Jipatie maarifa kutoka vitabu bora vilivyoandikwa na Dr Brighton shoo kuusu imani, sayansi, afya, teknolojia, asili, malezi, saikolojia na mazingira

MUZIKI WA KISASA UNAVYOUA UBONGO

MUZIKI WA KISASA  UNAVYOUA UBONGO Q42

UTANGULIZI

Miongoni mwa taalumu ambazo zimekuwa na utafiti mkubwa sana, ni juu ya sayansi ya muziki katika Ubongo. Hii taaluma ni pana sana, hii ni kutokana na kuwa na sehemu kubwa mbili. ambazo zote, zinahitaji utafiti mkubwa. Sehemu ya kwanza ni madhara ya muziki na sauti moja kwa moja katika ubongo. lakini pili, ni namna ambavyo muziki unavyochakatwa, na kuleta matokeo mbalimbali katika ubongo. Tukianza na sehemu ya kwanza, tutaangalia nini hasa hutokea katika ubongo pale mtu anaposikiliza muziki.

Kabla hatujaendelea ni muhimu kwanza kutambua sehemu ya muziki katika ubongo.

Sehemu ya Muziki katika Ubongo.          

Kama utafungua Ubongo kama inavyoonekana picha chini, basi kinachoonekana ndicho ‘’Auditory cortex’’, ambayo, imejipanga kwa frequency kama nota, ambazo ni mfano pia wa namna ambavyo huwa zikijipanga katika ‘’cochlea’’. Kwa Binadamu kwa kufatilia majina maalumu ya kila sehemu ya Ubongo, sehemu inayohusiana na Muziki, inapatikana upande wa pembeni wa Heschl’s gyrus na sehemu ya mbele pembeni ya A1 au ‘’primary auditory cortex’’. Kwa hiyo Muziki una eneo maalumu na sio tu kwa binadamu, bali kwa mammalia wengi kama vile nyani, mbwa, paka na wengineo

.ENEO LA KUCHAMBUA LUGHA  NA KUZALISHA SAUTI, YOTE YANACHANGAMANA NA UBONGO WA SAUTI

Haishangazi kuona eneo linalohusiana na kutambua maana ya maneno ‘’language comprehenssion’’ ambalo huitwa ‘’wernicles area’’ liponyuma tu ya ‘’auditory cortex’’, lakini pia eneo linalohusiana na kutoa sauti ‘’speech production’’ linaloitwa ‘’Broca’s area’’, nalo lipo mbele tu ya ‘’Auditory cortex’’ .

Na kwa kutumia neurons zinazoitwa ‘’arcuate fibers’’, inawezekana kwa sehemu hizi za ubongo kuwasiliana moja na nyingine

                                    


PREDICTIVE CODING MODEL

Hii ni nadharia maarufu zaidi katika sayansi za Ubongo, iliyoletwa na miongoni mwa wanasayansi wakubwa sana wa Ubongo, ‘’Neuroscientist mwanamuziki Peter Vuust’’ na wenginewe ikiwemo ‘’Maria A.G. Witek’’. Wanasayansi hawa waligundua kuwa, Ubongo una asili ya kukadiria matukio yanayofuata kwa kila tendo linalofanyika. Nadharia hii siyo mpya katika namna ya kimtazamo, maana tayari yalishakwepo masomo ya mfanano wake. Nadharia hii imechochea namna bora zaidi ya kuelewa namna ubongo unavyochakata ‘’matendo na mtazamo’’ kwa mfuatano au ‘’action-perception’’.

Nadharia hii rahisi sana kueleweka ina maanisha hivi, mfano ukiwa unamwangalia mchezaji wa mpira anakimbia na mpira huku akimwangalia kipa, ubongo hukadiria tayari matokeo ya kuwa atapiga atakapofika sehemu Fulani. Ubongo siku zote hukadiria matokeo yatakayo fuata hata kabla hayajatokea, kwa kutengeneza kielelezo cha matendo kipindi yanatendeka. Hii ni sawa na ukiwa unaandika kwa kutumia smartphone yako maneno kama haya ‘’I will come brother’’, kama utaandikia watu kadhaa sms hii, baada ya muda, utakapoanza tu kuandika ‘’I…’’ basi yatakuja maneno chini ya ‘’will, come, brother’’. Hizi ni algorithms za computer, namna zinavyojifunza, na kuunda kumbukumbu au memory. Na ndivyo ilivyo pia kwa ubongo. Unapokuwa unasikiliza muziki wa msanii Fulani ukiimba, ubongo huwa unatengeneza kumbukumbu katika namna ya kielelezo au ‘’Model’’. Model hii hutengeneza namna mabiti ya muziki yanavyoenda, yaani namna yanavyopiga na kuachiana muda, lakini pia hutengeneza kielelezo cha namna ambavyo frequency za muziki zinavyopiga, hutengeneza namna viwango vya sauti vinavyopishana ‘’Intensity’’ na hata nguvu ya midundo ya sauti ‘’music tone’’. Kwa hiyo hebu chukulia taswira ukiwa unaimba huu wimbo.

‘’TanzaniaTanzania   ,Nakupenda kwa Moyo wote’’                                                                            ‘’Nchi yangu Tanzania  ,????………………………………... ‘’

Hata kama mtu atakuwa hajui mstari au ‘’verse’’ ya mwisho katika mstari wa chini wa huu wimbo, tayari atakuwa ana uwezo wa kukadiria namna ya mabiti yatakavyokuwa katika mstari huo. Hiko kinacho muwezesha mtu kuweza kukadiria namna ambavyo muziki utakuwa katika verse hii, ndiyo ‘’Model’’ ambayo Ubongo huwa unaitengeneza popote pale unapokuwa ukiusikiliza muziki. Kila muziki unapokuwa ukiusikiliza, huwa unatengeneza model ya aina yake, na kutokana na hii model, ndipo tunapopata majibu yote ya msingi kuhusu tabia ya muziki na fiziolojia za utendaji wa ubongo.

Picha hii ni kielelezo kikubwa zaidi cha hii ‘’predictive coding’’. Katika hiki kielelezo, miongoni mwa  vitu ambavyo ni vya muhimu ni hisabati zinazoitwa ‘’Bayesian inference’’. Hizi ni hesabu ambazo, kwa huku hutumika kama kielelezo cha namna ambavyo, Ubongo kuchukua wastani wa mapigo ya muziki ambayo, yana msukumo  mkubwa zaidi katika kujenga kielelezo chake. hii ni sawa na kusema, sio kila biti hutumika kama kielelezo. Lakini pia katika usikivu huu. huwa kuna upendeleo au ‘’bias’’ ambayo, hutokana na asili ya nje ya mtu, kama vile jamii, tamaduni, nini mtu husikiliza mara nyingi zaidi n.k, hii ndiyo ile huitwa hamasa ya chini kuelekea juu ‘’down-top effect’’, lakini pia kuna ile namna mtu huvutiwa zaidi kusikiliza kutokana na biolojia yake mwenyewe, au mapenzi binafsi ya mtu na huitwa ‘’top-down’’. Kwa upande mwingine kielelezo hiki ni sawa na uangalie picha zifuatazo chini.

Picha hizi mbili ni sawa kabisa, lakini mtu atakapo angalia picha ya kushoto, ataona kana kama ni vyakula vilivyomo ndani ya beseni ‘’hii ni kutokana na uwepo wa model nyingi za mwonekano huu katika ubongo zikifanania beseni na vyakula’’ lakini picha ya kulia wengi wataona mwonekano wa mtu aliyejifunika kofia inayofanania na beseni, na tena akiwa na madevu mengi’’ hii nayo haitokani na uhalisia wa picha hii, inatokana tu na model za mionekano ya watu wenye taswira hizo, waliowahi kuonekana na kutunzwa kumbukumbu kwa mionekano yao.

Hii ndiyo namna pia Ubongo siku zote unapokuwa ukisikiliza muziki, huutengeneza model ambayo ndiyo huwa kielelezo cha kukadiria namna ambavyo muziki utakuwa ukipiga.

 SYNCOPATION

Hii ni namna ambavyo, kunatokea makosa katika Ubongo katika namna ambavyo ulikadiria mabiti au muziki utakavyokuwa, na ulivyokuwa baada ya kuifikia sehemu ya muziki kipindi cha usikilizaji. Mfano, hebu tafakari muziki Fulani ukiwa unapiga kwa namna Fulani ya mabiti, na kisha baada ya muda Fulani ukabadilika kwa namna Fulani, na ukawa unapiga kwa namna ya utofauti na awali. Au chukulia mfano kipindi ukiwa unasikiliza nyimbo iliyokuwa ikipiga kwa muundo Fulani, na wasanii wakifatiana na mabiti Fulani, halafu ghafla msanii mwingine akaingia kwa biti la aina ya kipekee, au verse za aina ya kitofauti na awali. Hapa kinachotokea ndicho kinachoitwa ‘’syncopation’’. Haya makosa huwa yanaitwa ‘’prediction error’’. Yaani hapa kinachotokea ni badiliko la muziki tofauti na ubongo ulivyotegemea. 

SYNCOPATION  KATIKA MUZIKI

MELODY

Hili ndilo wazo la muziki ambalo utalipata kwa kusikiliza tu ‘’verse’’ ya kwanza. Kwa mfano, katika shairi la wimbo wa Tanzania

‘’Tanzania  Tanzania   ,Nakupenda kwa moyo wote’’                                                                     ‘’Nchi yangu Tanzania, Jina lako ni tamu sana’’                                                                          

katika verse ya kwanza kabisa, huo mtiririko wa sauti ndiyo ‘’melody’’ nzima ya wimbo huu. Mtu anaposikiliza muziki wowote ule, huwa anatafuta kwanza kiini cha sauti za muziki, na hiko ndicho melody, hiko ndiko huunda msingi au ‘’framework’’ ya muziki wote mpaka unapoisha.  Hili ni eneo la kwanza kabisa, ambapo mtu anaweza kulibadilisha kwa kiwango Fulani, na kupelekea ‘’prediction errors’’ au syncopation. ambazo kwa kiasi cha kawaida sana, zinaweza kuleta msisimko, lakini mara nyingi sehemu hii, huwa haibadilishwi sana na hivyo kutokuwa msingi sana wa usisimuaji.

HARMONY

Hivi ni vichocheo vya Ladha ya muziki. Hivi huongezwa katika melody ya muziki. Katika muziki unaweza pata mamia ya vichombwezo. hasa katika miziki ya kizazi kipya. Harmony katika muziki zinaweza kuwa katika namna ya mabiti sindikizi ya muziki, au zinaweza kuwa sauti za mapigo yanayopiga kama ‘’background beats’’, sauti za vinanda, midundo ya ngoma n.k.

Harmony sio msingo wa melody ya muziki. lakini huiongezea Ladha, na kwa mantiki hii sasa, mtu angeweza kuweka harmony katika hatua yeyote ile ya muziki. na kwasababu hiyo, akapelekea kuwepo kwa ‘’prediction errors’’, au syncopation, ambazo, miongoni mwa matokeo yake ni msisimko na kuhisi Ladha ya muziki

RHYTHM

Hii ni namna ambayo vina vya muziki, vinakuwa na sauti zinazofanania kimapigo, kwa kila baada ya vituo. Hizi rhythms unaweza ziona kupitia maneno katika muziki, au kupitia mabiti ya muziki. Hapa unaweza tengeneza ‘’syncopation’’ kwa kubadilisha mfuatano huu kwa kiwango Fulani.

Rhythms katika Ubongo, zina matokeo makubwa sana. kwa sababu, mwili wa binadamu pia una utendaji ulio katika muundo wa ‘’rhythms’’ mfano, mapigo ya moyo huwa yana rhythms, uhemaji una mapigo katika kutoa hewa nje na kuingiza ndani, mapigo ya mfumo wa umeng’enyaji ( tumbo, utumbo na mfumo wote huwa una mfululizo wa mapigo ambayo ni matokeo ya kujikunja na kujilegeza ili kukisogeza chakula mbele zaidi), pia Ubongo una mawimbi ya aina mbalimbali. Kwa ujumla mawimbi yaliyo katika mfanano wa sauti za muziki ‘’rhythms’’ yana ambatana sana na utendaji mzima wa fiziolojia ya mwili.

Makosa haya huwa katika ngazi mbalimbali. kuanzia katika makosa makubwa sana ‘’high prediction error’’ kama pale ambapo biti lina badilika kabisa au halieleweki, kuna makosa ya kati ‘’moderate prediction error’’  kama pale ambapo  Producer anaongezea mbwembwe, kwenye melody za muziki. au DJ au MC au msanii anaweka vichochea, na kubadilika badilika katika staili za uimbaji. pia kuna makosa ya chini kabisa ‘’low prediction error’’ kama pale ambapo wimbo unakuwa hauna mabadiliko badiliko mengi katika uimbwaji wake, au muziki wake.

MATOKEO YA SYNCOPATION

Ubongo hufurahia sana syncopation. huwa ukiongeza msisimko wake wa furaha kuanzia makosa kidogo, na kuwa na msisimko mkubwa sana kwa makosa ya kati ‘’moderate prediction error’’. msisimko wa Ubongo huwa mdogo mpaka kuisha kabisa kwa makosa makubwa kabisa ‘’high prediction error’’.wanasayansi wengi wa Ubongo wamejaribu kutafuta sababu za msingi zinazopelekea Ubongo kusisimka zaidi, kwa makosa haya ‘’prediction errors’’. lakini mtazamo pekee unaotambulika mpaka sasa kwa wanasayansi wa Ubongo, ni kuwa ‘’Ubongo huongeza msisimko wake siku zote kunapokuwa na makosa, kwa sababu ya kujifunza zaidi’’

Hii ni sawa na kusema ‘’unapokosea, ubongo huongeza msisimko wake kwa lengo kuu moja la kukuhamasisha, ili uwe makini na ujifunze zaidi’’, Ubongo siku zote hupenda kujifunza vitu vipya. Ubongo haupendelei kurudia rudia taarifa zinazofahamika, na hii ndiyo sababu yake ya kutovutiwa sana na mapigo ya muziki yasiyobadilika badilika ‘’very low prediction error’’. Jibu hili ijapokuwa linatokana na mtazamo unaoaminika zaidi wa kisaikolojia, lakini unaungana na nadharia yangu kubwa zaidi niliyoielezea katika kitabu changu cha injili ya sayansi sehemu ya pili, ambapo nilielezea kuwa, Ulimwengu huwa na asili ya kuvutwa kuelekea kwenye utofauti, ambako ndiko kwenye msingi wa thamani za upendo’’.

Ubongo huzalisha homoni za Dopamine za msisimko kwa wingi sana, pale kunapokuwa na ‘’syncopation’’, na misimko hii huanzia ndani kabisa ya ubongo, katika mfumo unaoitwa ‘’mesolimbic dopaminergic system’’ mfumo huu ndio msingi wa hisia za msisimko kwa muziki, lakini hasa kwa kusisimua kwa mfumo mwingine unaozalisha hisia za raha katika ubongo ‘’endogenous opioid system’’, ambao, huzalisha kemikali za raha pale mtu anaposikiliza muziki. kinachotokea ni namna ambavyo, mtu anapokuwa akitegemea biti liende kwa namna Fulani, kama litabadilika kiaina Fulani hivi, basi mtu huyo ubongo wake utasisimka kwa kuzalisha kiwango kikubwa cha homoni ya dopamine. Mfumo huu wa dopamine unahusiana na mfumo mzima wa hisia ‘’limbic system’’, na hii ndiyo sababu ya mtu kusisimka kwa kusikiliza mabiti haya.

RHYTHM NA METER

Haya ni maneno yanayofahamika sana kwa kila muimbaji, kama yatatafsiriwa kwa Kiswahili kama ‘’rhythm’’ kumaanisha ‘’kujirudia rudia kwa sauti za kumuziki’’, nyimbo isipokuwa na ‘’rhythm’’ maana yake haina vituo vinavyofanana kwa mtiririko wa sauti ‘’vocal sounds’’ na kwa upande wa ‘’meter’’, hapa tunazungumzia mgawanyo wa kipindi cha muda kwa kila mfuatano wa ‘’rhythms’’ Fulani.

Hivi ni vitu vya msingi kabisa, ambavyo, Ubongo huvizingatia pale unapokuwa ukisikiliza muziki. Inapotokea kuna badiliko katika mifuatano hii, hiyo ndiyo hasa sababu ya ‘’syncopation’’ .

LADHA YA MUZIKI ‘’GROOVE’’

Hii ndiyo Ladha ya muziki ambayo mtu anaihisi anapokuwa akisikiliza muziki. Groove inahusisha mfano matokeo ya kisaikolojia yanayotokana na usikilizaji wa miziki kama ya hip hop au funk na mingineyo ambayo huwa na ‘’rhythm’’ ngumu sana ‘’complex’’ ambazo hupelekea hisia za misisimko ‘’pleasurable drives’’ ya miondoko. kama kucheza, au kurukaruka, au kukimbia ‘’Urge to  Move’’ ambapo hisia hizi huwa ni matokeo ya mapigo yake.

Matokeo haya huwa yanahitaji midundo ya kiufundi sana katika kutengeneza rhythms, au Ladha za vina vya muziki. ‘’rhythmical complexity’’. Ladha hizi katika miziki mingi ya namna hii husababishwa pia na kubadilika kabisa kwa midundo ya kivina ‘’cross rhythms’’ mfano ni namna ambavyo unaweza kuta ‘’Msanii akirap au akiimba kwa spidi kubwa sana, na kisha biti likabadilika kwa muda,  na baada ya muda biti linajirudia lile kama la awali, na msanii anabadilisha staili tena’’, hizi ndizo ‘’cross rhythms’’ ambazo  ukichanganya na kitu kitu kingine, katika ubongo kinachoitwa ‘’Microtiming’’, ambayo ina maanisha tofauti ndogo ndogo, zilizojaa katika mapigo ya kimuziki, ambayo muda wote yanakuwa yakipelekea ‘’prediction errors’’ ambazo kwa ujumla wake wote, basi hupelekea kiwango kikubwa sana cha msisimko.

POLYRHYTHMS

Kwa miziki kama ya Jazz, na mingineyo unaweza ona sifa ya uwepo wa ‘’Rhythms’’ nyingi sana, kiasi kwamba ikawa ni vigumu hata kwa msikilizaji kugundua ule mfuatano wa vina, kwa kila baada ya muda ambao unaitwa ‘’meter’’. Polyrhythms hufanya Ubongo wa msikilizaji muda wote kutabiri lipi linaweza kuwa biti la muziki baada ya muda Fulani, maana hakuna ‘’meter’’. Hapa pia huusisha zile ‘’cross- rhythms’’ ambapo, kuna kuwa na ‘’rhythms’’ mbalimbali ambazo, zinakuwa zikipigwa kwa Pamoja au kwa vituo na kuacha Ubongo ukiwa unasikilizia kuwa nini inaweza kuwa ‘’rhythm’’ ya muziki baada ya kipindi Fulani.                        

Zipo meter mbili za kutambua hizi ‘’polyrhythms’’.                                                                       

Triple meter 

katika namna hii kuna kuwa na mapigo yanayoenda na midundo inayoachana  (time signatures)  kwa ¾, ambapo Hapa ni sawa na upige ubao mara tatu katika mkono wako mmoja, kwa wakati huo huo uwe unapiga ubao mwingine mara nne, kwa mkono mwingine. Na mapigo haya kipindi yanapigwa, yawepo mengine yanayoenda na mtindo (time signature) ya 4/4, haya yawe yanapiga kama muitikio wa yale ya ¾, haya ya 4/4 kwa hapa yanaitwa ‘’counter metric pattern’’

Duple meter.                                                                                                                                    Hapa inakuwa ni kunyume na kwenye ‘’triple meter’’, hapa mapigo ya 4/4 yanakuwa yakipiga kama sauti kuu, na yakiitikiwa na yale ya ¾  ambapo hapa, ndiyo yenyewe yanaitwa  ‘’counter metric pattern’’. Inafahamika kuwa duple ndiyo mtindo wa muziki unaopigwa sana, na wasanii wa aina nyingi sana.  Wengine huisi ni kutokana na kuwa, ni mapigo pendwa zaidi kwa miziki ya magharibi za ulaya na marekani.

Upigaji wa mabiti haya kwa Pamoja, hupelekea pia muda mwingine mtu kuhama katika ile namna anavyouhisi muziki, kutokana na Ubongo kuhama katika midundo hii, kipindi cha kusikiliza.

 MUZIKI NA HISIA ZA KUSOGEA, TEMBEA AU CHEZA ‘’URGE TO MOVE’’

Miziki mingi huamsha hisia hizi za kutaka kutumia misuli, unaweza ona namna baadhi ya mabiti yanavyosisimua kucheza, na huku mengine yakitoa morali ya kukimbia. lakini pia kuna mabiti ambayo husisimua hata kutingisha kichwa, au mikono. au miguu, au vidole. Yote hii huitwa kama ‘’urge to move’’.  Hali hizi zote zinatokana na sababu moja kubwa ya kuwa, sehemu zinazochakata muziki katika ubongo, zinahusiana na sehemu zinazochakata miondoko. Tuliona kuwa sehemu zinazochakata sauti, zipo kwa wingi sana katika ubongo, na katika uwingi ule, kwa sehemu kubwa sana, huusiana na sehemu ya miondoko ‘’motor cortex’’.

Kuna channel ya msisimko wa miondoko katika Ubongo, inayoitwa ‘’Nigrostriatal dopaminergic pathway’’, hii channel inafahamika kwa kuchakata taarifa za midundo ‘’meter’’ Pamoja na vipindi vya midundo ‘’timing’’. Na hii huwa na Ushahidi mkubwa sana kwa wagonjwa wa ‘’Parkison’s disease’’, watu hawa huwa na shida katika channel hii ya ‘’dopamine nigrostriate pathway’’. na hatimaye, huwa na shida ya kutembea, lakini pia, hushindwa kutofautisha ‘’rhythms’’ mbalimbali za miziki.

Yapo maswali mengi sana yanayohusiana na nini hasa, ni sababu ya kufanya muziki, uweze kuhamasisha hizi hisia za kutembea, au kurukaruka, au hata kucheza, na kukimbia. Lakini yote yana logic kadhaa zinazofanana kama vile,

MIMESIS

Hii ni ile hali ya vitu kujirudiarudia, hapa utaona kwa mfano, mtu anapoimba nyimbo au anapokuwa akisikiliza nyimbo. nyimbo inavipengele vya kujirudia rudia kama ‘’rhythms’’ lakini pia matendo ya kutembea au kukimbia pia yanasifa ya kujirudia rudia, hebu chukulia mfano, unapotembea unarudia rudia hatua zako, na hata mikono yako inarudia rudia miondoko yake, kwa hivyo, kuna uhusiano mkubwa sana kati ya muziki na miondoko. kwa kuwa, yote ina tabia ya kujirudia rudia. Ukiangalia mtu anayecheza pia hurudia rudia steps zake, kama ilivyo pia kwa mabiti yanavyojirudia. Kwa hapa hakuna jibu la moja kumpelekea mwingine, lakini unaweza ona namna ambavyo moja, linaweza kumhamasisha mwingine kwa namna wanafanana.

KUCHEZA ILI KUONGEZA ATTENTION

Nyimbo nyingi zinazosisimua sana kucheza. ni nyimbo zenye mabiti mengi ‘’polyrithms’’, huku kwetu Tanzania kwa kusikiliza nyimbo kama ya Singeli, mtu anaweza akaanza kucheza.

Sababu kubwa huwa ni uwingi wa mabiti yake, ambayo huufanya Ubongo kutafuta ni nini hasa ndilo biti kuu ‘’accent meter’’. na katika namna hii, Ubongo hutumia viungo vyake ili kulifatisha biti Fulani kwa umakini sana, bila kulipoteza, kwa kulifuata kimapigo. Ambapo, huonekana mithili ya mtu akitikisa kichwa au mguu (hii ni kulifuatisha biti kuu), hapa Ubongo hutumia viungo ili kuongeza ‘’attention’’ yake kwa biti kuu, usilipoteze kwa uwepo wa mabiti mengi. Na hii ni sababu ya moja kwa moja ya namna ambavyo, muziki ungeweza kusababisha muondoko Fulani wa kiungo, kwa lengo la kulitambua kiundani kabisa. Zipo sababu nyingi za kucheza hii ni mojawapo tu.

ENTRAINMENT NA EMBODIEMENT

Huwa kuna tabia ya Ubongo ya kujiungamanisha na kufuatisha mapigo ya sauti Fulani, na mapigo yake binafsi. Hili hudhihirishwa zaidi kwa namna ambavyo mtu anayekimbia, angependezwa na mabiti ya namna Fulani tu. Kiufupi mtu anaposikiliza mabiti, na namna Fulani, hupelekea Ubongo wake kuanza kuendana na mabiti hayo, kitu ambacho huitwa ‘’entrainment’’. Sababu hii hutumika kuelezea kuwa, mapigo haya ndiyo mwanzo wa kuhamasisha miondoko. Ambayo, huchangiwa na mawimbi ya mapigo haya.

Lakini kwa upande wa ‘’embodiement’’, hufahamika kuwa, kadri mtu anavyosikiliza muziki, basi yale mawimbi hupelekea mabadiliko ya kifiziolojia, ya kuendana na ule muziki, kwa lengo moja. Ambalo, ni kuufanya ubongo uweze kuuelewa muziki kwa kina kabisa, kumbuka kuwa, lengo la ubongo tokea awali, lilikuwa ni kuelewa na kutabiri kila kitu katika muziki.

JE WAJUA SABABU YA KUKINAI MUZIKI!!

Baada ya kusikiliza sana muziki Fulani, ubongo hupunguza kuvutiwa sana na huo muziki. Na sababu kubwa hasa huwa  ni kuwa, umeshatambua kwa kina model ya muziki husika, na hivyo basi kuwa na kiwango kidogo sana cha ‘’prediction errors’’, na hata kwa wale wanaosikiliza nyimbo za zamani au zenye hisia, huvutiwa zaidi na kumbukumbu za hisia zilizohusiana na hizo nyimbo, kuliko hata ‘’prediction errors’’ zinazotokana na hizo nyimbo.

DYNAMIC ATTENDING THEORY ‘’DAT’’

Hii huelezea kuwa, kwa namna ambavyo Ubongo huchakata kazi zake katika namna ambayo huwa ya kimabadadiliko badiliko kwa kila muda, basi huendana sana na muziki ambao, nao huwa ukibadilika badilika kwa kila baada ya muda Fulani. Nadharia hii huusiana pia na utendaji mzima wa mfumo wa ‘’prediction coding’’.


JE WAJUA!!

           




Ubongo hupunguza nishati, ndiyo maana watu hawapendi kazi, na wanapenda kula. Nishati hupunguza Ubongo, ndiyo maana Pesa nyingi huleta maamuzi dhaifu. Nishati hupunguza muda, ndiyo maana Nguvu nyingi, humaliza kazi ndani ya muda mfupi sana. Muda mwingi, hupunguza nishati, ndiyo maana, ukiongeza muda sana, nguvu chache tu yaweza kutumika. Muda hupunguza Ubongo, ndiyo maana, watu hawapendi kusubiria sana, au kuchelewa. Na mwisho, Ubongo hupunguza muda, ndiyo maana, watu hupenda kutumia mashine kufanya kazi kwa muda mfupi. Muziki, marazote Hublock uchakataji wa muda katika ubongo, na hivyo nishati kubwa sana huweza kutumika bila mtu kutambua. Hii humpatia faida mtendaji kufanya kazi kubwa zaidi kwa kutumia muziki bila kuchoka.

Kutokana na uhusiano mkubwa wa channel za miondoko ‘’motor pathways, prefrontal cortex, Orbitalfrontal cortex, basal ganglia, nigrostriatal dopaminergic tracts na channel za kusikia na miziki’’. Sehemu hizi huusiana na utambuzi wa muda .unaweza rejea tafiti za (DANIELSEN,A.,HAUGEN,M.R.,&JENSENIUS, A. R.2015. Timing and Time Perception, 3, 133–154).

Utambuzi wa muda  hutawala ‘’regulate’’ matumizi ya nishati katika ubongo (ubongo huwa ukipunguza matumizi ya nishati yake kwa kutengeneza hisia ya kuwa muda umeenda sana)

Ubongo hupima muda kama kipimo cha kazi (ukiwa unafanya kazi ngumu, ni rahisi kuhisi umetumia muda mwingi sana, ubongo hufanya hivyo kwa lengo la kuzuia matumizi makubwa ya nishati). Mtu anaposikiliza muziki akiwa anafanya shughuli, uchakataji wa muziki huusiana na misisimko mikubwa sana ambayo hufunika ‘’mask’’ hisia za muda kutokana na namna channel za shughuli za miondoko ya misuli huchangamana na  channel za misisimko ya miziki. (muziki hupeleka uwezo  mdogo wa ubongo kutambua muda kwa kipindi cha kuusikiliza).

Ubongo ungetumia kemikali zake ‘’inhibitory neurotransmitters’’ kwa lengo la kudidimiza hisia za kazi kwa kutengeneza hisia za uchovu ili kutunza nishati, lakini muziki huchangamsha mfumo mzima wa miondoko mpaka na kuzalisha ‘’norepinephrines’’ kemikali zinazohusiana na kuchangamka. Na matokeo yake huwa ni mtu kufanya kazi kubwa bila kuchoka. Ijapokuwa wapo wanasayansi baadhi waliokwisha husianisha uchakataji huu wa muda, lakini nadharia ya shoo imeweza kuelezea kwa uhusiano rahisi zaidi na wa moja kwa moja.

Mfano, unapomsubiria mtu halafu huyo mtu anachelewa. Ni rahisi kuhisi kuwa umetumia muda mwingi sana katika kumsubiria huyo mtu, Hata kama itakuwa ni tofauti ya muda mdogo sana. Hii ni kwa kuwa, unapomsubiria mtu, unapunguza matumizi ya misuli iliyokwisha chochewa kwa kazi ‘’hii ni kama kupiga breki kwa gari linalotembea’’, unapunguza nguvu ya motisha katika ubongo ‘’nigrostriatal dopaminergic system’’, matendo haya yanatumia nishati kubwa sana ya ubongo, na hivyo ubongo unachochea hisia ya kuhisi umetumia muda mwingi sana, ili kupambana na upotezaji wa nishati na motisha zaidi katika ubongo.

UTAFITI WA SHOO: BONDE LA AFRIKA LA KATI KUELEKEA KUSINI NA KUSTAWI KWA MIZIKI YA KUCHEZA

NADHARIA                                                                                                                                            Katika historia ya muziki inatambulika kuwa muziki wa kucheza wa kizazi kipya ulianza sehemu mbalimbali lakini hasa ilikuwa ni marekani. kwa kuchochewa na waafrika waliokwenda marekani kipindi cha biashara ya Utumwa. Hakuna msomi wa historia za muziki asiyetambua muziki wa ‘VOODOO’’ kama ndiyo chanzo cha miziki  yote ya kisasa iliyoanzia marekani, kwa kupitia hatua mbalimbali kama  kipindi cha zama za ‘’The Blues’’ , Rock n’ Roll ‘’The Beetles’’ na wengine wengi wanaoweza rejewa kwenye historia’’. Muziki wa Afrika wa Voodoo ambao ndio msingi wa miziki ya ‘’Polyrythms’’ ya kucheza ambayo ilianza Afrika na sehemu baadhi kwenye ibada za kipagani, ulipitia zama mbalimbali za mabadilisho mpaka ukawa bora kwa masikio kama mziki wa leo wa kizazi kipya wa Marekani na sehemu nyingine nyingi duniani. Ukweli huu unarejea tena kwenye udhihirisho wake kwa namna muziki wa Afrika upo juu sana kwa midundo ya kucheza. Hii ni kusema tu kuwa Muziki wa kucheza umeshamiri sana Afrika ukilinganisha na sehemu zingine. Afrika ni kitovu cha ‘’Polyrhthmic musics’’.

KISIO LA SHOO ‘’HYPOTHESIS’'                    

Kadri mtu anavyosikiliza zaidi muziki ndivyo ubongo wake unavyoendelea zaidi katika uwezo wa kuuchakata huo muziki ‘’neuroplasticity from continuous musical hearing’’.(Eric kandel, Principles of neural science, Pg 669). Kadri mtu anavyotembea sana na kutumia sana misuli, ndivyo sehemu za Ubongo wake za miondoko zinavyoendelea sana, hii nayo ni kwa msingi uleule wa ‘’cortical plasticity’’.  kila jamii hutumia zaidi miziki katika miondoko yake ili kupunguza gharama ya matumizi ya nishati kama nilivyoeleza katika ‘’shoo masking theory’’. watembeaji wa umbali mrefu huwa bora zaidi katika mifumo hii miwili. Hii  ni kama ilivyo ile hoja ya ‘’mimesis’’, matumizi makubwa ya ‘’rhythms’’, huambatana na ufanisi mkubwa zaidi wa utembeaji, Pamoja na uwezo mkubwa wa uimbaji wa miziki ya miondoko.                           

USHAHIDI1. 

Kitabu kikubwa zaidi cha sayansi ‘’Biblia’’ kinaonesha asili ya Waafrika ni Watoto wa Ham, au ‘’Hamites’’ ambao walitoka maeneo ya kati ya Dunia ‘’Middle east’’ na kushuka katika bonde la bara la Afrika, hivyo maeneo yote ya kusini yanahusisha watu waliotembea umbali mrefu zaidi katika historia ya dunia, na hivyo tutegemee wakiwa na sifa nyingi za kimiondoko na muziki.

USHAHIDI2.

Maeneo mengi ya Afrika ya kati kuelekea kusini, yanahusisha watu wenye sifa kubwa za miondoko.  Mfano, uwezo wa kukimbia na namna za kufanania za kutumia misuli ‘’Athletic characters’’ ukilinganisha na sehemu zingine. Sifa hizi zinatabiri uwezo wao wa kimuziki wa mtindo wa miondoko na kucheza kutokana na uhusiano wa moja kwa moja kati ya mifumo hii miwili.

USHAHIDI’’3

Watu wengi wenye miili mikubwa zaidi duniani kwa historia ya kipindi Fulani cha hapo awali, walikuwepo maeneo ya Afrika. Nikirejelea ripoti maarufu ya wanasayansi ‘’Bergmann na Allen’’ hawa walionyesha ukubwa huu wa Afrika ulitokana na faida za kibiolojia za kuwawezesha kupoteza joto kirahisi mwilini, kutokana na uwepo wao katika nyanda za Equator zenye Joto kubwa sana. tazama mfano ukubwa wa makabila kama ya wabantu, Nilotics kama Maasai, wanubi, n.k. Pia Afrika ilihusisha makabila mengi sana ya wawindaji, kulikuwa na vyakula vingi sana Afrika, na hata maendeleo ya magonjwa mengi, na madhara ya usasa mwingi, yalichelewa sana kuwadhoofisha watu wa Afrika.

Hoja ni kuwa, kadri Mwili unavyokuwa mkubwa, mapafu makubwa, uwezo  mkubwa wa misuli ya kupumua, haya yote huongeza uwezo mkubwa sana wa Uimbaji. Tazama mfano, Sololist wakubwa zaidi huwa ni watu wanene, au wenye miili mikubwa kwa wastani. Hii ni hoja inayochangia ubora wa Afrika katika muziki ulikuwa na sababu nyingi sana.

USHAHIDI’’4

Utazamaji wa filamu za kutisha, huambatana na matumizi ya mabiti ya muziki ya kutisha. Mabiti haya, huwa na msingi mmoja mkubwa ambao msikilizaji anapoyasikiliza tu, hujua kuna tatizo linaenda kutokea, mfano, Jini, zombie, n.k. mabiti haya huwa yanaongeza Frequency zake mpaka kufikia ya juu sana ndani ya muda mfupi sana, tena huongeza kwa kasi na yakishafika juu kabisa, huwa kama yakistop kwa ghafla, kutengeneza ‘’big prediction error’’, na tena, hii ambayo unaweza iita ‘’exponential frequency increase’’, hufanana na mabadiliko ya asili ya frequency kitu kinapoenda kupasuka. Vuta taswira, mti unavyoanguka mpaka unapopiga chini kwa kishindo, huanza na sauti kwa ghafla inayoongezeka, na kisha hufikia juu kabisa ‘’maximum’’, na hustop. Mtu anapokimbilia kitu ili akikamate, anapoelekea kukikamata, Huongeza matumizi ya misuli mpaka mwisho, na anapokishika, hushuka ghafla. Anayekimbia ili apige mpira, au arushe jiwe wote hufata hizi namna. Hii inathibitisha, Muziki katika kiini chake, una utendaji sawa na mahesabu ya makadirio ya nishati, na muda katika ubongo.

TEGEMEO‘’PREDICTION’’1                                                                                                    

Ikipimwa watu wa maeneo ya mabonde ya kati kuelekea mpaka kusini mwa Afrika , watakutwa kwa wastani wakiwa na sehemu za ubongo za kuchakata muziki zilizoendeleaa zaidi (kama eneo la ubongo linaloitwa  Broadman area  ‘’BA’’47 na “BA’’40  na mengineyo). Na wakipimwa watu wa maeneo mengine wataonekana na maendeleo kidogo chini.

TEGEMEO‘’PREDICTION’’2                                                                                                       

Ikipimwa uwezo wa utambuzi wa muda katika ubongo kwa watu wanao kimbia wakiwa wanasikiliza muziki na wanaokimbia bila kusikiliza muziki, itaonekana kwa kadri mtu atakavyokuwa akivutiwa na muziki, basi uwezo wake wa utambuzi wa muda ukipingua na ukiongezeka kwa yule asiyesikiliza muziki.

LENGO LA NADHARIA                                                                                                                 

Ni kuonesha kuwa Muziki una sifa ya kuathiri uwezo wa utambuzi wa muda na nishati kama ambavyo pia wanasayansi wakubwa zaidi wa ubongo na muziki ‘’Katarina Jerotic, Peter Vuust na Mortem L. kringlbach’’ walivyoonesha katika jarida lao lililokuwa likielezea namna ambavyo muziki huwa na matokeo sawa na ya dawa za kulevya ‘’interplay of music and psychedelics’’. nadharia ya shoo, inatengeneza njia ya kuelewa zaidi uhusiano wa muziki,muda, nishati na kucheza. Inatoa sababu ya Ubongo kupenda kucheza kama namna ya kujilevya kutokana na sifa yake ya kuchukia matumizi ya nishati.

                 SAYANSI YA UDANGANYIFU WA MASIKIO NA UBONGO

Utangulizi.

Hakuna mfumo wa mlango wa fahamu uliojitawanya Sana katika Ubongo Kama mfumo wa kusikia. Channel za mfumo wa kusikia zimejichimbia zaidi ya mifumo yote mingine ya fahamu, katika ubongo. (Tumeona channel hizi katika Fiziolojia ya kusikia, tokea katika Ubongo wa medulla oblangata, pons, midbrain, cerebellum, basal ganglia, limbic system, auditory cortex na cerebral cortex). sehemu ya kusikia ina uhusiano na mfumo mzima wa lugha, ambao unachakata pia taarifa kutoka sehemu zote za ubongo. Pia sehemu ya Ubongo wa kusikia, ina uhusiano wa moja kwa moja na kuona, mtu anaposikia, hugeuka Mara moja, ukimsimulia mtu kwa mfano." Kuna jumba kubwa kwekikweli!! , Atakapo sikia tu, atatengeneza taswira. Yaani masikio Yana uhusiano mkubwa Sana na mfumo mzima wa fahamu, lakini pia mfumo wa kusikia, unahusiana moja kwa moja na mfumo wa hisia, mfano unaposikia mtu akikutukana, Hasira huja Mara moja. Mtu anaposifiwa, husikia na Mara moja hujisikia Raha. Lakini hata hivyo Mfumo wa kusikia unasifa moja kubwa sana.

SIFA KUU YA MFUMO WA KUSIKIA

Huu Ni mfumo ambao huruhusu zaidi Kufikiria. Msingi mkubwa zaidi wa kufikiria umejikita katika kusikia. Mara nyingi watu huwa hawafikirii vitu wanavyoviona. Ukimwona rafiki yako akipigwa risasi, utaamini na kuumia Mara moja. Ukiambiwa rafiki yako amepigwa risasi, utafikiria!! Je Ni kweli? kwanini? wapi? n.k, lakini hata Kama rafiki yako angepigwa risasi kipindi unamuona, Kama ungetaka kujua zaidi, ungepaswa kuuliza na kusikiliza!! Ili ujue sababu. Watu wengi hawajui kuwa mtu akiwa anasoma vitabu, huwa anasikiliza!! Unaposoma mfano, "hapo mwanzo kulikuwepo na neno!!, Hapo mtu anasoma kwa macho, lakini hasa anasikiliza simulizi iliyoandikwa. na hata namna ambavyo mtu anachakata taarifa hizi, huwa Kama mtu anayesimuliwa na sio anayeona. Hii ndiyo sababu pia sikuhizi Kuna "audio books", vitabu unavyosoma kwa kusikiliza, havina tofauti na unavyosoma kwa kuangalia. Sasa Basi, kwanini vitabu na masimulizi? Huwezi kufikiria Kama hauna vya kuvifikiria!! Kufikiria Ni kukusanya taarifa zilizopo, na kujenga maana au hoja. Watu wanaofikiria Sana, huonekana kuwa na akili Sana "intelligent", Einstein anafahamika kwa kufikiria Sana, je angeweza kufikiria Sana bila kusoma Sana, " au kusikiliza zaidi",  ndiyo maana huwa Wana msemo unaosema toka enzi ya Newton, "reaching far, by standing on shoulders of Giants", yaani Kama unataka kufika mbali, Basi Ni kwa kusimama juu ya mabega ya wakubwa, ambayo hiyo Ina maana, unahitaji kuwasoma zaidi waliopita. Biblia pia inathibitisha hoja hii, Danieli anasema "nimejua mengi kwa kusoma Sana",  neno akili au "intelligence" linahusisha maneno mawili "inter - na legal", yaani akili Ni kulinganisha, taarifa zilizokwisha kuwepo, maana yake uwe umekwisha zisikia au zisoma", msingi wa maarifa na akili sio kuona, Ni kusikiliza. Leo hii tunajua kilichotokea miaka 3000B.C na hatukuwepo, lakini kwa kusikiliza. Biblia pia inasema "Imani huja baada ya kusikia neno la Mungu", neno Imani Ni kuwa na uhakika, katika Sayansi huwa tunarudia rudia majaribio ili tuwe na uhakika, tunafanya experiments kuthibitisha tuwe na Imani na study fulani. Msingi wa kufikiria Ni kusikiliza, unaposema kitu chochote katika sayansi, utaulizwa " kitu chako kinahusiana vipi na kinachofahamika tayari". Maana yake kila kitu kinachohusiana na kufikiria kinahusiana na kusikia.

KWANINI KUNA UHUSIANO WA KUSIKIA NA KUFIKIRIA

Mtu anapofikiria huwa hata akifumba macho, au akiangalia lakini asiwe anaona anavyoviangalia, mpaka atakapo maliza kufikiria. Siri kubwa iliyojificha hapa ni hii.

Maarifa= Jumla ya taarifa( To-Tt) +Jumla ya taarifa(ESo-ESt)

Hapa katika hii hesabu. kwanza tunaona Maarifa Ni kujua maana zote za vitu toka siku ya kwanza ya uumbaji wa Ulimwengu mpaka kufikia Duniani leo hii(To-Tt), Leo hii watu Kama "Michio kaku, Richard Dawkins" wanasikilizwa Sana kwa kuonekana Wana akili Sana. hasa kwa kuelezea historia za ulimwengu kwa kutumia Bigbang na kwa msaada wa uwezo wao wa kutumia sayansi za kifizikia au jenetikia. lakini pia hata watumishi wengi wa Imani husikilizwa Sana, hii ni kwa kuweza pia kuzungumzia matukio ya awali kabisa katika uumbaji, na kutabiri yatakayotokea baadae katika Dunia kwa ujumla. Hoja ya msingi hapa ni hii,  kwa wote wanaoamini dunia aidha Ina miaka bilioni 13.8 au wanaoamini Ina miaka 6000. Je kwa miaka 70 ya Ubongo wa binadamu, Nani anaweza kujua Siri za ulimwengu kwa huu muda mfupi kiasi hiki? Hakuna namna. lazima mtu asikilize waliotangulia, ili japo aongeze kujua taarifa za wakati uliopita, na makisio ya wakati ujao. na Kisha akishasikiliza, Basi Sasa anaweza kufikiria! Kwa hiyo, lazima mtu asikilize na sio aone. utaona nini miaka 70?

Pili, Maarifa Ni kujua Siri za ulimwengu kwa sehemu zote za ulimwengu(Eso-Est), kuanzia ndani kabisa katika atomu za DNA za seli za mwili, Kama ubongo, mpaka kila sehemu katika dunia, na ulimwengu kwa ujumla. Sasa, Ni Nani anayeweza kuwa kila sehemu katika ulimwengu. Unapaswa usikilize!! je unaweza kuona kinachotendeka kwa Sasa marekani, au Sweden, au China?? Au hata tu kwa jirani yako? Ndiyo maana inahitaji kusikiliza taarifa za habari au kusoma , ili uwe na akili, au Maarifa, au ili iweze kufikiria.

JE WAJUA SIFA ZA UVIVU WA KUSIKILIZA! 

watu walio wavivu wa kusikiliza, wakitumia muda mwingi kutazama vitu vilivyo mbele ya macho yao, mfano, mtu anatumia muda mwingi kazini kwake tu, kwenye burudani Kama michezo, kuangalia vinavyotendeka tu kwa muda huo!! Watu hawa huwa Wana uwezo mdogo Sana wa kufikiria. kwa maana, hawana taarifa nyingi. Utaona mtu mmoja akisema kuwa "haiwezekani kwenda na spidi ya sauti!!, Huyu mtu hawezi kufikiria vizuri katika maswala ya spidi za vitu, na ndiyo maana hata ameweza kusema hoja hii, hii ni kwasababu ana taarifa chache. huyu hasikilizi Mambo yaliyokwisha fanyika, au yanayofanyika katika maeneo mengine ya dunia. Biblia inasema " enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima". wenye hekima, Wana Maarifa ya kusimulia, jamii nyingi huamini wazee ni watu wenye Maarifa zaidi, hoja Ni kwa kuwa wameona mengi " wana taarifa nyingi' na kwahivyo "husimulia zaidi" na msikilizaji "Masikio yake hupokea zaidi".          

Msikilizaji mzuri huwa na Maarifa Mara nyingi zaidi ya mtazamaji mzuri. Masikio husikiliza hata mtu anapolala,  masikio hayafumbwi!! Watu huweza kuona taarifa zilezile, lakini kila siku husikiliza taarifa mpya, huoni unachokisia Kama ambavyo usivyoona mawazo. Ni rahisi kutazama, lakini sio rahisi kusikiliza, na kufikiria kwa pamoja.

UBONGO KIPINDI CHA KUFIKIRIA NA KUVUTA TASWIRA.

Ubongo unapokuwa unatafakari Jambo lolote Lile, iwe utatuzi wa changamoto fulani au ujio wa mbinu fulani, huwa unafanya baadhi ya hatua. Katika ubongo, Kuna network zinazohusiana na Hali za kufikiria. Zipo kuu mbili na moja ambayo Ina control badiliko la kutoka moja kwenda nyingine inaitwa "salience network". Ya kwanza inaitwa "Central executive network" au CEN", hii hutawala fikra zozote zile zinazohusiana, au zinazotokana na shughuli za nje, mfano, Nina njaa, ninawezaje kupata chakula. Au unapokuwa unafanya maamuzi, unapokuwa unatafakari, unapokuwa unawaza Jambo lolote Lile. Na Mara nyingi CEN huambatana na mawimbi makuu mawili ya Beta "Beta waves" ambayo huwa na frequency kuanzia 13-30Hz na Gamma waves zinazoanzia 30-100Hz. hii network pia huitwa "frontoparietal network kwa namna huusisha zaidi ya maeneo ya Ubongo wa mbele juu, na pia Ubongo wa kati. Lakini pia huwa Kuna network nyingine inayoitwa "Default mode network", hii huusiana na fikra zote mtu anazozifanya akiwa anatengeneza taswira "imagine" na meditations, ndoto za mchana "day dreaming", Hali za kutulia Sana kipindi mtu anasinzia, na Mara nyingi huusiana na mawimbi ya alpha waves, ambayo huwa yanaanzia frequency za 8-12Hz, na pia theta waves yanayoanzia 4-7Hz. Na hii hupatikana Sana maeneo ya Ubongo wa mbele ndani, na pembeni chini. Lakini pia Kuna network za hisia ambazo hizo huitwa "limbic system" ambazo huusiana Sana, na sehemu za ndani za ubongo. na huusiana pia na sehemu zingine za

ubongo Kama sehemu za ladha na harufu, na hata sehemu za

Namna zote hizi za kutafakari au kuvuta taswira zinachangiwa na sehemu zingine, vijedwali vya chini vina maneno kama ‘’Top-down control’’-hii inamaanisha Mawazo huathiri matendo mengine, sensory input-hii inamaana hisia za mazingira kama unachoona, sikia, mguso na ladha huathiri Mawazo. limbic input-humaanisha hisia ‘’emotions’’ huathiri Mawazo. self referential processing humaanisha tathmini binafsi.

Mtu anapofikiria, mfumo wa mawimbi ya umeme ambayo yanajibadilisha badilisha, kulingana na Jambo au Mambo anayoyafikiria, huonekana ukitamalaki katika Ubongo. Mfumo wa mawimbi na umeme,  Ni wa msingi Sana katika utendaji wa ubongo, ukisikia mtu ana kifafa, Basi Ni huu mfumo unaoathiriwa hata kupelekea kuripuka kwa msisimko wa umeme wa ubongo, na kusababisha baadhi ya sehemu za mwili kuanza kuhemka tofauti na matakwa ya mtu. Lakini pia, hata matumizi ya madawa yanayopooza mihemko ya ubongo, huusiana na kuzuiwa kwa baadhi ya kemikali za ubongo "neurotransmitters" zinazohamasisha mihemko ya ubongo. Kadri tutakavyokuwa tukiangalia sehemu hii, ni muhimu kutambua kuwa, Miziki na taarifa za sauti zote tutakazokuwa tukizizungumzia, Zina madhara katika makundi mawili.                                                                                           

1.madhara ya kifiziolojia yanayotokana na Sauti zinazosikilizwa

2.madhara ya kisaikolojia yanayotokana na taarifa zinazosikilizwa.                                            

Na katika kila kundi kuna sababu za msingi Sana, zinazoleta madhara makubwa Sana katika mifumo ya fahamu ya watu. Hebu tuangalie Sayansi za udanganyifu nyuma ya triki hizi.

TRIKI NA MADHARA YA KUSIKILIZA MIZIKI YA MIDUNDO HASA YA MISISIMKO

SAUTI INAVYOATHIRI MAUMBO YA MAJI

Mawimbi ya sauti huathiri kila sehemu ya vitu inavyovipitia, sauti husafiri kwenye chembechembe za hewa, maji au vyuma. Ukipiga kelele kwenye maji, utaona maji yakitikisika, lakini kubwa zaidi ni kuwa, sauti siku zote huathiri mpangilio mzima wa maji. Neno huathiri linamaanisha sauti, hubadili muundo wa maji, maji yanaundwa na molekuli za oksijeni na hydrogen. Molekuli hizi huwa na umbile lake la kawaida. Unapopitisha mawimbi ya sauti kwenye molekuli hizi, basi unapelekea umbile au maumbile yale ya awali ya maji  kubadilika. Mabadiliko haya ya maumbile ya maji hutegemea na kiwango au nguvu au frequency za sauti zitakazokuwa zikipita katika hayo maji. Mfano picha chini inaonesha namna maumbo ya maji yanavyobadilika kulingana na frequency mbalimbali za sauti za muziki

Ukichukua maji na kisha ukayaweka kwenye chombo kama cha bati, yakiwa yametulia kabisa, halafu ukaanza kupiga hiyo miziki hapo juu, basi maji yataonekana kwa maumbo hayo juu. Miongoni mwa watafiti  ambao wanatambulika kama ‘’Pseudoscientists’’ masaru emoto wa Japan, aliandika kitabu kinachoitwa ‘’taarifa zilizofichwa katika maji’’ au ‘’hidden messages in water’’ mwaka 2004, katika kitabu chake hicho ambacho kiliuza sana katika ‘’Newyork bestseller’’, alionesha kuwa, mapigo ya sauti hatari au mabaya, huusiana na maumbile mabaya ya maji ‘’ugly’’. na pia mapigo ya kutulia ya sauti, huusiana na maumbile mazuri ya maji. Ijapokuwa awali ilionekana kana kama ni nadharia za kufikirika zinazochochewa na wanasayansi wa nadharia za kufikirika ‘’pseudoscience’’, lakini ikaja kugundulika kuwa ni jambo la kweli na mpaka sasa tutaenda kuangalia athari za mabadiliko haya ya maumbile ya maji, kutoka katika sayansi na vyanzo vinavyoaminika zaidi duniani kwa tafiti.

Anasema muziki mzuri na maneno, hupelekea kuundwa kwa maumbo mazuri katika maji, kama hayo yanayooneekana katika picha upande wake wa kulia.

hapa pia akawa anaonesha kuwa, sauti zisizo na mipangilio mizuri Pamoja na miziki isiyomizuri, hupelekea maumbile yasiyo mazuri kwa maji.                                                            masaru emoto amenukuliwa kwa tafiti yake ya maji tu. ambayo pia imefanywa na wengine wengi, na sio mitazamo yake mingine kama inavyofanywa pia kwa wengine wanaonukuliwa!!

MSINGI WA KWANZA WA UHARIBIFU KATIKA MIZIKI YA MIDUNDO!!

Miziki mingi inayopigwa huwa ikipigwa katika frequency za 440Hz na miziki michache sana ile inayopigwa katika sauti za utulivu sana, hupigwa katika frequency za 432Hz. Sauti hizi nyingi za frequency za miziki inayopigwa sana yaani wastani wa 440Hz, huambatana na mabadiliko makubwa sana ya maumbile ya maji. Maji yanachukua asilimia zaidi ya 60% ya mwili wa mtu, tena kulingana na jinsia, umri au hata hali ya kiafya na kifiziolojia ya mtu.

Mjadala mkubwa sana ulioletwa na sayansi za mabadiliko, ya maumbile ya maji, kutokana na sauti ‘’cyamatics’’. Ni je, mabadiliko haya ya maumbile ya maji, hayawezi kuleta madhara katika miili ya binadamu? Watu wanaosikiliza sauti mbalimbali hata hizi zenye kuleta mabadiliko makubwa sana, je hawawezi kuathiriwa kwa frequency kubwa za sauti? Kibaya zaidi ni kuwa, miziki mingi huwa na frequency kubwa sana, tena zaidi ya hata hizo kubwa zinazofahamika yaani 440Hz. wasanii wengi maarufu huwa wakikubalika sana kwa nyimbo zao zenye frequency kubwa sana za sauti. kwa mfano (Mariah Carey, Ariana Grande, Beyoncé, Whitney Houston, Celine Dion, Adele, Sam Smith, Sia, Christina Aguilera, Bruno Mars, Demi Lovato, Justin Timberlake, Kelly Clarkson, Ed Sheeran, P!nk, Lady Gaga, Rihanna, Taylor Swift, John Legend, Katy Perry na wengine wengi kama baadhi ya nyimbo za Drake) wasanii hawa, pia huwa na nyimbo  baadhi zilizotulia. lakini mara nyingi nyimbo zao, wakati mwingine hufika mpaka 10,000Hz na hata 14,000Hz. 

Kadri ambavyo ilivyokuwa bado haitambuliki hasa je! ni kwa kiwango gani, sayansi inakubaliana na madhara makubwa yanayoweza pelekewa, na usikilizaji wa nyimbo za muundo huu, ambazo zinaweza pelekea mabadiliko makubwa ya maumbile ya maji, katika afya za watu, na kuleta madhara. ndipo utafiti mpya uliofanywa mwaka 2022 na kuchapishwa na ‘’Pubmed’’ ulidhihirisha haswa, madhara makubwa yanayoweza pelekewa au chochewa kwa hata badiliko dogo tu la frequency la 8Hz. tena katika frequency za miziki ya kawaida kabisa ya 440Hz, iliyojaa katika staili za miziki ya kisasa.

UTAFITI WA MADHARA YA SAUTI KUBWA KATIKA AFYA



MATOKEO YA UTAFITI

Sauti ina uwezo wa kusababisha matokeo ya kimekaniki ya kitu inachokutana nacho, kama ilivyo kwa kani zingine za mekaniki. Nguvu ya sauti katika fizikia inafahamika sana, japokuwa katika biolojia bado inafanyiwa utafiti zaidi.

Zipo tafiti nyingi zinazooonesha namna sauti inavyoweza kuathiri mifumo ya kibiolojia ya viumbe mbalimbali. Viumbe vidogo sana vinapowekwa kwenye maji, mawimbi kutokana na sauti inayopita katika maji, yameonesha kuathiri sana matendo ya biolojia ya viumbe, pia madhara ya sauti yameonekana kwa vimelea vya seli moja, kama bakteria, protozoa na wengine, pia madhara yameonekana kwa mimea.

Sauti na Ukuaji kwa viumbe.

Kuna tafiti imenukuliwa inayoonesha sauti za frequency kuanzia (38-689Hz) zilipopigwa, zilionesha kuathiri moja kwa moja Ukuaji wa viumbe, matendo yao ya kibiolojia au metaboliki za mwili. na pia, kwa viumbe hawa ambao wana seli za muundo wa bakteria ‘’prokaryotes’’ na seli kama za binadamu ‘’eukaryotes’’, ilionekana hata uwezo wa dawa kuwaathiri uliathiriwa.( Sarvaiya, N.; Kothari, V. Effect of audible sound in form of music on microbial growth and production of certain important metabolites. Microbiology 2015, 84, 227–235. [CrossRef] 9. Kothari, V.; Sarvaiya, N. Audible Sound in Form of Music Can Influence Microbial Growth, Metabolism and Antibiotic Susceptibility. J. Appl. Biotechnol. Bioeng. 2017)

Sauti na madhara ya DNA

tafiti iliyofanywa kwa mimea inayoitwa (chrysanthemum) ilionesha kuwa, mawimbi ya sauti yalichochea au huweza kuchochea uundwaji wa vinasaba vya jenetikia, vinavyoitwa RNA na protini. Hii inaonesha kuwa, Sauti ina uwezo wa kuwasha hata mifumo ya jenetikia. Ambayo, haipaswi kuwa ON. Au unaweza sema sauti zinaweza kuziwasha ‘’genes’’ za mwili, ambazo zimezuiwa na mwili zisilete madhara.

Zaidi tena ilionekana kuwa, Sauti iliifanya mimea inayoitwa (Arabidopsis), iweze kukaa kwa muda mrefu zaidi katika upungufu wa maji, ukilinganisha na mimea mingine ambayo ilikaa penye ukimya.

Uwepo wa genes mbili za mekaniki. Mfano, ya  (sauti) tu!

Tafiti hii ilionesha uwezo wa kusisimua vinasaba ‘’genes’’ 87. Ambapo katika genes hizi, nyingi zake huusiana na stress zisizotokana na matokeo ya kibiolojia, madhara ya kujikinga ya vimelea hatarishi, na mabadiliko ya kikemikali ya mabadiliko ya ‘’oxidation na reduction’’, na ajabu ni kuwa, ilionekana zipo genes 2 zinazohusiana moja kwa moja na mabadiliko ya kimekaniki.(Hii ina maanisha kuwa, unaweza kufanya mabadiliko ya kiumbe kwa kutumia tu sauti)

Sauti na mabadiliko ya maumbo ya protini                                      

Madhara ya sauti kwenye biolojia za viumbe yalichunguzwa kiundani, na kuonesha kuwa, sauti husababisha mabadiliko ya maumbo ya protini, zilizo ndani ya mwili ‘’protein crystallization’’ na mabadiliko haya ya kimaumbo, hutegemeana na frequency. Kwa hiyo sauti kubwa sana, yaweza pelekea madhara makubwa zaidi.( Zhang, C.-Y.; Liu, J.; Wang, M.-Y.; Liu, W.-J.; Jia, N.; Yang, C.-Q.; Hu, M.-L.; Liu, Y.; Ye, X.-Y.; Zhou, R.-B.; et al. Protein Crystallization Irradiated by Audible Sound: The Effect of Varying Sound Frequency. Cryst. Growth Des. 2019, 19, 258–267).

Sauti na neva za fahamu

Sauti ilionekana pia kuleta madhara, kwa kuathiri uwezo wa seli za mwili, kuwasiliana ‘’signal pathways’’. tena uwezo huu, ulionekana kuathiriwa kwa mimea, na kwenye mfumo wa fahamu wa Wanyama.

Muziki Na Kula Sana Na Ongezeko La Uzito

Katika kujifunza matokeo mbalimbali ya muziki wa frequency kuanzia 432Hz mpaka 440Hz. katika tabia za kula, na uzito, kwa panya. Iligundulika kuwa, mawimbi mbalimbali au frequency mbalimbali za muziki, huathiri chembechembe za protini zinazoitwa ‘’peptide’’ za aina mbili. zilizopo katika seli za fahamu. Muziki ulionesha kuathiri uwezo wa chembechembe hizi, kujiunda, katika hatua ya kijenetikia ‘’expression’’. protini  hizi zinazopatikana katika sehemu ya ubongo, inayoitwa ‘’hypothalamus’’, ni za muhimu sana katika uwezo wa ku control hamu ya kula, na hivyo, madhara ya kushindwa kujionesha yalipelekea kuongezeka kwa hamu za kula kwa panya, hata kupelekea ‘’kuzidi kwa uzito’’. Na hii ni  kwa panya waliosikilizishwa muziki wa frequency za muziki wa kisasa, wa 440Hz. maana walikula sana, na kuongezeka sana uzito, ukilinganisha na wasiokuwa wakipigiwa frequency hizo za muziki, wale ambao waliosikilizishwa frequency za 432Hz.( Russo, C.; Russo, A.; Gulino, R.; Pellitteri, R.; Stanzani, S. Effects of different musical frequencies on NPY and Ghrelin secretion in the rat hypothalamus. Brain Res. Bull. 2017, 132, 204–212.)

Muziki Wa Pole Hushusha Presha Kwa Wenye Presha

Ilionekana katika tafiti kuwa, kusikiliza sauti zenye frequency za 432Hz, kulipelekea kushuka kwa mapigo ya moyo kwa viumbe wenye presha kubwa ya damu ‘’high blood pressure’’. (Halbert, J.D.; van Tuyll, D.R.; Purdy, C.; Hao, G.; Cauthron, S.; Crookall, C.; Babak, B.; Topolski, R.; Al-Hendy, A.; Kapuku, G.K. Low Frequency Music Slows Heart Rate and Decreases Sympathetic Activity. Music Med. 2018, 10, 180–185)

Mabadiliko Ya Muziki Toka 440-432hz Hupelekea Kushuka Kwa Presha Na Hali Ya Kutulia Ya Mwili

Ijapokuwa ukipigiwa muziki wa 432Hz na 440Hz unaotumika zaidi, ni kama inafanana. lakini tofauti ipo. Na badiliko la kuelekea katika frequency za 432Hz ,hupelekea kushuka kwa presha ya damu na mfumo wa upumuaji. Hii humfanya mtu kuhisi ku relax, ukilinganisha na muziki wa frequency za 440Hz. Muziki wa 432Hz pia hupelekea usingizi mzuri, hata kwa wagonjwa wa uti wa mgongo, na huongeza uwezo wa kujitambua ‘’perceived arousal’’ (. Calamassi, D.; Pomponi, G.P. Music Tuned to 440 Hz Versus 432 Hz and the Health Effects: A Double-blind Cross-over Pilot Study. Explore 2019, 15, 283–290.)

Muziki Wa 440hz Na Hisia Mbaya Kama Hasira

Tafiti ilionesha pia kusikiliza muziki wenye frequency za 440Hz. (muziki wa mtindo wa kisasa zaidi) huambatana na hisia za Anxiety ( hali ya kutotulia kiakili, mithili ya hisia ya kukandamizwa maeneo ya juu ya tumbo kuelekea kifuani, wakati mgumu, kutokuhisi wepesi, kutoelewa elewa, kuwaza mbali kinamna ya msongo, kuchanganywa ), nervousness na aggression( hali ya kuwaka kwa hasira, kukakamaa kwa ghadhabu, udhaifu, kuongezeka kwa hisia za tempa, kuwa mkali), hali hizi zote zilionekana kuambatana na aina hii ya muziki. waweza pia kurejea (Calamassi, D.; Pomponi, G.P. Music Tuned to 440 Hz Versus 432 Hz and the Health Effects: A Double-blind Cross-over Pilot Study. Explore 2019, 15, 283–290)

Mabadiliko Ya Mawimbi Ya Muziki Na Madhara Katika Dna

Tafiti iliyofanywa juu ya madhara ya sauti, katika vinasaba vya ndani kabisa vya jenetikia ya viumbe yaani DNA. Yalionesha kuwa, DNA ya binadamu inahisi au sense sana Muziki. ‘’DNA is sensitive to music’’. Na ikaonekana kuwa, kwa kupiga muziki wa frequency mbalimbali katika seli mama za viungo ‘’stem cells’’( hizi ndizo hupelekea kukua kwa seli zingine zote, zenyewe huwa na utendaji mkubwa sana wa DNA, katika kuumba seli zote za mwili), huweza kupelekea kubadilishwa kwa utendaji wa asili wa seli, na viungo hatimaye. Hii ni sawa na kusema, kwa kupitia miziki, unaweza kubadilisha kabisa fiziolojia ya kiumbe kuanzia ngazi ya jenetikia ya ndani kabisa. Unaweza rejea ( Muehsam, D.; Ventura, C. Life rhythm as a symphony of oscillatory patterns: Electromagnetic energy and sound vibration modulates gene expression for biological signaling and healing. Glob. Adv. Health Med. 2014, 3, 40–55. )

Bado Sehemu Kubwa Haifahamiki Kuhusu Utendaji Wa Muziki

Pamoja na tafiti hizi kujitahidi sana katika kuchambua, undani wa madhara ya muziki katika biolojia za viumbe, lakini bado, sehemu kubwa haifahamiki. Lakini kitu pekee kinachotishia sana ni kuwa, kuna uwezo wa kutumia mawimbi ya sauti, katika kuathiri matendo mbalimbali ya kibiolojia ya viumbe. Tena, katika kiwango cha chini kabisa. Sayansi inaendelea kupambana ili iweze kufikia kiwango cha kutambua, namna sauti inavyoweza kuathiri chembe moja moja katika mwili wa kiumbe, kitu kinacho fahamika mpaka sasa, ni namna ambavyo sauti, inaweza kuathiri matendo ya kibiolojia kwa ujumla kwa viumbe. (Stoilov A, Muncan J, Tsuchimoto K, Teruyaki N, Shigeoka S, Tsenkova R. Pilot Aquaphotomic Study of the Effects of Audible Sound on Water Molecular Structure. Molecules. 2022 Sep 26;27(19):6332. doi: 10.3390/molecules27196332. PMID: 36234868; PMCID: PMC9573228.)

MADHARA YA MUZIKI KATIKA SAIKOLOJIA YA WASIKILIZAJI

Utangulizi

Jedwali La Maeneo Ya Ubongo Yanayosisimuliwa Na Muziki

Maeneo ya ubongo yanayosisimuliwa mtu anapokuwa akisikiliza muziki. Maeneo haya yanaeleza namna muziki, ulivyo wa msingi sana. hii ni kwa kuwa, ni maeneo ambayo yanashughulika na sifa mbalimbali za msingi za tabia za watu.

Region (Brodmann Area)

Temporal cortex (YANAHUSIANA NA SAUTI, MUZIKI, LUGHA,KUMBUKUMBU, TAARIFA ZA VITU )

Right

Primary auditory cortex (41)

Secondary auditory cortex (22 and 42)

Superior temporal sulcus (21 or 22)

Temporal pole (22 or 38)

Middle temporal gyrus (21)

Left

Primary auditory cortex (41)

Superior temporal sulcus (21 or 22)

Limbic areas ( YANAHUSIANA NA HISIA NA KUMBUKUMBU)

Right

Anterior insula

Hippocampus

Left

Retrosplenial cortex (29 or 30)

Anterior cingulate cortex (32)

Anterior insula

Subcallosal cingulate gyrus (11 or 25)

Others brain areas (YANAHUSIANA NA TABIA ZA KUIGA)

Lingual gyrus (18 and 19)

Inferior parietal lobule (39)

Maana Ya Msingi Ya Jedwali

Muziki husisimua moja kwa moja sehemu zinazohusiana na hisia, kumbukumbu na sehemu za lugha, tabia na kujifunza.  Kama ukimuambia mtu akumbuke maneno yaliyo katika wimbo, na maneno yaliyo katika kitabu, basi itakuwa ni rahisi sana kwa kukumbuka maneno yaliyo katika wimbo. Hii ni kwasababu, muziki unapendwa sana na kupewa sana kipaumbele na ubongo. hii ni kwasababu, muziki umeungana sana na hisia. na pia, una husiana sana na misisimko ya kujisikia raha, kama tulivyoangalia katika sayansi ya muziki katika ubongo.

Katika sehemu hii tutaangalia ni kwa namna gani, mtu anaweza kutumia uhusiano huu wa muziki, katika kuleta madhara makubwa sana, katika saikolojia ya msikilizaji.

MISINGI YA UHARIBIFU WA SAIKOLOJIA ZA WATU KUPITIA MUZIKI

Kutumia Mabiti Ya Nyimbo Zenye Midundo Kuondoa Uwezo Wa Kutafakari

Tumeshaona kupitia tafiti mbalimbali, namna ambavyo nyimbo zenye mabiti mengi sana (polyrhythms) hupelekea msisimko mkubwa sana wa ubongo. kama yalivyo madawa ya kulevya. (unaweza rejea nukuu ya Peter vuust: interplay of music and psychedelics). Na kwa mantiki hiyo, misisimko hiyo ambayo huchochea miondoko ambayo inaweza kupelekea kucheza, au hisia za raha sana (fananisha, watu wanapokuwa wameshinda kombe hushangilia sana, muda mwingine hata kutokujali kama wanaweza kujidhalilisha), hizi zote zinaelezwa kwa nadharia hii hii moja ya tabia za muziki, kudhoofisha uwezo wa kutafakari.

KWANINI WATU WANACHEZA 

Kucheza kuna maanisha, mabiti ya muziki yameingia hata ndani kabisa ya Ubongo, na kushabiiana na mawimbi ya mwili mzima. (rejea :entrainment na embodiement) na kitendo hiki cha kushabiiana, humfanya mtu Kwenda na mabiti haya, kwa kuyacheza, kwa lengo la kuongeza msisimko mzima wa mapigo haya (rejea: freeing attention with dancing), sasa basi, nyimbo zote zenye mabiti ya kuchezeka, huondoa utaratibu na uwezo wa ubongo wa kutafakari (rejea:disturbance in beta waves), na hii ndiyo sababu, mtu hawezi kutafakari mipango yake kwa ufasaha, akiwa anakimbia, au anafanya kazi ya kuchosha misuli. kwasababu kubwa moja, kufikiria, kuna husisha kusitisha kupokea taarifa toka viungo vya fahamu. (ukiwa unawaza, unaweza fumba macho kumaanisha ‘’hupokei taarifa za kuona’’, unaweza acha kusikiliza kelele, na mazungumzo ya watu. ‘’kumaanisha, hupokei taarifa za masikio’’, unaweza acha kuhisi maumivu madogo madogo ya viungo na uzito ‘’kumaanisha hupokei taarifa za ngozi’’, unaweza pia usisikie hata Ladha ya chakula kilicho mdomoni ‘’kumaanisha hupokei taarifa za ulimi’’ na mwisho unaweza usihisi harufu nzuri au mbaya zinazokuzunguka ‘’kumaanisha hupokei taarifa za harufu za puani’’). na sasa basi, sifa hizi zote haziambatani na kucheza, au kufanya kazi, ambako, kunahitaji sana kuangalia, ili uwe makini usiumie au anguke. Hivyo ukitaka watu wasifikirie, wewe wapigie nyimbo za midundo ya kucheza.

Mlevi aliyelewa kisawasawa, hata nyimbo yenye mapigo ya kawaida kabisa, yeye hujisikia kucheza. Huwezi elewa hili mpaka utakapojua kuwa, siku zote Ubongo wa kufikiria (prefrontal cortex una matabaka sita) umejaa channel zinazozuia mihemko ya hisia. (rejea: mtu mwenye akili hata akiwa na hasira, au mhemko, huwa hazioneshi hisia zake kirahisi ) sasa basi, Pombe hufanya prefrontal cortex ishindwe kabisa kufanya kazi yake (rejea sehemu ya pombe:kutokana na mgandamizo unaosababishwa na uharibifu wa kazi za kemikali za GABA, na Glutamate), kitendo hiki hupelekea mabiti ya muziki, yanapochakatwa kwenye sehemu za ubongo hasa wa hisia, kusababisha ‘’entrainment’’ au ubongo kuendana moja kwa moja na mapigo haya, na kuanza kusisimua misuli kucheza, ukiongeza na kujaa kwa mhemko wa kemikali za mhemko ‘’dopamine’’ basi mlevi lazima acheze hata kama kwa udhaifu sana.

Je wajua                                                                                           

Mara nyingi nyimbo za midundo ya kucheza, hupigwa maeneo ambayo watu huwa hawafikirii sana. Mfano kwenye ‘’Night clubs, vilabuni, Casino, Sherehe za kushangilia aidha ushindi, au kitu fulani’’, sehemu hizi pia huchangamana na unywaji wa pombe, maana muziki na pombe, ni kama pete na kidole, kila mmoja ana lengo moja la kuulevya ubongo mpaka mwisho.

Huwezi piga nyimbo zenye midundo ya kucheza, katika sehemu ambayo watu wanahitaji kuwa makini watafakari. Usikilizaji uliokithiri wa nyimbo zenye midundo, huanza kupelekea matatizo ya kudumu ya udhaifu katika uwezo wa kufikiria. Tafiti nyingi zinaonesha, usikilizaji wa nyimbo za midundo, hupelekea tabia za kuzoelea mihemko. kitu ambacho, huchochea uraibu wa kutaka kusikiliza nyimbo zenye midundo zaidi na zaidi, na hata baadae kuwa watu wenye maamuzi ya juu juu, na ya hatari, kwa kutokuwa na busara.

Sayansi  Ya Muziki Iliyofichika Ya Utofauti Wa Nyimbo Za Midundo Ya Kucheza Na Nyimbo Za Utulivu.

Watu wengi huchanganyikiwa katika uchaguzi wa muziki, maana kuna wengi ambao waliamini kuwa, nyimbo za dini ni nyimbo zilizotulia sana. Na nyimbo zisizo za dini, ni nyimbo zenye shida sana ya midundo. Lakini cha ajabu hata nyimbo za dini nazo, siku hizi zimeshamiri staili ya midundo, hebu tuangalie nini hasa ni sababu ya kushamiri kwa midundo.


Nilieleza awali kuwa Rhythm ni kujirudia rudia. Ukichukua kipisi  kimoja cha nyimbo. mfano ya Bongo flavour, ukikisikiliza unaweza sikia mabiti zaidi ya manne yakipigwa kwa kufuatana, na kujirudia rudia, lakini pia msanii anaweza kuimba nyimbo yenye mashairi ambayo, yana vina vingi sana vya namna ya kujirudia rudia, hizi zote ndizo ‘’rhythms’’ kuwa nyingi. Na nyimbo zikishamiri sana ‘’rhythms’’ zinazopigwa kwa mara moja, huwa zinaitwa ‘’polyrhythms’’. Nikiwa jeshini, tulikuwa tukiimba nyimbo wakati wa jogging, yenye maneno manne tu, lakini tukakimbia kwa umbali mrefu sana, hii ni kwasababu, katika nyimbo hiyo, tungerudia rudia maneno hayo hayo kwa mara nyingi sana. na tena, kwa haraka haraka, na nyimbo huleta morale ya kukimbia parefu sana, huo pia ni mfano wa ‘’rhythms’’, neno lolote lile kama mtu atalisema mara nyingi sana, akilirudia rudia mara nyingi, basi litakuwa ni nyimbo, na kama mtu ataliongezea mbwembwe (kama ataongezea mabiti, makofi,vinanda n.k) basi utakuwa wimbo mzuri kabisa, hiki unachokiongezea, ndicho kinaitwa ‘’Harmony’’. Mfano neno ‘’Honey’’ linalotamkwa ‘’Hanii’’, mtu akilisema mara moja, haliwezi kuwa wimbo, akilirudia mara mbili kwa kulipa mpishano wa muda maalumu ambao unatengeneza ‘’Meter’’. Yaani

 ‘’Honey…Honey…’’(limeshatengeneza‘’melody’’),

kama atalirudia mara nne, tayari limeshaunda ‘’verse’’, kama ataongezea na mabiti au ‘’Harmony’’, tayari umeshakuwa wimbo. Nyimbo nyingi sana zisizo za dini, hutumia tekniki ya kurudia rudia au ‘’polyrhythms’’ kutengeneza nyimbo zenye mihemko. Japokuwa zipo hata za dini siku hizi hutumia mbinu hii.

Siri Ya Ubongo Wasiyoijua Wasanii Na Wapenzi Wa Nyimbo Za Kizazi Kipya

Ubongo hasa wa kufikiria ‘’prefrontal cortex, orbitalfrontal cortex, cingulate cortex, n.k.’’ haupendi kurudia rudia vitu. Na ndiyo maana, ukishaiangalia filamu, haitakuvutia sana tena. au hata nyimbo ukiisikiliza sana, hautavutiwa nayo sana. Au hata kitu ukikizoea sana, hautavutiwa nacho sana. Sasa basi, Nyimbo hizi za kujirudia rudia mara nyingi, ili zimvutie mtu, inapaswa ziende kwa haraka haraka. Hii ni kwa lengo la kwanza kabisa, la kuudanganya ubongo kuwa, kuna verse mpya inakuja baada ya muda mfupi sana (fananisha na umakini wa mtu unapoongezeka, unapomwambia, hebu subiria mara moja!!!). sasa basi, baada ya kipindi kifupi panapokosekana mabadiliko, ubongo wa mbele ‘’PFC’’ huachana kabisa na kutafakari huu mziki. Na hii huwa inatokea hata kipindi cha Jogging, baada ya muda, Ubongo huwa unapoteza kabisa mvuto wa nyimbo na kiongozi hupaswa kubadilisha. Sasa basi, kwa wasanii wa nyimbo za kizazi kipya, mara nyingi ili kuendelea kuchukua umakini au ‘’attention’’ ya ubongo, basi hutumia mabiti yaliyopangiliwa kwa ufundi sana ‘’polyrhytmic sound beats’’, na kwa haya mabiti, ubongo hupagawa ukiendelea kutafakari, lipi hasa ndilo biti mama ‘’accent meter’’ kwa namna yalivyo mabiti mengi. Haya yote yakiambatana, hupelekea hali ya Ubongo kupumbazwa, na ilihali umechangamshwa. Hii ni sawa na mgonjwa wa kifafa, anakuwa anasisimka huku hajitambui. Na ndiyo maana, utakuta mtu anacheza lakini hasa haelewi nini kinachomsukuma acheze, mcheza mpira hukimbia akiwa na lengo maalumu la kuukimbilia mpira, au kipa huruka kwa lengo la kuutafuta mpira hewani, mcheza mziki hata hawezi kuelewa hasa kwanini anacheza. Ila anachohisi ni kuwa, amesisimka kwa raha, na zinamsukuma kucheza ili kukazia hisia zake za raha.

JE KUCHEZA NI VIBAYA??



Hapana, Watoto hucheza sana maana Ubongo wao bado hauna uwezo wa kujizuia, na hisia kwao zina nguvu sana. na ndiyo maana, mtoto ni rahisi kulia na akacheka ghafla, bado ubongo wake ‘’cerebrum’’ haijakomaa na hisia zina nguvu sana. Lakini pia mtoto hucheza cheza sana ili kutumia sana misuli yake. kuongeza ukuaji wa sehemu za Ubongo. kupitia kucheza cheza huongeza uwezo wa kuelewa namna viungo vinavyopaswa kuwa, na balansi katika pande kuu tatu za dunia. mtoto mdogo hujifunza kila muda, kwa kuwa bado, hajui vitu vingi, na hii ndiyo sababu pia, Ubongo wake huwa hautulii, ili aende kila sehemu, akijifunza mazingira yake. Watoto hufundishwa kwa namna ya kutumia viungo, wakicheza na nyimbo. Mfano, sote tulianza kukarii irabu kwa kuimba ‘’a,e,i,o,u’’. na hivyo hivyo kwa silabu zote. Hii inadhihirisha namna ‘’kucheza kunavyokazia umakini na kumbukumbu, mtu anayecheza muziki, pia anakazia tafakari za mabiti bila yeye kujua! 

Mtoto kadri anavyokuwa tabia hizi huisha, huwa hapendi kucheza cheza mbele za watu (maana huwa sio hisia rahisi kufurahisha kwa wengi, wengine huisi kama ni udhaifu kuanza kucheza mbele za watu, kama ukiwaambia ghafla watu 10 unaofahamiana nao, waanze kucheza mbele za watu, hata kwa nyimbo wanazozipenda, ni asilimia ndogo sana watakuwa na ujasiri!) kucheza ni matokeo ya udhaifu wa kushindwa kujizuia, na ndiyo maana, kuna mabiti yanapopigwa tu, watu hata bila kutaka, hujikuta wanaanza kucheza au kuhisi hali za kutokuwa na utulivu. Pia hisia za kucheza, huwa na nguvu mtu anapokuwa peke yake, au na watu anaowaamini sana, ni rahisi kwa mtu kucheza na mpenzi wake, au rafiki zake, hii inarejea kulekule kwa nadharia ya kucheza na udhaifu. Kwa hivyo, Watoto huacha kucheza cheza kadri umri unavyosonga mbele. Ingawa, matumizi ya mabiti ya ‘’polyrythms humrudisha mtu katika umri wake wa utoto kwa kucheza’’.

Narudia kucheza sio vibaya hata kwa watu wazima, ni hisia ya asili ya ubongo. ila, kucheza hakuambatani na utendaji kazi wa kifikra pana, kama kutafakari, kuwa na kiasi, n.k. ‘’Central executive network’’ haifanyi kazi unapocheza kiuhalisia. ubongo kwa muda wote mtu anapocheza, huwa bize kufatisha mawimbi ya mabiti, kuwa makini na balansi ya mwili, sehemu za hisia huwa juu sana, na motisha ya matumizi ya misuli huwa juu kadri ubongo unavyohangaika kufatisha mabiti yaliyo complex.

Pia, ni raha na rahisi kumwangalia mtu akicheza, lakini sio rahisi kwa mchezaji hata atakapokuwa mzoefu. Kisaikolojia, hapa huwa sawa na mtu anayepiga chabo mtihani wa mwenzake. Ubongo hupenda kuona namna kazi yake iliyopaswa kuifanya, ikifanywa na mwingine vizuri zaidi. Wengi tunapenda starling anavyopigana katika filamu ya kivita, kwa kuwa kupitia ‘’mirror neurons’’ tunajiona sisi ni kama yeye. Watazamaji wa ‘’Pornograph’’, hutamani sana wanayoyaona, ingawa wanajua ni matendo ya udhaifu, na hakuna mtazamaji ambaye angetamani aanikwe yeye vile katika udhaifu. Hivyo basi, Ijapokuwa wengi hupenda kutazama udhaifu kwa wengine, wao wenyewe wasingeukubali, au wangeukubali katika siri tu, na ndiyo maana, wengi wetu hucheza sana miziki tunapokuwa sirini, au na wale tunaowaamini sana, au labda kama tayari mtu ashapata saikolojia mpya ya kupuuzia udhaifu wake!!

Kucheza Sio Kushangiilia!!

Baadhi huchanganya kauli hizi mbili, kushangilia ni mihemko ya kusheherekea. kwa kuongeza hatua za misuli, na hata kuruka ruka, hii ni hisia ya kila mtu mzima atakaye shinda. Na mtu hushangilia akiwa na sababu maalumu, zilizotangulia. Lakini kucheza, kuna maanisha tendo linaloanzia katika msisimko unaotengenezwa na Muziki. (kushangilia kunaanzia na ushindi, labda vitani, mtihani au chochote kile). Utagundua pia kushangilia, hakuna steps maalumu. lakini kucheza, kuna steps maalumu.

Sio Nyimbo Zote Zisizo Za Dini Zina Madhara Na Sio Kila Nyimbo Ya Dini Haina Madhara.   

Nyimbo zisizo na madhara ya hapo juu, huwa na sifa ya kuwa na kiwango kikubwa cha ubora wake katika ‘’Melody’’. Melody ni kama vile kusema, nyimbo inakuwa imejikita zaidi katika ubora wa mashairi huku ikiwa haijaegemea katika mabiti.  Mfano mzuri wa hizi nyimbo, hebu tafakari nyimbo ya taifa ya Tanzania

’Mungu Ibariki Afrika, Wabariki viongozi wake,                                                                                           Heshima uhuru na umoja, hizi ni ngao zetu,                                                                                              Afrika na watu wake, Ibariki Afrika,                                                                                                          Ibariki Afrika,  Wabariki Watoto wa Afrika.’’

Katika hii nyimbo, kuna Rhythm. Lakini sehemu kubwa imejikita katika melody ya nyimbo. Na ndivyo ilivyo pia kwa nyimbo nyingi za vitabu vya zaburi. Msanii wa singeli angeweza kuchukua tu neno ‘’Mungu ibariki Afrika’’ na akatengeneza nyimbo kwa kujaza ‘’Rhythms’’ na harmony (mabiti na vionjo)

Wapo wasanii wanaoimba nyimbo zisizo za dini na wakiimba agenda za msingi tu katika Maisha, na huimba kwa kuzingatia melody ‘’ambapo ndipo uwezo wa msanii hupimwa’’. Kumbuka dini ni Imani ambayo kila mtu anayo, kukosa dini ni kukosa Imani ya uwepo wa chanzo cha maadili, kwa kigezo cha nadharia ya ‘’evolution’’ kitu ambacho ni hatari sana kwa maendeleo ya sayansi. mtu asiye na dini na haamini ‘’evolution’’ huyo bado haijui ‘’evolution’’ ila ndiyo anaiishi, ni sawa na kuchukua uraia wa marekani na kuikana Tanzania, hiyo wala haiathiri Utanzania wa Mtu kama alizaliwa Tanzania.

Je Wajua Kuna Nyimbo Za Dini Zilizojaa Rhythms!!

Unaweza kuta nyimbo moja ina dakika kuanzia 9 mpaka 14 hata 20 muda mwingine. Na inarudia maneno yaleyale, na mabiti ya frequency ndogo ndogo. Nyimbo hizi nazo huua uwezo wa ubongo wa mbele ‘’Prefrontal cortex’’, kwa kuwa ubongo usingependa kurudia rudia, ni kama tu ambavyo, ungekasirika  kama mtoto wako angekuwa anakuita ita kila baada ya muda, kwa kitu kilekile. Baadhi ya watu huwa wanaenda kwenye mikusanyiko mikubwa ya watu, na kupiga nyimbo za mtindo huu wakupooza, huku wakirudia rudia maneno.

na walivyo wajanja wasimamizi wa haya matamasha ‘’pia hutumia taa za mianga dhaifu’’ ili kudhoofisha zaidi na zaidi uwezo wa ‘’prefrontal cortex’’, madhara yake ni watu kupoteza kabisa uwezo wa ku focus, na hapo pia tutaangalia katika sehemu inayofuata madhara yake ni nini.

Pia zipo nyimbo za dini zenye mabiti ya midundo mikubwa sana ya kucheza, mara zote midundo ya nyimbo hizi huwa na misingi ile ile ya usisimuaji kwenye Ubongo, kama zile nyimbo za midundo zisizo za dini.

Je Wajua: Msifu Mungu Kwa Kucheza!!! Neno Kucheza Sio ‘’Dance’’ Ni Kifaa

Kuna baadhi ya watu walihisi labda Biblia ilipoandika msifuni Mungu kwa kucheza, ilimaanisha kucheza kama ‘’kitenzi’. Neno kucheza lilitafsiriwa kutoka neno ‘’Dance’’ ambalo katika Lugha yake ya asili, lilikuwa likitumiwa kama kifaa hiko hapo juu. Na katika fungu la zaburi 150 lilipotajwa neno ‘’dance’’ ulikuwa ni mfuatano uliokuwa unaorodhesha vifaa tu.  Lakini pia katika vifaa vyote vilivyoorodheshwa, hakukuwepo na Ngoma au ‘’Drums’’, ambazo ndizo msingi wa mabiti ya kucheza.

Hii ina maana gani?

Iwe kwenye sayansi za jamii, iwe kwenye evolutionary science , iwe kwenye neuroscience na mwisho iwe katika Biblia. Kote kutaleta jibu lile lile kuwa,  kucheza ni dalili ya moja kwa moja ya madhara ya kisaikolojia ‘’Psychopathognomic sign’’.

Kuna baadhi huuliza, kama ni hisia mbaya, kwanini ipo katika Ubongo? kucheza sio hisia mbaya, ni hisia za ndani za udhaifu, kama tu zilivyo hisia za kutaka kufanya mapenzi. kucheza kunahitaji upweke, uwe na mpenzi wako, familia, na marafiki. Kitaalamu lazima kuwepo ‘’Privacy’’, hakuhitaji kufanywa kwa umma, mfano, Kanisani, taasisi za elimu, vyombo vya serikali, au kiufupi ‘’Public’’.

URAIBU WA MIDUNDO SEHEMU YA KWANZA

Mtu anaposikiliza sana midundo ya nyimbo zenye kuhamasisha kucheza, katika ubongo wake anakuwa akimwaga homoni nyingi sana za ‘’Dopamine’’. Ambazo, huambatana na homoni za raha ‘’endorphins’’, hizi humfanya ajisikie raha. Na sasa basi, anapoisikiliza nyimbo kwa muda Fulani, na ubongo ukawa umeshauelewa wimbo vizuri, hakuna tena ‘’syncopation’’ na Ubongo hausisimki zaidi, basi huyu mtu hushuka ghafla sana, toka kwenye msisimko mkubwa, mpaka kwenye msisimko mdogo kabisa, kitu ambacho humfanya asijisikie raha kabisa.

Na hii shida sasa humfanya atafute nyimbo nyingine. hasa mpya, kwa ubongo, ili aweze kuuchanganya tena, Ubongo usisimke. mpaka utakapouelewa wimbo vizuri, ubongo usisimke zaidi, basi atakuwa na mwingine mpya tayari. Hii ndiyo siri ya waraibu wa hii miziki, kuwa na nyimbo nyingi sana katika ‘’playlists’’ zao. Na ukiwa msomi mzuri mchunguzi, sifa hii pia wanayo ‘’watazamaji wa filamu, waangaliaji wa video za ngono, waraibu wa mitandao ya kijamii n.k’’ hawa wote wapo katika kundi la uraibu, ambalo madhara yake huwa ni ‘’anxiety’’, ambayo huwafanya wawe na hisia kama za upweke, au kutoona wepesi, mpaka watakapopata vitu vya kuwasisimua zaidi.

Mpenzi wa nyimbo zilizojaa ‘’Rhythms’’ na harmony nyingi sana, hupenda sana kucheza ‘’kama ambavyo mlevi hupenda kucheza akishalewa’’. Madhara yake ni kuwa huyu mtu huwa inakuwa ngumu sana kuja kupenda nyimbo zisizo za aina hii.

Sifa Ya Nyimbo Zenye Melody Nyingi Zaidi Ya Rhythms

Mara nyingi hizi huwa hazileti uraibu. Lakini pia mara nyingi nyimbo hizi, huambatana na ujumbe ambao msanii huuwasilisha, na mtu anaweza kuzisikiliza nyimbi hizi, huku akitafakari lengo kuu la mtunzi. Hii inawezekana tu kwasababu, msikilizaji huwa huru katika Ubongo wake kutafakari ujumbe wa nyimbo, msikilizaji hashambuliwi na midundo ya ‘’rhythms’’ ambayo inamtengenezea misisimko ambayo, atake asitake atakumbana nayo tu.

Je Wajua Mabiti Yote Ya Kucheza Hufanana??

Ingawa ni ngumu mtu kugundua kirahisi, lakini mabiti yote ya kucheza katika kiini chake hufanana, na hata ukivuta asili yake kabisa, utarejea kwenye ‘’polyrhythmic patterns za tangia miziki ya enzi za voodoo’’. Mara nyingi mabiti haya huwa ya asili ya Polyrhythms za Druple (4/4 kwa 3/4). Hizi druple ndizo biti pekee zenye connection au zenye channel zinazoenda kwenye sehemu ya Ubongo inayoitwa ‘’Basal Ganglia’’ ambayo huusiana na uchakataji wa miondoko. Na ndiyo huko huchangamana na channel zingine za mihemko, hata kuishia na kucheza.

Ushahidi Wa Nje Wa Watu Kukosa Uwezo Wa Kutafakari Kupitia Mapigo Ya Mabiti

i.Kuwepo kwa kesi za watu wanaovua Nguo Majukwaani. Hakuna mtu ambaye angeweza kufanya hivyo kirahisi, ijapokuwa wapo ambao wangeweza kwa sababu zao binafsi, lakini uwingi wa kesi hizi unathibitisha kuwa, watu hawa wamelevya na mabiti haya ya mihemko

ii.Kuongezeka kwa hisia za mapenzi katika clubs au vilabu vyenye namna hizi za miziki. Watu wengi wanaojaa katika viwanja vya mapigo ya mabiti haya, hujawa na mihemko ya kimapenzi. na ndiyo maana, utakuta mara nyingi wakicheza kwa kushikiliana katika staili za mapenzi.                  

Hii moja kwa moja inathibitisha kupungukiwa nguvu katika sehemu ya ubongo wa kutafakari ‘’PFC au prefrontal cortex’’. PFC ilipaswa kuzuia mihemko ya kimapenzi, mpaka watu wawe sehemu iliyo ya siri.( PFC huruhusu hisia za mapenzi sehemu yenye usiri tu, au giza, na ndiyo maana, katika sayansi ya uzazi, husemwa kuwa kwa viumbe wengi, kushuka kwa yai la uzazi kwa wanawake au ‘’ovulation’’ hufanyika gizani, lakini katika Ubongo inatambulika kirahisi kuwa, wakati wa usiku, jua linapozama ‘’kiwango cha homoni ya Norepinephrine’’ inayokinzana na utulivu unaopelekea mihemko ya kimapenzi , hushuka. Na hivyo kuruhusu mhemko mkubwa wa hisia za mapenzi, wapo viumbe wengi sana wasiozaliana hata kuwe na giza, au sirini) lakini uwezo wa kuonesha hisia za kutaka kufanya mapenzi hadharani, ni tatizo kubwa kabisa la Ubongo ‘’psychopathology’’ ambalo, linatokana na kuisha kabisa kwa uwezo wa kuhisi aibu. Aibu ndiyo msingi wa utu, watu hawa hawana kabisa ubinadamu. ni kama Wanyama, maana Wanyama baadhi kama mbuzi au kuku huweza hata kuzaliana mbele ya Watoto wao, au na Watoto wao. wakati Wanyama walio na akili kama nyani tu, au sokwe, hujikinga pia na hadhara kwa ajili ya mapenzi, hii inathibitisha mabiti ya muziki ni hatari kwa ubongo.

iii.kuweza kutamka na kusikiliza maneno machafu bila kushtuka. Wengi wa wasanii kama ungewaambia wayaseme maneno yao, kipindi cha ‘’interview’’ wanayoyaimba kwenye majukwaa, wasingeweza kirahisi. Lakini huyaimba kirahisi jukwaani. Katika mabiti haya watu huweza hata kutukana wazazi wao, na wasiwaze. Hii inathibitisha madhara ya kisaikolojia yamekithiri katika ubongo wa wasikilizaji

iv.Kushuka kwa nguvu ya elimu na uwezo wa kufikiria.                       

jamii zote duniani kwa zama hizi zimejaa vijana, na Watoto wapenda shari, wasio na huruma, na wasio na kujizuia. Hizi sifa ni kinyume kabisa na maarifa. na mwisho wake mkubwa, ni kuongezeka kwa changamoto zisizo na mwisho

v.Kuporomoka kwa maadili.

vi.kushuka kwa uwezo binafsi wa wasanii.

vii.Kushuka kwa mvuto na nguvu kwa nyimbo za maadili, na za dini. Watu wengi hawajui kwanini miziki ya dini haina nguvu tena kama ilivyokuwa zamani. Sababu kubwa ni kuwa, wasikilizaji wengi wameshaleweshwa na ‘’rhythms’’. hawawezi tena kuzielewa ‘’melody’’. Wasanii wa nyimbo za dini pia, wengi wameshaathiriwa pia, maana sanaa ya mabiti ina nguvu sana hasa kwa mtu asiye elewa siri zilizo nyuma ya mabiti na ubongo.

Kutumia Kuchanganyikiwa Kwa Watu Kuingiza Tabia Mbaya Hasa Za Uhuru Wa Tabia Za Kichafu





Falsafa Tatu Katika Zama Za Muziki Na Sayansi Katika Zama Za Usasa

Watu wengi wasiojua sayansi kiundani kabisa, hawatambui kuwa sayansi na muziki vyote vimepitia zama kuu tatu.

PRE-MODERN ERA ( tokea zamani za kale mpaka 1789)

hizi zama ndizo zama zilizoanzia toka uumbaji wa dunia. kwa wanaoamini Biblia miaka 6000 iilyopita, ambayo kwa miaka ya 1789, basi ingekuwa toka uumbaji mpaka miaka 5789. Na kwa wasioamini uumbaji wa Mungu, basi kuanzia miaka ya Bilioni 13.8 mpaka miaka ya 1789. Katika zama hizi sifa kubwa kabisa ilikuwa ni ‘’Upo Ukweli Ambao Unatoka Kwa Mungu’’ au wengine huuita ‘’Absolute truth’’.

Katika zama hizi, kila msingi wa maarifa ulitengenezwa. Na waasisi wa kila elimu au taaluma walianzia katika zama hizi.

Mfano

Falsafa zote za kina Socrates, Plato, Aristotle, Hippocrates, Pythagoras, Democratius. kusambaa kwa taaluma za kigiriki kwa nguvu ya utawala wa Alexander the great. Ukija kwenye Taaluma za matibabu au medicine za awali kabisa, tokea enzi za Galen mpaka zama za kuinuka kwa dola ya uislamu na kina Al Ibn issa, kuinuka kwa Imani ya Kikristo kuanzia miaka ya 30 AD, kuja kuinuka kwa dola ya kiislamu miaka ya 600AD, kuinuka falme za ulaya baada ya kuanguka kwa dola ya rumi ya magharibi miaka ya 395AD, kukua kwa taaluma za uinjinia tokea dola za china mpaka maendeleo makubwa ya taaluma za ujenzi za Rumi,  kukua kwa uprostestanti miaka ya 1500’s kulikochochewa na kina Martin Luther, maendeleo ya sayansi za Fizikia kuanzia kwa kina Copernicus, Galilei, Newton ,Leibniz, Descartes, na wengine wengi, kukua kwa sayansi za kemia kutokea ‘’alchemy’’ mpaka kwa kina ‘’Antoine Lavoisier’’. Falsafa nyingi sana na misingi mingi sana ya elimu ilianzia katika karne za hawa watu.

Zama hizi hakukuwa na mjadala kuwa kipi ni sahihi na kipi sio sahihi, ukweli ulikuwa unafahamika. Na ndiyo maana, utakuta mwanafizikia mkubwa kabisa kuwahi kutokea sir Isaac Newton akitengeneza nadharia ambazo ndizo msingi wa sayansi yote ya fizikia ya leo, lakini bado akisema Mungu ndiye aliyeshikilia ulimwengu, na bado akatumia miaka mingi sana kusoma Biblia. Ijapokuwa inafunirahisha leo hii ukijitambulisha mwanasayansi, na kisha ukaonesha unamwamini Mungu, watu wanakushangaa, kiufupi sayansi ilianzia kwenye imani hii.

Muziki katika zama hizi ulikuwa ni muziki wa ibada tu. Kipindi hiki muziki ulikuwa ni sehemu ya ibada. na sio muziki wa matumizi mengine kama katika zama hizi. Pia muziki ulitumika kwa heshima sana katika nyumba za kifalme, na matibabu kwa baadhi ya nukuu. Hakukuwa na miziki ya kucheza wala polyrhythms, katika sehemu kubwa za jamii za watu. hasa ambapo rekodi za historia zilizonukuliwa kwa jamii kubwa za watu wa Eurasia ‘’Ulaya na sehemu za Asia’’ sehemu zilizoendelea zaidi za awali, na kaskazini mwa Afrika. ijapokuwa maeneo yaliyokithiri upagani yakisiwa kuwepo tayari kwa mtindo huu wa midundo.

MODERN ERA (tokea zama za 1789 mpaka 1970)

Hizi zama katika historia ya Dunia, ndizo zama zilizojenga misingi ya kuua kabisa kizazi kilichofuata baada yake, kizazi hiki ndicho kizazi kilichoua dunia  kabisa. Katika kizazi hiki kulitokea mapinduzi makubwa sana ya sayansi, baada ya watu kuweza kufanyia kazi maarifa ambayo walikuwa tayari wameyasoma sana. Na hapa kulitokea mapinduzi makubwa katika nyanja zote. Katika upande wa sayansi ya Fizikia, kulitokea mapinduzi makubwa ya fizikia ya nadharia kwa kuamka kwa nadharia za fizikia ya kisasa, kama nadharia za Albert Einstein, ambazo, zilionekana kana kama zimekuja na majibu pale Isaac Newton aliposema kuna  mkono wa Mungu, na ikaonekana kana kama imani kwa Mungu ni kukosa majibu ya maswali ‘’God of Gaps’’, nadharia za albert einstein ambazo ziliitwa ‘’General na Special Relativity’’ zilikuwa zinakataa uhalisia mmoja wa kitu, bali zilikuwa zinasema kitu hubadilika kulingana na mazingira yake, katika namna bora zaidi ya kifiziikia, lakini pia zilikuja na namna ya kuelezea zaidi ‘’Gravitation’’ kama hali na sio kani au Force, watu walifurahia sana na hata Albert mwenyewe hakuamini Mungu ambaye Newton alimwamini. ( kumbuka Einstein mwenyewe kuna ushahidi mkubwa sana kuwa, nadharia zake nyingi alikopi kwa wenzake, poincare, na Lorentz, na wengine wengi, hakuna kubwa jipya alilofanya zaidi ya kuja na fasiri zake mwenyewe zenye kuathiri kabisa uelekeo wa fizikia bora ya utendaji) Pia nadharia za Quantum Physics, ambazo zilitengeneza hoja za kifalsafa, kana kama, katika viwango vya chini kabisa vya chembechembe, hakutabiriki! Hivyo, hakuna sheria za utendaji za kudumu, ni kama vile, asili ya vitu ni uhuru, usio na mipaka! Lakini hata hivyo, katika zama hizi tokea kabla ya hawa jamaa, alikwepo mwanasayansi kama Laplace ambaye naye alionesha kutoona sababu ya kuamini Mungu, kumbuka fizikia ndiyo sayansi iliyokuwa ina nguvu zaidi. na hivyo, comment kutoka kwa wanasayansi hawa zilikuwa na nguvu ya kubadili hata jamii. Zama hizi pia ziliibuka na mapinduzi makubwa ya sayansi za uinjinia, kwa kuja na sayansi za mionzi iliyopelekea mabomu, sayansi za uinjinia wa umeme, sayansi za uinjinia wa magari na vyanzo vya usafiri, sayansi za uinjinia wa vifaa vya muziki na kurekodia, kamera na video, mwanzo wa kukua kwa teknolojia za satalaiti na uinjinia mkubwa sana wa teknolojia za leo. Zama hizi zilikuja na mapinduzi ya kibiolojia ambapo anatokea Charles Darwin. ambaye nae, anapingana na misingi yote ya kuamini kuna muumbaji Mungu. kama ilivyokuwa tokea zama za kina Aristotle. Darwin akiwa na sapoti kubwa kuliko hata hoja zake baadhi, anapokelewa kama Einstein wa sayansi za uhai, hata kwenye Jiografia wanaibuka kina Charles Lyell. ambao wanachochea uumbaji wa dunia bila Mungu. tofauti na sayansi za waliokuwa tu nyuma yao tena kwa kufuatana ‘’George curvier’’ ambae alithibitisha uumbaji wa Mungu, katika masomo ya mabaki ya vitu katika ardhi, wapo waliokuja na nadharia za kila aina za kutokuwepo kwa Mungu na kuwa, Sayansi pekee inaweza toa majibu ikichanganywa na uwezo wa binadamu wa kufikiria. na hapa pia, wanasayansi wakwanza kabisa wa Ubongo, kina Sigmund Freud, walianza na nadharia za kukataa uwepo wa Roho kwa kuchukua kila kitu katika ufahamu kama matokeo ya ubongo. na mengineyo mengi.

Muziki katika zama hizi rasmi ulianza kubadilika katikla muundo wake. Wengine huziita hizi zama kama ‘’Romantic era’’ na muziki ulitumika sana katika namna ya kuwasilisha mawazo ya watu. Na dunia ilionekana sio sehemu bora ya utukufu kama awali, bali ilionekana kama sehemu ambayo haina Mungu, na mtu anaweza kufanya chochote kile. Matumizi ya Piano yalianza. Baadhi ya historia hunukuu pia kuwa, waafrika waliokuwa maeneo ya Marekani katika kuchangamana katika ibada na wazungu, waliokuwa na asili ya muziki ule wa awali uliokuwa hauna midundo ya aina nyingi. basi walianza kuunganisha vipengele mbalimbali ambavyo viliendelea kuwa na chembechembe za polyrhythms. Hizi ziliendelea kuboresheka kwa kadri muda ulivyokuwa ukienda mbele, na hata kupelekea muziki wa kwanza wa muundo wa muziki wa kisasa wa leo, kutoka kwa wasanii kama ‘’Robert Johnson’’’ au unaweza mwita ‘’first bluesman’’.

MWANAMAPINDUZI HASI ASIYESEMWA!!!

Kuna mtu mmoja aliyekuwa anaitwa ‘’Aleister Crowley’’,  huyu aliandika kitabu maarufu sana kwa zama hizo za marekani kilichoitwa ‘’Kitabu cha sheria’’ au ‘’Book of the Law’’. Katika kitabu hiki aliandika sheria moja kubwa ilikyokuwa inasema ‘’FANYA UNACHOJISIKIA’’ au ‘’Do what thou wilt’’. Pichani ni Jay Z akiwa na tishati iliyoandikwa, fanya unachojisikia. Falsafa hii na dini hii imesambaa kwa kila sehemu.

kwa kipindi hiki marekani ilikuwa na idadi kubwa sana ya wakristo, hasa kutokana wengi kukimbia toka ulaya. kukimbia ugandamizaji wa Papa kwa zama zile, na  tokea zama za giza ‘’dark ages’’. Na sasa basi, kutokana uwingi wa wakristo. na ukristo kuwepo kwenye mifumo mingi ya kiutawala. Shida ilianzia pale ambapo, bado kulikuwa kuna namna mbalimbali za kiukandamizaji, kwa watu wa matabaka ya chini. na hasa waliotoka hali za kitumwa. Watu hawa walichukia sana watawala wanaojitangaza kwa sera za kikristo lakini wana mitindo ya ukandamizaji, kwa hiyo sera za ukinzani kama Hii, ilichochea ujumbe huu wa fanya unachojisikia’’ ilikubalika sana. ilikuwa ni habari njema sana. Ulikuwa ni mithili ya wito wa amani, na hata ukisikiliza wasanii wengi wa Hip Hop wa marekani, waliotoka katika familia za kimasikini, utagundua ni kana kama aidha walikuwa wanalaani ugandamizaji, au wanalaani wagandamizaji wanaomtumia Mungu kuficha ugandamizaji wao, au walikuwa wanalaani mifumo na hata kutoamini Mungu wao. Bwana Alister Crowley anatambulika kwa kuanzisha kanisa la shetani ‘’Satanic Church’’, lakini wikipedia na vyanzo vingi pia humtambua kama muanzilishi wa siasa za ‘’Humanism’’ au imani za mtu kujiamini yeye mwenyewe, na kutotishiwa na mitazamo ya imani za kikristo.

Siogopi kusema kuwa yupo shetani, lakini kinachojulikana ni kuwa, wasanii wote wakubwa wa kizazi kipya cha muziki ambao nao ulikuwa katika mapinduzi makubwa hata kuzaliwa kwa ‘’Rock n Roll’’, Pop, Jazz na mingineyo. Wote walikuwa katika falsafa hii ya huyu bwana. Picha zote walikuwa wakiwa na nembo za jamii hii mpya. na wengi walikuwa wakiimba moja kwa moja kuwa ‘’hawaamini kabisa uwepo wa Mungu’’ au kuonesha wana mdhihaki. Na hata alipokufa Crowley, bado falsafa zake ziliendelea kwa uwepo wa wanaharakati wa aina yake wakubwa tena kama ‘’Anton Lavey’’ na hawa watu walikuwa na mafanikio makubwa sana, kwa kuibadilisha jamii kubwa sana ya watu. hii ni kwa kuwa, walikuwa wanatumia muziki, na pili walikuwa wanafanya mambo yao huku asiwepo mtu wakuwazingatia. Maana, ni taasisi za siri. Ni kama hivi leo msanii akionesha ishara za kishetani hakuna anayejali kwa kuwa haina msingi katika maana ya kawaida. Lakini kwa msomi mzuri wa sayansi, lazima ajue kila kinachoendelea na ndiyo maana, utamkuta ‘’Isaac Newton’’ akiwepo kwenye ‘’Alchemy’’ na hata Albert Eintsein akionesha imani yake, kwa Mungu wa Spinoza (anaamini asili ndiyo Mungu, huitwa pia Pantheism). kiufupi Swala la imani linahusiana moja kwa moja na uwezo au IQ ya mtu, kujitathmini yeye ni nani.

Ajenda kuu  za muziki mpya zilikuwa ni uhuru, wa kufanya vitu ambavyo jamii ingevizuia, kwa kutishia hofu za imani. Na watu wengi hawajui kwanini jamii kubwa za watu wa marekani, na Ulaya, hawana kabisa maadili. Unaweza kuta mtoto mdogo kabisa tayari anajihusisha na mapenzi, na hakuna anayejali, unaweza kuta watu wanafanya ushoga hadharani kabisa, unaweza kuta watu wanatembea uchi barabarani, unaweza kuta mauaji hayashangazi watu, unaweza kuta wanaume wanavaa milegezo mpaka chini kabisa ya suruali, unaweza kuta watu wanatukana mbele ya wazazi wao, unaweza kuta watu wanajichorachora, unaweza kuta watu wanalipua mabomu kama hiroshima na nagasaki vita ya pili ya dunia, unaweza kuta watu wanafanya tafiti za sayansi za kubadilisha jenetikia za watu, unaweza kuta watu wanafanya biashara ya vidole vya watu, kama wakoloni walivyofanya Congo, unaweza kuta nchi ina asilimia 85% ya watu hawana dini na waliobakia bado sio wadini, kama Netherland. Yote hayo yalianzia katika  muziki na yalianzia katika falsafa hizi katika kizazi hiki cha ajabu zaidi.                                          

 1960-1980: kuliongezeka asilimia 400% kwa ndoa za watu wasioona. Sababu:muziki!!               

Toka Uumbaji wa dunia- 1960:kulikuwa na magonjwa mawili tu yakuambukiza kwa njia ya ngono, leo hii kuna magonjwa 25.                                                                                                                                  Mauaji ya kimashambulizi yameongezeka kwa asilimia 995%.

Falsafa za Humanism na Satanism ambazo zimejikita katika hakuna muumbaji ‘’Atheism’’ , imani ya ‘’Evolution’’ na fanya unachojisikia, ilipata nguvu mpaka Serikalini rasmi. Na kwa mara ya kwanza miaka ya 1920’s. Shule zote zikaanza kufundisha hakuna Mungu, bali tumetokana na mabadiliko tokea ujiuji wa miamba, seli za vimelea, samaki, jamii za manyani mpaka watu. Na hivi ndivyo kila mtu amefundishwa, haikuwa hivi miaka michache tu nyuma.

Sababu Za Kutumia Taarifa Za Mihemko Ya Uchafu

Imani hizi hasa zilipata nguvu kutokana na kutumia sana mapenzi, katika kitovu cha kuondoa uwepo wa Mungu. Watu wengi hawajui Biblia iliposema Mpende Bwana Mungu wako, kwa Moyo wako wote, kwa Akili zako zote, na kwa Nguvu zako zote. Ili maanisha kuwa, Upendo ni mjumuisho wa moyo+hisia+nguvu. Hakuna kitu cha kufanania kupokea hizo sifa zaidi ya hisia za mapenzi. kupitia kuweka mapenzi, mtu angeweza kuigiza ibada hapo. Na ndiyo maana, imani hizi huambatana na sanaa za kusisimua hisia za ngono, na hata picha zao nyingi huwasilishwa katika muundo wa picha za uchi. Mwanaume anaweza kutumia nguvu zake zote ili amridhishe mwanamke, akatumia moyo wake wote na akili zake zote. Tayari mwanamke amekuwa kama Mungu. Na vivyo hivyo kwa mwanamke, na ndiyo maana, utakuta nyimbo nyingi za watu hawa wakisifia sana wapenzi wao. tena husema wewe ni ‘’Nyota ya maisha yangu, au kila kitu kwangu, au hata husema wewe ni Pumzi ya uhai wangu, ukiniacha napoteza uhai wangu”, kwa mtu asiyeelewa kuwa hiyo tayari ni ibada, ni rahisi kuupenda huu wimbo, bila kujua siri iliyo nyuma yake. Hakuna hata sehemu moja Suleiman alipomsifia mpenzi wake kwa sifa za muundo huo. Nyimbo zote zimejaa ajenda za mapenzi na ngono, au hasira na migogoro au ulevi na visasi. Wanasayansi wa kweli hutambua sababu hii.

Msingi wa pili wa imani hizi, ni kutumia sana Nguvu za sehemu za mamlaka ya umma na vyanzo vikubwa vya fedha. Jambo hili hulificha kwa siri sana ili lisionekane, na ndiyo maana, utakuta hata katika sayansi, pamoja na kitabu kama hiki kuwa kizuri sana, utaambiwa hakikidhi vigezo tu kwa sababu kinamtaja Mungu (rejea sababu ya Prof Damadian kunyimwa Nobel prize baada ya kugundua MRI, kwasababu tu ni Mkristo). Ukirejea Crowley angewezaje kupata nguvu kwa kiasi kile?, na kwanini zama hizo hizo?, na falsafa hiyo hiyo, iwe inakuwa maeneo yote ya dunia kama Russia?, ambako ilibidi hata kutokee mapinduzi makubwa, ambayo chanzo kabisa alikuwa ni Karl Marx, ambaye naye alikuwa na imani za kisatanist. Ambazo alizirithi Vladmir Lennin, ambaye nae alimpindua hata Tsar kwasababu alikuwa na imani ya Mungu. na wao sasa walianza rasmi kuingiza falsafa za Humanism Russia. Pia kwanini China? Kwanini Cuba? n.k. Mpaka hapa unaweza kujua kuwa, hata wale wasanii wengi walipata Nguvu kubwa kutokana na kuwa, walikuwa wanatumia sanaa ya kuteka akili za watu, lakini walikuwa wakifadhiliwa sana na mamlaka za siri zenye ajenda ya kuingiza falsafa za ki humanism. Huu ni muziki uliokuwa ibada, katika kubatiza zaidi vijana.

POST-MODERN ERA (kuanzia 1970 mpaka leo)

Zama zilizopita za modern era za kuanzia miaka ya 1789-1970. Iliaminiwa kuwa Sayansi, falsafa na logic zina uwezo wa kumuelekeza mtu katika ukweli au "absolute truth". Na hivyo Sayansi iliheshimiwa Sana, Kama chombo ambacho kina uwezo wa kumuelekeza mtu katika kuujua ukweli. Akili ya mwanadamu ilionekana ndiyo inamtengeneza Mungu, na sio Mungu anaitengeneza akili. Lakini Cha muhimu zaidi hapo nikuwa, bado kulikuwa na msingi wa ukweli, Ila haukutoka kwa Mungu, ulitoka kwa akili za wenye Maarifa.

Kilichofelisha Zama Za Modern Era

Zama zile zilizotegemea akili za watu, katika kuamua ukweli. ziliishia na migogoro mikubwa zaidi kuwahi kutokea katika historia ya dunia. Vita vya kwanza vya dunia, Vita vya pili vya dunia, mapinduzi ya damu katika sehemu mbalimbali za dunia, milipuko ya magonjwa ya kutengeneza, milipuko ya migogoro ya kijamii, kisiasa na kifalsafa. Maporomoko makubwa zaidi ya maadili.

Haya yote yalipelekea jamii zote za watu, kuishiwa kabisa Imani juu ya maarifa, Tena juu ya watu walioaminiwa kuweza kuwa na maarifa. Hii Ni kwa kuwa, maarifa ambayo walitegemewa kuwa nayo, ndiyo yameishia kutengeneza matatizo makubwa zaidi. Mfano mzuri, Ni namna taaluma za masomo Kama ya fizikia, yalivyo chochea uundwaji wa mabomu hatari zaidi duniani, masomo ya kemikali yakiishia uundwaji wa sumu hatarishi zaidi, na hata masomo ya maisha yakiishia na uundwaji wa magonjwa mengi zaidi ya awali. Zama zote hizi hakukuwepo na Biblia ya kurejea, kipi Ni kweli! na kipi si kweli! maana tayari kilionekana Ni kitabu Cha masimulizi ya kusadikika, na kisicho na hadhi ya kitaalamu. Na Hili ndilo lilikuwa hasa lengo na mwanzo tu wa dini mpya ya "Humanism''. ambayo ili Hali duniani haikutambulika kwa wazi, lakini ndiyo ilikuwa inachochea Kasi hasa kupitia Miziki pamoja na Nguvu za umma.

Kuzaliwa Kwa Zama Za Post-Modern Era

hizi ndizo Zama kuanzia miaka ya 1970. Katika Zama hizi Sasa, Dunia Haina wa kumsikiliza. Hakuna Sayansi, Wala falsafa, Wala logic na Wala Biblia. Zama hizi ndizo ile misingi ya dini mpya "Humanism''" imetawala kwa falsafa zake za fanya unachojisikia. "Do what thou want". Zama hizi Ni mfanano halisi wa kipindi Kama kile, baada ya falme ya Rumi ilipoupokea Ukristo. na kupelekea karibia dunia yote kuambukizwa ukristo. au Zama zile baada ya kuanguka kwa Alexander the great, ambapo karibia dunia yote iliambukizwa tamaduni za kigiriki. Na hivyo Basi Zama hizi, Ni kana kwamba sehemu kubwa ya dunia iliambukizwa tamaduni za "fanya unachojisikia". Matokeo ya Zama hizi Ni kuwa na jamii ya watu wenye mafundisho mengi zaidi, ambayo ndani yake hushindwa kabisa kuchambua kipi Ni sahihi, na kipi si sahihi. kila mtu Ni Mwalimu, kwa kuwa Hakuna standard au kipimo maalumu Cha kupima maarifa Kama awali. Zama za nyuma ingetumika Biblia, Zama za Kati ingetumika Sayansi na falsafa, lakini Zama za mwisho Hakuna kipimo!! Hizi ndizo Zama ambazo, zinamaliza kabisa uwezo wa binadamu wa kimaarifa, maana kila taaluma Haina thamani Tena.

Siri Nyuma Ya Msukumo Wa Vipaumbele Vya Elimu

Mfumo wa elimu hubadilika kwa kila zama, kulingana na uhitaji wa hizo Zama. Mfano, Zama za dhiki za migogoro ya kivita, elimu iliongozwa zaidi katika masomo ya ufundi, na fizikia, kwa lengo la kujenga silaha nzito, pamoja na ujenzi wa miundombinu mikubwa ya kiuchumi, na ulinzi. Kwa Zama baada ya migogoro, elimu huelekezwa zaidi katika taaluma za kutatua changamoto za matokeo ya migogoro, Kama vile, taaluma za kuboresha kilimo, matibabu, utunzaji wa mazingira na ukuzaji wa uchumi. Katika Zama hizi za post modern era, hakuna elimu Tena za muundo huu, maana hata watu hawajui matatizo yao. Elimu za uinjinia za maroboti, na akili za kisasa, zinapamba Moto zaidi! huku tatizo likiwa ni kukosekana kwa kazi, kwa watu, kwa kila sehemu. Hii Ni sawa na kusema, elimu inachochea Moto zaidi kuwachoma iliyopaswa kuwaokoa. jamii bado halilijui tatizo. Idadi ya matatizo ya akili, na kisaikolojia, yameongezeka Mara elfu zaidi ya Zama zote zilizopita. Dini inatumika Kama falsafa, falsafa Kama Sayansi, Sayansi Kama dini, kila mtu na mitazamo wake.

Sifa Za Zama Za Post-Modern Era

Kuongezeka kwa ubinafsi kwa Hali ya juu zaidi. Zama zote watu wangetoa maarifa yao kusaidia jamii zao, lakini Zama za PME, watu wenye maarifa hutumia maarifa yao, kujiweka juu zaidi, au kukandamiza zaidi wa chini. Hii ndiyo sababu ya matumizi makubwa ya maarifa, katika kubadilisha jenetikia za watu. ili kuwaathiri, kutengeneza vyakula vyenye madhara, kutumia teknolojia kushusha uwezo wa watu, kutengeneza Rocket za kwenda sayari za mbali, lakini kushindwa kutatua matatizo ya ajira. Asilimia karibia tisini ya Mali za duniani, zipo kwa asilimia kumi tu ya watu wote. Serikali zimejaa ubepari na migogoro. sio Tena nchi na nchi tu, Bali hata ndani ya wananchi.

Kupungua Sana kwa wasomi wakubwa, na watu wenye maarifa, Kama Zama zilizopita. Kila Zama zilizopita ungekutana na watu wenye maarifa, na kupendwa Sana na jamii zao. Lakini Zama hizi za PME bila hata aibu, unaweza kuta hata wasanii walio mfano mbaya kabisa, wakipewa tuzo za watu wenye hamasa zaidi. Sasa Watu watajifunza wapi? Leo hii Huwezi kumuelewa mwanafizikia Kama Michio kaku, au Brian green, au Penrose Roger, kama mtu mwenye maarifa zaidi, Kama hawezi hata kuelewa kuwa Hakuna ushahidi kabisa wa uumbaji usio wa akili, kupitia taaluma za Sayansi za biolojia. Matatizo yote yameanza baada ya watu kufundishwa nusu nusu tu.

Kuzidi kwa matatizo katika kila nyanja. kuanzia kijamii, kwa kuisha kabisa kwa maadili, kuongezeka kwa matatizo ya kiafya, matatizo ya kiuchumi, matatizo ya kisiasa, matatizo ya kiakili kwa kuongezeka Sana hofu. zinazotokana na changamoto za Maisha, zisizo na mwisho. kuzidi kwa uongo katika kila sekta, sio elimu , sio siasa, sio dini kumejawa na unafiki. hizi ndizo Zama ngumu zaidi kuwahi kutokea na zinaleta hofu Sana, katika kutabiri mwisho wake.

Kazi Ya Muziki Kama Msingi Katika Zama Mpya

Miziki ndiyo silaha kubwa ya dini ya "Humanism''. Inasikitisha namna ambavyo wasanii wengi wa Miziki ya kisasa, wasivyotambua suala hili. na hujikuta wakiendeleza utume wa dini hii, bila wao kujua. Wasanii hutumia mbinu kadhaa katika kusogeza falsafa hii.

Mbinu za Kisaikolojia za Wasanii, wasizozijua hata wenyewe.

Kufanya Vitu Kitofauti."kisanii"

Neno Usanii, kutumiwa Kama "utofauti" huanza kuharibu saikolojia za msanii mwenyewe, kabla ya watakaomsikiliza. Binadamu wote ni sawa katika kila hatua na hata tabia. Msanii hapaswi kujiona Ni mtu wa tofauti. Usanii Ni kujiongeza kitaaluma, kutokana na kipaji, sio kujibadilisha kitaaluma kutokana na kipaji. Sasa Basi, falsafa hii hatari huwafanya wasanii muda wote kujihisi wapo sahihi kwa kuenenda Kitofauti na jamii zao. Unaweza rejea interview nyingi za Beyonce ambae kwasasa Ni Kama "Malkia wa mziki wa kizazi kipya kwa dunia mzima", huwa anasema "nikiwa kwenye stage, huwa nakua sio Mimi Tena, Kuna mithili ya kitu huniingia na kunifanya niwe mtu mwingine kabisa, na Hali hiyo hunifanya nifanye Mambo yote ninayoyafanya pale,ambayo kwa akili zangu nisingeweza kuyafanya". Mfanano wa stori hizi huwa kwa Wasanii wote, kuaminisha zaidi umma kwa ajenda za kweli, au Wenda sio za kweli, lakini zote Ni kumtambulisha msanii Kama mtu wa tofauti na mtu wa Kawaida. Hivyo msanii atafanya vitu vyote ambavyo mtu wa Kawaida "aliyeumbwa na Mungu" asingeweza kuvifanya. Hii maana ya msanii Ni Kama inamtambulisha msanii, Ni mtu mwenye matatizo ya akili, au mtu mwenye pepo. Kitu pekee ambacho huwashangaza hata Wasanii wenyewe, Ni namna ambayo Mara zote, utofauti wao hukubalika!!, Wasanii baadhi hufanya vitu viovu kabisa! hata wao wasingetamani kuvifanya kisanii, lakini bado hushangaa kuona wanawafuasi wengi. Hii Sasa huwafanya wawe watumwa wa akili zao wenyewe. Hebu angalia kwa mfano, sifa zifuatazo za msanii Kama mtu wa tofauti.

Msanii Ni mtu ambae anaeweza kuvaa nusu uchi, na jamii bado ikamkubali

Msanii Ni mtu ambae hapaswi kuvaa nguo, Kama ilivyo kawaida ya watazamaji wake

Msanii Ni mtu ambae anaruhusiwa kutukana, na kuzungumzia lugha chafu, bila kushangawa

Msanii Ni mtu ambae kila anachofanya, anapaswa kukidhihirisha kwa umma

Hii Ni mifano tu ya matatizo ya awali kabisa ya kisaikolojia, yanayojengwa kwa Wasanii. Na matatizo haya huwafanya wengi  Wa Wasanii, wawe Ni watu ambao muda wote huwa wanahangaika kufanya Vitu Kitofauti na maadili, tofauti na mitazamo, tofauti na mategemeo, na hata tofauti na mamlaka zozote zile zilizopo. Wenda Ni dini, serikali, familia , taasisi na zinginezo nyingi Kama familia.

Kutegwa kutamani umaarufu Kama mafanikio toka kwa mashabiki

Hapa Kuna saikolojia kubwa Sana kwa Wasanii wengi. Ndoto zao huwa Ni kuwa na wasikilizaji wengi Sana, na hasa kwa kufatiliwa Sana, na kuwa maarufu. Lakini tatizo kubwa Sana ambalo huwa hawalijui Ni kuwa, mafanikio hayatokani na umaarufu, na mafanikio hayatoki mbali. Kupitia kuwa na wafuasi wengi, kwenye mitandao ya kijamii, hakumfanyi mtu kuwa na mafanikio yoyote hata ya kiuchumi. maana mitandao yote inayotawala biashara za internet na Aina zake mfano "Spotify" au apple" yote huwa chini ya taasisi za watu wenye ajenda zilezile za kutawala watu. Matokeo yake huishia tu wasanii wakijiona Ni maarufu, lakini bado wanachangamoto kubwa za kiuchumi, na kijamii. na kibaya zaidi, jamii haiwategemei kuwa katika Hali hizo, maana sivyo wanavyojionesha katika nyimbo zao. Na kwa mantiki hiyo, Wasanii wengi wakubwa hujikuta wanaingia katika hatari ya kuingia katika mkataba wowote ule, ambao utatumia umaarufu wake, kuwasilisha ajenda. na ili Hali itawaachia namna walau Bora ya kuishi, kwa viwango vya umaarufu wao.

Biashara zote za wireless technologies, au teknolojia za Mitandao, hazifanyiki kama utendaji wa biashara za moja kwa moja. Mitandao ipo chini ya uongozi wa moja kwa moja wa vituo vikubwa kabisa vya mawasiliano. Ambavyo, hutawala mawasiliano kulingana na ajenda zao. Mitandao Ni ya kuwa nayo Makini Sana. Hata kwa wasomi wazuri wa Sayansi za kompyuta, hushauri hivyo. utendaji wake Ni Dhahiri, lakini, unapaswa kutazamwa kwa umakini, hata Kama mtu ataona ametazamwa na watu bilioni moja. Je yeye ana uhakika gani? Amewaona? Waliomtazama wamevutiwa naye? Walikuwa na lengo la kumtazama? Hayo yote yanaweza kumaanisha kuwa, umaarufu hutengenezwa, au huweza kuharibiwa.

Hali Za Wasanii Maarufu Zisizosemwa!

Wasanii wengi walio maarufu, wengi hujutia hali zao baada ya muda tu, aidha hadharani au sirini. Lakini wote hujutia Hali zao. Wasanii wengi Kama Michael Jackson, wamewahi kuonesha kabisa hadharani kuwa wanateseka, au wapo kifungoni. Wengine hawana kabisa amani, na hukiri kuwa hawafurahii, Ila hawana namna. Unaweza tazama namna Wasanii wengi hawana familia za kudumu, ili Hali katika nyimbo zao, huonesha hufurahia mahusiano yao ya ndoa!!

Kuaminishwa kuwa Mapenzi Ni mazuri Kuliko ndoa.

Wasanii wengi huaminishwa kuwa, kupitia kutembea na mabinti wazuri wa mionekano ya sura, na maumbile. au wanaume wazuri wamionekano, na utajiri. basi wanaweza pata faraja kubwa sana. nyimbo nyingi huyatukuza Mapenzi, Kama faraja yenye hisia za kiungu "divinity na eternity". Falsafa hii unaweza iona kwa namna nyimbo nyingi zina ajenda za Mapenzi, na hufanyiwa video kwa kushirikisha ma videovixens. na hivyo hivyo kwa wanaume. Hii mitazamo dhaifu kabisa ya kisaikolojia, huanza kuisha baada tu ya mtu kuanza kuvuka Zama za ujana, na kuanza kuingia hatua za utu uzima. hisia Kali za Mapenzi huwepo ujanani, kwa lengo la kutafuta mwenzi na kuzaa. Ila baada ya hapo, hupoa au kushuka kwa lengo la kulea na kuishi na familia (haimaanishi huisha, ila hushuka!) Na tabia za kutembea na wanawake wengi, huondoa kabisa uwezo wa ustahimilivu kifamilia. maisha huwa mabaya asilimia zote. Kwa kukosa familia, kwa kuhisi hatia na kwa kudhalilika nafsi.

Namna Jamii Inavyoharibiwa Saikolojia Kwa Kusikiliza Nyimbo Hizi

Kwanza kabisa nyimbo hizi huambatana na mapigo ya nyimbo za mabiti, au polyrhythmic beats, ambazo, tulishaona katika sehemu iliyopita namna zinavyoharibu ubongo. Nukuu mbalimbali huonesha namna ambavyo usikilizaji wa mabiti yanayojirudia walahu Mara tatu au nne tu, huifanya sehemu ya ubongo wa mbele kupoteza kabisa hamasa na kuuacha ubongo ukiwa huru, kwa mihemko ya moja kwa moja ya mabiti, kutoka katika sehemu ya hisia kupitia kitendo kinachoitwa "Entrainment". Sasa Basi, baada ya ubongo kupoteza kabisa uwezo wake wa kushikilia umakini, Nini hufuata ambacho huua ubongo.

Taaluma Ya Kuingiza Mitazamo Katika Ubongo Wa Msikilizaji Bila Msikilizaji Kujitambua

Kuingizwa kwa falsafa za msanii katika ubongo wa msikilizaji moja kwa moja, katika sehemu za hisia ambazo kitaalamu huitwa "subconscious mind". Wachache Sana wanaoweza kujua hii mbinu Makini Sana ya kisaikolojia, ya Hali ya juu. Sehemu za ubongo za hisia, zinachangamana moja kwa moja na sehemu za kumbukumbu. Ndiyo maana, unapokumbuka tu kitu, huja na hisia zake. Au watu hukumbuka Sana vitu vinavyowaumiza Sana, au wafurahisha Sana, Kuliko wanavyokumbuka vitu vyenye mhemko mdogo wa hisia. Mfano mwalimu aliyekuwa anachapa sana, utamkumbuka zaidi ya yule wa kawaida. Sasa basi, kitendo Cha watu hawa kuleweshwa na mabiti, hata kuondoa uchujaji wa kinachotakiwa kukumbukwa. ambayo ndiyo kazi ya prefrontal cortex, basi ubongo wa kumbukumbu na hisia hupokea moja kwa moja mitazamo ya msanii. hata bila ya msikilizaji kujua, Kama anawekewa kumbukumbu bila yeye mwenyewe kujua.

Madhara yake hujikuta msikilizaji akiwa tayari ameshaambukizwa tabia, na falsafa za msanii wake, hata bila yeye mwenyewe kuamua. Tuliona katika sehemu ya juu namna ambavyo wimbo wa matukano, mtu angeogopa kusikiliza, lakini baada ya kusikiliza Mara mbili au tatu. Hujikuta tayari ameweza hata yeye kuyatamka matukano yaleyale bila shida!! Msanii anaweza kufundisha namna kadha wa kadha ya tabia za uchafu, na msikilizaji ambaye hujidanganya kuwa anasikiliza tu Wala hatafuata, hujikuta tayari na yeye akitenda yaleyale. Sheria Ni ile ile ya utendaji wa Miziki, ambao, hufukuza kwanza mlinzi wa Ubongo. ambaye, Ni prefrontal cortex. na kusisimua mifumo ya kumbukumbu ya fahamu, na kuingiza moja kwa moja falsafa zake.

Ushahidi mkubwa unaweza kuangalia tu, namna tabia za watu zinavyofanana, na Aina ya nyimbo zao wanazozisikiliza. msikilizaji wa nyimbo zenye mabiti ya hip hop, ambayo hufahamika kwa sifa ya ku "drain off" au kupumbaza kabisa mawimbi ya Beta waves ya kwenye ubongo. na hatimaye kupelekea mtu kuingizwa falsafa za msanii, ambae Mara nyingi huwa mtukanaji au mpinzani mwenye Hasira.

Kutumia Mabiti Ya Mawimbi Ya Mihemko Ya Kingono Na Sauti Za Mivuto Ya Hisia

Mbinu hii huwasaidia Sana Wasanii kuwalevya zaidi wasikilizaji wao. Kama msanii atatumia mabiti yanayoendana sawa na frequency za matendo ya kimapenzi. kipindi Cha entrainment, Ubongo utahemka zaidi kimsisimko huo huo wa mabiti, na msanii atakapoongezea na maneno yake. Basi atapelekea kuwepo kwa mtu ambaye tayari Ni mlevi wa Mapenzi. Hii ndiyo sababu Mara nyingi wasikilizaji wa nyimbo hizi, huwa wanamisisimko mikubwa Sana ya kingono. ukilinganisha na wasio wasikilizaji, ni kwasababu huwa mifumo yao ipo juu juu Sana.

Video Za Miziki Ya Midundo, Taa Za Mianga Hafifu Na Maonesho Ya Taswira Za Kimivuto Ya Mapenzi

Nyimbo nyingi zimejaa video za mtindo huu. Utaona Wasanii wakiwa wamevaa kimivuto ya kimapenzi, wakiwa maeneo ya kuvutia, na mianga hafifu wanayoitengeneza kwa teknolojia nilizozielezea sehemu ya udanganyifu wa macho. Sasa hebu changanya vitu hivi vitatu kwa Pamoja, halafu uone Nini kinatokea katika Ubongo!!

Ubongo unakorogwa kabisa maana mfumo mzima wa Fiziolojia ya kuona, inayohusiana na Imani pia, unakuwa umeshambuliwa Kama tulivyoona kule juu. Lakini pia mfumo mzima wa Fiziolojia ya kusikia, unaoambatana na  kufikiria, unauwawa. Na zaidi mfumo wa hisia, unasisimuliwa moja kwa moja, hii Ni hatari kubwa ambayo madhara yake kwa kuangalia tu Mara moja, yanaweza mfanya mtu aathiriwe kwa kiwango kikubwa Kama hatakuwa mraibu.

Watu wengi hudharau madhara haya, ili Hali wao wakiwa ndiyo wahanga wakubwa zaidi wa kitabia, na wakipitia matatizo makubwa wanayoshindwa kuyatatua, kwa kukosa kabisa uwezo wa kufikiria. Zama hizi zenye changamoto zote, Kama tulivyoona katika sehemu iliyopita, changamoto zote zimetokana na video hizi ambazo, ndizo ibada mpya katika kizazi Hiki Cha hatari kabisa kuwahi kutokea.


INJILI YA SAYANSI TUNAKUPENDA SANA MSOMAJI WETU.

MAWASILIANO ZAIDI 

DR. BRIGHTON GODWIN SHOO

+255 6139 069 30

brightonshoo7@gmail.com

 

  Kupata full soft copy link👇👇👇

Pay Now