubwa sana ambazo, hupelekea mmomonyoko wa udongo, na kupelekea ardhi kupungukiwa sana virutubisho. Unaweza kuona namna ambavyo mikoa kama ya Morogoro namna ambavyo hupatwa sana na majanga ya mafuriko, na hata udongo wake ni mwekundu kwa maeneo kadhaa. Changamoto hizi zote hutokana na kiwango kikubwa cha mvua.

Pia, maeneo haya huwa na joto, na mvuke mwingi sana. Ambao, huchochea sana kushamiri kwa vimelea vya magonjwa ya mimea ‘’pests’’, na magonjwa ya mimea kwa ujumla. Hii ni tofauti kabisa na mikoa ya sub-tropiki, ambayo, kiwango kikubwa cha baridi, huchochea sana kutoshamiri kwa vimelea, na magonjwa. Na hii huyafanya kuwa na uzalishaji mkubwa zaidi. Bado maeneo ya sub-tropiki huwa na hali ya baridi ambayo, hupunguza kukauka kwa mimea, na jamii nyingi hutumia namna za umwagiliaji katika kilimo.

Hii pia hufanyika nyanda za juu kaskazini, na ndiyo sababu ya Kilimanjaro na Arusha bado kuwa juu kiuzalishaji kuzidi Morogoro na Pwani. Kumbuka, ukame huathiri sana kilimo kwa maeneo ya nyanda za juu, lakini madhara huwa makubwa zaidi kwa ukame katika maeneo ya kusini ambao hulima sana mazao ya muda mrefu, na huwa hawatumii sana namna ya umwagiliaji.

BIOLOJIA ZA WATU KWA ASILI KWA MAZINGIRA YA KUSINI JUU.

Kufanya Sana Kazi na Kuwa na Nguvu.

Watu wa maeneo haya huwa wanafanya sana kazi. Hii ni kwa kuwa, hali nzuri ya hewa isiyo na jua kali sana, huwapa muda mwingi sana ndani ya siku wa kuweza kufanya kazi. Maeneo haya huwa na baridi kali sana, ambayo, huwa haisapoti sana kulala sana, watu wengi wa maeneo haya hata kufanania na ulaya, huwa na usingizi wa juujuu sana, ambapo inapofika asubuhi, huwahi kuamka na kuingia kazini, wakifanya kazi hata muda wa jioni sana.

Maeneo haya kutokana na mazingira yake kijiografia, vituo vingi vya huduma huwa mbali sana na makazi ya watu. Unaweza kuta makazi ya mtu mmoja mmoja mpaka kufika shuleni, au shambani, au hospitalini, au popote pale, kunahusisha mabonde, au milima. Hii huwafanya watu hawa kuwahi sana kuamka, na kutumia nguvu sana hata kufika katika maeneo husika.

Itamhitaji mtu kukusanya kuni za kutosha kwa ajili ya kupata moto kipindi cha baridi, kulima mlimani ni kazi ngumu kuliko bondeni, kutokana na ugumu wa ardhi. kutoka sehemu moja hata nyingine katika jiografia hii huwa ni shughuli ndefu sana, watu wa maeneo haya huwa wakiishi mbalimbali kwa wastani, hivyo watu hujitahidi sana kufanya kazi sana, ili kupunguza utegemezi wa vitu vidogo vidogo kwa wengine kama ilivyo kwa watu wa maeneo ya chini pwani.

Watu wa maeneo haya huwa ni watu wenye nguvu sana. Hii hutokana na Maisha yao ya kimazoezi kila siku, lakini kutokana na lishe zao. Watu wa maeneo haya huwa na lishe bora sana zinazotokana na matunda mengi, mbogamboga nyingi sana, na protini toka kwa Wanyama na mimea. Kwa Nchi kama ya Tanzania mara nyingi zaidi Ghala za Nchi nzima huwa zikijazwa na watu wanaoishi toka katika kanda hizi za juu kusini. Kuna wakati watu wa maeneo haya huwa hata wakiwa hawana muda sana na Watoto wao kwa namna wakiamka tu, hudamkia mashambani, na hiyo hupelekea changamoto baadhi za afya kwa Watoto.

Kuwa na Mapafu imara na Mwonekano wa wastani wa Ufupi.

Mara nyingi hata kwa takwimu za watu wanaoishi miinuko ya Himalaya, Andes, na Ethiopia. Watu wa maeneo ya nyanda za juu zenye baridi, huwa na maumbo ya ufupi kwa lengo la kupunguza saizi ya mwili usipoteze joto sana kutokana na baridi kali. Maeneo ya miinuko huwa na oksijeni chache kwa wastani ukilinganisha na maeneo ya mabondeni, hii huyafanya mapafu ya watu hawa kuongezeka ukubwa ili kuweza kuchakata zaidi oksijeni iliyopo katika anga lao.

Kuwa Na Mwonekano wa Weusi

Kutokana na anga la maeneo ya nyanda za juu kuwa na kiwango kidogo sana cha hewa, au kuwa jepesi. Mionzi mingi sana ya ‘’UV-Rays’’ hulipita anga hata kuweza kuwakuta watu wa maeneo haya. UV-Rays husababisha uzalishaji mkubwa sana wa Melanin, kwa lengo la kujikinga na mionzi hii. Melanin mara zote hufyonza mionzi, na kupunguza madhara yake kutoathiri moja kwa moja tishu za ndani ya Ngozi. Kadri melanin inapozalishwa, ndipo mwonekano wa Weusi unapoongezeka.

Watu baadhi huchanganya kwa kuhisi kuwa ni baridi inayochochea mwonekano wa Weusi. Si kweli! baridi hata Ulaya ipo kali zaidi lakini watu wa kule ni weupe zaidi. Ni mionzi ambayo maeneo ya nyanda za juu huwa kwa wingi zaidi, kutokana na kupita kiurahisi. Maeneo mengi ya Afrika ya kaskazini, na Ulaya-Asia, huwa kwenye Latitude ambazo zipo mbali na equator, na Jua huwa lipo mbali kidogo kutokana na kukunjika kwa umbile la dunia katika maeneo kuelekea kaskazini. Hii hupelekea mionzi kutembea kwa umbali mrefu zaidi, na kadri inavyotembea umbali mrefu, basi hupoteza sana nguvu, na hata inapofika, watu wa maeneo haya kutokana na baridi kali, huwa wakivaa nguo za kujifunika sana, hivyo hupata mionzi kidogo sana, na huzalisha melanin kidogo sana, na huwa weupe sana.

Kuwa na Kinga sana ya Mwili

Kwanza kabisa baridi huupa mwili kiwango kidogo cha stress ambayo, huuchochea mfumo wa kinga kuwa imara zaidi. Hiki kitendo kitaalamu kinaitwa ‘’hormesis’’. Lakini matendo kama ya kutetemeka huambatana na uzalishaji wa protini kama ‘’Irisin’’ ambayo ina umuhimu sana katika afya ya matendo mengi sana ya kibiolojia, ambayo mtu angeyapata angefanya mazoezi tu, lakini kutetemeka tu huizalisha kwa wingi sana. Mafuta bora kabisa yanayoitwa ‘’Brown Fats’’ huzalishwa katika maeneo ya baridi, na uzalishaji wa mafuta haya, huambatana na uzalishaji wa chembechembe za kinga zinazoitwa ‘’cytokines’’, hizi huboost zaidi mfumo mzima wa kinga.

Bacteria wengi, virusi, fangasi, protista na minyoo. Huwa kama wamehifadhiwa kwenye friji katika maeneo ya baridi kali. Baridi huwapunguzia sana spidi ya kuzaliana, na pia spidi ya kuambukiza. Hii huifanya mifumo ya kinga ya wakazi wa maeneo haya, kuwa imara sana.

Mara mtu ametetemeka na kupelekea mishipa ya damu kuingia ndani zaidi ya Ngozi ikijikunyata ‘’vasoconstriction’’, au ghafla baridi imepungua, mishipa ya damu sasa ime relax tena, sasa imefanya ‘’vasodilation’’ ikitokeza sana nje na ngozi. Mfululizo wa matendo haya, hupelekea watu hawa kuwa na mfumo imara kabisa wa damu.  Na pia inatambulika kuwa, baridi kali huchochea uzalishaji wa seli nyekundu za damu ‘’RBC’s’’, ambazo, husaidia kukusanya zaidi hewa ya oksijeni.

Mfumo wao wa upumuaji upo imara sana, mapafu yao huwa makubwa sana yakiweza kutoa uchafu kirahisi sana. Na hii hupunguza sana kusambaa kwa vimelea vya magonjwa ya mfumo wa upumuaji.

Inatambulika pia kuwa baridi huchochea sana pia uzalishaji wa seli nyeupe za damu ‘’leucocytes’’.  Na pia, baridi hupunguza uvimbe, kama tu wachezaji wanapojiwekea barafu wanapovimba.  Hivyo baridi husaidia kupunguza uvimbe sugu.

Pia kutokana na uzoefu wa kawaida wa maeneo haya, huwa kuna kiwango kidogo sana cha hewa chafu, hii ni kwa kuwa, huwa kuna kiwango kidogo sana cha joto, lenye kuweza kupelekea molekuli nyingi za hewa chafu kuunda gesi chafu ‘’evaporate’’ na kuchafua mazingira yote. Hii husaidia sana kupunguza matatizo ya mfumo wa upumuaji.

Tabia za Ulaji

Watu wengi wa nyanda za juu kusini, kutokana na hali ya hewa ya baridi, na jiografia za maeneo haya. Huwa  ni watu ambao hula sana. Hii ni kwa kuwa, ili kuzalisha nishati ya kutosha kupambana na joto linalopotea. Watu wa maeneo haya hula kiwango kikubwa sana cha vyakula vya wanga, kwa wastani, ukilinganisha na watu wa nyanda za chini.

Ulaji wa watu hawa hutofautiana kati ya maeneo na maeneo. Baadhi ya watu wa maeneo haya hupata changamoto kubwa sana ya kupata virutubisho vya kutosha katika mazingira yao, hasa pale wanapokuwa wapo upande unaopokea kiwango kidogo cha mvua. Maeneo hayo huwa na kiwango kidogo cha mimea yenye virutubisho vya kutosha, lakini pia huwa hata na Wanyama wachache kuweza kutosheleza mahitaji ya protini kwa walaji wa nyama. Jamii zenye sifa hizi kuna wakati zimewahi kuonekana kupendelea hata ulaji wa wadudu, au Wanyama wadogo  sana, kwa lengo la kukidhi mahitaji ya upungufu wa virutubisho kadhaa.

Kwa jamii zote ambazo huwa na upungufu wa lishe, au virutubisho, kwa mazingira ya baridi kali na kazi nyingi, yanayohitaji nishati kubwa hasa kwa Maisha ya kila siku ambayo tayari huitaji nguvu nyingi kwenye kanda hizi zenye milima na mabonde, basi watu wa maeneo hayo huishia kuwa na miili midogo, kama namna ya ukuaji mdogo kulingana na deni kubwa la nishati inayoingia ukilinganisha na nishati inayotoka.

SAIKOLOJIA ZA WATU KWA ASILI KWA MAZINGIRA YA KUSINI JUU.

Asili Ya Upole Na Kutowehuka Kirahisi

Wanasaikolojia wote ulimwenguni wanatambua kuwa, kuna uhusiano kati ya Joto, na Hasira au hata Ukatili. Na wao, hutumia kielelezo walichokigundua na kukiita ‘’CLASH’’ yaani, ‘’Climate, Aggression, and Self Control in Humans’’. Sababu wanazotumia kuelezea uhusiano wa joto na ukatili, au hasira, huwa wanauita ‘’Short time life strategy’’. Kwamba, kwa kuwa maeneo ya joto huwa hakuna mabadiliko sana ya hali za nchi ‘’less seasonal variations’’. Basi, maeneo haya watu huwa hawawazi sana kuweka au kuwekeza vitu kwa msimu wa baridi utakapofika, ambapo hawataweza kufanya baadhi ya shughuli.

Kwa hiyo husema, asili hii ya kutowazia sana siku za mbeleni kwa kuwa mara nyingi hali huwa zipo sawa tu kwa wakati mwingi sana. Huwafanya kuwa ni watu wa kufanya vitu kulingana na hisia na uhitaji wao tu kwa wakati huo. Na sio kwa ajili ya wakati wa baadae. Wanasaikolojia hawa wanasema, hii huwasukuma kuwa na tabia kidogo sana ya kujizuia ‘’self-control’’, mfano, anapohitaji kuzaa, atazaa hata Watoto wengi sana, atakapojisikia hasira, atapambana.

Na husema kwa maeneo ya joto ambayo hata viumbe wengi wenye sumu huwepo, tabia hii huwa na faida sana kwa watu, lakini ndiyo huwachochea kuwa wenye tabia za kuripuka kwa kutenda.

Baadhi ya wanasaikolojia katika kielelezo hikihiki wakaongezea tena kwa kusema, kiwango kikubwa cha joto huwafanya watu wengi kuwa nje ya nyumba zao, au kuzurura nje kujikinga na joto kali la ndani. Na kadri watu hawa wanavyokuwa nje mara nyingi, basi huwa na asilimia kubwa sana ya kuwa na migogoro mingi kati ya wao, kwa wao.

Kielelezo hiki kinaelezea uhalisia wa matokeo ya joto, na hisia za kulipuka hasira, au ukatili kwa usahihi kabisa. Lakini kinafeli kwa asilimia kubwa sana kuweza kueleza sababu za msingi za tabia hizi za hasira kwa watu wengi wa maeneo yenye joto kali. Na sababu hizo nitazielezea kiusahihi zaidi katika wakati tutakapoangalia maeneo ya joto. Kumbuka, kielelezo hiki hutumika kuwatenganisha au ‘’group’’, watu wa ukanda wa equator, na watu wa ukanda wa mediterranean, na latitude za juu zote. Hapa unazungumzia maeneo mengi ya Afrika kama watu wa kanda za joto, na watu wa Ulaya-Asia kama watu wa kanda za baridi. Lakini bado kuna ukweli mwingi sana wanaouzunguka, na kuukwepa, au hata kutougundua ambao tutauangalia.

Baridi huchochea hali ya upole, hali ya kutulia, au hali ya kutolipuka kirahisi kwa mihemko ya hasira. Haimaanishi kuwa watu hawa huwa hawalipuki kwa hasira, ila ina maanisha, huwa na uwezo mkubwa sana wa kujizuia. Zipo sababu mbalimbali ambazo huwafanya watu hawa kuwa si wepesi wa kuwehuka.

Kwanza kabisa, ni uwezo wao mkubwa wa kustahimili presha ya damu, ambapo hasira huanza na mlipuko wa mfumo wa ‘’Sympathetic nervous system’’, ambapo mwili huzalisha chembechembe za ‘’adrenaline’’ za kutosha ambazo huchochea presha ya damu, na sehemu katika ubongo ‘’amygdala’’ husisimka juu sana ikichochea motisha ya matumizi ya misuli hasa ya mikono, na misuli mingine kama ya mapafu kubana hewa nyingi, kwa ajili ya kupambana, na matendo haya, kwa watu wa maeneo ya baridi, huwa hayana urahisi wa kusisimka kwa kuwa, nishati kubwa sana hutumika kuanzia katika kuuchochea mwili upate joto la kutosha la hasira, mishipa ya damu ijitanue ili hali kuna baridi, mfumo wa damu uongeze spidi kufika hata katika ubongo, au adrenaline isambae vya kutosha katika mwili mzima, na watu hawa huwa na mifumo mizuri sana ya damu, hivyo hata presha huwa haina nguvu sana ya kuwachochea. Wengi wao pia sio wala nyama sana, hivyo kiwango kidogo cha ‘’SFA au Triglycerides’’ huwafanya kuwa na uwezo mkubwa sana wa kubalansi presha yao, hii huwafanya kutolipuka kwa urahisi kama upande wa watu wa kwenye joto.

Chukulia mfano huu, una watu wawili. Mmoja ameshashuhudia ndugu yake akiuwawa kwa kupigwa risasi kwa bunduki, na mwingine hajawahi kushuhudia. Ikitokea watu hawa wakasikia risasi zikipigwa nje tu na eneo walilopo, yupi atakayesisimka sana? Jibu bila shaka ni yule aliye na historia na risasi. Hivyo hivyo, watu wa maeneo ya baridi kwa asili huwa na mihemko ya chini kutokana na usumbufu wa mazingira yao kuwa mdogo, hata anapokutana na usumbufu, huwa anatumia muda mrefu, na kuwa na uwezo mkubwa sana wa kuji control. Hii ndiyo ile niliyoiita ‘’low environmental-brain sensory potentials’’.

Msukumo Mdogo Wa Utandawazi na Teknolojia

Maeneo mengi sana ya nyanda za baridi kusini, huwa na kiwango kidogo nyuma cha teknolojia na utandawazi ukilinganisha na maeneo ya pwani chini. Sababu kubwa sio watu kuwa hawapendelei hatua hizi. Bali ni wawekezaji wengi ambao huvutiwa zaidi na maeneo ya pwani, na miji ya kati, ambayo, huwa na kiwango kikubwa sana cha watu, ambao kwa wao, huwa na faida kubwa sana za kibiashara.

Tabia nyingi na mitindo mingi sana ya usasa, haiendani na maeneo ya baridi kali sana. Hii ni sababu iliyojificha ya sanaa na usanii ‘’Media’’’ nyingi sana kutawaliwa sana au zaidi, na watu wa Marekani, na watu wa Afrika. Hii ni kwa kuwa, ni rahisi sana kwa binti kuvaa nusu uchi katika mazingira ya joto, tena akiwa pwani ya Bahari, lakini sio rahisi kwa binti huyu kufanya hivi akiwa njombe milimani. Mazingira ya baridi huchochea sana matumizi ya misuli, na kujiandaa kujikinga na  baridi, zaidi ya usanii wa kifua wazi ukirekodi studio. Kumbuka pia, maeneo mengi ya baridi kali, huwa hayana msongamano mkubwa wa watu, hii ni kwa kuwa, maeneo ya kujenga huwa yakitenganishwa sana na mabonde na milima, hii hupunguza nguvu kubwa ya utandawazi kwa watu.

Uwezo Mkubwa Wa Kitaalamu Na Kitaaluma.

Hata baada ya wengi wa marafiki zangu kutoka Denmark katika mafunzo yao ya ‘’Internship’’, wengi wao hukiri kuwa mfumo wa Maisha katika miji ya baridi, huusisha watu walio serious sana na kazi zao, kwa mara nyingi zaidi. Hivyo hivyo ndivyo ilivyopia hata katika miji yetu, ni rahisi kukuta ‘’Vigoma vya Vigodoro vikipigwa hata kila siku kwa miji kama ya Ifakara, Morogoro, pwani, Dar es salaam, n.k. miezi fulani’’ lakini sio rahisi kukuta vigoma hivi kwa miji kama ya Mbeya, songwex, tunduma, Iringa, na Njombe. Ni rahisi Ifakara kukuta wazee wakianza kucheza Draft saa 4 za asubuhi, lakini huwezi kukuta jambo hilo Sumbawanga, au Iringa.

Miji mingi ya nyanda za juu zenye baridi, huusisha watu ambao huwa wapo serious sana na kazi zao. Hii huwapa faida za kuwa bora sana katika kazi zao, au taaluma zao. Ukifika nchi ya Tanzania na ukawa ukipitia wanafunzi wa mikoa mingi sana ya nyanda za baridi, kuanzia kaskazini, mpaka kusini. Na kisha ukaanza kupitia nyanda za chini kati, mpaka pwani. Utagundua wanafunzi wengi wa nyanda za juu wakiwa serious sana na elimu, huku wengi wa wanafunzi wa nyanda za kati mpaka pwani wakiwa ni vijana wa usasa mwingi, na utandawazi.

Taaluma na Utaalamu huitaji sana mazingira yaliyotulia sana. Huitaji usumbufu mdogo sana toka kwenye mazingira, na toka kwenye jamii. Baridi huchochea uwezo mkubwa wa kukesha usiku kwa kazi, na pia huchochea ufanyaji kazi kwa muda mrefu. Haya yote, huchochea katika kuwafanya watu wengi wa maeneo ya baridi kuwa na ubora mkubwa sana. Lishe bora ya mbogamboga na matunda ya asili, matumizi kidogo ya protini za Wanyama, na uwezo mkubwa wa kimisuli na nishati, huchochea watu wengi wa maeneo ya baridi kufanya vizuri zaidi katika taaluma, na kazi zao.

Maendeleo Makubwa

Miji mingi ya baridi hata leo, na hata katika mabara ya mbali, huwa na maendeleo makubwa sana. Hii ni kwa kuwa, huwa kuna maeneo makubwa bado yakiwa na nafasi ya watu kujenga, na kuwekeza. Miji hii tokea zamani haikuwa na watu wengi, na hivyo bado huwa na maeneo makubwa sana ya uwekezaji.

Miji ya pwani ambayo ilishajaa tokea zamani, huwa na ushindani mkubwa sana wa kupata nafasi za uwekezaji. Vijana wengi hukimbilia miji ya pwani kwa kuwa ni rahisi kupata kazi, na kupata fedha za kukidhi mahitaji ya msingi. Lakini hata hivyo, miji ya pwani huwa haina uwezo wa kumuwezesha kijana akakua kwa kiwango kikubwa sana kwa kuwa, huwa haina nafasi, wala malighafi za kumtosheleza mtu mmoja tu hata akafika mbali sana kiukuaji wa kiuchumi, na kijamii, tofauti na miji ya baridi, ambayo mingi yake haina ushindani mkubwa, lakini changamoto yake kubwa katika uwekezaji ni matumizi  makubwa ya nguvu, na wakati katika kuanza.

CHANGAMOTO ZA KISAIKOLOJIA ZA WATU WA NYANDA ZA JUU KUSINI